Thursday, February 1, 2018

MAISHA YA SHAHIDI PART 1

Asalaam Aleiykum

Leo naanza Darsa kwa kuuliza swali ambalo ntakusaidia kujibu lakini uwe mkweli kabla ya kuendelea kuichambua darsa hii ujiulize Mwenyewe hivyo nilikua najua jawabu.
Swali: Hivyo kama nitakuuliza unajua nini maana ya kufa Shahidi? utanijibu vipi?.

Najua jawabu lako litaegemea kwenye matendo ya huko kufa Shahidi lakini sio maana asilia ya kufa Shahidi, utanambia kufa kwenye vita vya dini, au baharini, au uzazi na hivi na vile, lakini maana na kusudio lenyewe hulijui, basi kuanzia leo utapata maana yake si ya kufa Shahidi tu bali pia ya kuishi kama Shahidi.

Hakuna Jambo gumu kwa Mwanaadamu kama hilo la kuishi Kama Shahidi, Linashindikana jambo hili kutokana na Mwanaadamu kamilikiwa au (Shape)na Jamii au (Community). Kilicho mlea na kumkuza katika maisha yake ni yale mafunzo ya Tabia, hisia na muelekeo mzima wa (Eviroment)anayoishi, (Something very Powerful) Imeota kwa Mwanaadamu huyu inayoitwa (Ego) ambayo imetawala na kuweka kivuli mpaka kufikia kuwa haoni tena au hajui kama yeye ni Shahidi.
Vipi ? atakua Shahidi Wakati katawaliwa na Tabia, vipi awe Shahidi wakati karithi Tabia za Baba na Mama, vipi atakua Shahidi wakati kichwani humo kuna Mwalimu anakaa humo, Umetawaliwa na Kabila lako, umemilikiwa na unaongozwa na Jamii, vipi utakua Shahidi wakati kwenye (Mind) yako umejaa umbea, ndani humo kuna magonvi, wanawake na wanaume wanaishi humo, Dhiki ya maisha imo humo, kila mambo ulojifunza na kuyaona yamejaa humo mpaka umesahau sasa kuwa wewe Roho au Akili.
Kwenye (Stage) ulofikia Akili imeshachukua madaraka Kamili na sasa inaendesha maisha yako huku wewe ukifata Amri yake, Jiangalie kwa undani utaona kila kitu chako kimekua (Influence by the other), Hata hiyo Imani yako ya Dini unayoitegemea Masheikh ndio wameishika, unasikiliza nini wamesema, wewe Mwenyewe umekua huwezi hata kuwasiliana na Mollah wako Mpaka upitie Kwa Masheikh, umeishia unasema mimi naamini lakini hujui unaamini nini.
Na hilo linakutia wasiwasi huwezi kwenda kwa Mollah wako na moyo ulosalimika, Nini kitakacho kujulisha huo moyo ulosalimika?, hakuna chengine ila kurudi ili uwe Shahidi, kumbuka Shahidi ndio pekee anokwenda akiwa salama kwa Mollah wake. Sasa vipi Unakua umetawaliwa, itabidi nikurudishe kwenye Sala uone vipi ushahidi unavokutoka, vipi usingizi ulivokushika, au vipi hiyo (Mind) au Akili inavotawala mpaka ukawa huna ushahidi.
Wewe unapewa vipindi vitano vya Sala kuwasiliana na Mollah wako, Lakini wapi ukisimama kwenye hiyo Sala kitu cha mwanzo chenye kukujia vipi utakula sadaka ya msikitini, dukani umemuacha nani, Leo barazani wamesema nini, Kila ukikaa Akili yako masaa 24 inachambua habari mpya au ya zamani, siri za ngono, au magazeti, vipi mtamfukuza Imam, mbona hasalishi vizuri, hadith fulani inasemaje, leo hakuja kusali na sisi, sala yake haikubaliwi, utaona kadhia hii imejaa misiskitini na makanisani kwa jumla, utaona Mwili(Body)Upo Msikitini lakini (Mind) Akili ipo kwengine kabisa, sasa jiulize hapo Shahidi yuko wapi?
Endelea part 2




No comments:

Post a Comment