Asalaam Aleiykum
Kila jambo katika Ulimwengu huu lina mwenza au (Pair)yake(Mfano)Usiku na Mchana, Mwanamke na Mwanamme, Ardhi na Mbingu, Baridi na Joto, Uhai na Mauti, na mengi mengineyo ya kila aina katika Ulimwengu huu, Inatajwa habari hii katika Quraan sura ya (adh-Dhaariyat aya ya 49)وَمِن ڪُلِّ شَىۡءٍ خَلَقۡنَا زَوۡجَيۡنِ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
"Na katika kila kitu tumeumba Dume na jike ili mpate kufahamu
. Leo Hapa Nakuchukua katika Ulimwengu wa Ndani na Mwenzie Nje, Nisije kusema Ndani na nje ukaanza kukimbilia kwenye Nyumba, leo sio kusudio lake hapa, Nilokusudia kukufahamisha hapa ni ile Ndani ya Maumbile yako ambayo unayo ishi.
Katika Ufalme wako wa Fahamu (Conscious) Una athari mbili ambazo unazozitumia za ima kwenda nje au kubakia ndani, (Mfano)Katika matendo ya kubakia ndani unaweza kuficha siri katika kifua chako, unaweza kufuga chuki, unaweza kuzuia hamaki, unaweza kuota ndoto usimwambie mtu, kuna mambo chungu nzima unaweza kuweka katika kifua chako ikawa mtu yoyote hajui isipokuwa wewe na Mollah wako ndio wenye kujua nini umekificha katika kifua chako, huko ndio ndani nnapo kusudia katika darsa hii ya leo, huko ndiko kwenye mahusiano na (Akhera) Na kule nje unako kwenda kutembea ni huku kwenye makelele, kwenye karata, kwenye kushea (Joke) kwenye Mazungumzo, kwenye magonvi, kwenye maasi, kwenye husda choyo na chuki, kwenye fujo zote za maisha na harakati za (Dunia) huko ndio nje ambako pia ntafahamisha madhara yake.
Kama kawaida yangu ntaichukua aya 4 zilizomo mwisho wa kwenye Sura ya (Fajir) ili itupeleke katika safari hii ya ndani na nje, Hapa itabidi mnisamehe nianze safari hii kutokea ndani kwenda nje ili tupate faida zote mbili.
Kwanini nikaanza Ndani kwa sababu hiyo ndio (Nature)yako, huko ndiko unakotokea, nje unakua umepotea.
Basi kabla ya kuzichukua aya hizo za mwisho za sura ya (Fajir)wacha nikuonjeshe aya ili ikubebe katika safari hii ya ndani akhera na nje duniani ili upate kufahamu vizuri.
Quraan aya ya 20(Ash-Shura)
مَن كَانَ يُرِيدُ حَرۡثَ ٱلۡأَخِرَةِ نَزِدۡ لَهُ ۥ فِى حَرۡثِهِۦۖ وَمَن كَانَ يُرِيدُ حَرۡثَ ٱلدُّنۡيَا نُؤۡتِهِۦ مِنۡہَا وَمَا لَهُ ۥ فِى ٱلۡأَخِرَةِ مِن نَّصِيبٍ
"Mwenye kutaka Jaza(Malipo)ya Akhera tutamzidishia katika jaza yake hiyo, Na anayetaka jaza ya dunia tutampa, Lakini Akhera hatakuwa na sehemu yoyote ile ya kheri".
Natoa msisitizo amkeni usiku msali na ikisha msome Quraan, au nyakati za alfajiri ili upate ushuhuda au ufunuo wa maneno haya mazito yaloteremka katika dini hii ya Uislam.
Aya imeanza Mwenye kutaka jaza, mimi nikasema neno(Malipo)kwa ukweli sio malipo umefanya nini hata ulipwe, lakini ili unifahamu ndio nikasema neno (malipo)lakini aya imesema Jaza, na Jaza ikatiwa neno tutamzidishia, ina maana unayo tayari, ila ukitaka jaza ya hiyo Akhera utazidishiwa, kivipi? na vipi utataka? Jaza ya kutokea upande wa pili wewe unayo, kama afya njema, furaha, unalala na kuamka, umepewa mke au umepewa mume, ndio aya ikasema tutamzidishia, kuzidishiwa hapa ni kule kupewa kwako katika hayo maeneo mawili ya (Akhera na Duniani) na kutaka kwako ni huko kufanya (Taqwa)ndio aya ikasema tutamzidishia(Ndani kiko na nje unaongezewa).
Na huyo Mwenye kutaka vya Dunia pia na yeye tutampa, hapo aya imebadilika, mwanzo utazidishiwa, sasa imekuja na neno tutampa, kupewa maana yake huna, unapewa, kupewa ni kwa muda, mara unanyanganywa, mara kinamalizika, mara ulikua tajiri na sasa umekua masikini, huko ndiko kupewa, halafu ukaambiwa ukipewa ujue Akhera utakua huna kitu, kwa sababu kupewa ni kwenye Dunia(Temporary), na dunia ni yenye kukusahaulisha na kila kitu chenye mahusiano na Akhera. Ndani Akhera nje Duniani.
Endelea Part 2
Sunday, March 13, 2016
NDANI AKHERA NJE DUNIANI PART 2
Asalaam Aleiykum
Unasoma aya hizi jitahidi usipite kama (Kasuku)utakua hupati maana, au utakua unapata tafsiri zako za kichwani halafu unajijibu (Imefanana) isikilize aya inasemaje, zama uitizame inakwambia nini?subiri ikufungulie miujiza yake. Kama ipi?
Quraan (Fajir 27)"يَـٰٓأَيَّتُہَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَٮِٕنَّةُ "
"Ewe Nafsi" Kwanini ikatajwa nafsi na sio Mwanaadamu, Kwanini isisemwe ewe Kiumbe, Unajua maana yake?. Ni kwa sababu ya kukuonesha ishara ya kitu fulani muhimu, kukufahamisha kuwa kuna siku utavuliwa hilo guo ulilovaa(Body)Mwili, kwamba kuna siku utarejea kama (As Pure Being), Wacha kudanganyika na Ndevu, Nywele, uso mzuri, mara umetia (Make-up)vyote hivyo sio wewe, wewe nani?.
Wewe ndio hiyo Nafsi inayoitwa hapo juu au kwa jina jengine (Roho), Katika huo Mwili wewe unaishi kama unavoishi kwenye nyumba yako lakini bado hujijui.
Naam sasa kwanini ukaitwa Mwenye matumaini?, Neno hili asili yake limezaliwa katika mzizi wa neno (Tumaanin)likimaanisha utulivu, Nini utulivu? Utulivu ni (Peace)Amani, Na hiyo Amani ina njia mbili kupatikana kwake, ya kwanza inakua umeridhia hali yoyote ulo nayo, Na ya pili ni ile hali ya kupigana vita au kushindwa na kitu au jambo hapo tena ukawa huna hila au wala njia ila ku(Surrender).
Nini (Surrender)? Kiarabu (surrender) ndio hiyo (Islam). Kwa hiyo hapo unaitwa "ewe Nafsi ulo (Surrender) ukawa Muislam wa kweli, baada ya kugundua au kufahamu yakua mbio zako zote za Nje(Duniani)hazina faida na wewe, Wizi, Uzinifu, Choyo,Tamaa,Hasada,Hamaki,Chuki,Uongo,Ugonvi,Jeuri,Fitina,Uadui, ukaona vyote hivyo sasa havina faida na wewe, na umekua ukivifata Nje(Duniani)kwenye Umri wako wote na havijakupa ila madhara na mashaka matupu.
Vipi Mambo ya kidunia yana mashaka, hapa itabidi nikupe mifano ili upate kunifahamu kwa uzuri. kila kitu katika Ulimwengu huu kiko (Pairs) na mwenzake, Kama (Chungu mwenzie Tamu)Raha mwenzie Maumivu, kucheka Mwenzie kulia, sasa ukiangalia kwa undani utajua hakuna hata siku moja ukapata chungu ikawa chungu pekee, lazima kuna wakati utaonja tamu, hiyo ndio hukumu ya Ulimwengu huu vitu viko(Pair's). Sasa utakapogundua hayana faida kila siku mara chungu mara tamu unateseka tu, ukilielewa hilo hapo wewe ndio unakua tayari ushajiandaa kuanza (Jihad ya Nafsi).
Utajiuliza nini Jihad Nafsi?Mimi ntakujibu au Utajibiwa na quraan kama utaifahamu, Jihad ya Nafsi maana yake bakia ndani(Akhera)usende Nje (Duniani).
Niliposema mimi ntakujibu kwa sababu mimi rahisi kunifahamu, tunaongea lugha moja, Lakini Quraan ni maneno mazito "Siku zote inakwambia hichi haramu na hichi halali, unaacha vya halali na unafanya vya haramu", jee hapo unaifahamu. Sasa vipi ubaki Ndani? na Kwa nini ndani nikaita Akhera.
Endelea part 3
Unasoma aya hizi jitahidi usipite kama (Kasuku)utakua hupati maana, au utakua unapata tafsiri zako za kichwani halafu unajijibu (Imefanana) isikilize aya inasemaje, zama uitizame inakwambia nini?subiri ikufungulie miujiza yake. Kama ipi?
Quraan (Fajir 27)"يَـٰٓأَيَّتُہَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَٮِٕنَّةُ "
"Ewe Nafsi" Kwanini ikatajwa nafsi na sio Mwanaadamu, Kwanini isisemwe ewe Kiumbe, Unajua maana yake?. Ni kwa sababu ya kukuonesha ishara ya kitu fulani muhimu, kukufahamisha kuwa kuna siku utavuliwa hilo guo ulilovaa(Body)Mwili, kwamba kuna siku utarejea kama (As Pure Being), Wacha kudanganyika na Ndevu, Nywele, uso mzuri, mara umetia (Make-up)vyote hivyo sio wewe, wewe nani?.
Wewe ndio hiyo Nafsi inayoitwa hapo juu au kwa jina jengine (Roho), Katika huo Mwili wewe unaishi kama unavoishi kwenye nyumba yako lakini bado hujijui.
Naam sasa kwanini ukaitwa Mwenye matumaini?, Neno hili asili yake limezaliwa katika mzizi wa neno (Tumaanin)likimaanisha utulivu, Nini utulivu? Utulivu ni (Peace)Amani, Na hiyo Amani ina njia mbili kupatikana kwake, ya kwanza inakua umeridhia hali yoyote ulo nayo, Na ya pili ni ile hali ya kupigana vita au kushindwa na kitu au jambo hapo tena ukawa huna hila au wala njia ila ku(Surrender).
Nini (Surrender)? Kiarabu (surrender) ndio hiyo (Islam). Kwa hiyo hapo unaitwa "ewe Nafsi ulo (Surrender) ukawa Muislam wa kweli, baada ya kugundua au kufahamu yakua mbio zako zote za Nje(Duniani)hazina faida na wewe, Wizi, Uzinifu, Choyo,Tamaa,Hasada,Hamaki,Chuki,Uongo,Ugonvi,Jeuri,Fitina,Uadui, ukaona vyote hivyo sasa havina faida na wewe, na umekua ukivifata Nje(Duniani)kwenye Umri wako wote na havijakupa ila madhara na mashaka matupu.
Vipi Mambo ya kidunia yana mashaka, hapa itabidi nikupe mifano ili upate kunifahamu kwa uzuri. kila kitu katika Ulimwengu huu kiko (Pairs) na mwenzake, Kama (Chungu mwenzie Tamu)Raha mwenzie Maumivu, kucheka Mwenzie kulia, sasa ukiangalia kwa undani utajua hakuna hata siku moja ukapata chungu ikawa chungu pekee, lazima kuna wakati utaonja tamu, hiyo ndio hukumu ya Ulimwengu huu vitu viko(Pair's). Sasa utakapogundua hayana faida kila siku mara chungu mara tamu unateseka tu, ukilielewa hilo hapo wewe ndio unakua tayari ushajiandaa kuanza (Jihad ya Nafsi).
Utajiuliza nini Jihad Nafsi?Mimi ntakujibu au Utajibiwa na quraan kama utaifahamu, Jihad ya Nafsi maana yake bakia ndani(Akhera)usende Nje (Duniani).
Niliposema mimi ntakujibu kwa sababu mimi rahisi kunifahamu, tunaongea lugha moja, Lakini Quraan ni maneno mazito "Siku zote inakwambia hichi haramu na hichi halali, unaacha vya halali na unafanya vya haramu", jee hapo unaifahamu. Sasa vipi ubaki Ndani? na Kwa nini ndani nikaita Akhera.
Endelea part 3
NDANI AKHERA NJE DUNIANI PART 3
Asalaam Aleiykum
Kitu cha mwanzo itabidi ukitafute nini kinacho kushawishi utoke Nje(Duniani) kinachokupa ushawishi huo hakuna chengine isipokua hiyo Akili yako(Mind)inakupa amri zote kwa njia ya (Memory)"Wewe Bwana unageuka Mtwana", Sasa vipi unakwenda Nje, Ni kwa ajili ya fikra zako, zimekutawala na mambo ya Nje, itizame (Mifano). Fulani atasemaje, Kajenga vipi mimi nishindwe, Mbona kahamaki, Kwanini anavaa vizuri mimi siwezi, Kuna siku ntawakomesha, Mbona kanicheka, Utajiri kapata wapi,nikimpata atanikoma, vipi nimuibie, kutwa nzima wewe ni Mwenye kuishi nje kwenye Madhanmbi, Ndio maana "Bwana Mtume s.a.w" Akaashiria kwenye kifua akihimiza watu warudi ndani kwenye (Taqwa).
Taqwa au Ucha Mungu uko Ndani, huko nje mnako kimbilia ni dhanmbi tupu. Kwa hiyo aya ya 28 inaendelea kwa kusema.
ٱرۡجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً۬ مَّرۡضِيَّةً۬
Rudi kwa Mollah wako hali yakua utaridhika na (Mollah)wako aridhike na wewe. Watu wengi wanadhani usubiri mpaka mauti yamehudhuria ndio urejee, marejeo yalokusudiwa hapa ni yale ya (Taqwa)Ucha Mungu.Urejee uwe unaishi ndani(Akhera)vipi utarejea huna taqwa, hujatenda mema, vipi wewe utarejea na mijidhanmbi yako, kinachotakiwa hapo urudi ungali uko hai, Na kurejea ukiwa hai ni huko kuishi ndani, vipi utarudi kwa Mollah wako?, Wanojua hawaulizi swali hili kwani wanajua hiyo Roho imetokana na yeye, kwa hiyo ukirudi ndani unakutana na Mambo ya Akhera, na huo ndio Ucha Mungu.
Unarejea Vipi? Pata habari hii ndio iwe ngao yako, iwe ndio sababu ya kubadilika kwako, wepi wanorejea kama huwajui wacha nikujulishe ni hawa hapa.ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَـٰمً۬ا وَقُعُودً۬ا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَڪَّرُونَ فِى خَلۡقِ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَـٰذَا بَـٰطِلاً۬ سُبۡحَـٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ
"Ambao humkumbuka Mwenye enzi Mungu wakiwa wamesimama na wakikaa na wakilala, Na hufikiri umbo la Mbingu na Ardhi,(Wakasema)Mollah wetu hukuviumba hivi bure, Utukufu ni wako,Basi tuepushe na adhabu ya moto."
Hao ndio wenye kuishi ndani, Ukiishi ndani unakua huna mawazo mengine isipokua kumkumbuka Mollah na hiyo ndio (Taqwa) Na huko ndani ndio unaipata hiyo (Tafakuri)huko ndio utakapofunguliwa mambo ukaijua yakini kuwa kweli hakuumba vitu hivi bure, na huko ndani ndiko utakapogundua kweli Moto upo na utaomba uepushwe nao, inayotakiwa ni hiyo (Tafakuri) nini Tafakuri,ni hali ya kwenda (Beyond mind) unayoipata ukiishi ndani.
aya inasema "Rudi utaridhika"(Umeridhika)kuridhika kwenyewe ni huko kukaa ndani, ukawa hutaki mali, hutaki umaarufu, hutaki Uadui, hutaki Uongo, Hutaki wanawake au wanaume, hutaki siasa wala kumchukia mtu, hutaki mambo yote ya kipuuzi yaliyopo nje(Duniani).
Ukisharidhika ikawa umekubali hali ulo nayo, na ukawa kiukweli hutaki tena vilivyopo nje, Basi (automatic)unabakia ndani(Akhera), Na kubakia ndani hakuna chengine isipokua unakutana na Taqwa,(Kamailivotajwa katika hiyo aya hapojuu), Na kumbuka wewe ukiridhika kikweli basi haichukui muda hapo hapo Mollah wako na yeye anaridhika na wewe.
Unageuka kuwa mtu wa aina nyengine kabisa, Unapata mambo mengine kabisa sio ya Ulimwengu huu, kwa sababu ndani hakuna kawaida unayo ifahamu wewe ya tamu na chungu, Raha na maumivu, ndani unakwenda (Beyond)kukutana na kitu kiitwacho(Bliss)ndio mwanzo wa darsa aya ikasema"Unazidishiwa"kama utataka vya Akhera, hiyo (Bliss) siwezi kukuhadithia inabidi uende ndani Mwenyewe ukaonje, lakini shuruti lake kwanza lazima uridhike, ikisha ndio upewe zawadi hiyo ikaayo ndani.
Halafu tena aya ya 29 inaendelea kwa kusema.
فَٱدۡخُلِى فِى عِبَـٰدِى
Basi ingia katika waja wangu.
Hapo sasa kuna mabadiliko (Mwanzo ilikua Nafsi) na sasa unaitwa kwa jina la (Abdi)Mja, Sababu hiyo Roho ni yenye (Bliss) tupu ili ku(Enjoy)au ku (Experience)unahitaji(Body)"Kutokana na hiyo Ardhi nyinyi tumekuumbeni, tunakufisheni na kukufueni kwa mara nyengine tena"Kwa hiyo sasa unaitwa Mja ili uwe katika waja wake ambao hawakutajwa wepi, na sababu kubwa wako wa aina nyingi, inategemea na Ucha Mungu wako na daraja uliyonayo kwa Mollah wako, kuna Ibad Swalihunna, Muhsinuna,Muslihunna,Muttaqinna, na wengi wengineo, kwa hiyo sasa na wewe unaitwa ukiwa Ume(Surrender)na daraja yako utaijua ukiingia ima ndani au kama aya inavomalizia.
وَٱدۡخُلِى جَنَّتِى
Ingia Peponi
Kumbuka huko ndani ndio kwenye hiyo Pepo. Na kwanini urudi kwa sababu mwanzo ulikua huko peponi(Hukumbuki kisa cha Baba yetu Adam)mwanzo tulifukuzwa humo peponi na sasa unaambiwa umesamehewa na Mollah wako karidhika na wewe, kwa kuwa umetubu, umeacha uliyokua ukiyapenda kwa ajili yake, na wala hurejei tena. Basi ukiwa umelijua hilo nakutaka utambue mwanzo rejea ndani upate hiyo (Taqwa)ikisha utaupata huo mlango wa kuingia peponi, hiyo ndio maana ya Ndani(Akhera)Taqwa, na Nje(Duniani)Dhanmbi. Basi mpaka unasoma darsa hii najua bado uko nje, kwa hiyo una hiyari yako ima kuingia ndani au kubaki nje.
Kitu cha mwanzo itabidi ukitafute nini kinacho kushawishi utoke Nje(Duniani) kinachokupa ushawishi huo hakuna chengine isipokua hiyo Akili yako(Mind)inakupa amri zote kwa njia ya (Memory)"Wewe Bwana unageuka Mtwana", Sasa vipi unakwenda Nje, Ni kwa ajili ya fikra zako, zimekutawala na mambo ya Nje, itizame (Mifano). Fulani atasemaje, Kajenga vipi mimi nishindwe, Mbona kahamaki, Kwanini anavaa vizuri mimi siwezi, Kuna siku ntawakomesha, Mbona kanicheka, Utajiri kapata wapi,nikimpata atanikoma, vipi nimuibie, kutwa nzima wewe ni Mwenye kuishi nje kwenye Madhanmbi, Ndio maana "Bwana Mtume s.a.w" Akaashiria kwenye kifua akihimiza watu warudi ndani kwenye (Taqwa).
Taqwa au Ucha Mungu uko Ndani, huko nje mnako kimbilia ni dhanmbi tupu. Kwa hiyo aya ya 28 inaendelea kwa kusema.
ٱرۡجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً۬ مَّرۡضِيَّةً۬
Rudi kwa Mollah wako hali yakua utaridhika na (Mollah)wako aridhike na wewe. Watu wengi wanadhani usubiri mpaka mauti yamehudhuria ndio urejee, marejeo yalokusudiwa hapa ni yale ya (Taqwa)Ucha Mungu.Urejee uwe unaishi ndani(Akhera)vipi utarejea huna taqwa, hujatenda mema, vipi wewe utarejea na mijidhanmbi yako, kinachotakiwa hapo urudi ungali uko hai, Na kurejea ukiwa hai ni huko kuishi ndani, vipi utarudi kwa Mollah wako?, Wanojua hawaulizi swali hili kwani wanajua hiyo Roho imetokana na yeye, kwa hiyo ukirudi ndani unakutana na Mambo ya Akhera, na huo ndio Ucha Mungu.
Unarejea Vipi? Pata habari hii ndio iwe ngao yako, iwe ndio sababu ya kubadilika kwako, wepi wanorejea kama huwajui wacha nikujulishe ni hawa hapa.ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَـٰمً۬ا وَقُعُودً۬ا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَڪَّرُونَ فِى خَلۡقِ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَـٰذَا بَـٰطِلاً۬ سُبۡحَـٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ
"Ambao humkumbuka Mwenye enzi Mungu wakiwa wamesimama na wakikaa na wakilala, Na hufikiri umbo la Mbingu na Ardhi,(Wakasema)Mollah wetu hukuviumba hivi bure, Utukufu ni wako,Basi tuepushe na adhabu ya moto."
Hao ndio wenye kuishi ndani, Ukiishi ndani unakua huna mawazo mengine isipokua kumkumbuka Mollah na hiyo ndio (Taqwa) Na huko ndani ndio unaipata hiyo (Tafakuri)huko ndio utakapofunguliwa mambo ukaijua yakini kuwa kweli hakuumba vitu hivi bure, na huko ndani ndiko utakapogundua kweli Moto upo na utaomba uepushwe nao, inayotakiwa ni hiyo (Tafakuri) nini Tafakuri,ni hali ya kwenda (Beyond mind) unayoipata ukiishi ndani.
aya inasema "Rudi utaridhika"(Umeridhika)kuridhika kwenyewe ni huko kukaa ndani, ukawa hutaki mali, hutaki umaarufu, hutaki Uadui, hutaki Uongo, Hutaki wanawake au wanaume, hutaki siasa wala kumchukia mtu, hutaki mambo yote ya kipuuzi yaliyopo nje(Duniani).
Ukisharidhika ikawa umekubali hali ulo nayo, na ukawa kiukweli hutaki tena vilivyopo nje, Basi (automatic)unabakia ndani(Akhera), Na kubakia ndani hakuna chengine isipokua unakutana na Taqwa,(Kamailivotajwa katika hiyo aya hapojuu), Na kumbuka wewe ukiridhika kikweli basi haichukui muda hapo hapo Mollah wako na yeye anaridhika na wewe.
Unageuka kuwa mtu wa aina nyengine kabisa, Unapata mambo mengine kabisa sio ya Ulimwengu huu, kwa sababu ndani hakuna kawaida unayo ifahamu wewe ya tamu na chungu, Raha na maumivu, ndani unakwenda (Beyond)kukutana na kitu kiitwacho(Bliss)ndio mwanzo wa darsa aya ikasema"Unazidishiwa"kama utataka vya Akhera, hiyo (Bliss) siwezi kukuhadithia inabidi uende ndani Mwenyewe ukaonje, lakini shuruti lake kwanza lazima uridhike, ikisha ndio upewe zawadi hiyo ikaayo ndani.
Halafu tena aya ya 29 inaendelea kwa kusema.
فَٱدۡخُلِى فِى عِبَـٰدِى
Basi ingia katika waja wangu.
Hapo sasa kuna mabadiliko (Mwanzo ilikua Nafsi) na sasa unaitwa kwa jina la (Abdi)Mja, Sababu hiyo Roho ni yenye (Bliss) tupu ili ku(Enjoy)au ku (Experience)unahitaji(Body)"Kutokana na hiyo Ardhi nyinyi tumekuumbeni, tunakufisheni na kukufueni kwa mara nyengine tena"Kwa hiyo sasa unaitwa Mja ili uwe katika waja wake ambao hawakutajwa wepi, na sababu kubwa wako wa aina nyingi, inategemea na Ucha Mungu wako na daraja uliyonayo kwa Mollah wako, kuna Ibad Swalihunna, Muhsinuna,Muslihunna,Muttaqinna, na wengi wengineo, kwa hiyo sasa na wewe unaitwa ukiwa Ume(Surrender)na daraja yako utaijua ukiingia ima ndani au kama aya inavomalizia.
وَٱدۡخُلِى جَنَّتِى
Ingia Peponi
Kumbuka huko ndani ndio kwenye hiyo Pepo. Na kwanini urudi kwa sababu mwanzo ulikua huko peponi(Hukumbuki kisa cha Baba yetu Adam)mwanzo tulifukuzwa humo peponi na sasa unaambiwa umesamehewa na Mollah wako karidhika na wewe, kwa kuwa umetubu, umeacha uliyokua ukiyapenda kwa ajili yake, na wala hurejei tena. Basi ukiwa umelijua hilo nakutaka utambue mwanzo rejea ndani upate hiyo (Taqwa)ikisha utaupata huo mlango wa kuingia peponi, hiyo ndio maana ya Ndani(Akhera)Taqwa, na Nje(Duniani)Dhanmbi. Basi mpaka unasoma darsa hii najua bado uko nje, kwa hiyo una hiyari yako ima kuingia ndani au kubaki nje.
Subscribe to:
Posts (Atom)