Asalaam Aleiykum
Kitu chenyewe kionacho ndani na nje ni hiyo wewe ambayo(Eternal)Roho yako, au Tuite Shahidi.
Hii Roho au Shahidi inaponza kufanya kazi yake ndipo (Mind)au Akili ina (Stop)Na Akili ikisimama ndio inaanza kufata amri zako, Na ukianza Maisha ya Shahidi inakua vigumu kwako kutenda kosa lolote kwa sababu Shahidi ana mahusiano na Mapenzi, toka lini ukasikia Mwenye mapenzi anaua, Mwenye kuua ni yule Mwenye chuki, Kwa sababu Shahidi hajui Uadui, ila Shahidi Akilala Akili au (Mind) ndio inatenda Makosa, ndio maana ukiwa kwenye mapenzi una (Lost your mind)watu wanashikwa karogwa huyo, hajarogwa abadan, anafanya mambo kinyume cha nyinyi wenye chuki, ndio maana mnaona karogwa, mbona anamsomeshea watoto wake, hii kamnunulia nyumba, utajiri wote kamuachia Mwanamke huyo ndio Shahidi(Nimekupa Mfano).
Niliposema Shahidi hajawahi kutenda kosa ila alikua kalala hapo nilikosea kidogo, kwa sababu huko kulala pia kunategemea Akili(Mind) ndio maana ukiwa Jasiri unaweza kuuona usingizi unapokuvaa, taratibu unapoingia nyayoni unapanda mpaka kwenye Akili yako, lakini unatakiwa Ujasiri(Siku ya mwanzo nilipokua nafanya zoezi hilo nilidhani nakufa mambo yanatisha)
Naam Napenda ujue yakua Shahidi halali, yeye hapati usingizi, Sasa utakua bado unajiuliza ni nani huyu Shahidi?. Wacha nikupe jawabu Shahidi ni yule ambaye Habadiliki ndani yako, kila kitu kinabadilika isipokua Shahidi, toka akae kwenye hiyo Nafsi hajawahi kuondoka, Shahidi huyu hata ukiwa kwenye Usingizi mzito yeye anaangalia(Ndio maana ukaambiwa Uhai)Yeye anaendelea kuangalia ndoto zako, Na hata ukiwa huna ndoto basi yeye anaendelea kuangalia usingizi wako wa nafsi ulio mzito, Na pale unapoamka Shahidi anaendelea kuangalia Ulimwengu, Na unapolala inaangalia Ulimwengu wako wa ndani, Haijawahi kusimama hata sekunde kuangalia mambo yote yanozunguka Ulimwengu wa nje na kwenye nafsi yako, Na ukiijua hali hiyo ya Ushahidi ndipo Akili ina simama na dhanmbi zinatoweka, Na ukifanikiwa kuwa Shahidi ndio utaona Hamaki zinakuja zinapita, matatizo yanakuja yanapita, maradhi yanakuja yanapita, magonvi yanakuja yanapita, Raha zinakuja zinapita, shida zinakuja zinapita, Baridi inakuja inapita, joto linakuja linapita, sio kazi rahisi lakini inawezekana ndio maana tukaambiwa tujaribu kuangalia kwenye nafsi zetu asaa tunaweza kufanikiwa kuona kitu.
Sasa ili ufanikiwe kumpata Shahidi ndio wema walopita wakatafuta mbinu nyingi ili wawe mashahidi, Madhumuni yao yote ilikua kuisimamisha Akili(Mind), Wakaja na (Tasbih)nazitaja baadhi ya nyezo walotumia ambazo leo mnaelezwa haramu, haifai, lakini watu hawakujua nini kusudio la mambo hayo ya kuanzishwa (Dhikiri)Mtu kukaa na udhu, Kusema (Astrafullah)mara elfu kumi, yote ni katika nyenzo ya kuisimamisha Akili, na Akili ikisimama hapo hapo unakutana na Shahidi na huyo shahidi ndio wewe na wala sio mwengine.
Vipi unaweza kuisimamisha Akili itabidi uisome hiyo aya hapo umepewa (Trick)(Just Watch your Mind)ndio katika nafsi zenu hamuoni, anza kidogo kidogo kujiangalia vipi unakula, vipi unazungumza, ukiwa kimya isikilize akili yako inavoongea, ukikoga fanya upate hisia ya mwili wako, punguza kuongea kama mchiriku, Ukisali sikiliza Quraan unayosoma, jaribu kurejea kwenye Nafsi yako kidogo kidogo utaona Akili ina (Dissappear) na Shahidi ana (Appear).
Hapo ndio tunaingia aya ya pili, kumbuka huwezi kuingia aya hii mpaka umekua Shahidi.
"وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزۡقُكُمۡ وَمَا تُوعَدُونَ
"Na Katika Mbingu ziko riziki zenu na mliyoahidiwa"
Kumbuka ukifanikiwa kuwa Shahidi Muono wako wa Ulimwengu huu unabadilika, Na hapo unaanza kufunguliwa baadhi ya siri, ndipo unapokutana na ukweli wa ithbati kuwa katika hiyo Mbingu ndiko kunako gaiwa Riziki yangu, mimi hata nikifanya nini siwezi kuzidisha wala kupunguza vile ambavyo inavoamriwa huko Mbinguni riziki yangu iwe ya kiasi gani, ndio utaona yule ambaye anauza mchanga anatajirika na wewe Mwenye kuuza dhahabu bado umasikini, Na hapo inakufungukia yakini kuwa siku uhai wangu utakapomalizika basi na mimi ntaelekea huko Mbinguni katika kupata yale nilohaidiwa."Mollah wetu tujaalie Maisha ya Ushahidi na utufanye katika watakaopata pepo yako Mollah wetu".
Amin.
No comments:
Post a Comment