Sunday, January 15, 2017

SAFARI YA MAISHA PART 2

Asalaam Aleiykum

Naam tunaendelea na darsa hii ya Safari ya maisha  kusudio langu likiwa kukufahamisha wewe nani, Na hapa Ulimwenguni unafanya nini?. Soma kwa utulivu pengine utapata kujijua wewe nani na hapa ulimwenguni unafanya nini. Na ukijijua sasa hivi wakati huu unaoishi basi ni furaha kubwa ilioje, usisubiri mpaka siku ya kufa kwako ndio ukashituka kumbe huyu ndio mimi, kumbe mimi ndio nilokua naidhulumu nafsi kwa kuiamrisha itende dhanmbi, mimi ndio nilokua nashirikiana na Ibilis kufanya visa hivi vyote kwenye (Kitabu)hiki.
Aya ya mwanzo imeanza kwa kutushangaza, zama na mimi kwenye aya hizo ili uibuke na lulu, Soma Quraan kwa njia ya Kiroho upate ufunuo wake. imeanza vipi?, Imeanza na hofu (What is fear)Katika darsa hii ntakustaajabisha sana ili upate kunielewa, Nini hofu? hofu ni kitu chenye kujulikana, kitu usochikujua huna hofu nacho, wacha tulete (Mfano)Moto ukikuunguza au umemuona mtu anaungua, hapo inakua hofu imeshakuingia, unajiuliza itakuaje nikichomwa mimi, nikitiwa motoni nitakua hali gani?, Na (Mfano) Mwengine wakutokua na hofu utaona kwa mtoto mdogo, utaona hata ukimpa moto anaushika bila ya kuogopa, ukimuunguza analia na kwa mara ya pili hachezi tena karibu ya huo moto.
Ndio maana utaona hata wale wenye kutafuta watu wa kujiua kwa mabomu wanawatafuta vijana kwa sababu hawana woga. Hata jeshi linafanya ajira kwa vijana kwa sababu hiyo hiyo. Wewe Mwenyewe binafsi zamani ulikua ukikoga baharini unakwenda maji ya mbali zinapopita Meli, Leo ushazeeka maji ya kisigino unaanza kukohoa, Nini kimetokezea?.
Hofu kubwa mja inayokuvaa si nyengine ila ni hofu ya kufa, ile taarifa uliyonayo kwamba sasa ushazaliwa basi na kufa ni lazima, Na kila miaka ikizidi na huku hesabu zako zinaongezeka na hofu nayo inazidi, kila mtu au ana hofu lakini tumekua mabingwa wa kuficha hofu zetu. Unaishi katika Ulimwengu huu lazima upite katika misukosuko ya hiyo mitihani, Na ndani ya misukosuko hiyo unapewa hii (Awareness)ya jambo hilo la Umauti, tenda utendavyo elewa kuna siku utarudi ulikotokea, kutokana na ubishi na ukaidi wako ndipo na wewe hukubali unaanza kutafuta dawa  zikukinge na maradhi, lakini hiyo ni mbinu zako za kukikwepa kifo, unafanya maarifa na kupigana vita eti usife, Jitizame wewe ukifanyiwa uchunguzi hospitali unakuwaje wakati wa kusubiri majibu yako.
Kama unataka faida ya kukufanya uupate Uislam wa kweli, upate Ku(surrender)basi mtizame mnyama asiyekua na habari ya Umauti, akiumwa hata na (cancer)hashughuliki, akiumwa chochote yeye kamuachia yule aliyemuumba afanye matarajio yake, ama amponeshe au arejee Nyumbani, Na kutokana na Rehma za Mollah wake kinapona kinyama hicho bila ya dawa yoyote ya kumdhuru Afya yake, sisi wanaadamu tunapita katika maisha haya tunawakabidhi wenzetu wenye kufanya majaribio ya madawa na kutupa tutumie, huku wanatwambia zina (side affect)unapewa dawa na hofu juu yake, hizo ndio harakati za safari hii ya maisha.
Sasa nini kinachokufanya uwe na hofu, kama nilivosema mwanzo ile desturi tulo nayo ya kujuwa (knowing) jee na Mauti tunayajua?, inawezekana kuwa jawabu ndio tunayajua, na inawezekana kuwa sio, mie nakita ushahidi wangu kwenye neno la mwanzo ndio tunayajua, kwa sababu mwanzo tumepita kwenye hali hiyo ya Umauti, sasa kwanini hofu imetushika kwa sababu Roho ni yenye kujua ilipotoka na wapi itarejea, Sasa kwanini tunasahau kule (original)tulipotokea, sababu kubwa ni mazingira yetu ya safari hii ya maisha yanatufanya tushughulike na mambo ya nje kupita kiasi, (Mfano)Macho yanaona Nje, Mdomo unaonja vya nje, Masikio yanasikiliza Nje,Pua inanusa vya Nje, Mikono imeshughulika na kazi za nje, miguu nayo ni yenye kutembea nje, Akili inawaza mambo yalopita na kupanga yajayao, hakuna hata kimoja chenye kushughulika na mambo ya ndani, (Wizara hii imewachwa bila ya muangalizi)Na ndio wizara muhimu sana, mambo ya ndani ya kiharibika (Automatic) na nje kunaharibika.
Sasa ili ukumbushwe kama kuna mambo ya ndani, ujue kuwa yupo mwenye kuongoza hivyo vyote vyenye kushughulika na nje, Ndio Bwana Mtume s.a.w akaamrisha waislam wende kudhuru "Makaburi, Wahudhurie shughuli za maziko wasikose, na huo ni muongozo wenye hekima kubwa kutoka kwa Mtume s.a.w..  Najua siku hizi kumezuka watu wanakukatazeni msende kudhuru makaburi, na nyie bila ya kuuliza sababu mnakubali, lakini bora walivosema msende, haijambo kuna kitu kimebakia, nacho huo wasia wa Bwana Mtume s.a.w wa kuhudhuria, wangekwambieni msihudhurie ingekua balaa, wangeondosha kitu adhimu kwenye dini hii, kwanini nikasema hivyo, (Kumbuka tuko kwenye safari ya maisha ni wajibu kuchambua mambo yanohusu),Kwa sababu kwenda na kuhudhuria ni vitu viwili tafauti, Najua utashangaa lakini wacha nikufafanulie. Unaweza kwenda lakini usihudhurie, na unaweza kuhudhuria lakini usende, Inakujia habari kama hii unatakiwa uitie Akilini ili upate kurekebisha (safari yako ya maisha).
Vipi inakua hali hiyo? Utaona Watu wanakwenda Mazikoni pengine na wewe umo, Kwa ile hofu ya Umauti walonayo wanaanza kuchat kwenye simu, au mazungumzo ya kipuuzi, au ndio wanakwenda kukutana na watu ambao hawajaonana siku nyingi. Lakini yule alohudhuria pale makaburini anakua hataki kuchat, wala mazungumzo wala kukutana na mtu ila chenye kumshughulisha pale kuona vipi umauti unavokua, vipi analitizama dongo linavorejea kwenye dongo lenzie chini ya Ardhi, au anaweza kupata fahamu ya vipi alivyoumbwa kwa udongo na sasa anarejeshwa kuwa udongo, Mtu huyu ikiwa bahati yake kahudhuria kikweli anaweza kwenda (Beyond death)au akazingatia kuwa karibu zamu yake itafika na aanze kuifanya mizigo yake iwe mepesi.Anaweza Mtu huyo kuhudhuria mazikoni akiwa Moga na hofu imemjaa, na kurejea akiwa shujaa hana hofu tena kakutana na Umauti yungali akiwa hai.
Endelea part 3

No comments:

Post a Comment