Thursday, February 1, 2018

MAISHA YA SHAHIDI PART 2

Asalaam Aleiykum

Utaona Mtu anasali miaka 40 hata siku moja hajapata (Something of beyond) Vipi wewe unakua Muumin halafu hupati ishara yoyote, umejiuliza kwanini husogei kwa Mollah wako ukaoneshwa japo taa, Kwani wewe siku zote si unalala Akhera ukiamka duniani?, Baadhi ya wakati huwauliza Masheikh wenu jee wewe kuna chochote kimetokezea kutoka kwa Mollah wako, una dalili yoyote katika maisha yako kwamba utakufa na kufufuliwa, jee umepata alama zozote za Imani yako, au zawadi kutoka mbinguni?, utawaona mashavu yanawacheza hawana la kujibu na hivi ndio sote tunavoishi, na (Quraan) ina tu (Challange) katika sura ya (Dhaariyat aya ya 21 na 22)

"وَفِىٓ أَنفُسِكُمۡ‌ۚ أَفَلَا تُبۡصِرُونَ"
"Na Katika Nafsi zenu(Pia zimo Alama)Je Hamuoni"(21)
Alama ziko nyingi mie leo ntazungumza chache ya Alama hizo ambayo imetajwa katika aya hiyo, nini kimetajwa "Jee kwenye Nafsi zenu hamuoni" Hamuangalii, Jiulize nani huyu anayeambiwa ajiangalie, katika kujiangalia lazima viwepo vitu vitatu, ntavitaja ya Mwanzo hiyo nafsi, Yapili hiyo inayoangalia na ya Tatu ni hiyo inayoona viwili hivyo, Na huyo ndio Shahidi au kwa jina lengine hiyo Roho Yako, au kwa njia nyengine "weka Kioo, halafu kutakua na Kioo, ikisha kuna wewe unayejiona kwenye kioo, lakini kuna watatu hapo huyo Shahidi kajificha anatizama kioo na nafsi, ndio maana utaona kwenye kioo umeona nafsi ama (Body)lakini hujamuona Shahidi.
Ulipoambiwa kurejea uwe Shahidi utizame nafsi yako, kusudio lake uwe Shahidi (Complete)Kwani ukiwa Shahidi ndio unasita kutenda dhanmbi kabisa, Shahidi hajawahi kutenda dhanmbi, ndio maana tukiomba dua tunasema (Ewe Mollah Mimi nimeidhulumu Nafsi dhuluma kubwa kabisa naomba unisamehe)hili nitalitolea ufafanuzi kwenye darsa za mbeleni, leo wacha tumchambue Shahidi tuone ana siri gani anataka kutwambia.
Unaendelea na darsa ya Shahidi fanya umuhimu uishi maisha ya ushahidi ili upate kufanikiwa hapa duniani na huko Akhera uendako. Kwa ajili hiyo ndio napenda kukumbusha tena ukisikia Mtu kafa Shahidi maana yake kafa hana Dhanmbi.
Sasa na wewe huna haja ya kufa ukiwa Shahidi unaweza kuishi katika Ulimwengu ukawa na wewe pia Shahidi, kwa maana hiyo utakua matendo ya dhanmbi huyatendi, Na hiyo ndio Darsa yetu ya leo na Faida zake.
Wewe hapo ulipo Maisha yako yote Umefunikwa na Akili, unachotakiwa kufanya ufunue pazia, umeiwachia Akili yako inafanya kazi masaa 24 bila ya mapumziko, mpaka ukilala unasema na kugombana usingizini, sasa umefika wakati uipumzishe (Computer)Chukua madaraka kamili ili uwache kuamuliwa mambo yako na Akili, ndio kwenye hiyo Aya ukaambiwa basi kwenye nafsi zenu hamuoni, na moja katika la kutizamwa ni hii Akili, kwani Akili ni Nyenzo katika nafsi yako, ndio maana wakati wengine unaambiwa wewe hutumii Akili yako.
Wewe Mwenyewe ndio umeifundisha Akili yako kukufanyia kazi zako, si vibaya inafanya zile za muhimu na nzuri, lakini kwa bahati mbaya umeifundisha mabaya vile vile na kwa kuwa Walimu walikuwa wengi ndio maana kichwani umekuwepo mtafaruku mkubwa sana, kutokana na mtafaruku huo ndio umeamua kuiweka kwenye (Automatic mode) ikisha huyo umelala, ninachofanya mimi kukuamsha na kukwambia rejea kwenye (Manual Mode) na ukirejea kwenye (Manual) ndio unakutana na huyo |shahidi ambaye ni wewe Mwenyewe (Original)Jijue wewe ni (Holy) wala Mtu asikwambie vengine.
Sasa Ukitaka kuwa Shahidi ina maana Uchukue (Control)lazima urejee kwenye (Basic)na jambo la mwanzo kufanya huwezi kwenda kwenye (Basic)lazima uisimamishe Akili yako kufanya kazi,(Stop your mind)Ndio maana aya ikatwambia (Hamuoni)kwanini haijasema hamtizami, kwa sababu kutizama ni kitu cha mbali, lakini kuona ni kitu cha karibu, utizame ndani, Kwa kawaida macho yetu yamekua (Trained)au Kufundishwa kuona Nje, Sasa hapo unatakiwa kujifunza kuona ndani, basi ni kitu gani hicho kinotizama ndani na nje?.
Endelea part 3

No comments:

Post a Comment