Friday, May 4, 2018

DARSA YA RAMADHAN PART 1

Asalaam Aleiykum

Hutaki nikupe siri itakayokufanya Funga yako iwe bora na yenye kukubaliwa na Mollah wako, Hupendi wewe kuwa na furaha moyoni mwako kwa kujua Mwaka huu kwa mara ya mwanzo nimeipata Taqwa, huna hamu yakuwafahamisha wengine yakwamba funga iko namna hivi, basi ikiwa Mwenye kuyataka hayo wacha nikufahamishe sababu za weye kuambiwa ufunge.
Tuliza macho kwenye darsa hii nikuchukue katika safari fupi ili upate kunifahamu vizuri.
Siku zote Masheikh wanaanza na aya hii iliyomo sura ya (Baqarah aya ya 183)
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡڪُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِڪُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ 
"Enyi Mloamini Mmelazimishwa Kufunga kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu".
Wacha nikuchukue  twende kwenye Bustani tukachume tunda la Saum na hakuna kwengine lilipoanzia Tunda hili ila huko Mbinguni pale Mwenye enzi Mungu alipowaambia Malaika kwenye sura ya (Hijr aya ya 28 na 29)
وَإِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَـٰٓٮِٕكَةِ إِنِّى خَـٰلِقُۢ بَشَرً۬ا مِّن صَلۡصَـٰلٍ۬ مِّنۡ حَمَإٍ۬ مَّسۡنُونٍ۬ 
"Na Mollah wako alipowaambia Malaika, Hakika Mimi nitamuumba Mtu(Binaadamu) kwa Udongo Mkavu unaotoa Sauti, Wenye kutokana na matope meusi yalovunda".
فَإِذَا سَوَّيۡتُهُ ۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِى فَقَعُواْ لَهُ ۥ سَـٰجِدِينَ
"Basi nitakapomkamilisha na kumpulizia Roho inayotokana na Mimi, basi Mumuangukie kwa kumtii(Sujud)".
Hapo kwenye aya hizo mbili kuna mambo lazima uyatupie macho upate faida zake, Mambo yepi?, la kwanza lenye kuonesha udhaifu wako kuwa wewe ni udongo mkavu unaotoa sauti, tena ulovunda ndio maana ukifa unaanza kutoa harufu.
Na hiyo aya ya Pili inakupandisha daraja kubwa yakuwa wewe ni Roho iliyotokana na Mwenye enzi Mungu, basi nitakapomaliza kumuumba poromekeni kumtii, msujudieni hichi kiumbe changu. Sasa jambo la mwanzo kujitambua wewe ni (Khalifa)wala usikubali mtu mwengine akakwambia vengine, kwa hayo unayotenda labda itakua dunia imekulevya, Na umejisahau kama wewe ni (Khalifa) katika Ardhi hii.
Hili neno (Khalifa)likazie macho sana lina maana kubwa katika Darsa hii ya Ramadhan. Naam sasa umeshajijua kwamba wewe ni (Khalifa)na hapa Ulimwenguni unapita tu, (Ndio maana Mtu akifa tunasema sote ni wa Mwenye enzi Mungu na kwake tunarejea) ilipotajwa kuhusu (Khalifa)"Malaika kwenye aya ya (30)Sura ya (Baqarah)"wakasema Utaweka humo watakaofanya Uharibifu humo na kumwaga damu,"Mwenye enzi Mungu akawajibu"Hakika Mimi nayajua msiyoyajua".
Sasa hapo Malaika walijuaje kuwa tutafanya visa Ardhini, Jawabu ni kutokana Majini walotutangulia walileta uharibifu kwenye Ardhi hii, Mollah wetu akatufundisha na anaendelea kutufundisha chungu ya Mambo yaliyomo kwenye Ardhi hii, haya ma(Computer)magari,meli,Madege, kila machine iliyomo kwenye Ardhi hii ni kutokana na elimu anayotufunulia yeye na sisi kuweza kutekeleza. Sasa haya yote yamehusiana nini na Saum. 
Endelea part 2


DARSA YA RAMADHAN PART 2

Asalaam Aleiykum

Mwanaadamu ukijua cheo chako kikubwa ulichopewa na Mwenye Enzi Mungu utakua furahani Milele, ndio maana (Ibilisi)akasema laa siwezi kumsujudia kiumbe huyo. Tizama vipi Mwanaadamu thamani yako ilivyo, ndio sasa katika Mwezi huu wa Ramadhan unaitwa, lakini sio wote wenye kuitwa ila wale (Masikini kwenye Ibada)wale wenye kuutaka Ucha Mungu ndio watakao rithi Ufalme au Pepo ya Mwenye enzi Mungu.
Kwanini ikawa hawa tu ndio watarithi kwa sababu wao wameamini, ndio maana aya ya kuamrisha kufunga haikusema Waislamu kwa sababu lazima iwepo Imani ndio uweze kufunga, sasa hawa wenye kuamini wanakubali kwa karibu zaidi Mwenye enzi Mungu yupo na Amri zake zipo lakini hawajui vipi kuipata yakini hiyo, ndio imeletwa Ramadhan ili utoke kwenye Imani upige hatua ya kwenda kwenye Taqwa au (Uthibitisho).
Na hiyo ni (Stage)ya Pili kabla ya kuingia ile ya tatu ya (Ushuhuda au Shahid) au wengine wanaita (Truth). Kwa hiyo hapo Wanaitwa "Enyi Mloamini"Njooni mpate kufundishwa nyinyi hamjui kitu, kuna mambo mawili ndani ya hii Ramadhan, yepi mambo hayo Mawili?, Umo kwenye darsa ya Ramadhan fanya hima ujiandae uwape habari njema na wenzio ili na wao wapate faida ya kufunga.
Ama hilo jambo la kwanza ndio hilo Wasomi wanalipigia kelele, funga utapata Afya, funga Mwili(Body)inajitibu yenyewe, kila kitu kinaambatana na body, (Unakumbuka kule Mwanzo Mwenye enzi Mungu aliposema Ntamuumba kwa udongo mkavu unotoa sauti)basi naam hiyo ni sehemu katika sehemu moja ya hii kuamrishwa kufunga, ila kuna sehemu hii ya pili wengi hawajui, hawajapata (Ushahidi)(Truth)Na hichi cha pili ndio sababu kuu ya Ramadhan.
Kitu gani hichi cha pili?.
Kumbuka Miezi yote kumi na moja umezama kwenye mambo ya dunia, umemsahau Mollah wako, ndio katika Mwezi huu Mmoja Mollah wako kakuita "Ewe Kiumbe"changu rudi kwa Mwezi huu mmoja uwe na mimi, Nini (Saum)? Saum ni (Union with god) hiyo ndio Taqwa, Khalifa anakutana na Mfalme wake.
Nini kitapatikana iwapo Khalifa huyu atafunga inavotakiwa?.
Hapa itabidi nieleze faida itakayo patikana hapa Ulimwenguni, Ama ile ya Akhera ajuwae yeye Mollah wetu, Ama hapa Ulimwenguni zipo faida Mbili, ya kwanza  yule Mwenye kupata (Union)na Mollah wake, na hiyo ya pili ya yule Mwenye kupata (Total Union).
Ama yule Mwenye kupata (Union)tu, yule atakua kapata hiyo Taqwa, na huyo pekee ndie Mwenye kuweza kuhadithia lakini kwa dalili tu naweza kukwambia yanatokezea (Mapenzi)kwenye nafsi yako na mfano wake (Kaisome aya ya 177 sura ya Baqarah)ndio utajua, sio mapenzi haya ya kawaida ya kumpenda Mwanamke au vitu bali inakuwa (Total love) hiyo ndio Taqwa, inakuaje, wewe unajua vipi mapenzi yanavoingia katika Akili, sasa Taqwa ndio inakua mapenzi ya Mollah wako na wewe ndio unaingia katika ile aya ya "Wanaomkumbuka Mollah wakiwa wamesimama, wamekaa mpaka wakiwa wamelala" ukiipata hali kama hiyo hapo ndio Taqwa inakua ime (Happen) na hicho ndio kinachotakiwa katika Ramadhan ukipate(Focus)yako yote iwe kwa Mollah wako.
Hazikutoki fikra za Mollah wako hata mara moja na uwepo kokote pale, uwepo Mpirani au senema uwepo harusini au kwenye futari Mollah wako haondoki tena kwenye mawazo yako, ikikuta hali kama hiyo basi utaona unafatiwa na furaha na manukato ya kheri unangara kwa wanaadamu wenzio.
Ama yule Mwenye kupata (Total Union)Yeye anapotea kabisa anakua mtu mwengine kabisa, kauli zake ni zengine kabisa, Nuru yake ni nyengine kabisa(Feeling)zake nyengine anaishi kwenye (Bliss)utamuona (Something of beyond happen) kitu chenyewe ni hiyo ilotajwa  kwenye sura ya (Al-Qadir).
"إِنَّآ أَنزَلۡنَـٰهُ فِى لَيۡلَةِ ٱلۡقَدۡرِ "
"Hakika Tumeiteremsha(Quraan) kwenye Usiku wa Heshima(Wa Nguvu)"(Usiku wa Ramadhan)
Nini hicho kiloteremshwa katika usiku huo ni hii Quraan, aliyoteremshiwa Bwana Mtume s.a.w. lakini kuna mengine yamo humo huwa yanateremshwa ambayo nitafafanua yametajwa kwenye sura hiyo.
Endelea part 3

DARSA YA RAMADHAN PART 3

Asalaam Aleiykum

وَمَآ أَدۡرَٮٰكَ مَا لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ 
"Na Jambo gani litokujulisha Nini huo Usiku Wa Laylatul Qadir"
Kuna baadhi ya watu hapa wanasema ni kushushwa kwa Quraan kwenye (Lahwi Mahfoudh)Sasa ikiwa Mwenye Kufahamu utajua kuwa huko Mbinguni hakuna Mchana wala Usiku, ilipotajwa Usiku kusudio lake (Usiku huu Wenye Heshima wenye Nguvu) Ni ule Usiku Aloteremshiwa Bwana Mtume s.a.w Hii Quraan. 
Sasa Kwanini ukaambiwa nini kitokujulisha Wewe Usiku huu?. Hapo inaonesha unatakiwa Wewe kuujua Usiku huu, Lakini Kujua na kujulishwa ni mambo mawili tafauti kujua itakua kama wengine unajua kuwa Usiku huu umo ndani ya Ramadhan, kwa Mwaka mara moja tunapita ndani ya Usiku huu, Lakini Kujulishwa hapo ni ile (Experience)ukotokezee Usiku huu ndani ya Nafsi yako.

لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ خَيۡرٌ۬ مِّنۡ أَلۡفِ شَہۡرٍ۬ 
"Huu Usiku wa Heshima(Nguvu)ni Bora kuliko Miezi Elfu"
Hapa kuna Tafsiri Mbili inabidi tuzipitie, Umo katika Darsa ya Ramadhan pata faida ya kujua mambo ili upate mafanikio. Tafsiri ya kwanza "Kama utaupata Usiku huu" basi hata kama kama utaishi hiyo Miaka 83 basi haiwi bora kama Usiku huu, Ibada zote ulizozifanya na kheri zote unozijua wewe hazifanani na Usiku huu.
Ama Tafsiri ya Pili (ambayo wengine wameitetea kuwa ndio sahihi)"Usiku huu ukiupata (Power)yake au Nuru yake inotokozea kwenye Roho yako ni kupita miezi elfu imurike kwa pamoja kwenye Ulimwengu huu, hapo ndio likapatikana kwa Wale walo (Experience) Wakaita Nyota ya Jaha", Mtu hajui la kusema anaona kageuka Nuru juu ya Nuru, Ndio Maana utaona hata katika ule Mlima nje kidogo ya Makka alipopewa hiyo Quraan Bwana Mtume s.a.w kwa mara ya Mwanzo panaitwa (Jabar Noor).

تَنَزَّلُ ٱلۡمَلَـٰٓٮِٕكَةُ وَٱلرُّوحُ فِيہَا بِإِذۡنِ رَبِّہِم مِّن كُلِّ أَمۡرٍ۬ 
"Huteremka Malaika na Roho (Za viumbe watakatifu)katika (Usiku)huo kwa Idhini ya Mollah wao kwa kila Jambo."Hapo ndipo niliposema Ukiipata ile (Total Union)Basi unapata cheo cha Utakatifu(Pure Born again)Unakua safi kama ulozaliwa leo, "Ndio maana ikasemwa ni Bora kuliko hiyo miaka 83 utakayoishi". Unakua Umesamehewa ungali uhai na unapewa Nguvu fulani na uwezo fulani inakua hata Binaadamu wenzio wanahisi kuna mabadiliko fulani, mara utasikia dua yake hairudi, yule ana (Makarama) na hivi na vile.
Unapata hayo kwa ajili ya Idhin ya Mollah wako.
 سَلَـٰمٌ هِىَ حَتَّىٰ مَطۡلَعِ ٱلۡفَجۡرِ 
"Ni Amani (Usiku)huo mpaka mapambazuko ya Alfajiri".
Ukiamka unakua (New Man Transform)(Your past is gone).
Naam tulikua tunachuma tunda sasa wacha turejee kwenye Mzizi wenyewe wa Mti wa Saum. Sasa Neno Funga linatajwa siku zote unalisikia na kulisoma lakini pengine hujawahi kwenda (Deep)ukalifahamu maana yake, Funga kwa Mwanaadamu imekusudiwa uzuie kitu kisiingie ndani.
Sasa utajiuliza kwanini Mwanaadamu anatakiwa afunge, Unatakiwa Ufunge kwa ajili urejee kwenye (Basic)yako ya Maumbile, Au Msingi wako wa Kuumbwa, au kupatikana ile (Separation) Niloitaja mwanzo (Ya Dongo kavu linotoa sauti na Roho yako).Sasa vipi unatakiwa Ufunge uipate hiyo Taqwa, au utoke kwenye Dongo urudi kwenye Roho,(Ndio maana Ramadhan ikaitwa Ustaadh Mwenye kulea Roho)hapo kuna Mambo (4)lazima uyapate ili funga yako itimie, Na funga ikitimia basi (Automatic) unakutana na Taqwa. Napenda Uelewe hiyo Taqwa inatokea au unaijua au imo ndani ya kifua chako, wakati wakuipata Wewe ndio utakua Shahidi wa hilo, Na ukishuhudia kuwa umeipata Taqwa basi moja kwa moja Jijue Sauwm yako imekubaliwa Na Mollah wako Mlezi.
Mambo gani hayo yanotakiwa katika hiyo funga?.
Unapewa darsa hii kabla ya Ramadhan ili na wewe Uwe katika walofunga mwaka huu, Mambo gani hayo (4)Yanokuchukua kukupeleka mji wa Saum ili kuitafuta hiyo Taqwa. (1)Jambo la kwanza unotakiwa ulifunge ni Chakula , Nini kinatokea?, Unaponyima (Body) Mwili wako chakula unaupa (Shock)nini kimetokea, mbona huyu hatupi huduma yetu, hapo mwili unatoka kwenye (Automatic mode)unakwenda kwenye (Manual) unaanza kujihudumia wenyewe kwa kwenda kwenye (Akiba)zake, ukianza kwenda kwenye Akiba ndio unapita kila pahala kutizama wapi kumeharibika, wapi kuna vuja unaanza kujikarabati(Kujitibu)ndio ukaambiwa kufunga siha.
(2)Jambo la pili Baada ya chakula usiruhusu kitu kuingia Mwilini mwako, kama (Sex)na mengineyo kwani yataishughulisha (System) yako isijue inafanya nini.
(3)Jambo la Tatu Ni Mashikio na Macho Usisikilize Nyimbo(Music)Mambo machafu, Habari za Uongo, na vyote vibaya vyenye kupita kutumia sauti, na jicho lisitizame mambo ya kidunia yenye (Munkar) Funga vipasha habari vyote (Tv, wassup, facebook, instagram)hama kwenye mwezi huu.
(4)Na jambo la nne ambalo ndilo litaweza kukujulisha nini hiyo Taqwa ni hili la kuzungumza, ukiweza jiepushe kuongea sana kwani ukiongea sana una(Miss)yanotokea kwenye nafsi yako, kwa sababu hukai kimya, ukikaa kimya unaweza "Kuona Mawazo yako yanavo zaa Maneno, Na Maneno yako yanakua vitendo, Na vitendo vyako vinakua tabia, Na Tabia yako ndio inakua (Nembo) yako fulani (Mchiriku)kweli, anaongea sana, Na Mtu Mkimya pia anatajwa fulani hazungumzi, basi katika Mwezi huu na wewe kuwa asiyezungumza, hapo ndio utakapoipata Saum kwa kujizuia kuongea sana kama alivosema Bibi Maryam kwenye (sura ya Maryam aya 26)
فَإِمَّا تَرَيِنَّ مِنَ ٱلۡبَشَرِ أَحَدً۬ا فَقُولِىٓ إِنِّى نَذَرۡتُ لِلرَّحۡمَـٰنِ صَوۡمً۬ا فَلَنۡ أُڪَلِّمَ ٱلۡيَوۡمَ إِنسِيًّ۬ا
"Na kama ukimuona Mtu yoyote (akakuuliza habari ya mtoto huyu)Sema Hakika mimi nimeweka Nadhir kwa (Mollah)Mwingi wa Rehma ya Kufunga, Kwa hivyo leo sitosema na Mtu".
Naam na wewe jizuie, kuongea sana, ndio maana mkaambiwa ikisha Mkakae msikitini(Kimya) Kumbuka kila kitu kinatokea kwenye Ukimya, ukijizuia na vyote hivyo Akili inakua haina la kufanya, Na Akili ikisimama Taqwa inatokezea na hiyo ndio Saum. Mollah wangu ni Mwenye kujua zaidi, Nakutakieni Mwezi wa Kheri na Baraka na saum zenye kukubaliwa, Mollah atujaalie Ufalme wake sote tuingie katika pepo yake, Atusameh dhanmbi zetu zilopita za sasa na zinokuja, Awasamehe pia walotangulia kabla yetu awatilie nuru katika makaazi yao huko walipo. 
Amin.