Wednesday, February 1, 2017

KIFO CHA MAPENZI PART 1

Asalaam Aleiykum

Wanauliza wenye kuuliza nini siri ya Ndoa yenye kudumu muda mrefu?. tupe habari hizi ili nasi tufanikiwe, Waulizaji wa swali hili wanaonesha ushupavu mkubwa wa kuuliza, si wengi wenye ushujaa huu wa kuweza kuuliza swali kama hili, kwenye chumba cha Mtihani kila mtu anakaa kimya, na hivi ndivo lilivo kwa watu wengi wenye matatizo ya ndoa.
Leo mmenitoa kwenye (Darsa zangu)Menileta kwenye uwanja wa mapambano ili nipate kuchangia habari hii ya (Kifo cha Mapenzi)kwenye ndoa zetu, ndani ya majumba yetu, ukiulizwa swali una njia mbili za kujibu, moja ya kukinga ujinga wako unafanya unajua, na njia ya pili kutoka kwenye werevu wako ulojaa hisia za hekima zisokua na hatia. Isikilize habari hii iwe na faida na wewe ili upate muongozo fulani wa kukaribisha furaha kwenye maisha yako.
Jawabu:
Nini Kinatokea chenye kwenda kinyume na aya iliyomo katika sura ya (Al-Rum 21)?
"وَمِنۡ ءَايَـٰتِهِۦۤ أَنۡ خَلَقَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٲجً۬ا لِّتَسۡكُنُوٓاْ إِلَيۡهَا وَجَعَلَ بَيۡنَڪُم مَّوَدَّةً۬ وَرَحۡمَةً‌ۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَـٰتٍ۬ لِّقَوۡمٍ۬ يَتَفَكَّرُونَ "
Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsi yenu ili mpate utulivu kwao, Naye Amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Bila shaka katika haya zimo ishara kwa wenye kujua(Wenye kufahamu).
Umezitizama wewe Alama? Umeshakaa ukajiuliza vipi umekutana na huyo uliyenaye hivi sasa?, na kwanini ikawa huyo?, nani alokukutanisha.?"Na kwa Alama zake amekuumbieni wake zenu" Mbona wewe umeacha wote umekwenda kumuoa huyo ulonae? ushawahi kujiuliza swali hilo, umejiuliza mbona tabia zimelingana?, mbona tumezoeana?, kwanini tunaishi pamoja?, imekuaje tumepata Watoto hawa?, kuna Hikma gani kwa Mollah wetu kutufanya sisi kuwa(Family)?.
Umepata kukaa kujiuliza maswali hayo, au unakwenda huku umefunga macho, basi kama umeyafunga nakuomba ufungue, kwani juu yako kuna siri kubwa ya wewe kupewa baraka hizo za kuishi na mwenzio(au kukutanishwa na huyo ulo naye mkeo), huyo Mwenzio umepangiwa wewe na yule ambaye humuoni wala humsikii, na katika Ishara zake "Amekuumbieni wake zenu" katika jinsi zenu, basi Picha hujui kutizama, basi huoni mkeo kuna mambo kafanana na wewe, basi hata ishara huzioni?."Utulivu"ulokua nao umepotelea wapi"?,mbona hutulii (What Happen).
Kumbuka nikizungumza Jaala nazungumza kitu chenye kuja na kuondoka, kama ilivyo huruma ni mfano huo huo, Mlipoambiwa Mmejaaliwa mapenzi na huruma baina yenu hiyo ni zawadi jee mliipokea zawadi hii au hamjui kama mmeletewa, basi nakwambieni zawadi hiyo ipo kinachotakiwa ni kurekebisha fahamu zenu ili na nyinyi muingie katika kundi la watu wenye kujua akama walivotajwa mwisho wa hiyo aya. Mapenzi yapo kwenye Ulimwengu huu kama yalivo Maua.
Sasa swali la kujiuliza mbona hatuyaoni mapenzi, mbona hatuoneani huruma, mbona tunatesana, Naam sababu kubwa Meshughulika kuyatafuta Nje, Mmekazana lazima muyaone yanavoteremka kutoka Mbinguni na hilo ndio tatizo kubwa la wana ndoa wa siku hizi.
Nini Ndoa?, Kwa Tafsiri ya haraka Ndoa ni Ndoana, Kama huijui ndoana ni kifaa cha Mvuvi ambacho anatia chakula kumvutia Samaki, yule samaki akiona hukifata na kukila chakula kile na hapo tena huwa kanasa, Hapo ndio inaitwa ndoana,  na humfanya atakavyo huyo samaki. Sasa iwapo wewe itakua mume mvuvi itakua una anaanzisha matatizo kwenye ndoa yako.Na Samaki ukishampata huna shughuli tena, ukiwa na mawazo kama hayo ndugu yangu umo hasarani.
Vipi Matatizo yanaanza?, Matatizo yanakuja pale nyie nyote wawili kusahau kuwa mapenzi na huruma mnajaaliwa, Mnasahau jambo hilo na kusikiliza Familia inasemaje, Wakwanza kabisa kuyaua mapenzi ni hao Ndugu zako, unasikiliza watu wenyewe wana matatizo makubwa, nini wanafanya?, Wana Itikadi zao sijui zimetokea wapi, utaona anaambiwa sio kampende Mkeo au Mumeo ila anafundishwa, ukenda kumshika kichwa mkanyage mguu asije akakutawala, nuia awe chini yako, maskin sio kapendaneni ila kagombaneni, (Massage)waloipata maharusi hawa ni hiyo, kwa hiyo kila mmoja anakwenda kajiandaa kivita, wasia huo unakwenda(very deep). Tahadharini mafunzo hayo yanapelekea kuharibu maisha ya wanandoa hao.
Sasa kwa kuwa washapewa  mafunzo ya kupandiana vichwani, penzi halina nafasi tena ya kushuka kwenye moyo, linabakia akilini, kazi kutazamana, mara fikira hizi mara fikira zile, harusi mwezi wa kwanza mtu kashika kulinda simu,tayari ana hasira na wivu. Mbona imekua hivi, mbona tabia zake namna hii, mbona kanenepa, kwanini anakoroma, Baada ya hapo sasa kwa kuwa umetoa mahari linaingia lile kubwa la (possession)Utawala, unamfanya sasa ni mali yako, unahisi umemnunua huyo Mwanamke, kumbuka hiyo ni zawadi ulompa huyo Mwanamke hayo (Mahar).
Endelea part 2


KIFO CHA MAPENZI PART 2

Asalaam Aleiykum

Mwanamke ni Mwenye kuja katika maisha ya ndoa akiwa na moyo wenye kuamini, anajitolea maisha yake kuishi na wewe akiwa na yakini ndoto zake zote zitakua kweli, kwanini nikazitaja kuwa ndoto, kwa sababu kwenye ndoto ukiamka hamna chochote, majumba yote na magari, na maua yote unayaacha usingizini.
Sasa kwa kuonesha Shukrani zako kwa huyo Mwanamke ndio unaambiwa mpe zawadi ya kukubali kwake, Lakini wapi ukisha kukubaliwa mipango yako yote unafanya upate kumtawala huyo mwanamke(Umekua kama Mvuvi). Na Mwanamke akiona kuna vita vya kutawaliwa na yeye anajiunga, japokua anajiunga kwa ustadi mkubwa na wanaume wengi hawalijui hilo, Na yeye anataka atawale.
Ndio utaona hapo (Kifo cha mapenzi)kinatokezea, Nyumba hiyo utakuta yanabaki mazoea, Rohoni kila mmoja anasema tukiachana wazee watasemaje, Majirani watazua nini, kila kitu kinawahusu watu wa nje, (What about you)?. Utaona katika maisha hayo ya ndoa kila mmoja anaota kucha zake, Mume anaona kanunua kitu, anamgeuza Mkewe (as Thing)anasahau kabisa kama harusi ni muungano wa (Two Beings)Waja wawili waloamua kuishi pamoja, na katika maisha hayo hakuna mtawala, kwa sababu nafsi yoyote haichukui madhila ya kutawaliwa, kuna siku itatafuta uhuru wake.
Kwa hiyo Ndoa ikiwa ya hali hiyo ule Mlingoti wa Bendera ya mapenzi unageuka na kuelekea upande wa chuki.
Mwanamke daima anakuja kwenye ndoa akiwa na mbegu ya Mapenzi, anakuja hana chengine cha ku(Offer) ila ana moyo ulojaa (Trust)kwa Mumewe, atakuta hichi na kile, atafanyiwa hivi na vile, Ndio maana utaona maharusi wote wamo furahani, ni kazi ya Mume kulipalilia shamba hilo la mapenzi, ni kazi ya mume kulitilia maji na linapokuja kuchanua basi Maua yake ni mapenzi matupu.
Vipi utaanza kazi hiyo ya Mkulima, jambo la kwanza kabisa lazima Mkeo awe Rafiki yako, lakini wapi, angalia Tabia zako, Marafiki wa nje ndio wanakua washauri wako, wao ndio wanakua wanapewa safu ya mwanzo katika maisha yako. Kutokana na sababu hiyo ndio utamuona Mwanamme anapigana vita ya nje asionekane yeye (Mume Maridhia)anaogopa watu wasiseme mbona haji mpirani, mbona hatumuoni barazani, Marafiki na watu watasemaje, Na akirudi nyumbani anapigana vita vya ndani, mimi mumeo, ndio nishasema, ukitoka nje talaka yako,(Kifo cha Mapenzi)kinatokezea, hapo tena na yeye Mwanamke anatafuta mashoga vinaanza visa vya kusemana kwa marafiki na kwenye familia.
Tayari inakua mizizi ya fitna ishapandwa, baada ya kuota penzi linaota tunda la chuki, Mambo yanaanza kubadilika, hata kauli zinakua hichi changu, Na changu ni cha peke yangu, kwa kuwa (Nature)yako tayari ina mapenzi unaanza kupenda vyengine, Maskini na Mwanamke kwa kuwa yuko ndani anaanza kuteseka, anaanza kufanya kazi ya kuondosha mapenzi juu yako, mapenzi yanamtesa moyoni, hana uwezo, haviwezi vita vya Mwanamme, ndani mapenzi hakuna ila kuna jeraha.
Ndugu wanaingia kati, usidai talaka, stahamili, ishi kama maiti hamna neno sote tunaishi kama (Mazombie)ndani ya majumba, zitizame ndoa nyingi majumbani kwetu utaona wawili hao wanaishi kama (Maiti mbili zilokufa kifo cha mapenzi). Ndani ya Kaburi hilo hakuna masikilizano, hakuna mapenzi, na Rehma ishaondoka siku nyingi sana, Yamebaki mazoea, pengine mtu anaogopa asije akaumwa au kufa peke yake, umebaki wajibu ulotawaliwa na chuki na mashambulizi, masimango hayeshi, maneno ya ajabu yanatoka vinywani mwao(Matusi)ikifikia hali hiyo utamuona Mwanamme huyo anaenda kutafuta Mwanamke wa Nje(Kimada).
Na Mwanamke naye anageukia senema anaanza kwanza kumpenda Mwanamme wa senema(Govinder)mara (Sharukhan)hapo inakua hamkani si shuwari tena, Inapatika (Destruction of family life).
endelea part 3 

KIFO CHA MAPENZI PART 3

Asalaam Aleiykum

Kama pamezaliwa watoto hapo tena magonvi yanaanza kuwadhuru na watoto, mama anakuwa mgonjwa na baba pia wote wanaumwa, Wanaumwa maradhi ya mapenzi, na ukiumwa maradhi haya unakuwa huna furaha, na ubaya wake unakuwa hujijui, kwa sababu umekikataa kitu adhim kutoka kwa Mollah wako. Unawadhuru mpaka watoto wako katika maisha yao ya ujanani na uzeeni hawawezi tena na wao kupenda.
sasa yote haya yanatokea wapi?. Sana kwa Wanaume na tatizo kubwa ni woga, itakuwaje watu wakisikia mimi (Mume Maridhia). hapa itabidi nikupeni hadith moja ya Mfalme wa India aliyekua Shujaa, (Very Powerful) siku moja"alibishana na mkewe pale alipomwambia Wanaume wote (Ni Maridhia), Mfalme huyo akiitwa Akbar, hakukubali maneno ya Mkewe akaamua kufanya uchunguzi akamwita mmoja katika washauri wake wakubwa aitwaye abiral, ""Akamwambia jana usiku mimi na mke wangu tulikua tunabishana akanambia wanaume wote ni maridhia"Abiral akamwambia kwanini usimpige kibao, Mfalme Akbar akajibu Mke wangu nampenda itakua ugonvi namie nitakua sina raha, akauliza Akbar kwani wewe Abiral vipi sio Maridhia, Abiral akasema msema ukweli mpenzi wa Mwenye enzi Mungu, hata mimi nyumbani ni Maridhia, basi Mfalme Akbar akamwambia hebu nenda ukafanye uchunguzi katika Mji huu tujue kama yupo mume ambaye sie Maridhia, chukua zawadi ya Farasi wawili ukimkuta mume asiyekua Maridhia basi mzawadie farasi, Akatoka Abiral na Farasi wawili mweusi na mweupe na kupita nchi nzima, kila anomkabili anamwambia hata mie Maridhia, akiwa katika hali ya kuchoka na kukata tamaa akamkuta kipande cha baba wa miraba sita, ananyanyua gari la farasi kwa mkono mmoja, kumbuka siku hizo farasi ndio kama ndege siku hizi, akamfata akamuuliza hebu nambie hivyo wewe una mke, akasema ninaye, mkeo ana kauli yoyote juu yako, akimaanisha kuwa wewe ni Maridhia, akasema wee unanitania, nani atonifanyia upuuzi huo mie, pembeni kuna mwanamke mfupi ikisha mwembamba anapika anasikiliza yale mazungumzo, basi Abiral akamwambia yule mtu kweli wewe umeshinda, sio Maridhia, sasa kuna zawadi Farasi hawa wawili mweusi na mweupe chagua unamtaka yupi?. Kabla ya kuchagua yule Mwanamke akaruka pembeni chagua Mweupe ukichagua mweusi utanitambua""Abiral akamwambia basi hakuna zawadi na wala hakuna Mwanamme asiyekua Maridhia.
Kwa hiyo usione haya kuwa Maridhia, ni kawaida sisi sote Maridhia, ndani ya Maridhia ndiko linapokaa Paenzi. Vipi utalifufua penzi lako lilokufa.(Fanya First aid)unaweza kuliwahi, penzi kama usiku na mchana, linaingia na kutoka, na huruma hivyo hivyo, unachotakiwa tafuta mbolea lima tena(practice love)halafu (True Love)inafatia yenyewe.
Anza kupanga mambo yenu pamoja, anza kumfanya mkeo au mumeo Rafiki, kumbuka mpaka mekutanishwa kwenye Ulimwengu huu basi Mollah wako kakukutanisha na (Your other Half)sasa umekamilika, Anzeni kupanga mambo yenu kwa pamoja, ombaneni msamaha, mpigie simu au mfate kazini akikuuliza umekuja kufanya nini mwambie nimekuja kusema(I love you)hakuna makosa yoyote kufanya hivyo, muachie kibarua kwenye mto kuwa unampenda, acha kwenda nje ili utumie wakati na mkeo, Fanyeni wakati wenu mahsusi wa maongezi bila ya simu au nyimbo, saidianeni kazi za nyumbani, mwanamme usikhisi vibaya kukosha vyombo(Mbona hotel unakosha), nendeni matembezi ya pamoja, pangeni wiki hii zamu yako kunikanda, hapana aibu, peaneni zawadi, kuwa mwepesi mtu akitamka kitu wewe uwe wa mwanzo kumfanyia, nendeni kwa wazee au ndugu wa pande zote mbili kwa pamoja, safirini pamoja, usione haya kununua maua, unajua kwanini maua, kwa sababu Mollah wetu katupa zawadi katika Ulimwengu huu wa maua, litizame ua linavokuja, nani alolipamba, nani alolitia harufu na rangi zake, ukimpelekea mtu zawadi unamwambia, huko yalokotokea maua haya na penzi langu pia limetokea huko nakupa(something of beyond)Ngoja nikukumbushe wapi yalipotokea Maua.
(Al-Aaraf 19)وَيَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ فَكُلَا مِنۡ حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَـٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ .
Ewe Adam Kaa peponi pamoja na mkeo, na kuleni mnapopenda, lakini msiukaribie mti huu msije kuwa miongoni mwa waliodhulumu(Nafsi zao).
Huko ndiko yalipotokea maua, japokua tumefukuzwa huko lakini tumepewa nafasi ya kustarehe hapa Ulimwenguni kama ilivotajwa katika aya ya (24)kwenye sura hiyo hiyo.
Kwa hiyo huna haja ya kudhulumu nafsi yako na yamwenzako, jifanyie (Garden)yako hujakatazwa, Umeambiwa kuleni, pikeni vyakula vizuri, tokeni kama mna uwezo mkale nje, hamna uwezo furahia chakula kilopikwa na mkeo, mpaka utahisi unakula mkono wake kwa utamu, kwani chakula ni (Part of your body), Kumbuka (Body)nafasi yake (Sex) lakini Mapenzi sehemu yake ni kwenye Roho, na chochote chenye kugusa Roho ni (Bliss),basi ghafla utafunikwa na kitu kitokeacho Mbinguni, ghafla utakua umegubikwa na mapenzi, ghafla kuna kitu kitakaa moyoni, ghafla machozi yatakudondoka na ukilijua penzi basi utakua unajua na siri ya maua na harufu inapotokea, utajua nini kitu kiitwacho(Bliss)(Then)yakiondoka huruma inabaki, huruma ikiondoka mapenzi yanarejea, viwili hivyo vinapshana kama usiku na mchana, na hapo utakua na uwezo kuwapenda wanao, kupenda wazee wako, kupenda viumbe vyengine, utaanza kuupenda Ulimwengu na hatimaye kumpenda Mollah wako kwa Baraka alizokupa, utapata fahamu kuwa ipo (Power behind you)ambayo inakumiminia Mapenzi hayo, na wewe huna la kufanya ila Kusema Alhamdulillah. hiyo ndio Afya, hiyo ndio furaha, na huo ndio Uhai, kinyume cha hayo weye ushakufa ungali hai.