Asalaam Aleiykum
Katika sura ya (Mulk)kumetajwa mambo mawili ambayo yanapaswa tuyazingatie kwa undani, Maneno yenyewe ni haya "Mwenye enzi Mungu ameumba Mauti na maisha" viwili hivi vimetuzunguka na tunaishi navyo lakini wengi hatuna ujuzi wa kuvijua.
Leo umefika muda wa kujua kikoje kivuli hicho cha Mauti, Na kwanini naishi nacho halafu nikawa sikijui. Sasa Kabla ya kuendelea na darsa yetu napenda kukupa dondoo ya "Kivuli cha Mauti" ili nipate kukujulisha vilivyomo pembeni mwa "Kivuli"hicho.
Wewe Mwanaadamu yaweza kuwa pengine umeghafilika au hujui kabisa pembezoni mwa kivuli cha Mauti kuna kaa nini, Ukiangalia vizuri katika umri huu ambao unaishi katika Ulimwengu huu kuna hesabu ya Namba 7 imekuzunguka, kama Mbingu 7 na Ardhi mfano huo huo wa 7, Basi na maisha yako pia yamezungukwa na Namba hiyo ya 7, kila baada ya miaka 7 maisha yako yanabadilika ndani na nje kuanzia Riziki mpaka maumbile, ukitaka ushahidi wa hilo lifanyie uchunguzi nakujulisha wapi kwa kuanzia, rudi nyuma ulipozaliwa mpaka ukafika miaka saba ulikua unaishi ndani ya kivuli hujali kitu, huna fahamu, huogopi kufa wala chochote, ulipoanza kufika miaka saba ukaanza kupewa fahamu kidogo kidogo ndio maana hekima ya kuambiwa watoto wakifika miaka saba wafundishwe kusali, kufunga, wakiachiwa kipindi hicho kama hakijatiwa kitu kwenye Akili wakakizoea basi watakua hawafahamu tena, Sasa ilipofika saba ya pili(14) unafunguliwa raha ya (Sex).
Ulipofika Miaka (21) Pengine umemaliza (Uni au School)Ukaolewa au ukaoa, na ulipoingia saba ya nne(28)sasa unakabidhiwa utu Uzima na hapo ndio kidogo unaanza kukutana na Kivuli, unaanza kujua kumbe jua litakuchwa, kuna usiku utanivaa, kivuli kinakuja na hivyo ndio Mauti yanapowasili kwa kujitambulisha umebakiza muda sio mrefu na mimi nichukue nafasi yangu.
Sunday, April 15, 2018
KIVULI CHA MAUTI PART 2
Asalaam Aleiykum
Unapotaka kufahamu ukweli wa Kivuli hicho kwanza lazima upite kwenye Muongozo wa kitabu cha Quraan aya ya pili iliyomo sura ya (Mulk) inayosema.
ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلۡمَوۡتَ وَٱلۡحَيَوٰةَ لِيَبۡلُوَكُمۡ أَيُّكُمۡ أَحۡسَنُ عَمَلاً۬ۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡغَفُورُ
"Ambaye ameumba Mauti na uhai ili kukujaribuni, ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri, Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye Msamaha".
Nakuomba zama au nenda (Deep)lazima utakutana na vitu viwili Maisha na Mauti, katikati ya mambo hayo mawili ndio kuna hicho kivuli, Sasa tuliza Akili yako nikuchukue kwenye Umahiri wa lugha ili upate kujua vipi unaishi katika viwili hivi. Napenda ufahamu kuna kitu kimoja hichi kiitwacho uhai, hiki wewe una uhakika nacho, ukiamka unajijua mimi niko hai, lakini nina hakika hujawahi kujiuliza nikilala nakwenda wapi, au niko katika hali gani, au naishi vipi?.
Nakuomba ukae ulizingatie swali hilo ambalo ndani yake kuna mazingatio makubwa kabisa ambayo sio ya Ulimwengu huu. Aya inasema "Yameumbwa Mauti na Uhai"Jee unaishi katika viwili hivi?, Na kama unaishi ile (Final)ambayo hurejei tena inaitwa nini?Ikiwa kuna Uhai au haya (Maisha)tunayoyajua basi elewa unaishi pia katika kitu kiitwacho(Mauti)ndio maana ukaambiwa viwili hivi vimeumbwa na vinaenda sambamba, kila ukenda kulala unakwenda katika hiyo awamu ya pili ya (Umauti), nisije kusema hivi ukaja kudhani zile ndoto zako ndio Ulimwengu wa (Mauti) huwezi kuufikia Ulimwengu huo mpaka upewe Hijjaza na Mollah wako, au ufanye mazoezi uweze kuuona usingizi wako.
Utakapoona usingizi wako ukashuhudia Mwili wako umelala na wewe tafauti na kiwiliwili chako una uangalia, hapo utajua nini maana ya hilo kusudio la "Kivuli cha Mauti", Ndio maana nikasema ukitegemea ndoto utakua bado unaishi kwenye Akili, Na itakua kama jua limepatwa giza limetanda, Na ukitaka kujua kwamba bado uko kwenye Akili zitizame ndoto zako zitakujulisha pale unapoota mtu wako alokufa, siku zote utamuona katika umri wa ujana au alivokua mtoto, Ni kwa sababu hiyo ndoto yako inatokea kwenye (Memory), Lakini ukimuona kwenye hali ambayo ya hivi sasa basi hapo itakua umekwenda(Beyond).
Nimesema kuna njia mbili za kuangalia hiki kivuli ama ile ya kwanza ni usingizi ambayo ni ngumu sana kwetu sisi kupata habari zake. Ama njia ya pili ni hii iliyomo kwenye sura ya.
Endelea part 3.
Unapotaka kufahamu ukweli wa Kivuli hicho kwanza lazima upite kwenye Muongozo wa kitabu cha Quraan aya ya pili iliyomo sura ya (Mulk) inayosema.
ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلۡمَوۡتَ وَٱلۡحَيَوٰةَ لِيَبۡلُوَكُمۡ أَيُّكُمۡ أَحۡسَنُ عَمَلاً۬ۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡغَفُورُ
"Ambaye ameumba Mauti na uhai ili kukujaribuni, ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri, Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye Msamaha".
Nakuomba zama au nenda (Deep)lazima utakutana na vitu viwili Maisha na Mauti, katikati ya mambo hayo mawili ndio kuna hicho kivuli, Sasa tuliza Akili yako nikuchukue kwenye Umahiri wa lugha ili upate kujua vipi unaishi katika viwili hivi. Napenda ufahamu kuna kitu kimoja hichi kiitwacho uhai, hiki wewe una uhakika nacho, ukiamka unajijua mimi niko hai, lakini nina hakika hujawahi kujiuliza nikilala nakwenda wapi, au niko katika hali gani, au naishi vipi?.
Nakuomba ukae ulizingatie swali hilo ambalo ndani yake kuna mazingatio makubwa kabisa ambayo sio ya Ulimwengu huu. Aya inasema "Yameumbwa Mauti na Uhai"Jee unaishi katika viwili hivi?, Na kama unaishi ile (Final)ambayo hurejei tena inaitwa nini?Ikiwa kuna Uhai au haya (Maisha)tunayoyajua basi elewa unaishi pia katika kitu kiitwacho(Mauti)ndio maana ukaambiwa viwili hivi vimeumbwa na vinaenda sambamba, kila ukenda kulala unakwenda katika hiyo awamu ya pili ya (Umauti), nisije kusema hivi ukaja kudhani zile ndoto zako ndio Ulimwengu wa (Mauti) huwezi kuufikia Ulimwengu huo mpaka upewe Hijjaza na Mollah wako, au ufanye mazoezi uweze kuuona usingizi wako.
Utakapoona usingizi wako ukashuhudia Mwili wako umelala na wewe tafauti na kiwiliwili chako una uangalia, hapo utajua nini maana ya hilo kusudio la "Kivuli cha Mauti", Ndio maana nikasema ukitegemea ndoto utakua bado unaishi kwenye Akili, Na itakua kama jua limepatwa giza limetanda, Na ukitaka kujua kwamba bado uko kwenye Akili zitizame ndoto zako zitakujulisha pale unapoota mtu wako alokufa, siku zote utamuona katika umri wa ujana au alivokua mtoto, Ni kwa sababu hiyo ndoto yako inatokea kwenye (Memory), Lakini ukimuona kwenye hali ambayo ya hivi sasa basi hapo itakua umekwenda(Beyond).
Nimesema kuna njia mbili za kuangalia hiki kivuli ama ile ya kwanza ni usingizi ambayo ni ngumu sana kwetu sisi kupata habari zake. Ama njia ya pili ni hii iliyomo kwenye sura ya.
Endelea part 3.
KIVULI CHA MAUTI PART 3
Asalaam Aleiykum
Alama yetu ya pili kukijua kivuli hichi ni aya iliyomo sura ya Yaasin aya ya 68.
"وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَڪِّسۡهُ فِى ٱلۡخَلۡقِۖ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ "
Na tunayempa Umri (Ikisha)tunamrejesha nyuma katika umbo lake basi jee hawayatii Akilini(Kuzingatia).
Alama yakua sasa kivuli kinaondoka ni kupoteza kwako kwa uwezo wa mambo mengi katika Mwili wako, unatakiwa uyazingatie kuwa hivi karibuni safari itawadia ya wewe kuondoka kwenye (Maisha) na hicho kiitwacho (Mauti) viwili vyote hivi vinatoweka, na dalili zipo nyingi tunapewa ili tujiandae, viwili hivi vinaondoshwa kidogo kidogo pasi wewe kushituka, Ama kwenye maisha huwezi kwenda mbio, nywele kuwa nyeupe, huwezi harakati nyingi, Maradhi yanawasili kutokana na muda wa viungo kutenda kazi ushamalizika, na katika kadhia ya (mauti)mpaka usingizi una punguziwa, ukiona vitu vyote hivi vimewasili basi elewa sasa wakati wowote unatarajiwa urejee nyumbani, unatakiwa kulala ule usingizi wa moja kwa moja, uondoke kwenye Uhai, upite kwenye mauti ili urejee nyumbani kwa aliyekuumba.
Yote hayo yanafanyika lakini kuna kitu unakiona kivuli chake bado kipo, daima jitizame ukiumwa, ukiwa mzee, kuna kitu kinakujulisha kiko (The same)hakibadiliki, Kitu hicho kitu gani daima kipo na wewe kwa mfano wa kivuli, siku utakapo kigundua kivuli hicho ndio siku yako ya kurudi nyumbani, tegemeo langu utapokelewa kwa salama na Msamaha kutoka kwa Mollah wako kama alivosema Mwenyewe kwenye sura ya Mulk aya hiyo ya pili.
Alama yetu ya pili kukijua kivuli hichi ni aya iliyomo sura ya Yaasin aya ya 68.
"وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَڪِّسۡهُ فِى ٱلۡخَلۡقِۖ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ "
Na tunayempa Umri (Ikisha)tunamrejesha nyuma katika umbo lake basi jee hawayatii Akilini(Kuzingatia).
Alama yakua sasa kivuli kinaondoka ni kupoteza kwako kwa uwezo wa mambo mengi katika Mwili wako, unatakiwa uyazingatie kuwa hivi karibuni safari itawadia ya wewe kuondoka kwenye (Maisha) na hicho kiitwacho (Mauti) viwili vyote hivi vinatoweka, na dalili zipo nyingi tunapewa ili tujiandae, viwili hivi vinaondoshwa kidogo kidogo pasi wewe kushituka, Ama kwenye maisha huwezi kwenda mbio, nywele kuwa nyeupe, huwezi harakati nyingi, Maradhi yanawasili kutokana na muda wa viungo kutenda kazi ushamalizika, na katika kadhia ya (mauti)mpaka usingizi una punguziwa, ukiona vitu vyote hivi vimewasili basi elewa sasa wakati wowote unatarajiwa urejee nyumbani, unatakiwa kulala ule usingizi wa moja kwa moja, uondoke kwenye Uhai, upite kwenye mauti ili urejee nyumbani kwa aliyekuumba.
Yote hayo yanafanyika lakini kuna kitu unakiona kivuli chake bado kipo, daima jitizame ukiumwa, ukiwa mzee, kuna kitu kinakujulisha kiko (The same)hakibadiliki, Kitu hicho kitu gani daima kipo na wewe kwa mfano wa kivuli, siku utakapo kigundua kivuli hicho ndio siku yako ya kurudi nyumbani, tegemeo langu utapokelewa kwa salama na Msamaha kutoka kwa Mollah wako kama alivosema Mwenyewe kwenye sura ya Mulk aya hiyo ya pili.
Subscribe to:
Posts (Atom)