Asalaam Aleiykum
Ametukuka yule aliyeumba Nafsi moja ikisha Akutajaalia Fahamu, Namuomba atupe Fahamu ya kuelewa kuwa kwenye enzi yake sote tuko sawa na hatuna tafauti, Ila kuna ubora kwa yule atakaye mpenda Mollah wake zaidi na kumtii.
Kabla ya kuingia kwenye darsa hii kuna kitu napenda nifahamishe ili msije kuifananisha darsa hii na darsa ya (Sala ya Msikiti), kwa sababu kuna baadhi ya watu wanaona kuwa (Kaka na keki)ni neno moja, kumbe ni maneno mawili tafauti na wala hayana mahusiano.
Kwenye hii darsa ya (Sala ya Jamaa)tunakwenda kuchambua jambo lengine kabisa lenye faida na wewe ikiwa utalizingatia, Kwanini nikasema hivyo, kwa sababu unaweza kwenda Msikitini kusali lakini usisali sala ya "Jamaa" ila ukasali sala ya "Msikitini".
Najua unashangaa, ni vizuri kushangaa ndio mwanzo wa kujua, huko ndio kuweka wazi mifupa ya fahamu ili (Nipate kuifanyia Operation). Kufanya hivyo utapata kuelewa vizuri ipi Sala ya Msikitini na ipi sala ya Jamaa, Sasa tuingie kwenye darsa, Ipi Sala ya msikitini?, Sala ya Msikitini ni ile ambayo wengi wetu tunakwenda tukifika hapo tunasalishwa na "Maimam" wenye viburi, au ana mambo sio mema kwenye jamii yalochanganya kila kitu, na nyinyi mnajua ila mnanyamaza kimya na kumuachia aendelee kukuongozeni kwenye Sala zenu, Au Nyinyi wenyewe mna "Viburi"(Ego)Huu Msikiti wetu wa kundi fulani, unakwenda kwenye nyumba hiyo ya Ibada unanuia kusali Rakaa nne na katika manuizi yako unanuia maamuma japo unajua Imam ana mushkeli fulani, au una yakini hapa ninaposali haruhusiwi Imam au Sheikh Mwengine kusalisha, isipokua awe mtu wenu, hiyo ndio Sala ya Msikitini, ambayo sio mbaya ila utalipwa kama (indivisual) na sio Jamaa.
Halafu kuna aina nyengine ya Sala ambayo leo tutapiga mbizi ili tuogelee kwenye hii Sala ya Jamaa tuone ikoje Sala hii halafu utaamua mwenyewe unataka kusali sala ya msikitini au sala ya Jamaa, uamuzi ni wako wewe, basi kabla ya kuchupa kwenye bahari hiyo wacha tupate faida mbili tatu za baadhi ya mambo ili upate kujua, usije ukakatazwa usifanye kumbe vina faida na wewe.
Kuna baadhi ya makatazo unakatazwa na wewe bila ya kufikiria unayakubali hata hujiulizi ni faida yake, kama kutia nia kuna clip zinasambazwa kukataza jambo hilo, sawa hatukatai lakini wacha na sisi kabla ya kukataa tuangalie kwanini jambo hili lililetwa?.
Endelea Part 2
Friday, June 15, 2018
SALA YA JAMAA PART 2
Asalaam Aleyikum
Naam nini Nia?, Nia ni kusudio la kutenda jambo, sasa swali wapi kusudio hili linaishi na vipi linakuja mpaka likawa hai?. Tendo hili la Nia linaishi kwenye (Moyo) hiyo ni kwa lugha nyepesi, Kwa lugha ngumu tutaita kwenye (Roho) au lugha ya sayansi tuite (Subconscious)yako.
Ndio Maana hadith maarufu ya (Mtume s.a.w)ikasema "Hakika ya Amal yoyote ni kwenye Nia yako", Unaweza kuingia kwenye Ibada bila ya kutamka chochote, hiyo ni sawa na vizuri sana, lakini kufanya hivyo kuna shuruti lazima wewe uwe katika wale wenye kutajwa wanamkumbuka Mollah wao wakiwa wamesimama au kukaa au wamelala, hao wanaweza kufanya Ibada zao bila ya manuizi, kwa sababu wao wakati wote wako pamoja na Mollah wao, lakini matatizo yanakuja pale mimi na wewe ambao nusu tumelala na nusu tuko macho, sisi nini tunatakiwa tufanye inabidi tuamshwe, ndio ikawekwa Adhana, kukumbushwa wakati wa sala, halafu inatubidi mimi na wewe tukurupuke sio kama hatujijui ila tunafanya manuizi ili kuunganisha (subconscious na conscious)kumbuka dakika tano zilopita ulikua pengine unatizama mpira au kusikiliza nyimbo, kwa hiyo ili uipate Sala yako kikamilifu unaondoka kwenye (Conscious)ya kusikiliza mazungumzo unaipeleka kuungana na kile kilichokuja kika kukumbusha sasa hivi kusali, ikiwa utakwenda kwenye sala bila ya kujipiga nyundo, na hivyo ndio unavotakiwa ufanye kutokana na mfundisho ya kuto kunuia, basi utajikuta kwenye hiyo Sala hujajisaidia chochote ila unaendelea kufunga mahesabu, au unapanga miadi au unaendelea kusikiliza nyimbo ndani ya sala, unapata upande sala upande nyimbo au mazungumzo.
Nikisema hivyo bado wengine watakua na wasiwasi wa jambo hilo, basi wacha nitoe mfano wa Msahafu au juzuu nzima unayo umehifadhi, unakwenda Msalani au(Chooni)haziji zenyewe zile sura mpaka utake kuzisoma, zipo (somewhere)lakini wakati ule huzihitaji kwa hiyo haziji kwenye (Conscious)yako mpaka utake.
Sasa Ulimi unahusika vipi?, ipate darsa hii ili upate kufahamu vizuri kwanini unatia nia tena kwa sauti, na hao waloleta waligundua nini katika hili?. Ulimi kwa njia ya kuitamka (Nia)una kazi mbili, Kazi ya kwanza unaiamsha Akili yako kukaa tayari kwa Ibada, kwa sababu huwezi kusema huku ukawa unafikiri, lichunguze hilo utabaini mwenyewe, Na jambo la pili kujulisha viumbe vyengine (Kama Malaika)na vyengine avijuavyo Mollah wako kwamba sasa wewe unaingia ndani ya Ibada, Ulimwengu na vilivyomo vinakusikia(Napenda uelewe sauti yako inabaki milele haipotei kabisa) Ndio maana utaona kwenye Ibada zote tunatoa sauti, ingekua Ulimi hauna nafasi basi kwenye Sala ilikua haina haja ya kutamka chochote, ila tungesema (Hakika ya Ibada zetu kwenye nia) hapa sina haja ya kupinga kauli zote mbili nazikubali za kutamka na kuto tamka zinakubalika na wala hazina mushkeli inategemea na daraja yako upo katika (Level)gani ya Kumkumbuka Mollah wako, Na wala hakuna makosa katika hilo.
Halafu kabla ya kuingia katika hiyo Sala ya Jamaa unaingia katika jambo la pili, kumbuka jambo la kwanza ni nia, Na hili la pili ni (Tohara Udhu), kusafisha Mwili wako kwa ajili ya kwenda kuungana na Mollah wako.
Na katika Udhu kuna mazingatio makubwa vile unavojisafisha kiwiliwili chako, inokwenda kusali ni Roho yako, lakini vipi utakwenda wewe na guo lilochafuka kwa Mollah wako, ndio hapo unaingia Udhu, unasafisha Mikono (Symbolic) kama kiwiliwili hichi kimeshika vya haramu, au Uso na macho vimeona vya haramu, au miguu ilipita au kwenda kwenye haramu, au masikio yalisikia vya haramu sasa mimi najisafisha ili kusogea na kuungana na Mollah wangu nikiwa safi. Sasa tutaingia katika sala Ya Jamaa,
Endelea part 3
Naam nini Nia?, Nia ni kusudio la kutenda jambo, sasa swali wapi kusudio hili linaishi na vipi linakuja mpaka likawa hai?. Tendo hili la Nia linaishi kwenye (Moyo) hiyo ni kwa lugha nyepesi, Kwa lugha ngumu tutaita kwenye (Roho) au lugha ya sayansi tuite (Subconscious)yako.
Ndio Maana hadith maarufu ya (Mtume s.a.w)ikasema "Hakika ya Amal yoyote ni kwenye Nia yako", Unaweza kuingia kwenye Ibada bila ya kutamka chochote, hiyo ni sawa na vizuri sana, lakini kufanya hivyo kuna shuruti lazima wewe uwe katika wale wenye kutajwa wanamkumbuka Mollah wao wakiwa wamesimama au kukaa au wamelala, hao wanaweza kufanya Ibada zao bila ya manuizi, kwa sababu wao wakati wote wako pamoja na Mollah wao, lakini matatizo yanakuja pale mimi na wewe ambao nusu tumelala na nusu tuko macho, sisi nini tunatakiwa tufanye inabidi tuamshwe, ndio ikawekwa Adhana, kukumbushwa wakati wa sala, halafu inatubidi mimi na wewe tukurupuke sio kama hatujijui ila tunafanya manuizi ili kuunganisha (subconscious na conscious)kumbuka dakika tano zilopita ulikua pengine unatizama mpira au kusikiliza nyimbo, kwa hiyo ili uipate Sala yako kikamilifu unaondoka kwenye (Conscious)ya kusikiliza mazungumzo unaipeleka kuungana na kile kilichokuja kika kukumbusha sasa hivi kusali, ikiwa utakwenda kwenye sala bila ya kujipiga nyundo, na hivyo ndio unavotakiwa ufanye kutokana na mfundisho ya kuto kunuia, basi utajikuta kwenye hiyo Sala hujajisaidia chochote ila unaendelea kufunga mahesabu, au unapanga miadi au unaendelea kusikiliza nyimbo ndani ya sala, unapata upande sala upande nyimbo au mazungumzo.
Nikisema hivyo bado wengine watakua na wasiwasi wa jambo hilo, basi wacha nitoe mfano wa Msahafu au juzuu nzima unayo umehifadhi, unakwenda Msalani au(Chooni)haziji zenyewe zile sura mpaka utake kuzisoma, zipo (somewhere)lakini wakati ule huzihitaji kwa hiyo haziji kwenye (Conscious)yako mpaka utake.
Sasa Ulimi unahusika vipi?, ipate darsa hii ili upate kufahamu vizuri kwanini unatia nia tena kwa sauti, na hao waloleta waligundua nini katika hili?. Ulimi kwa njia ya kuitamka (Nia)una kazi mbili, Kazi ya kwanza unaiamsha Akili yako kukaa tayari kwa Ibada, kwa sababu huwezi kusema huku ukawa unafikiri, lichunguze hilo utabaini mwenyewe, Na jambo la pili kujulisha viumbe vyengine (Kama Malaika)na vyengine avijuavyo Mollah wako kwamba sasa wewe unaingia ndani ya Ibada, Ulimwengu na vilivyomo vinakusikia(Napenda uelewe sauti yako inabaki milele haipotei kabisa) Ndio maana utaona kwenye Ibada zote tunatoa sauti, ingekua Ulimi hauna nafasi basi kwenye Sala ilikua haina haja ya kutamka chochote, ila tungesema (Hakika ya Ibada zetu kwenye nia) hapa sina haja ya kupinga kauli zote mbili nazikubali za kutamka na kuto tamka zinakubalika na wala hazina mushkeli inategemea na daraja yako upo katika (Level)gani ya Kumkumbuka Mollah wako, Na wala hakuna makosa katika hilo.
Halafu kabla ya kuingia katika hiyo Sala ya Jamaa unaingia katika jambo la pili, kumbuka jambo la kwanza ni nia, Na hili la pili ni (Tohara Udhu), kusafisha Mwili wako kwa ajili ya kwenda kuungana na Mollah wako.
Na katika Udhu kuna mazingatio makubwa vile unavojisafisha kiwiliwili chako, inokwenda kusali ni Roho yako, lakini vipi utakwenda wewe na guo lilochafuka kwa Mollah wako, ndio hapo unaingia Udhu, unasafisha Mikono (Symbolic) kama kiwiliwili hichi kimeshika vya haramu, au Uso na macho vimeona vya haramu, au miguu ilipita au kwenda kwenye haramu, au masikio yalisikia vya haramu sasa mimi najisafisha ili kusogea na kuungana na Mollah wangu nikiwa safi. Sasa tutaingia katika sala Ya Jamaa,
Endelea part 3
SALA YA JAMAA PART 3
Asalaam Aleiykum
Nini Jamaa?
Jamaa maana yake ni ku(Unified oneness together) kwanini ikawa hivyo, Quraan (An Nisai aya 1).
يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّاسُ ٱتَّقُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِى خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٍ۬ وَٲحِدَةٍ۬ وَخَلَقَ مِنۡہَا زَوۡجَهَا وَبَثَّ مِنۡہُمَا رِجَالاً۬ كَثِيرً۬ا وَنِسَآءً۬ۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِى تَسَآءَلُونَ بِهِۦ وَٱلۡأَرۡحَامَۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَيۡكُمۡ رَقِيبً۬ا
"Enyi Watu Mcheni Mollah wenu ambaye amekuumbeni katika Nafsi Moja, Na akamuumba mkewe katika nafsi ile ile, Na akaeneza Wanaume wengi na Wanawake kutoka katika wawili hao, Mcheni Mwenye enzi Mungu ambaye kwake (Mnaomba)Mnaombana, Na Muwatazame Jamaa, Hakika Mwenye enzi Mungu ni Mlinzi juu yenu".
Vipi inakua, nakupa nafasi ili na wewe uijue Sala ya Jamaa kwa njia ya Tawhid, Nyinyi jiangalieni kwanza kwa njia ya nje vipi mlivo fanana hakuna tafauti, uwe mweupe au mweusi uwe kabila au dini yoyote lakini nyote mefanana katika Maumbile, Wanaume wako sawa na Wanawake wote wako sawa, Na hali hiyo hiyo ndani yenu pia Meungana kama Nafsi moja ila hamjachunguzana, kama utajaaliwa kupewa macho ya Mcha Mungu ukaiona Miujiza ya Roho utaona kumbe sote tuna Nafsi Moja, Kumbe mimi na yule ndani yetu ni kitu kimoja.
Mollah wetu huyo huyo Mwenye Kuamrisha wewe uzaliwe na Kufa ndie Yeye Mwenye kuamrisha Mwengine azaliwe na kufa kwa njia hiyo hiyo, Nani Mwenye kukupa Wewe uwezo wa kuona ndio alompa Jirani yako, ndugu yako, rafiki yako, Mzee wako uwezo huo huo wa kuona na kusikia, Nani Mwenye kutupa sote kwa pamoja uwezo wa Kuhema bila ya Amri yetu isipokua yeye Mollah wetu anatupa kwa pamoja tunahema bila ya masharti sote tukiwa chumba kimoja, pumzi ndani pumzi nje, nini habari yetu sisi kama zitazuiliwa zisije tena.
Hiyo nakupa kwa uchache ili upate kujua kumbe sisi wanaadamu sote ni (One Unity)ulichokua nacho wewe na mwenzako ana hicho hicho, ukishagundua hilo basi kuna mabadiliko yatatokea katika Nafsi yako, Na Wakati huo ndio utajua kwanini unasali Sala ya Jamaa. Utaelewa Umuhimu wakuwa na Imam Muadilifu, utatambua vilevile Wakati unasali Sala za Eid, au Sala ya Alfajiri, Magharib na Isha umuhimu wa kuitikia Amin, utaiona vipi Aamin yenu inavofungika na kutoka kwa pamoja na mkanyamaza kwa pamoja bila ya kufanya (mazoezi) yoyote ya jambo hilo.
Vipi utajua Umeipata Sala ya Jamaa pale Fikra zitakapotea, Moyo utakapo jaa ghushuu, na kama Sala ya kutoa Sauti utaona unaisikia kwa njia ya Moyo sio kichwani, na Kama ikenda (Deep)utaona machozi yanakulenga lenga, hapo utajijua umeipata Sala ya Jamaa na hata ikimalizika huna haja yakutoka mbio Msikitini bado (Energy)ya Sala iko na wewe, na hata ukitoka bado unaendelea kuwemo katika hali ya Ucha Mungu. Ukiyapata hayo ndio inakua Sala imekutokezea wewe kwenye Nafsi, Na ndio inaweza kukuepusha Na Machafu, Madhanbi, Viburi na mengineyo hapo ndipo utafahamu nini Tafauti ya Sala ya Msikitini na Sala ya Jamaa.
Nini Jamaa?
Jamaa maana yake ni ku(Unified oneness together) kwanini ikawa hivyo, Quraan (An Nisai aya 1).
يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّاسُ ٱتَّقُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِى خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٍ۬ وَٲحِدَةٍ۬ وَخَلَقَ مِنۡہَا زَوۡجَهَا وَبَثَّ مِنۡہُمَا رِجَالاً۬ كَثِيرً۬ا وَنِسَآءً۬ۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِى تَسَآءَلُونَ بِهِۦ وَٱلۡأَرۡحَامَۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَيۡكُمۡ رَقِيبً۬ا
"Enyi Watu Mcheni Mollah wenu ambaye amekuumbeni katika Nafsi Moja, Na akamuumba mkewe katika nafsi ile ile, Na akaeneza Wanaume wengi na Wanawake kutoka katika wawili hao, Mcheni Mwenye enzi Mungu ambaye kwake (Mnaomba)Mnaombana, Na Muwatazame Jamaa, Hakika Mwenye enzi Mungu ni Mlinzi juu yenu".
Vipi inakua, nakupa nafasi ili na wewe uijue Sala ya Jamaa kwa njia ya Tawhid, Nyinyi jiangalieni kwanza kwa njia ya nje vipi mlivo fanana hakuna tafauti, uwe mweupe au mweusi uwe kabila au dini yoyote lakini nyote mefanana katika Maumbile, Wanaume wako sawa na Wanawake wote wako sawa, Na hali hiyo hiyo ndani yenu pia Meungana kama Nafsi moja ila hamjachunguzana, kama utajaaliwa kupewa macho ya Mcha Mungu ukaiona Miujiza ya Roho utaona kumbe sote tuna Nafsi Moja, Kumbe mimi na yule ndani yetu ni kitu kimoja.
Mollah wetu huyo huyo Mwenye Kuamrisha wewe uzaliwe na Kufa ndie Yeye Mwenye kuamrisha Mwengine azaliwe na kufa kwa njia hiyo hiyo, Nani Mwenye kukupa Wewe uwezo wa kuona ndio alompa Jirani yako, ndugu yako, rafiki yako, Mzee wako uwezo huo huo wa kuona na kusikia, Nani Mwenye kutupa sote kwa pamoja uwezo wa Kuhema bila ya Amri yetu isipokua yeye Mollah wetu anatupa kwa pamoja tunahema bila ya masharti sote tukiwa chumba kimoja, pumzi ndani pumzi nje, nini habari yetu sisi kama zitazuiliwa zisije tena.
Hiyo nakupa kwa uchache ili upate kujua kumbe sisi wanaadamu sote ni (One Unity)ulichokua nacho wewe na mwenzako ana hicho hicho, ukishagundua hilo basi kuna mabadiliko yatatokea katika Nafsi yako, Na Wakati huo ndio utajua kwanini unasali Sala ya Jamaa. Utaelewa Umuhimu wakuwa na Imam Muadilifu, utatambua vilevile Wakati unasali Sala za Eid, au Sala ya Alfajiri, Magharib na Isha umuhimu wa kuitikia Amin, utaiona vipi Aamin yenu inavofungika na kutoka kwa pamoja na mkanyamaza kwa pamoja bila ya kufanya (mazoezi) yoyote ya jambo hilo.
Vipi utajua Umeipata Sala ya Jamaa pale Fikra zitakapotea, Moyo utakapo jaa ghushuu, na kama Sala ya kutoa Sauti utaona unaisikia kwa njia ya Moyo sio kichwani, na Kama ikenda (Deep)utaona machozi yanakulenga lenga, hapo utajijua umeipata Sala ya Jamaa na hata ikimalizika huna haja yakutoka mbio Msikitini bado (Energy)ya Sala iko na wewe, na hata ukitoka bado unaendelea kuwemo katika hali ya Ucha Mungu. Ukiyapata hayo ndio inakua Sala imekutokezea wewe kwenye Nafsi, Na ndio inaweza kukuepusha Na Machafu, Madhanbi, Viburi na mengineyo hapo ndipo utafahamu nini Tafauti ya Sala ya Msikitini na Sala ya Jamaa.
Subscribe to:
Posts (Atom)