Asalaam Aleiykum
Zimekujia taarifa kama hivi karibuni utanyanganywa zawadi yako ulopewa, Hakuna zawadi njema ulopewa kama hii ya Uhai, ila ina masharti kuwa ni lazima baada ya muda ichukuliwe, Na kabla ya kuchukuliwa zawadi hii unaletewa dalili ili upate kujiandaa kuishi bila ya zawadi hiyo.
Umeshawahi kukaa na kuzichunguza dalili hizo ili upate kujua nini cha kufanya. Basi ikiwa bado hujafanya, nakupa nafasi usafiri na mimi ili kuzishuhudia dalili hizo na kuweza kuzifanyia kazi kwa dhumuni la kupewa tena zawadi hiyo ya uhai kwa mara ya pili.
Uhai utakaopewa kwa mara ya pili una mambo mawili Ima Furaha na Raha isokatika, Au Shida na Tabu za milele za kuendelea. Bado unayo nafasi ya Kubadilika, kwanini nikasema kubadilika nisiseme kugeuka, kugeuka ndio kawaida yako kama kinyonga, Mfano na wewe Mwenyewe jitizame unavo geuka Ukiwa na Mkeo Umehamaki, mara akiingia Rafiki unacheka, Mara umekua Sheikh mara unaasi, Mara hichi haramu, mara kile halali, wakati wowote unageuka, lakini mfano mmoja tu wa kubadilika utakutosha nao ni Kama vile (Butterflies)anavobadilik kutoka kwenye (Caterpiller)na kuwa Kipepeo.
Dalili gani zitakufanya ugeuke kabla ya mwisho wa uhai wako?. Mwenye Enzi Mungu simwenye kumdhulumu Mja wake katoa nafasi mpaka dakika za karibu ya Mwisho nafasi hiyo ipo, Lakini kwa Mwenye kutaka kuitumia, ziko dalili hizi kwenye Quraan lakini kwa Mwenye kusoma kwa Njia ya (Fahamu) ikiwa umesoma (Siri ya Fahamu)utajua nimekusudia nini.
Kwenye Quraan yamesemwa maneno yaloficha Hekima ndani yake, wakati ule ulipokua kijana na jeuri zako, mbishi husikilizi mtu uliambiwa maneno haya yaliyomo kwenye sura ya Tariq aya ya (5-6-7)."فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَـٰنُ مِمَّ خُلِقَ"
"Hebu ajitizame mtu, ameumbwa kwa kitu gani" Binaadamu umeumbwa kwa mali ghafi ya maji ya uhai, maji haya ni (Very Powerful)ulipoambiwa yatizame ili ujue uwezo wa maji hayo ambayo ukiyatoa yanaweza kutengeneza kiumbe kama wewe.
"خُلِقَ مِن مَّآءٍ۬ دَافِقٍ۬ "
"Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa" Kutokana na Dalili hiyo kinochupa chochote kinatoka juu na kwenda kutua chini, na hiyo ndio (Sex)lau ungekua unaweza kuzuia yasichupe maji hayo basi Miujiza mikubwa ingetokea juu yako, ndio maana (Watawa na Makasisi wanajificha) ili kuzuia (Gravitation)hii isitokee, kwa sababu kama haitokei (Gravitation)lazima Sheria ya maumbile ya mrengo wa pili wa (Levitation)ichukue nafasi yake, na hapo ndio yanatokea hayo (Mabadiliko)Rehma, Miujiza ita utakavyo.
Lakini maji haya (Nature)yake lazima yachupe yakitokea.
"يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآٮِٕبِ"
"Yatokayo katikati ya mifupa ya mgongo na Kifua"
Wewe hujapata au hujui kuyasikiza inakuaje yakitokea huko hali yake au Raha zake zinakua vipi, kwa sababu ya kushughulika kwako na akili ziko kwengine unashituka sekunde za mwisho, maskini hasara yako, mpaka unaondoka kwenye Ulimwengu huu hujapata kujua inakuaje ladha ya maji haya yakianza kuondoka kifuani au mgongoni hali inakuaje.(Hapa siko kwenye darsa ya mambo hayo ila nagusia na kupita njia tu). Nafahamisha kuwa zipo raha zaidi ukiwa una weledi wa mambo.
Wacha kutoa macho endelea part 2.
Sunday, October 15, 2017
MWISHO WA UHAI PART 2
Asalaam Aleiykum
Siri ya hayo maji tuliyoitaja kwenye part 1 inatokezea hata wakati wa kulala au wa kufa kwako, nyakati nyengine lazima maji hayo yamiminike au yashuke ndio upate usingizi. Hiyo ni sehemu ya kwanza ya dalili za uhai ambazo zinakufanya huwezi kujizuia, maji lazima yatoke, fujo tupu mtaani watu wanachunga watoto wakiume na kike, ile isitokee fujo mitaani, mwanamke kafungiwa na wanaume wanaranda kama simba anatafuta swala, watu wanakwiba, wanadhulumu ,wanagombana yote sababu ya maji haya yanochupa kwa kasi.
Hiyo ni dalili ya kwanza ya Uhai, ikisha kuna dalili ya pili ya mwisho wa uhai. Soma taratibu kwa uangalifu mkubwa ili upate kufahamu kusudio ya darsa hii ili upate kubadilika, kumbuka sio kugeuka. Aya gani inayo tukumbusha Mwisho wa Uhai?
Sura ya Yaasin aya ya (68)
"وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَڪِّسۡهُ فِى ٱلۡخَلۡقِۖ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ"
"Na tunayempa Umri tunamrejesha nyuma katika umbo(Lake)(Anakuwa kama mtoto)basi jee, hawayatii Akilini(Mafunzo haya).
Hapo kuna siri nzito ya kujiandaa na mwisho wa Uhai, katika aya hiyo kumetajwa umbo na Akili, Umbo linaondoshewa nguvu lina rudi kama ulivokua mtoto, Baba akiweza kukupiga, ulipokua mkubwa una nyanyua vyuma huoni kaacha kukupiga, na sasa hivi wewe kizee, kijana wakati wowote anaweza kukunasa vibao, Umbo linarejeshwa kama mtoto, unaona mwenyewe magoti hayafanyi kazi uzuri, miguu huwezi kukimbia, moyo unakunyima pumzi, macho na masikio haviwezi kutenda kazi kama zamani, meno yashapungua, sasa ushaanza kukaa ndani kipindi kirefu, habari za kutamani zimeshatangulia na wakati, mambo huyawezi tena, sasa kama huzijui dalili hizi ndio unaanza kukimbilia madawa ya kila aina ujirejeshe ujanani, ndio mnaambiwa hamyatii Akilini?.Kuyatia Akilini maana yake rudi kwenye (Siri ya Fahamu).
Lakini ilipotajwa akili ni kwa Tafsiri yetu ya kiswahili, ama tafsiri ilo karibu zaidi ni ile ya kizungu inayosema (Sense), lakini Tafsiri ilotimia ni kurudi kwenye Fahamu. Vipi kurudi kwenye Fahamu ni wewe kujitenga na (Body)ukajua sasa mwili umekwisha kazi yake, na sasa nimepewa nafasi niangalie upande wa pili huu ulonileta hapa ulimwenguni,(Kumbuka wewe ni Body na spirit) Kumbuka uliletwa kipindi cha mwanzo ulikua mtoto na sasa hivi unarejeshwa kwenye udhaifu uleule wa mtoto lakini ukiwa na kitu adhimu kabisa cha kujijua kuwa ulipita katika njia tatu hizi, ile ya kwanza ulikua hujijui, ukapita ya ujanani ukawa na desturi ya kutokujali au kusahau kwa njia ya ulevi wa kila aina, mara (gossip)mpira,tv, mambo chungu nzima, na sasa umeingia kwenye uzee ukiwa na fahamu yako nzuri umeshapata kujiuliza jee maji haya sasa yanakwenda wapi?.
Endelea part 3
Siri ya hayo maji tuliyoitaja kwenye part 1 inatokezea hata wakati wa kulala au wa kufa kwako, nyakati nyengine lazima maji hayo yamiminike au yashuke ndio upate usingizi. Hiyo ni sehemu ya kwanza ya dalili za uhai ambazo zinakufanya huwezi kujizuia, maji lazima yatoke, fujo tupu mtaani watu wanachunga watoto wakiume na kike, ile isitokee fujo mitaani, mwanamke kafungiwa na wanaume wanaranda kama simba anatafuta swala, watu wanakwiba, wanadhulumu ,wanagombana yote sababu ya maji haya yanochupa kwa kasi.
Hiyo ni dalili ya kwanza ya Uhai, ikisha kuna dalili ya pili ya mwisho wa uhai. Soma taratibu kwa uangalifu mkubwa ili upate kufahamu kusudio ya darsa hii ili upate kubadilika, kumbuka sio kugeuka. Aya gani inayo tukumbusha Mwisho wa Uhai?
Sura ya Yaasin aya ya (68)
"وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَڪِّسۡهُ فِى ٱلۡخَلۡقِۖ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ"
"Na tunayempa Umri tunamrejesha nyuma katika umbo(Lake)(Anakuwa kama mtoto)basi jee, hawayatii Akilini(Mafunzo haya).
Hapo kuna siri nzito ya kujiandaa na mwisho wa Uhai, katika aya hiyo kumetajwa umbo na Akili, Umbo linaondoshewa nguvu lina rudi kama ulivokua mtoto, Baba akiweza kukupiga, ulipokua mkubwa una nyanyua vyuma huoni kaacha kukupiga, na sasa hivi wewe kizee, kijana wakati wowote anaweza kukunasa vibao, Umbo linarejeshwa kama mtoto, unaona mwenyewe magoti hayafanyi kazi uzuri, miguu huwezi kukimbia, moyo unakunyima pumzi, macho na masikio haviwezi kutenda kazi kama zamani, meno yashapungua, sasa ushaanza kukaa ndani kipindi kirefu, habari za kutamani zimeshatangulia na wakati, mambo huyawezi tena, sasa kama huzijui dalili hizi ndio unaanza kukimbilia madawa ya kila aina ujirejeshe ujanani, ndio mnaambiwa hamyatii Akilini?.Kuyatia Akilini maana yake rudi kwenye (Siri ya Fahamu).
Lakini ilipotajwa akili ni kwa Tafsiri yetu ya kiswahili, ama tafsiri ilo karibu zaidi ni ile ya kizungu inayosema (Sense), lakini Tafsiri ilotimia ni kurudi kwenye Fahamu. Vipi kurudi kwenye Fahamu ni wewe kujitenga na (Body)ukajua sasa mwili umekwisha kazi yake, na sasa nimepewa nafasi niangalie upande wa pili huu ulonileta hapa ulimwenguni,(Kumbuka wewe ni Body na spirit) Kumbuka uliletwa kipindi cha mwanzo ulikua mtoto na sasa hivi unarejeshwa kwenye udhaifu uleule wa mtoto lakini ukiwa na kitu adhimu kabisa cha kujijua kuwa ulipita katika njia tatu hizi, ile ya kwanza ulikua hujijui, ukapita ya ujanani ukawa na desturi ya kutokujali au kusahau kwa njia ya ulevi wa kila aina, mara (gossip)mpira,tv, mambo chungu nzima, na sasa umeingia kwenye uzee ukiwa na fahamu yako nzuri umeshapata kujiuliza jee maji haya sasa yanakwenda wapi?.
Endelea part 3
MWISHO WA UHAI PART 3
Asalaam aleiykum
Ukitaka kujua yanakwenda wapi itabidi ujitose kwenye sheria mbili za Ulimengu huu ya kwanza ile ya (Gravitation) na ya pili ile ya (Levitation),Mwanzo ilikua maji hayo yanashuka chini kwa kasi, na sasa yamesita lazima uchunguze nini kimetokea, jee yaweza kuwa ndio (Levitation) kupanda juu kumeanza kufanya kazi, na sio kila mtu anapata zawadi hiyo ya (Levitation)wengine maji yanabakia hapo hapo kiunoni kwenye chem chem mpaka yana haribika,lakini kama umeipata hiyo hali ya (Levitation) utaijua pale inapozaliwa hekima juu yako, ukagundua sasa matamanio yamekatika na mimi nimepewa nafasi ya kugeuka.
Itumie nafasi hii ya (Levitation)kwa kutafuta (Favour) kutoka kwa Mollah wako kuupata Ucha Mungu, utastarehe katika kipindi hichi kilichobaki cha Mwisho wa uhai wako, jikubalishe kuwa mtoto tena, ipate tena ile (Innocent) yako ya Utotoni, ukifanikiwa utaanza kusafisha dhanmbi zako, sio kwenda kwa waganga na (Doctor)Wamasai kutafuta nguvu, hayo yanakuharibu na kukupeleka kaburini kabla hujatumia nafasi ya mwisho wa uhai wako.
Kumbuka sasa hivi maji yametulia, inofanya zogo ni akili yako kwa ajili ya mambo ya zamani, ukiweza kuipuuza basi ile (System) ya pili ya (Levitation) inaanza kufanya kazi yake kama inavofanya (Brain)yako kwa kula 90% ya (Vitamin) kwenye chakula unacho kula.
Hapo ndio Maji hayo yanaanza kufata (System)mpya ya (Levitation)yanaanza kupanda juu, hayakai palepale na hapo ndio inaanza kuzaliwa au kufunguliwa hiyo (Hekima)kumbuka ulivokua mdogo miaka (14)ilifunguliwa na kwenda chini, Na hivi sasa imefungwa na ina kwenda Juu. Hapo tena Utulivu unarejea mwanzo ulikua ukitafuta mambo ya dunia, sasa unarejea kutafuta mambo ya Akhera, unaanza kupata khofu hii akhera ipo? nikenda itakuaje, Vipi ntakutana na aliyeniumba, hiyo ndio (Quest)ya Utu uzima, hapo tena unaanza kuhamia Msikitini, na ukilitizama hilo utaliona Wazee wamejaa misikitini na vijana wapo na dunia yao kwenye (Madisco).
Linatokea hilo kwa sisi Vizee kwa sababu tunajua (Mwisho wa Uhai)umekaribia, Ikifika hali kama hiyo sasa unatakiwa uwe na tahadhari kubwa, kwa sababu kuna jambo lengine jipya linakushughulisha ambalo linakujia wakati huu nalo ni la watoto na mali, Unaanza kuilinda mali ili isimalizike, na watoto wanaanza kukutesa huyu hivi yule vile, inapofika hali kama hii Mwenye Enzi Mungu anakukumbusha tena ili uwe makini kwa kukwambia maneno yaliyomo kwenye sura ya (Munafiqoon aya ya 9-11).
"يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُلۡهِكُمۡ أَمۡوَٲلُكُمۡ وَلَآ أَوۡلَـٰدُڪُمۡ عَن ذِڪۡرِ ٱللَّهِۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٲلِكَ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلۡخَـٰسِرُونَ"
"Enyi Mlioamini yasiku sahaulisheni mali yenu wala watoto wenu(Katika) kumkumbuka Mwenye enzi Mungu, Na wafanyao hayo, hao ndio wenye kuhasirika".
Onyo hili wanapewa wale wenye imani, Mwanzo ilikua starehe ya dunia na sasa imemalizika kuna chengine kinazuka ile Mali ulochuma na watoto wako ndio inakuja kukufisidi mwisho huu wa uhai, Unataka kulinda mali usifilisike, unaendelea kufunga mahesabu, unataka cheo chako kisiteremke, na kufanya hivyo kunakupelekea kumsahau Mollah wako kabisa, Na watoto wanakushughulisha kwa mahitaji yao na tabia zao inakua kwenye moyo wako wewe Mungu hakai kabisa, mambo ya Akhera huyataki kabisa na hiyo ndio hasara yenyewe.
"وَأَنفِقُواْ مِن مَّا رَزَقۡنَـٰكُم مِّن قَبۡلِ أَن يَأۡتِىَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوۡلَآ أَخَّرۡتَنِىٓ إِلَىٰٓ أَجَلٍ۬ قَرِيبٍ۬ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ "
"Na toeni katika yale tuliyokupeni kabla mmoja wenu hayajamfikia mauti, kisha akasema, Mollah wangu hunighairishii muda kidogo,(Ili)Nikatoa sadaka na nikawa miongoni mwa watendao mema".
Ama tendo la kutoa lina cheo kikubwa sana mbele ya Mwenye enzi Mungu, kwanini ikawa hivyo kwa sababu kutoa ni sifa ya Mwenye enzi Mungu, "Amekupa uhai, afya, mapenzi, Akili, Mali,watoto na mengi kadhalika unayoyajua na usiyoyajua"sasa katika mtihani wake alokupa mdogo tu, ni katika hiyo mali yako anakujaribu na kukutizama, kama unamuamini, Wewe Muislam wa kweli, Kipindi cha sala hakikupiti, unataka pepo yake, jee unaweza kutoa, ukiweza kufanya hilo basi pepo haina wasiwasi wako juu yako, lakini shuruti lake utoe uko hai una nguvu zako, sio uko kwenye kitanda unawaambia watoto watoe, Toa sasa hivi una nguvu zako, toa usijali wakakushughulisha watoto watarithi nini, hiyo sio tatizo lako, ila usiwaache wakapata shida, lakini kuwa mstari wa mbele katika kutoa.
Kwani usiwache tena ushakua mgonjwa taabani ndio una wasiwasi wa kufa ukaanza kujitia ucha Mungu unatarajia Mollah wako akupe muda ili upate kuwa katika waja wema.
"وَلَن يُؤَخِّرَ ٱللَّهُ نَفۡسًا إِذَا جَآءَ أَجَلُهَاۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ"
"Lakini Mwenye enzi Mungu Hatakhairisha nafsi yoyote inapokuja ajali yake, Na Mwenye enzi mungu anazo habari za Mnayoyatenda".
Usitake kudanganya unapigana kutokana na kuwa na khofu, hutaki kufa, sasa unataka na huko unakokwenda ukapate Raha, ndio moyoni unajisemesha nikhairishie kufa kwangu nikafanye mema, lakini inapofika mwisho wa uhai hakuna, msamaha kila mmoja wetu anakwenda, na Mwenye enzi mungu anajua yote mnayoyatenda. Kwa hiyo kabla Uhai haujamalizika zitoe mali zako, katake msamaha kwa makosa yako,zidisha kumkumbuka Mollah wako, tena mapenzi ya Mollah wako yatakushukia katika huu Mwisho wa uhai wako.
Ukitaka kujua yanakwenda wapi itabidi ujitose kwenye sheria mbili za Ulimengu huu ya kwanza ile ya (Gravitation) na ya pili ile ya (Levitation),Mwanzo ilikua maji hayo yanashuka chini kwa kasi, na sasa yamesita lazima uchunguze nini kimetokea, jee yaweza kuwa ndio (Levitation) kupanda juu kumeanza kufanya kazi, na sio kila mtu anapata zawadi hiyo ya (Levitation)wengine maji yanabakia hapo hapo kiunoni kwenye chem chem mpaka yana haribika,lakini kama umeipata hiyo hali ya (Levitation) utaijua pale inapozaliwa hekima juu yako, ukagundua sasa matamanio yamekatika na mimi nimepewa nafasi ya kugeuka.
Itumie nafasi hii ya (Levitation)kwa kutafuta (Favour) kutoka kwa Mollah wako kuupata Ucha Mungu, utastarehe katika kipindi hichi kilichobaki cha Mwisho wa uhai wako, jikubalishe kuwa mtoto tena, ipate tena ile (Innocent) yako ya Utotoni, ukifanikiwa utaanza kusafisha dhanmbi zako, sio kwenda kwa waganga na (Doctor)Wamasai kutafuta nguvu, hayo yanakuharibu na kukupeleka kaburini kabla hujatumia nafasi ya mwisho wa uhai wako.
Kumbuka sasa hivi maji yametulia, inofanya zogo ni akili yako kwa ajili ya mambo ya zamani, ukiweza kuipuuza basi ile (System) ya pili ya (Levitation) inaanza kufanya kazi yake kama inavofanya (Brain)yako kwa kula 90% ya (Vitamin) kwenye chakula unacho kula.
Hapo ndio Maji hayo yanaanza kufata (System)mpya ya (Levitation)yanaanza kupanda juu, hayakai palepale na hapo ndio inaanza kuzaliwa au kufunguliwa hiyo (Hekima)kumbuka ulivokua mdogo miaka (14)ilifunguliwa na kwenda chini, Na hivi sasa imefungwa na ina kwenda Juu. Hapo tena Utulivu unarejea mwanzo ulikua ukitafuta mambo ya dunia, sasa unarejea kutafuta mambo ya Akhera, unaanza kupata khofu hii akhera ipo? nikenda itakuaje, Vipi ntakutana na aliyeniumba, hiyo ndio (Quest)ya Utu uzima, hapo tena unaanza kuhamia Msikitini, na ukilitizama hilo utaliona Wazee wamejaa misikitini na vijana wapo na dunia yao kwenye (Madisco).
Linatokea hilo kwa sisi Vizee kwa sababu tunajua (Mwisho wa Uhai)umekaribia, Ikifika hali kama hiyo sasa unatakiwa uwe na tahadhari kubwa, kwa sababu kuna jambo lengine jipya linakushughulisha ambalo linakujia wakati huu nalo ni la watoto na mali, Unaanza kuilinda mali ili isimalizike, na watoto wanaanza kukutesa huyu hivi yule vile, inapofika hali kama hii Mwenye Enzi Mungu anakukumbusha tena ili uwe makini kwa kukwambia maneno yaliyomo kwenye sura ya (Munafiqoon aya ya 9-11).
"يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُلۡهِكُمۡ أَمۡوَٲلُكُمۡ وَلَآ أَوۡلَـٰدُڪُمۡ عَن ذِڪۡرِ ٱللَّهِۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٲلِكَ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلۡخَـٰسِرُونَ"
"Enyi Mlioamini yasiku sahaulisheni mali yenu wala watoto wenu(Katika) kumkumbuka Mwenye enzi Mungu, Na wafanyao hayo, hao ndio wenye kuhasirika".
Onyo hili wanapewa wale wenye imani, Mwanzo ilikua starehe ya dunia na sasa imemalizika kuna chengine kinazuka ile Mali ulochuma na watoto wako ndio inakuja kukufisidi mwisho huu wa uhai, Unataka kulinda mali usifilisike, unaendelea kufunga mahesabu, unataka cheo chako kisiteremke, na kufanya hivyo kunakupelekea kumsahau Mollah wako kabisa, Na watoto wanakushughulisha kwa mahitaji yao na tabia zao inakua kwenye moyo wako wewe Mungu hakai kabisa, mambo ya Akhera huyataki kabisa na hiyo ndio hasara yenyewe.
"وَأَنفِقُواْ مِن مَّا رَزَقۡنَـٰكُم مِّن قَبۡلِ أَن يَأۡتِىَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوۡلَآ أَخَّرۡتَنِىٓ إِلَىٰٓ أَجَلٍ۬ قَرِيبٍ۬ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ "
"Na toeni katika yale tuliyokupeni kabla mmoja wenu hayajamfikia mauti, kisha akasema, Mollah wangu hunighairishii muda kidogo,(Ili)Nikatoa sadaka na nikawa miongoni mwa watendao mema".
Ama tendo la kutoa lina cheo kikubwa sana mbele ya Mwenye enzi Mungu, kwanini ikawa hivyo kwa sababu kutoa ni sifa ya Mwenye enzi Mungu, "Amekupa uhai, afya, mapenzi, Akili, Mali,watoto na mengi kadhalika unayoyajua na usiyoyajua"sasa katika mtihani wake alokupa mdogo tu, ni katika hiyo mali yako anakujaribu na kukutizama, kama unamuamini, Wewe Muislam wa kweli, Kipindi cha sala hakikupiti, unataka pepo yake, jee unaweza kutoa, ukiweza kufanya hilo basi pepo haina wasiwasi wako juu yako, lakini shuruti lake utoe uko hai una nguvu zako, sio uko kwenye kitanda unawaambia watoto watoe, Toa sasa hivi una nguvu zako, toa usijali wakakushughulisha watoto watarithi nini, hiyo sio tatizo lako, ila usiwaache wakapata shida, lakini kuwa mstari wa mbele katika kutoa.
Kwani usiwache tena ushakua mgonjwa taabani ndio una wasiwasi wa kufa ukaanza kujitia ucha Mungu unatarajia Mollah wako akupe muda ili upate kuwa katika waja wema.
"وَلَن يُؤَخِّرَ ٱللَّهُ نَفۡسًا إِذَا جَآءَ أَجَلُهَاۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ"
"Lakini Mwenye enzi Mungu Hatakhairisha nafsi yoyote inapokuja ajali yake, Na Mwenye enzi mungu anazo habari za Mnayoyatenda".
Usitake kudanganya unapigana kutokana na kuwa na khofu, hutaki kufa, sasa unataka na huko unakokwenda ukapate Raha, ndio moyoni unajisemesha nikhairishie kufa kwangu nikafanye mema, lakini inapofika mwisho wa uhai hakuna, msamaha kila mmoja wetu anakwenda, na Mwenye enzi mungu anajua yote mnayoyatenda. Kwa hiyo kabla Uhai haujamalizika zitoe mali zako, katake msamaha kwa makosa yako,zidisha kumkumbuka Mollah wako, tena mapenzi ya Mollah wako yatakushukia katika huu Mwisho wa uhai wako.
Subscribe to:
Posts (Atom)