Sunday, April 17, 2016

ZAWADI KUTOKA MAKKA PART 1

Asalaam Aleiykum

Nina Desturi ya kumuuliza kila anorejea kutoka (Makka)swali hili, Jee kuna kitu gani kimetokezea kwako wewe ukiwapo huko Makka?. Swali hili nawauliza watu wengi, Masheikh na Maimamu na wengineo wenye kufanya ziara hii ya (Baitul Haram), basi huwa sipati jawabu ila mshangao, wengine wanatetemeka mashavu hawajui wanijibu nini au nimekusudia nini.
Kusudio langu ndio hii zawadi ambayo leo nataka kukupa zawadi hii ya Makka, ili kama umebahatika kwenda, uende ukapate faida za Hajj na Umra kwa ukamilifu. Kuna baadhi ya watu Wanamaradhi ya kuona vyeti, wanapopata bahati ya kusoma maandiko yangu wananiuliza "Cheti" au "Certificate"wajue nimesoma chuo gani, Mpaka naandika hivi, au nakuhadithia mambo ulokua huyajui bado unasisitiza nikupe cheti ndio uridhike, Ukiona unauliza maswali ya nimesoma wapi, basi jielewe bado umo kwenye Jela ya chuo chako au madhehebu yako, au umefungika na Maalim wako au Sheikh wako kwa hiyo unataka na mimi nizungumze au kuongea sawa sawa na Mulla wako.
Toka nje uwe huru, njoo nje kuna maajabu, pata fikra mpya , usikae kuuliza vitambulisho havina faida yoyote na wewe, Wewe soma Mwenyewe hiyo ndio elimu nzuri, nani alokufundisha kusema? Nani kakufundisha kuhema, nani kakufundisha kuona na kusikia, nani kakufundisha kutembea? hizo elimu umezipata na mpaka leo hujamuuliza alokufundisha shahada yake, sio kumuuliza, kumjua humjui. Umeshikilia Mtu lazima akuoneshe cheti, au aje na elimu yake akutie kichwani mwako na wewe ndio uwe umesoma, hiyo ni sawa sawa na kukopia.
Sasa pata zawadi kama hizi zenye kukutoa kwenye kiza na kukupeleka kwenye Nuru, Na huko ndiko niliko soma mimi. Naam katika darsa hii ya Zawadi kutoka Makka Ntakuchukua taratibu ili upate kunifahamu, nakutaka ufungue zawadi hii kwa utulivu uone nini nimekuletea kutoka Makka, Napenda uelewe haya ni mazungumzo baina yangu na wale walio safarini na mimi katika darsa zangu, ni mazungumzo ya Kiroho kwa wale wenye hamu ya kujua maajabu ya Mollah wetu na Alama zake,Ni mazungumzo baina ya viumbe viwili vilojitolea kuujua ukweli kwa njia ya kusema na kusikiliza, kwa njia ya mawasiliano ya kimoyo kwa wale wenye kutumia Akili  kwa ajili ya kutafakari.
Ama kwa wale wenye kupanda ndege wakajiendea tu, watabaki kuona Jumba la saa, watahadithia habari za watu na wengine watafika huko na kuendelea kuchat na masimu yao.
Sasa tuanze safari yetu kuelekea Mji Mtukufu wa (Makka)Nitazitia aya za (Quraan) ili upate kufahamu kusudio la maelezo yangu, wala aya hizo hazina mahusiano ya kufungamana na darsa hii, bali ni kukupa wewe msomaji muelekeo au (Dira) Ramani ili unifate kwenye safari hii kwa umakini mkubwa na unielewe kwa ukamilifu.
Aya yenyewe inasemaje? Quraan Israil aya ya mwanzo (1)

سُبۡحَـٰنَ ٱلَّذِىٓ أَسۡرَىٰ بِعَبۡدِهِۦ لَيۡلاً۬ مِّنَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ إِلَى ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡأَقۡصَا ٱلَّذِى بَـٰرَكۡنَا حَوۡلَهُ ۥ لِنُرِيَهُ ۥ مِنۡ ءَايَـٰتِنَآ‌ۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ
"Utukufu ni wake Yule ambaye alimpeleka Mja wake usiku kutoka Msikiti Mtukufu (Wa Makka) mpaka msikiti wa Mbali (Wa Baitul Muqaddas)ambao tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake(Tulimpeleka hivyo) ili tumuoneshe baadhi ya alama zetu, Hakika yeye (Mwenye Enzi Mungu) ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona".
Jambo la Mwanzo nikukumbushe huwezi kwenda pahala ila atake Mwenye Enzi Mungu, unaweza kulazimisha ukataka kwenda na kuachiwa uende lakini madhara ya safari hiyo ni makubwa kuliko faida zake, Sasa hapo aya inasema kachukuliwa Mtume s.a.w Kutoka Msikiti Mtukufu(Masjid Haram) mpaka Masjid (Baitul Muqqadas) ili tumuoneshe "Alama zetu" kwa Kupelekwa Mbinguni, pia ikatajwa Kubarikiwa kwa vilivyomo pembezoni mwake. Maneno ukiyasoma kwa makini ni mazito na yanataka uchambuzi wa ndani.
Endelea part 2


ZAWADI KUTOKA MAKKA PART 2

Asalaam Aleiykum

Huyo alikua ni Mtume s.a.w akipelekwa Mbinguni kuoneshwa Miujiza ya huko, Sasa na wewe umepata bahati ya kwenda kwenye Mji Mtakatifu, Masjid Haram ya Makka, umejaaliwa kwenda kwenye Nyumba anayoabudiwa Mwenye Enzi Mungu, Nyumba ilotajwa kwenye Quraan (Al-Imran aya ya 96)
"إِنَّ أَوَّلَ بَيۡتٍ۬ وُضِعَ لِلنَّاسِ لَلَّذِى بِبَكَّةَ مُبَارَكً۬ا وَهُدً۬ى لِّلۡعَـٰلَمِينَ "
Kwa yakini Nyumba ya kwanza iliyowekwa kwa ajili ya watu (kufanya Ibada) ni ile iliyoko Makka, yenye Baraka na uwongozi kwa ajili ya Walimwengu wote.
Katika Nyumba hii lazima ziko alama hizo za Baraka na uongozi lakini hasara yetu wengi wetu hatuzioni, Waweza kwenda ukaanza kushangaa  na (Al-kaaba) au ukawa unahijji kwenye Jumba la saa, au kutwa unaishia Madukani kufanya (Shopping), au kwa siku hizi inakua umevaa vazi la kuhijji lakini hupo kabisa kwenye hijja au umra wewe umo kwenye kuchat au (Facebook).
Sasa ikiwa kwenye Sala ya Ijumaa Waumin wanakumbushwa "Enyi Mloamini Kukiadhiniwa kwa ajili ya sala ya ijumaa nendeni upesi kumtaja Mwenye enzi Mungu na acheni biashara". Nini habari yako wewe mpita njia tu hapo Makka, mgeni wa Mwenye Enzi Mungu katika Msikiti Mtukufu wa Makka umeshughulika na kuchat na kufanya (Shopping).
Ewe Ndugu yangu unapotia Nia ya kufanya Ibada hii ya Hajj au Umra jifunge upate faida hizi ntazokusimulia ili upate hizo Baraka na Muongozo. Pata kwa ukamilifu Kufanya Ibada zako katika Misikiti hii miwili ya Makka na Madina ukiwa huna shaka ya kufanikiwa.
Kwanza kabisa Ibada hii kabla ya kuianza unatakiwa ujisafishe(tohara)Kwanini ujisafishe?
Quraan sura ya Hajj aya ya 29

ثُمَّ لۡيَقۡضُواْ تَفَثَهُمۡ وَلۡيُوفُواْ نُذُورَهُمۡ وَلۡيَطَّوَّفُواْ بِٱلۡبَيۡتِ ٱلۡعَتِيقِ
"Kisha Wajisafishe taka zao, Na watimize nadhiri zao, na Waizunguke Nyumba ya kale(Al-Kaaba).
Kwa hiyo sasa unajitia Tohara ya Nje ni kule kukoga na Tohara ya Ndani ni kutaka au (Kuomba)Maghfira kwa Wingi. Kuanza kwa nia yako ni kule kujifunga kwa kumtaja Mollah wako na kumkumbuka yeye pekee katika Ibada hii Maalum, Jambo la Pili unatakiwa Ku (Surrender)Unavuliwa Nguo zote na kubakishwa na vipande viwili vya kitambaa cheupe(Ihram) hii kuoneshwa wewe ni (Nothing)ni (Symbolic)sawa sawa na wengine wote, au kujionesha kwa Mollah wako mimi mbele yako sina cheo chochote, kwako sina Mamlaka, niko hapa naitikia ule Mwito wako wa kuidhuru Nyumba yako Tukufu. Na hiyo ndio Nafsi inayotakiwa ya yule alokwenda kudhuru Miji hii ya Makka na Madina, kama inavotaja aya ya (32)
ذَٲلِكَ وَمَن يُعَظِّمۡ شَعَـٰٓٮِٕرَ ٱللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقۡوَى ٱلۡقُلُوبِ
Namna hivi anaziheshimu Alama za (Dini ya)Mwenye Enzi Mungu , Basi hilo ni jambo katika Utawa (Ucha Mungu) wa Nyoyo.
Shukran zote Mollah wangu unastahiki wewe kwa kunipa Imani na Afya ya Mimi kuja kuabudu kwenye Ardhi hii, Neema zote hizi na Ufalme wa haya yote ni wako wewe Mollah wangu, Na wala huna Mshirika.
Endelea part 3

ZAWADI KUTOKA MAKKA PART 3

Asalaam Aleiykum

Nakukumbusha wakati unaingia Mji wa Makka kuna mambo yanakutokezea, kwanini sijasema yanatokea?, kwa sababu wewe bado huna (uwezo wa kuyaona)bado huwezi kuwaona majini nao Wakitufu, ndio maana nikasema au kukwambia ujitizame mwenyewe kwenye nafsi yako nini kina kutokezea.
Yasikilize mambo yanotokea, kama wewe ni (Nagative Energy) ambayo ni (Receptive)yenye kupokea, yenye desturi ya (surrender)basi moja kwa moja ukiiona (Al-Kaaba)utajiona unatokwa na machozi, au hali yako unabadilika pengine khofu inakujaa, usiogope kuna kitu kinatokezea, na hali kama hii inawapata hususan Wanawake wanayo Baraka hii ya (Nagative Energy of surrender-)Wanawake wao (Receptive) ndio maana wao rahisi kulia, kwa kuwa pahala kama hapa (Something of beyond happening)kuna kitu kinatokezea, basi ikikukuta hali kama hiyo usiogope jitupe kwa Mollah wako angua kilio cha kweli kweli kuomba kwa Mollah wako tumia wakati huo adhimu usije ukaukosa pengine hutolia tena mpaka unaondoka Mji Mtukufu.
Wala usione haya ukajizuia kugaragara kwa maombi ukawa unaona haya, mbona zamani ulikua ukicheza (dance) chacha, pachanga,(disco)huoni haya, leo uko kwenye nyumba ya Mwenye Enzi Mungu ndio unaona haya. utakapoona unajizuia basi jijue bado huja(Surrender).
Na Kwa wale wenye (Positive Energy of Giver)inachukua muda lakini mabadiliko (Transformation)yanatokea, Na kama umekwenda kwenye Mji huu ikawa hujapata mabadiliko yoyote basi Nakuusia Nenda tena, wewe bado hujenda, utakua umekwenda lakini utakua sawa sawa na wale (Maqureish) waliopo pale, wako chini ya (Al-Kaaba)lakini wameshughulika na biashara(Khamsa Riyal na Punch Riyal) Maskini hawana njia ya kujua kwenye nyoyo zao thamani ya pahala hapo.
Tumo tukiendelea kufungua zawadi yetu kutoka Makka na sasa tunakutana na swali hili la Mshangao, Mbona Makka kuko (active)mbona kumoto, watu wake wakali, wamechangamka, pirika pirika zimezidi?, Watu wote wameshughulika pana nini pahala hapa?.
Nisikilize kwa Makini jawabu yake ili kama na wewe utakwenda au kuna Mtu anakwenda umueleweshe mambo yalioko huko, kwanini ikawapo hali kama hiyo, Inapaswa ikumbuke pahala popote anapoteua Mfalme wa Mbingu na Ardhi basi sehemu hiyo inakua Takatifu, na eneo hilo lazima liwe liko katika jinsia ya (fire) au Moto, kuna mkusanyiko wa Majini na Malaika hapo. Ndio Maana utaona katika Safari ya Miraji Sydna Jibril a.s alimwambia Bwana Mtume s.a.w kuna sehemu mimi sifiki, nenda peke yako, (Lazima ipatikane Transformation fulani)Na hapo Makka kuna hilo Jiwe la (Hajral-Aswad)Ndani ya (Al-Kaaba), jiwe lilotokea Mbinguni ambalo hutokezea miujiza, ita utakavyo (Power, Energy)  lakini elewa hapo kuna kitu chenye kuwafanya wengine warukwe na akili, wengine wasihisi chochote, wengine hata wasione hiyo Kaaba, wengine wapate uongofu na  kama ilivompata Nabii Musa a.s, angalia nini kilimtokezea yule Msemezwa na Mollah wake.
Sura ya Taha aya ya 10.
إِذۡ رَءَا نَارً۬ا فَقَالَ لِأَهۡلِهِ ٱمۡكُثُوٓاْ إِنِّىٓ ءَانَسۡتُ نَارً۬ا لَّعَلِّىٓ ءَاتِيكُم مِّنۡہَا بِقَبَسٍ أَوۡ أَجِدُ عَلَى ٱلنَّارِ هُدً۬ى
Alipouona Moto, akawaambia watu wake (Alokua nao) Ngojeni, hakika nimeona moto, huenda nikakuleteeni kijinga katika huo(Moto)au Nitapata muongozaji katika moto huo.
Nabii Musa a.s kasema maneno mawili inatubidi tuyazingatie sana, la kwanza kasema huenda nikakuleteeni kijinga(ambacho hakina maana)au nitapata muongazaji. Sehemu yoyote Takatifu ukenda kumbuka utarudi na mambo mawili huenda ukarudi na (Kijinga)maneno mengi, habari chungu nzima, au utarudi umebadilika umepata uongofu kwa hiyo Tahadhari.
Ukirudi na habari ndio itakua Al-kaaba iko hivi, Jabal Nur liko vile, lakini ukirudi na Muongozo huna hadith, unakaa kimya, ukifunga macho ufunuo unakujia, vikija vishawashi unakua mwepesi wa kuviepuka, huku unasikia watu wanasema, karudi Makka siku hizi hachezi tena Ngoma, na hivi na vile.
Basi alipofika Nabii Musa a.s alijaa khofu alikuta Moto unawaka lakini hauunguzi chochote, akaambiwa vua viatu sasa uko kwenye Jangwa Takatifu la (Tuwa) na kilicho endelea hapo ni (History of ten commandments). Na hali kama hiyo inakutokea wewe ukifika katika Sehemu Takatifu, lakini pengine ukhisi kwa mizigo ya Dhanmbi ulobeba, au moyo una kutu bado hujajisafisha.
Nabii Musa a.s kuanzia hapo akapata (Transformation)akapewa (Wahyi)awapelekee mayahudi, Mayahudi wakanyanyuliwa kuanzia hapo kwa darja, Na kutokea hapo kwenye Mlima wa sinai na Makka sio masafa marefu,  Mtume Mohammad s.a.w akapewa Utume kwenye hilo Jabal Nur, akateremshiwa Quraan napo si mbali na hiyo Baitul Haram(Al-Kaaba)Na Maqureish nao wakanyanyuliwa na hizo Baraka zilzopo pembezoni(Mafuta Nk).
Ama kuhusu Madina hapo kuna (Receptive Energy), hapo ndipo alipozikwa yule ambaye ndani ya mifupa yake imepita hii Quraan, yule ambaye alipelekwa Mbinguni kwenye usiku Mmoja kuoneshwa miujiza ya huko, yule ambaye aliyeiona (Lailatul Qadir)akapata (Enlightement) baada ya Miaka 1400 (Energy)yake imebakia au Wasila unofanya Mji huo kuwa wa (Peace)kuwa wa (Surrender)Na kwa ajili hiyo kila anokwenda kwenye mji huo anapata kuhisi tafauti hiyo. Na kama hamjui siri iliyopo kwenye Mji huo wa Madina hebu waulizeni (Wa-Hindu)mbona nyote mkifa mnachomwa moto isipokua akifa (Sheikh)wenu hamchomi moto kwanini? jawabu lake linaweza kukusaidia kupata kujua hali ya utulivu unayokutana nayo Madina. Hapo ndipo alipolala yule aloaminiwa na Billion ya watu ulimwenguni kote, yule Mwenye kutajwa kila siku mara tisa. leo umehudhuria katika Mji alozikwa lazima upate (Experience) ya (Energy) inoendelea kumiminika kwenye Mji huo wa Madina, basi ukifika kakae Msikitini kwake upate shufaa, upate Faraja na Umasalimie Mtume wako bila ya woga.