Asalaam Aleiykum,
Kuna Msemo wa "Kiswahili Mzuri sana"unasema hivi"(Ukweli ukidhihiri uongo hujitenga) Hiyo ni kweli kabisa, hali kama hiyo Mwanaadamu unayo lakini bado hujaifanyia kazi, pengine dunia imekushughulisha, basi kutokana na makumbusho haya labda waweza kuanza kutafakari na kujiwezesha kuwacha kuishi kizani,utaanza kuishi kwa njia ya kutumia Taa ulonayo,Usikubali tena Umeme wa Nje Uzimwe na wa ndani kwenye Nafsi yako Uzimike.
Nini Taa?. Mpaka leo hakuna aliyeweza kutwambia au kuchambua , au kujua nini Taa, Si Wanasayansi wa Dunia wala wa Dini walofanikiwa kujua nini Taa, Wanasayansi wao wamechambua na kufikia kuieleza utendaji wake wa kazi, wakasema hakuna kitu kiendacho kwa kasi kama Taa(speed of light) na hivi karibuni wamegundua kuwa kila kitu mwishoe kinabadilika na kuwa hiyo Taa(Light), Lakini wakiulizwa Taa yenyewe ni kitu gani hawawezi kulijibu swali hilo.
Na Wanasayansi wa Kidini au niwaite(Wanazuoni)wao wamegundua kuwa kila ukenda ndani au kuzidisha Ibada unakutana na hii Taa(Light), Lakini pia hawajui nini uwezo wa hiyo Taa ya ndani, nini kazi yake?, ila wanaamini hii Taa ina uwezo wa kukuongoza kutoka kwenye giza kwenda kwenye Nuru, ziko dalili zinaonesha iwapo utapunguza Ibada au kutenda Dhanmbi inakua inapungua nuru ya taa hiyo.
Tukizungumza Taa inabidi tuieleze Taa ya aina gani, kwa sababu Taa ziko za aina nyingi japokua asili yake ni moja. Mfano Taa hii ya Jua ambayo ndani yake zinapatikana faida nyingi tu si za kuondosha usiku pekee mpaka (Vitamin D)imo kwenye Taa hiyo. Kwa hiyo taa ni nyingi na zina kazi tafauti, leo sisi tutaizungumzia Taa ya ndani, taa ya Nafsi yako, kabla ya kwenda mbali wacha tuutizame mfano mdogo ili utupe muelekeo wa Darsa yetu, na hapa tutaichukua Taa yetu ya kawaida(Umeme), Na wakati mzuri ni ule ambao Taa zimezimwa, Kiza kimetawala chumbani, nini kinatokezea?.
Inapokua kiza maana yake huoni kitu, lakini mara inapoletwa au kuwashwa Taa unaviona vitu vyote viliopo katika chumba hicho, na hivyo pia ndivyo Taa ya Fahamu inavofanya kazi yake, mfano ni uleule hakuna tafauti.
Sasa kwa Mwanaadamu Taa hii ina kazi mbili ama kazi ya kwanza nini kukutoa kwenye Ujinga na kukupeleka kwenye werevu au ita (Elimu)na kazi ya pili ni kukuonesha chumba chako cha Nafsi na Takataka, mavumbi, fanicha na vyote vilojificha kwenye Nafsi yako. Ndio maana tutatumia aya moja kutufahamisha kuwapo kwa Taa hii, na vipi "Ukweli Ukidhihiri uongo hujitenga", vipi inakua wakati ukiigundua taa hii, faida gani unaipata katika kuitumia Taa hii.
Sura ya Kiyama aya ya (14-15)
بَلِ ٱلۡإِنسَـٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٌ۬
Bali Mwanaadamu ni Shahidi(Mwenye kuona)Nafsi yake.
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُ
Ingawa anatoa Nyudhuru zake.
Naam ilipotajwa kuona au kuishuhudia Nafsi yako hapo inatakiwa ujiulize nini kimekusudiwa, Lazima ujiulize nini nafsi na nani Mwenye kuiona, na utafute maana halisi yakutambua kumbe kama najiona ina maana mimi ni tafauti na nafsi. Basi ikiwa tafauti kwanini naleta Nyudhuru, ukiweza kugundua mawili hayo hapo hapo utaelewa kumbe hii nyudhuru ndiko huko kuzima hiyo Taa.
Mwanaadamu unajiona matendo yako yote, na kuona huku ndio huo Muujiza, kwa sababu macho yanoona wewe una uwezo wa kuyaona, sasa hicho kinachoona nini?, kifanyie kazi upate kukijua, kama nilivosema wewe na Nafsi ni vitu viwili tafauti, ila unazidiwa na nafsi, Nafsi inakutawala nakuchukua madaraka yako, inatakiwa ufanye kazi kubwa sana kuishinda Nafsi, ndio Nabii Yusuf akathibitisha kwenye quraan sura ya Yussuf aya 53.
وَمَآ أُبَرِّئُ نَفۡسِىٓۚ إِنَّ ٱلنَّفۡسَ لَأَمَّارَةُۢ بِٱلسُّوٓءِ إِلَّا مَا رَحِمَ رَبِّىٓۚ إِنَّ رَبِّى غَفُورٌ۬ رَّحِيمٌ۬
Nami sijitakasi nafsi yangu , kwa hakika (Kila) Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu, isipokua ile ambayo Mollah wangu ameirehemu, Hakika Mollah wangu ni Mwingi wa Kusamehe na Mwingi wa Kurehemu.
Naam hiyo ndio Akili ina Mwenendo upi?
Endelea Part 2
Thursday, November 3, 2016
TAA YA FAHAMU PART 2
Asalaam Aleiykum
Akili ina mwenendo wa njia mbili, Njia ya kwanza kutupa kila kitu kwenye chumba chake, halafu inazima Taa, inajifanya haitazami tena, haina haja ya kuwasha Taa tena na kusafisha chumba, na njia ya Pili ambayo ya kusafisha hicho chumba au kuwasha Taa ukaona vitu vilivyomo huitumii kabisa, kumbuka kila kiingiacho chumbani kinahitaji kutolewa, na huwezi kuvitoa vitu hivyo mpaka uwashe Taa hii ya fahamu, Nikimaanisha jambo lolote linaloingia kwenye akili pia linashuka kwenye moyo, Sasa maradhi yote na matatizo yote yanakukuta sababu ndani ya chumba chako kuna takataka nyingi, vumbi limejaa, umebeba mizigo ambayo huna haja nayo katika safari yako.
Kwa hiyo unatakiwa ufanye jitihada kutupa yaliyomo ndani ili uishi kwenye Ulimwengu huu kwa Furaha, na kutokana na sababu hiyo ndio sasa nakutaka uwashe hiyo Taa ya fahamu ili upate kutoka kwenye kiza. Kumbuka Nabii Yusuf a.s anasema Nafsi ina amrisha maovu na kuna njia moja tu ya kuweza kuishinda nafsi ambayo yeye aliitumia na sasa ushafika wakati na wewe uitumie.
Aliendelea na kusema isipokua upate Rehma ya Mwenye enzi Mungu, vipi unaipata Rehma hiyo, kawaida yako wewe unafanya kazi ndani ya Rehma, maisha yako yote ni Rehma, na hakuna Rehma kubwa kama hii ya kuona. Sasa nini kinatokezea?kila jambo linatokezea unapeleka kwenye nafsi yako, Senema unaangalia wanawake au wanaume vimo humo, unafanya wizi na ufisadi, unasema uongo, unashuhudia maasi na kila machafu hayo yote kumbuka yanapita na kuingia kwenye chumba chako, ikisha unakwenda kulala wewe chumba kimejaa mambo, unazima taa huna wasiwasi, ukiamka unaanza tena na tena, sasa hata siku moja hujasafisha ndani ya chumba, unakata kucha, unapaka (Poda)unakoga unatia uturi, Nyumba nje Mashaallah inasafishwa kikweli, lakini nini habari ya ndani?, Nani basi wa kukusafishia isipokua Mwenyewe, na Chumbani kiza utasafisha vipi si lazima uwashe Taa.
Kumbuka yote uloyaona na kusikia yamo ndani na kusafisha kwenyewe lazima iwe (Reverse)kinyume chake. kumbuka Taa ikizimika Uharibifu wote ndio unatokea, kwa sababu umo gizani unajikwaa kwenye Furniture, unajikwaa kwenye kila Dhanmbi, unatibu watu wengine kumbe wewe Mwenyewe Mgonjwa, Watu wanakushangaa jamani huyu si Sheikh mbona anafanya mambo haya, kumbe hawajui wewe na wao nyote Taa zimezimwa.
Nabii Yusuf a.s aliposema sijitakasi Nafsi yangu alikua anajua hawezi kujichukulia dhamana na Nafsi pekee, nafsi ina vituko, imo kwenye kuamrisha ufisadi na maovu kutokana inaishi kwenye giza.
Sasa ufanye nini unatakiwa utoke gizani uelekee kwenye Nuru.
Endelea part 3
Akili ina mwenendo wa njia mbili, Njia ya kwanza kutupa kila kitu kwenye chumba chake, halafu inazima Taa, inajifanya haitazami tena, haina haja ya kuwasha Taa tena na kusafisha chumba, na njia ya Pili ambayo ya kusafisha hicho chumba au kuwasha Taa ukaona vitu vilivyomo huitumii kabisa, kumbuka kila kiingiacho chumbani kinahitaji kutolewa, na huwezi kuvitoa vitu hivyo mpaka uwashe Taa hii ya fahamu, Nikimaanisha jambo lolote linaloingia kwenye akili pia linashuka kwenye moyo, Sasa maradhi yote na matatizo yote yanakukuta sababu ndani ya chumba chako kuna takataka nyingi, vumbi limejaa, umebeba mizigo ambayo huna haja nayo katika safari yako.
Kwa hiyo unatakiwa ufanye jitihada kutupa yaliyomo ndani ili uishi kwenye Ulimwengu huu kwa Furaha, na kutokana na sababu hiyo ndio sasa nakutaka uwashe hiyo Taa ya fahamu ili upate kutoka kwenye kiza. Kumbuka Nabii Yusuf a.s anasema Nafsi ina amrisha maovu na kuna njia moja tu ya kuweza kuishinda nafsi ambayo yeye aliitumia na sasa ushafika wakati na wewe uitumie.
Aliendelea na kusema isipokua upate Rehma ya Mwenye enzi Mungu, vipi unaipata Rehma hiyo, kawaida yako wewe unafanya kazi ndani ya Rehma, maisha yako yote ni Rehma, na hakuna Rehma kubwa kama hii ya kuona. Sasa nini kinatokezea?kila jambo linatokezea unapeleka kwenye nafsi yako, Senema unaangalia wanawake au wanaume vimo humo, unafanya wizi na ufisadi, unasema uongo, unashuhudia maasi na kila machafu hayo yote kumbuka yanapita na kuingia kwenye chumba chako, ikisha unakwenda kulala wewe chumba kimejaa mambo, unazima taa huna wasiwasi, ukiamka unaanza tena na tena, sasa hata siku moja hujasafisha ndani ya chumba, unakata kucha, unapaka (Poda)unakoga unatia uturi, Nyumba nje Mashaallah inasafishwa kikweli, lakini nini habari ya ndani?, Nani basi wa kukusafishia isipokua Mwenyewe, na Chumbani kiza utasafisha vipi si lazima uwashe Taa.
Kumbuka yote uloyaona na kusikia yamo ndani na kusafisha kwenyewe lazima iwe (Reverse)kinyume chake. kumbuka Taa ikizimika Uharibifu wote ndio unatokea, kwa sababu umo gizani unajikwaa kwenye Furniture, unajikwaa kwenye kila Dhanmbi, unatibu watu wengine kumbe wewe Mwenyewe Mgonjwa, Watu wanakushangaa jamani huyu si Sheikh mbona anafanya mambo haya, kumbe hawajui wewe na wao nyote Taa zimezimwa.
Nabii Yusuf a.s aliposema sijitakasi Nafsi yangu alikua anajua hawezi kujichukulia dhamana na Nafsi pekee, nafsi ina vituko, imo kwenye kuamrisha ufisadi na maovu kutokana inaishi kwenye giza.
Sasa ufanye nini unatakiwa utoke gizani uelekee kwenye Nuru.
Endelea part 3
TAA YA FAHAMU PART 3
Asalaam Aleiykum,
Sasa nini ufanye Kiumbe wewe, Kumbuka Mwanaadamu una vitendea Kazi vitu viwili, Kimoja katika hivyo hakiguswi na chochote, hakuna jambo lolote linaloweza kufikia kitu hicho ambacho ndio hiyo Taa ya Fahamu(Pure Soul). Kama Mwanaadamu utakua unakitumia kifaa hiki au nikipe heshima kwa sababu ni kitu kitakatifu(Roho)kwa uerevu, basi daima utakua umo furahani, kwanini nikasema umo kwa sababu (Roho)(Nature)yake ni Furaha(Nisiseme hivi Mkasema kasema anaijua roho kitu hicho hakijulikani), lakini hasara yetu Wanaadamu Tunaishi au kutawaliwa na hicho chengine chenye kutupeleka kwenye kiza, kipi hicho?.
Akili(Hii ni sehemu ya Nafsi) ni nyenzo ambayo tunatakiwa kuitumia kwa uangalifu kwani ni (Very Powerful weapon)silaha kubwa sana, ukimilikiwa na Akili Binaadamu umekwisha, huna (Control) ya maisha yako kabisa.
Kwa sababu Akili inafanya kazi yake ya kukusanya, kupokea na kutupa kwenye hicho chumba, chumba hiki kiite (Memory or Subconscious)na kwa kuwa lolote lile lilopita kwenye taa yako ya Fahamu kumbuka liko humo chumbani umeliweka na wala halitoki, Sasa nini kinatokezea kuna baadhi ya nyakati Taa inawaka na kumurika yale mambo yaliyomo kwenye chumba iwe chuki, hasada, uzinifu, wizi, na ukimurika tu likija juu lazima ulitende kwa sababu hujalitupa ila umeliweka akiba, kwa hiyo tahadhari sana unapokwenda kwenye chumba chako, utakua unatenda mambo bila ya kukusudia, sasa kwa kuwa mambo yana kukera ndio unaamua kuzima Taa, na huku watu wanatumia ule msemo kajitoa fahamu.
Quraan imekuhurumia imesema unaleta nyudhuru yaani unazima Taa, ndio ikaendelea kukumbusha kuwa Mwanaadamu ni Mwenye kuiona Nafsi yake, ikimaanisha unao uwezo wa kuishinda Akili, tumepewa maarifa ya kukishinda kifaa hiki, kwanza kwa kujulishwa wewe na hicho kifaa ni tafauti, ndio maana ukaambiwa wewe unakiona kitu hicho, na una uwezo wa kukitumia usiache kikakutumia.
Sasa nini tumepewa ili ufike au urudi kwenye Taa yako ya fahamu, itabidi tuchukue mbinu hii ya Quraan ili tupate mafanikio ya kuitawala hii Akili badala ya Akili kututawala sisi, Napenda ufahamu ukitawaliwa na akili unakuwa mteja(addicted)na ukiitawala Akili unakua Mcha Mungu, hiyo ndio tafauti yake.Ndio maana tunajikuta huyu mteja wa mazungumzo, yule mteja wa wanawake, huyu mteja wa mali, mwengine yeye hafurahi mpaka agombane, mwengine mteja wa kuumwa tu haipiti siku bila ya kujipa maradhi, wengine wao wagonjwa wa (facebook)hiyo ndio Akili ilivyo ikikosa Balance, wengine wanataka wale tu akiona chakula hajiwezi, kuna maradhi ya kusema uongo, balaa zimetushukia wanaadamu na hatujui tufanye nini.
Sasa namalizia kwa kutoa dawa ifanye dawa hii na maajabu yake yatakua kama alivosema Nabii Yussuf a.s.. Ufanye nini?.
kitu kimoja anza zoezi hili la kuitizama Nafsi yako kwa kila ufanyacho, tabia zetu wanaadamu tunatizama yanotokea nje ya Nafsi zetu, sasa fanya kinyume chake tazama yanotokea ndani ya nafsi yako, utaanza kuona miujiza kidogo kidogo inatokezea, ukikitizama chakula wakati unakula basi hutokula mpaka tumbo livimbe utafikia pahala nafsi itakwambia nishatosheka, ukiitizima akili yako utaona Traffic ya mambo yanavopita, wewe tizama usjiunge na Traffic, Mwanamke au Mwanamme anapita wewe itizame akili yako na (Action)zake, kidogo kidogo utaona uteja unaanza kupungua, ukimaliza kutizama kwa njia hiyo sasa ukikaa kitandani umefunga macho tizama takataka za chumbani, anza kusafisha mavumbi, kidogo kidogo utaona unaanza kupunguza mambo yaliyomo kwenye chumba chako cha mawazo, kumbuka mambo yote yameingia kwa njia ya kutizama, na tumia njia hiyo ya kutizama ili uyatoe yote yalojaa kwenye Nafsi yako, mpaka ndoto za kipumbavu zinatoweka, taratibu utaona mwanga wa Taa yako ya Fahamu unaanza kuchomoza, na siku ambayo Taa itamurika chumba kizima siku hiyo ndio siku ya Rehma, ambapo akili inakukabidhi utawala wako unakua wewe ndio Mfalme wa nafsi yako, utakua kama mfano wa Nabii Yusuf a.s Mwanamke anakuja unakimbilia mlangoni na kanzu yako inachanwa kwa nyuma. ukifikia daraja hiyo elewa na Mollah wako anakusamehe madhanbi yako na hapo unaanza kuufahamu Ulimwengu huu vyengine kabisa, Akili ikaapo pembeni kila kitu unakiona kwa kutumia Nuru yako ya Fahamu, kama ulivokua utotoni ulipokua unaanza kupata Fahamu, kila kitu Miujiza, iwashe tena Taa hiyo na yote yalopita yatakua (History).
Kumbuka kutizama, kwanini nikasema kutizama na sio kuona, kwa sababu kutizama uko mbali na kuona uko karibu, na ukiwa karibu lazima ujiunge, "Waswahili wanasema utamu wa ngoma kucheza ukizunguka raha zimezidi" kwa hiyo na wewe usicheze utakuja kuzunguka, na ukizunguka hutoki kwenye duara, itakua unakera unafanya unatubu, unafanya tena unatubu, haina faida yoyote unateseka mpaka unaondoka kwenye Ulimwengu huu, utakuja kufufuliwa uteswe tena, hakuna atopata tabu isipokua wewe, unapewa njia itumie ili upate faida ya kurehemewa na Mollah wako. Hicho chumba nilichokitaja ni hiyo (Mind) ambayo uloijenga ukawa unaingia na kutoka, siku (Mind) itakaposita utabakiwa na (Brain) na Taa yako, hapo tena utakua Muhsin, Mja Mwema, kumbuka Mambo mema yanayafuta mabaya na huko ndio kusamehewa.
Sasa nini ufanye Kiumbe wewe, Kumbuka Mwanaadamu una vitendea Kazi vitu viwili, Kimoja katika hivyo hakiguswi na chochote, hakuna jambo lolote linaloweza kufikia kitu hicho ambacho ndio hiyo Taa ya Fahamu(Pure Soul). Kama Mwanaadamu utakua unakitumia kifaa hiki au nikipe heshima kwa sababu ni kitu kitakatifu(Roho)kwa uerevu, basi daima utakua umo furahani, kwanini nikasema umo kwa sababu (Roho)(Nature)yake ni Furaha(Nisiseme hivi Mkasema kasema anaijua roho kitu hicho hakijulikani), lakini hasara yetu Wanaadamu Tunaishi au kutawaliwa na hicho chengine chenye kutupeleka kwenye kiza, kipi hicho?.
Akili(Hii ni sehemu ya Nafsi) ni nyenzo ambayo tunatakiwa kuitumia kwa uangalifu kwani ni (Very Powerful weapon)silaha kubwa sana, ukimilikiwa na Akili Binaadamu umekwisha, huna (Control) ya maisha yako kabisa.
Kwa sababu Akili inafanya kazi yake ya kukusanya, kupokea na kutupa kwenye hicho chumba, chumba hiki kiite (Memory or Subconscious)na kwa kuwa lolote lile lilopita kwenye taa yako ya Fahamu kumbuka liko humo chumbani umeliweka na wala halitoki, Sasa nini kinatokezea kuna baadhi ya nyakati Taa inawaka na kumurika yale mambo yaliyomo kwenye chumba iwe chuki, hasada, uzinifu, wizi, na ukimurika tu likija juu lazima ulitende kwa sababu hujalitupa ila umeliweka akiba, kwa hiyo tahadhari sana unapokwenda kwenye chumba chako, utakua unatenda mambo bila ya kukusudia, sasa kwa kuwa mambo yana kukera ndio unaamua kuzima Taa, na huku watu wanatumia ule msemo kajitoa fahamu.
Quraan imekuhurumia imesema unaleta nyudhuru yaani unazima Taa, ndio ikaendelea kukumbusha kuwa Mwanaadamu ni Mwenye kuiona Nafsi yake, ikimaanisha unao uwezo wa kuishinda Akili, tumepewa maarifa ya kukishinda kifaa hiki, kwanza kwa kujulishwa wewe na hicho kifaa ni tafauti, ndio maana ukaambiwa wewe unakiona kitu hicho, na una uwezo wa kukitumia usiache kikakutumia.
Sasa nini tumepewa ili ufike au urudi kwenye Taa yako ya fahamu, itabidi tuchukue mbinu hii ya Quraan ili tupate mafanikio ya kuitawala hii Akili badala ya Akili kututawala sisi, Napenda ufahamu ukitawaliwa na akili unakuwa mteja(addicted)na ukiitawala Akili unakua Mcha Mungu, hiyo ndio tafauti yake.Ndio maana tunajikuta huyu mteja wa mazungumzo, yule mteja wa wanawake, huyu mteja wa mali, mwengine yeye hafurahi mpaka agombane, mwengine mteja wa kuumwa tu haipiti siku bila ya kujipa maradhi, wengine wao wagonjwa wa (facebook)hiyo ndio Akili ilivyo ikikosa Balance, wengine wanataka wale tu akiona chakula hajiwezi, kuna maradhi ya kusema uongo, balaa zimetushukia wanaadamu na hatujui tufanye nini.
Sasa namalizia kwa kutoa dawa ifanye dawa hii na maajabu yake yatakua kama alivosema Nabii Yussuf a.s.. Ufanye nini?.
kitu kimoja anza zoezi hili la kuitizama Nafsi yako kwa kila ufanyacho, tabia zetu wanaadamu tunatizama yanotokea nje ya Nafsi zetu, sasa fanya kinyume chake tazama yanotokea ndani ya nafsi yako, utaanza kuona miujiza kidogo kidogo inatokezea, ukikitizama chakula wakati unakula basi hutokula mpaka tumbo livimbe utafikia pahala nafsi itakwambia nishatosheka, ukiitizima akili yako utaona Traffic ya mambo yanavopita, wewe tizama usjiunge na Traffic, Mwanamke au Mwanamme anapita wewe itizame akili yako na (Action)zake, kidogo kidogo utaona uteja unaanza kupungua, ukimaliza kutizama kwa njia hiyo sasa ukikaa kitandani umefunga macho tizama takataka za chumbani, anza kusafisha mavumbi, kidogo kidogo utaona unaanza kupunguza mambo yaliyomo kwenye chumba chako cha mawazo, kumbuka mambo yote yameingia kwa njia ya kutizama, na tumia njia hiyo ya kutizama ili uyatoe yote yalojaa kwenye Nafsi yako, mpaka ndoto za kipumbavu zinatoweka, taratibu utaona mwanga wa Taa yako ya Fahamu unaanza kuchomoza, na siku ambayo Taa itamurika chumba kizima siku hiyo ndio siku ya Rehma, ambapo akili inakukabidhi utawala wako unakua wewe ndio Mfalme wa nafsi yako, utakua kama mfano wa Nabii Yusuf a.s Mwanamke anakuja unakimbilia mlangoni na kanzu yako inachanwa kwa nyuma. ukifikia daraja hiyo elewa na Mollah wako anakusamehe madhanbi yako na hapo unaanza kuufahamu Ulimwengu huu vyengine kabisa, Akili ikaapo pembeni kila kitu unakiona kwa kutumia Nuru yako ya Fahamu, kama ulivokua utotoni ulipokua unaanza kupata Fahamu, kila kitu Miujiza, iwashe tena Taa hiyo na yote yalopita yatakua (History).
Kumbuka kutizama, kwanini nikasema kutizama na sio kuona, kwa sababu kutizama uko mbali na kuona uko karibu, na ukiwa karibu lazima ujiunge, "Waswahili wanasema utamu wa ngoma kucheza ukizunguka raha zimezidi" kwa hiyo na wewe usicheze utakuja kuzunguka, na ukizunguka hutoki kwenye duara, itakua unakera unafanya unatubu, unafanya tena unatubu, haina faida yoyote unateseka mpaka unaondoka kwenye Ulimwengu huu, utakuja kufufuliwa uteswe tena, hakuna atopata tabu isipokua wewe, unapewa njia itumie ili upate faida ya kurehemewa na Mollah wako. Hicho chumba nilichokitaja ni hiyo (Mind) ambayo uloijenga ukawa unaingia na kutoka, siku (Mind) itakaposita utabakiwa na (Brain) na Taa yako, hapo tena utakua Muhsin, Mja Mwema, kumbuka Mambo mema yanayafuta mabaya na huko ndio kusamehewa.
Subscribe to:
Posts (Atom)