Asalaam aleiykum
Moja kwa moja naanza na maswali yenu mengi kuhusu mimi kama mnavo niuliza jee wewe Mganga?.
Jawabu ndio Mimi mganga tena mkubwa ila tatizo langu sitibu mtu, najiganga mwenyewe, na watu wachache wale ninao waona kweli wanahitaji utibabu, tena nafanya bure kwa kuwa mie nimejua bure, lakini ukija na shida zako za mahitaji mimi ni ghali sana sio kunilipa tu bali hata kunipata nikakufanyia huo uganga.
Sasa tuingie kwenye darsa yetu ya baraka za uganga.
Kwanza kabisa kabla ya kukoga kwenye bahari hii ya Uganga nataka nikufahamishe ili upate kujua kuwa Mganga mkubwa wa nafsi na Roho yako ni Mwenyewe aliyoiumba Rabbil-Allahu(Mwenye enzi Mungu). Ukiweza kuwasiliana naye utakua huna haja ya Waganga wadogo wadogo wa Kidunia.
Sasa Mtu wa mwanzo kutujulisha siri hii ya Mganga Mkubwa ni Rafiki wa Mwenye enzi Mungu Nabii Ibrahim a.s aliposema kwenye Quraan sura ya Shuaraa aya ya 80 "وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ "
"Na ninapoumwa Yeye ndiye anayeniponesha".
mmetaka tuzungumze mambo ya Uganga Uganga sasa wacha tuweke wazi baadhi ya siri za Kiganga ambazo mlikua hamzijui, kwa hiyo kuanzia leo kumbuka ukenda Hospital au ukija kwangu sie sio tunayekuponesha, sisi sote tunataka Idhini ya Mganga Mkuu ambaye ni Mollah wetu.
Na lakushangaza zaidi ambalo watu wengi hawalifahamu au kujiuliza kwanini wakati mwingi inasisitizwa Mgonjwa lazima alale au anapewa dawa ya usingizi au anakua kalala?, hapo kuna siri kubwa inafaa uzamie ili kupata kuijua. Leo tumo ndani ya darsa ya uganga wacha tuendelee na mambo ya kiganga na hakuna Mganga aliyetuonesha fani ya utibabu wa hali ya juu kama Nabii Isa a.s (Jesus).(Quraan Al-Imran- 49)
وَرَسُولاً إِلَىٰ بَنِىٓ إِسۡرَٲٓءِيلَ أَنِّى قَدۡ جِئۡتُكُم بِـَٔايَةٍ۬ مِّن رَّبِّڪُمۡۖ أَنِّىٓ أَخۡلُقُ لَڪُم مِّنَ ٱلطِّينِ كَهَيۡـٴَـةِِ ٱلطَّيۡرِ فَأَنفُخُ فِيهِ فَيَكُونُ طَيۡرَۢا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُبۡرِئُ ٱلۡأَڪۡمَهَ وَٱلۡأَبۡرَصَ وَأُحۡىِ ٱلۡمَوۡتَىٰ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُنَبِّئُكُم بِمَا تَأۡكُلُونَ وَمَا تَدَّخِرُونَ فِى بُيُوتِڪُمۡۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَةً۬ لَّكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ
"Na (Atamfanya) Mtume kwa wana wa Israili(Na kuwaambia) Nimekujieni na hoja (Muujiza) kutoka kwa Mollah wenu, ya kwamba nakuumbieni katika udongo(Natengeneza mfano)kama sura ya ndege kisha nampuliza mara anakua ndege, kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu, Na ninawaponesha Vipofu na Wenye Mabalanga(Ukoma)Na Ninawafufua (baadhi ya )walokufa, kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu, Na Ntakwambieni mtakavyovila na mtakavyoweka akiba katika nyumba zenu, Bila shaka katika hayo imo hoja kwenu ikiwa nyinyi ni watu wa kuamini.
Naam Mambo makubwa usidhani huo ni uchawi, tungetaka mambo ya kichawi tungemtafuta nabii Musa a.s lakini tupo tunachambua mambo ya Kiganga na tuna hadithiwa habari hii na yule Mganga aloletwa na Mollah wetu ili kuja kutupa taarifa na maalumati hayo, basi kwa uchambuzi zaidi endelea part 2.
Friday, July 14, 2017
BARAKA ZA UGANGA PART 2
Asalaam Aleiykum
Nabii Isa a.s kaja na mambo manne(4) Jambo la kwanza(1) kumtengeneza ndege kwa udongo ikisha akampuliza ndege huyo akaruka, kumbuka huo si uchawi kama vile (Magician)wanavo kutolea njiwa kwenye kofia. Halafu jambo la pili(2)Anaponesha Vipofu na wenye Ukoma. Jambo la tatu (3) Akawafufua baadhi ya walokufa. Na hilo la Nne (4)Ntakwambieni mtakavyokula na mtakavyo weka Akiba.
Hapo kuna mambo yanafaa kuzingatiwa wakati ukiendelea na darsa hii, katika hayo mambo manne tumefanikiwa kuyapata mawili tu nayo ni namba (2) na Namba (4), Nitayataja haya mawili tukiwa tunaendelea na darsa hii. Napenda Uelewe Uganga umegawika mapande mawili yenye sehemu mbili, Kama alivotuonesha Nabii Isa a.s hapo juu kuwa Uganga una sehemu ya (Body)yaani(Physical) hii unatibu kwa kutumia dawa za kienyeji na za kisasa na Una sehemu ya Roho nayo ni hiyo (Spiritual) hiyo tiba yake ni ya maombi na mambo mengine ya (Mystical), Wenzetu wa (Western)wamefanya jitihada kwenye utafiti wa (Physical)mpaka wamefanikiwa kuponesha maradhi mengi yakiwemo hayo ya ukoma na mpaka sasa wanajitahidi katika fani ya macho ili kuponesha upofu.
Na upande wa pili wa (Eastern)hapo zamani walikua wako (advance)katika mambo ya utibabu wa Kiroho na Kimwili lakini yalotokezea katika (History)ndio yalofanya mpaka leo hatujaendelea katika fani zote mbili isipokua kwa watu wachache sana walo bahatika au kubarikiwa.
Sasa nini Uganga?.
Kwa Mfano wa kwanza Uganga ni Baraka (Blessing)za Mollah wako unazopewa kuwatibu viumbe wenzio kama alivopewa Nabii Isa a.s, lakini Nabii Isa yeye alikua Mtume, na Uganga ni kama wakala, Ima uwe wa kusomea au wa kushushiwa na Mollah wako. Wakala huyo au Mganga ukenda kwake na shida zako au dhiki yako, au Maradhi yanayokusumbua basi atafanya elimu aliyojaaliwa na wewe kupona au kufanikiwa, au dhiki kukuondoka kwa njia usizozijua.
vipi anafanya endelea part 3.
Nabii Isa a.s kaja na mambo manne(4) Jambo la kwanza(1) kumtengeneza ndege kwa udongo ikisha akampuliza ndege huyo akaruka, kumbuka huo si uchawi kama vile (Magician)wanavo kutolea njiwa kwenye kofia. Halafu jambo la pili(2)Anaponesha Vipofu na wenye Ukoma. Jambo la tatu (3) Akawafufua baadhi ya walokufa. Na hilo la Nne (4)Ntakwambieni mtakavyokula na mtakavyo weka Akiba.
Hapo kuna mambo yanafaa kuzingatiwa wakati ukiendelea na darsa hii, katika hayo mambo manne tumefanikiwa kuyapata mawili tu nayo ni namba (2) na Namba (4), Nitayataja haya mawili tukiwa tunaendelea na darsa hii. Napenda Uelewe Uganga umegawika mapande mawili yenye sehemu mbili, Kama alivotuonesha Nabii Isa a.s hapo juu kuwa Uganga una sehemu ya (Body)yaani(Physical) hii unatibu kwa kutumia dawa za kienyeji na za kisasa na Una sehemu ya Roho nayo ni hiyo (Spiritual) hiyo tiba yake ni ya maombi na mambo mengine ya (Mystical), Wenzetu wa (Western)wamefanya jitihada kwenye utafiti wa (Physical)mpaka wamefanikiwa kuponesha maradhi mengi yakiwemo hayo ya ukoma na mpaka sasa wanajitahidi katika fani ya macho ili kuponesha upofu.
Na upande wa pili wa (Eastern)hapo zamani walikua wako (advance)katika mambo ya utibabu wa Kiroho na Kimwili lakini yalotokezea katika (History)ndio yalofanya mpaka leo hatujaendelea katika fani zote mbili isipokua kwa watu wachache sana walo bahatika au kubarikiwa.
Sasa nini Uganga?.
Kwa Mfano wa kwanza Uganga ni Baraka (Blessing)za Mollah wako unazopewa kuwatibu viumbe wenzio kama alivopewa Nabii Isa a.s, lakini Nabii Isa yeye alikua Mtume, na Uganga ni kama wakala, Ima uwe wa kusomea au wa kushushiwa na Mollah wako. Wakala huyo au Mganga ukenda kwake na shida zako au dhiki yako, au Maradhi yanayokusumbua basi atafanya elimu aliyojaaliwa na wewe kupona au kufanikiwa, au dhiki kukuondoka kwa njia usizozijua.
vipi anafanya endelea part 3.
BARAKA ZA UGANGA PART 3
Asalaam Aleiykum
Kabla ya kumjua vipi anafanya kwanza lazima uzijue sifa zake za kuwa huyu kweli ni mganga. Ama wale wa kidunia wao wanaweka matangazo na vyeti vyao, na wapi wamesoma na wamesomea nini, sasa huyu wa mambo ya kiroho utamgundua vipi na yeye hana cheti.
Vipi utamjua kama yeye ni Wakala wa Mwenye enzi Mungu, anazo Baraka kutoka kwa Mollah wake?. Jambo la kwanza kukujulisha ni Ucha Mungu wake, jambo la pili si mwenye kutaka sifa, jambo la tatu hana tamaa, hachukui pesa abadan, hata ukimpa hiyo ni hiyari yako, ukimpa kingi ni mafanikio yako ya haraka, na ukimpa kidogo na wewe mahitajio yako yatapatikana kidogo kidogo, huyo ndio mganga wa aina ya kwanza huyu yeye akinyanyua mikono dua yake hairudi, huyo ndio alopewa Baraka zitokazo kwa Mollah wake.
Ama Mganga wa aina ya pili ni yule mwenye kuijua au ku (Penetrate Third Eye) Nini kitakujulisha hiyo (Third Eye) hiyo ni (Sipiritual Eye) iliyopo Baina ya Macho yako mawili kati kati ya kipaji cha uso wako, kama uko Tanzania watizame Wagogo wanapo chanja, wao wanachanja hawajui maana yake wanasema inatibu maradhi, lakini kwa kujua zaidi watizame Mabaniani pale wanapotia alama zao kwenye paji la uso, hapo ndani yake ndio kuna hiyo (Third eye).
Hiyo (Third eye) ni jicho la Roho ambalo linakufanya uone mambo yalofichika katika Ulimwengu huu, lakini huwezi kuona hayo mambo mpaka ufunguliwe hilo jicho na Mtu anaefahamu elimu hizo, au lifunguke kwa Baraka za Mollah wako. Nini kinatokea Jicho likifunguka?, kwanza napenda uelewe vishindo vyake vikubwa, unaweza kudhani unapata wazimu, au kichwa kinangoka, au mfano kama vile unatumbukia kwenye shimo lisilokuwa na mwisho. Likifunguka jicho hilo unaona mambo ya ajabu, huoni tena kwa kawaida, miti unaona vyengine, kila kitu hutokiona kama mwanzo unavo viona, hapo tena kwa uwezo wa kuona mambo utaweza kuwa mtabiri, mtu akija na maradhi yake unaona kama (X-ray). Ndio maana ukenda kwa watu wengine wanakwambia wewe una jinsi kadhaa wa kadhaa, jua huyo anaona mambo (Live).
Hapo ndio unapata hiyo (Power) ya Uganga, unapata nguvu za kufanya mambo, unaweza kutumia kwa njia ya kheri ama ya shari, shauri linakua lako mwenyewe, unapata kuzijua dawa za ajabu, na unaweza kufanya mambo ya ajabu, ukazuia meli isiondoke, ukaharibu gari isiendeshwe,unaweza kudhuru watu, unaweza kuona viumbe vya ajabu ambavyo watu wengine hawavioni, unaweza kubadilisha matukio kutokana na huu uwezo wa (Third eye).huyo ndio Mganga wa aina ya pili.,
Halafu kuna Waganga wa aina ya Tatu, ambao wao wana uganga wa uongo, uganga wa kubahatisha, uganga wa nujum, uganga wa uramali, uganga wa Ramli, uganga wa (Numerology),uganga wa kutizama na kuisoma mikono ya watu. Mambo yao yote ya kubahatisha bahatisha, wakichangaya na miti shamba wanakwambia wao waganga, lakini hawana lolote isipokua mambo ya Uongo. Kwa hiyo namalizia kwa kusisitiza wanoweza kukusaidieni ni huyo wa kwanza na wapili kwa njia za halali na wala hakuna tatizo lolote, na hizo ndio Baraka za uganga mnazo niuliza kutaka kuzijua.
Kabla ya kumjua vipi anafanya kwanza lazima uzijue sifa zake za kuwa huyu kweli ni mganga. Ama wale wa kidunia wao wanaweka matangazo na vyeti vyao, na wapi wamesoma na wamesomea nini, sasa huyu wa mambo ya kiroho utamgundua vipi na yeye hana cheti.
Vipi utamjua kama yeye ni Wakala wa Mwenye enzi Mungu, anazo Baraka kutoka kwa Mollah wake?. Jambo la kwanza kukujulisha ni Ucha Mungu wake, jambo la pili si mwenye kutaka sifa, jambo la tatu hana tamaa, hachukui pesa abadan, hata ukimpa hiyo ni hiyari yako, ukimpa kingi ni mafanikio yako ya haraka, na ukimpa kidogo na wewe mahitajio yako yatapatikana kidogo kidogo, huyo ndio mganga wa aina ya kwanza huyu yeye akinyanyua mikono dua yake hairudi, huyo ndio alopewa Baraka zitokazo kwa Mollah wake.
Ama Mganga wa aina ya pili ni yule mwenye kuijua au ku (Penetrate Third Eye) Nini kitakujulisha hiyo (Third Eye) hiyo ni (Sipiritual Eye) iliyopo Baina ya Macho yako mawili kati kati ya kipaji cha uso wako, kama uko Tanzania watizame Wagogo wanapo chanja, wao wanachanja hawajui maana yake wanasema inatibu maradhi, lakini kwa kujua zaidi watizame Mabaniani pale wanapotia alama zao kwenye paji la uso, hapo ndani yake ndio kuna hiyo (Third eye).
Hiyo (Third eye) ni jicho la Roho ambalo linakufanya uone mambo yalofichika katika Ulimwengu huu, lakini huwezi kuona hayo mambo mpaka ufunguliwe hilo jicho na Mtu anaefahamu elimu hizo, au lifunguke kwa Baraka za Mollah wako. Nini kinatokea Jicho likifunguka?, kwanza napenda uelewe vishindo vyake vikubwa, unaweza kudhani unapata wazimu, au kichwa kinangoka, au mfano kama vile unatumbukia kwenye shimo lisilokuwa na mwisho. Likifunguka jicho hilo unaona mambo ya ajabu, huoni tena kwa kawaida, miti unaona vyengine, kila kitu hutokiona kama mwanzo unavo viona, hapo tena kwa uwezo wa kuona mambo utaweza kuwa mtabiri, mtu akija na maradhi yake unaona kama (X-ray). Ndio maana ukenda kwa watu wengine wanakwambia wewe una jinsi kadhaa wa kadhaa, jua huyo anaona mambo (Live).
Hapo ndio unapata hiyo (Power) ya Uganga, unapata nguvu za kufanya mambo, unaweza kutumia kwa njia ya kheri ama ya shari, shauri linakua lako mwenyewe, unapata kuzijua dawa za ajabu, na unaweza kufanya mambo ya ajabu, ukazuia meli isiondoke, ukaharibu gari isiendeshwe,unaweza kudhuru watu, unaweza kuona viumbe vya ajabu ambavyo watu wengine hawavioni, unaweza kubadilisha matukio kutokana na huu uwezo wa (Third eye).huyo ndio Mganga wa aina ya pili.,
Halafu kuna Waganga wa aina ya Tatu, ambao wao wana uganga wa uongo, uganga wa kubahatisha, uganga wa nujum, uganga wa uramali, uganga wa Ramli, uganga wa (Numerology),uganga wa kutizama na kuisoma mikono ya watu. Mambo yao yote ya kubahatisha bahatisha, wakichangaya na miti shamba wanakwambia wao waganga, lakini hawana lolote isipokua mambo ya Uongo. Kwa hiyo namalizia kwa kusisitiza wanoweza kukusaidieni ni huyo wa kwanza na wapili kwa njia za halali na wala hakuna tatizo lolote, na hizo ndio Baraka za uganga mnazo niuliza kutaka kuzijua.
Subscribe to:
Posts (Atom)