Tuesday, July 31, 2018

MAAJABU YA UHAI PART 1

Asalaam Aleiykum

Binaadamu tunaishi katika kiza kikubwa cha (Sahau) Ndani ya kiza hiki tunavishana vyeo vya kila aina, vyengine vya utajiri, umasikini, ushujaa, uhodari, na kadhalika lakini tunasahau Udhaifu wetu sisi kuwa hatuwezi kutenda lolote bila kupewa fursa hiyo na Mwenye enzi Mungu. Walimwengu tunajinasibu na mambo mengi tuyafanyao lakini tunasahau kuwa sio sisi wenye kutenda, Na linalotufanya kusahau ni kile kiburi cha sisi kumsahau yule alotuumba akatujaalia uwezo wa kutenda.
Kuna mambo mingi ya mfano ambayo kila ukenda (Deep)kwa kuyatafakari utajikuta kuwa sisi wanaadamu ni viumbe dhaifu kabisa na wenye kumtegemea Mollah wetu kwa kila kitu.
Hakuna kitu chenye kunipa furaha kama nikitafakari na kuisoma sura ya (Al-Qalam)aya ya 1-2, "Naapa kwa Kalamu, Na wayaandikayo (Kwa kalamu hiyo)""Kwa Neema ya Mollah wako wewe si Mwendawazimu".
Sasa nikiangalia Akili naona ni kitengo maalum cha Mwanaadamu kuwasiliana na Ulimwengu wa Nje, Na hii ni Neema kubwa kutoka kwa Mollah wetu, Na wala haukua huu ni wenda wazimu, ila wazimu tunajitia wenyewe pale tunapokwenda kinyume na kuandika yasotakiwa(Ita Dhanmbi, haramu)utaamua Mwenyewe mimi niko naogelea kwenye darsa ya Ajabu ya Maisha na hapa leo nakutana na ajabu hizo ambazo nimechagua ni (Share) na wewe.
Naam Ikiwa Akili kazi yake kuandika na kurekodi, basi lazima vipatikane vitu vyengine vyenye kuwasiliana na Akili(Medium)au vipeleka habari. Ukiwa unakubaliana na mimi tuendelee part 2 tupate habari zaidi ya (Ajabu ya Maisha).

MAAJABU YA UHAI PART 2

Asalaam Aleiykum

Vitu hivyo vyenye kuwasiliana na Akili vimepewa jina na kuitwa ( 5 Sense)"Kuona, kusikia,kutaste,kunusa na kugusa" vyote hivi vina(Report)kwenye Akili, Akili kazi yake kuandika au kurecord, Sasa ikiwa Akili inapelekewa kila kitu ina maana Akili ni nyenzo kama nyenzo nyengine za kutendea kazi katika Mwili wako, Tukiweza kuitenga Akili au kuiweka pembeni lazima tukubaliane kuzifata hizo (Sense)tujue nazo zinapata wa nguvu au uwezo wa kuripoti kwa Akili.
Inatubidi tujiulize nini (Source) yake, iweje hata tunaweza kuona, kusikia, kuhisi,kugusa,kutest, ni lazima kuna (Original source)ambayo inatoa (Command) hizo, na kama ipo basi itakua ndio inotuma (Massage) kwenye (Sense) na (Sense) ndio inapeleka (Massage) kwenye Akili, Na ni lazima hii (Source) iwe (Advance) kuliko (Sense) kuliko Akili yenyewe, kazi kubwa Mwanaadamu inatakiwa uifanye kuijua hii (Original source) Na Maajabu ya hii (Source)daima imejificha.
Ukiweza kuifahamu hii (Source), kwanini nikasema kuifahamu, kwa sababu ningesema kuijua ingebidi nitumie Akili, vitu vyote vinojulikana unatumia Akili, lakini visivojulikana inatumika Fahamu, ndio maana yakaitwa Maajabu, kuna vitu vinatokea havikai kwenye (Memory) unashangaa ilikuaje ikatokea vile, hesabu, maana zote zinapotea, huna (Reason) kabisa ya kuhusisha kilochotokea na maisha ya kawaida unabaki kunyamaza kimya huko ndiko kufahamu.
Ukiona unajua basi hiyo imetokea katika dunia ya Akili, kumbuka siku zote kujua kumehusiana na Akili. Naam Kwa hiyo hicho ninachozungumza sio cha Ulimwengu huu, hiyo (Source) huwezi kuigusa, huwezi kuiona, huwezi kuihisi lakini unafahamu hii (Source) ni Mimi, kama vile ukiamka unavojifahamu nimeamka, lakini cha ajabu ukilala hujifahamu kama umelala?, unajua kwanini kwa sababu ukiamka unatumia Akili kujua kuwa umeamka, mara moja moja ukiamka ghafla, au umeshituka bado hujawasiliana na Akili utajikuta unajiuliza mie nani, niko wapi hapo hujapata (Contact) ya kujua, lakini unajifahamu mie kitu fulani(The Being).
Sasa utatupa shida ukitaka tukufahamishe wewe nani, kwa sababu wakati unalala (Sense) zinaondoka lakini wewe uko pale pale.
Endelea Part 3

MAAJABU YA UHAI PART 3

Asalaam Aleiykum

Binaadamu ukipata bahati ya kwenda (Beyond) ya viwili hivyo utafika pahala yaani (Akili na Sense) utapata maarifa ya kuwa (Super Being) kwanini nikasema maarifa kwa sababu Akili haipo tena, sense hazipo tena, unabahatika wakati Mwengine kwenye usingizi wako, ukajiona unapaa unakwenda sehemu za ajabu lakini kama nilivosema unakua hujui nini kimetokea, hujui ni kweli au ndoto, lakini umeona mambo ya ajabu na unashindwa kuyaeleza, na tafauti ni hii ukiweza kuhadithia basi ujue ni ndoto, na ukishindwa kuhadithia basi ni hiyo daraja ya (super being).
Mambo hayo hayo unayaokutana nayo yakawa hayana maelezo, hujui useme nini na hayo hayo yako kwenye huu mfano hai, ambao kwa sasa unafahamu unaishi lakini hujui (Source)yako ya maisha, hujawahi hata siku moja kufanya maulizo ya maisha yako, wewe na mnyama mnaishi sawa sawa, tafauti moja mnyama hajui kama atakufa wewe unajua, lakini hujapata kujiuliza nini haya maajabu ya uhai, nini (source)yake kwanini na lala nikiamka?.
Ukipata Ushujaa wa kuanza kwenda katika maulizo hayo ya nini uhai, ndipo utajikuta kwamba wewe sichochote, unaishi ndani ya hiyo "(Qadir)ya Mwenye enzi Mungu alosema akitaka jambo liwe linakuwa". Utaanza kujua kidogo kidogo kumbe mimi hata uwezo wa kuhema sina ila Mwenye enzi Mungu wangu ndio Mwenye kunifanyia Neema hii ya kuvuta pumzi, utauona udhaifu wako, hata kuzaliwa kwako utaelewa kuwa umeletwa hapa duniani, utaacha kufanya (Birthday)zote, utashangaa ukijua kumbe kukutana kwa watu wawili kwa njia ya mapenzi ndio limetokea tukio la mimi kuja Ulimwenguni humu. Utafahamu uzuri zaidi ikiwa pumzi mpaka atake Mwenye enzi Mungu basi na huo Utajiri au Akili ulizonazo basi (Source)yake ni Mwenye enzi Mungu, yeye ndio anosababisha kila jambo katika Ulimwengu huu.
Ukiona unajenga majumba, unasaidia Maskini, unanunua magari basi ujue sio wewe kuna (Source)inayokuwezesha ili uwe hivo, Kwa Mapenzi ya Mollah wako umechaguliwa wewe kwa muda kushika madaraka hayo, ndio maana kuna msemo (Tumekuja bila ya kitu na tutaondoka bila ya kitu).La Muhimu (Find yourself) halafu ishi katika (Being)yako, hapo ndio kwenye makaazi ya Taqwa, hutegemei Akili tena katika kuishi ila Unamtegemea Mollah wako, hapo Kiburi kitaondoka, chuki haikai tena, Tamaa huna tena, mahitaji ya dunia utayapa mgongo, na kila kitakachotokea utakua unajua kwa uhakika kimetoka kwa Mollah wako na utakua Mwepesi wa kupokea, utakua umeunganisha maisha yako baina ya Ardhi na Mbingu una (Dis-Appear) ungali uhai, na hiyo ndio (Bliss).