Friday, May 9, 2025

NYUMBA YA ROHO

 Asalaam alekum 

Mwanaadamu ana usingizi wa aina mbili, usingizi wa kwanza ni wa kimwili halafu wa pili ni wa kiroho(Japokua Roho hailali)inayo lala ni (BODY)yako tu. Sasa leo itabidi tujiulize swali, kwani Roho ina nyumba?.Jawabu ndio Mwili wa binaadamu ndio Nyumba yake. Kivipi inakua huu mwili ni nyumba?. Kulijibu swali hili inabidi tuiangalie sayansi na maendeleo yake, tumeshuhudia katika zama hizi za karibuni vipi elimu ya (A I) ilivo fanikiwa kutengeneza (Robot) ambalo lina uwezo wa kufanya kazi zote zinazofanywa na Binaadamu , katika hilo kuna mazingatio makubwa kwa wenye Akili kulitizama kwa undani. Imefika wakati wana sayansi wadini tutoe maelezo ambayo yapo karne nyingi lakini tulikua hatuelewi. Inabidi sasa niseme hata wewe huo Mwili wako ni (Robot)Lakini ilotengenezwa na Mbora wa kuumba (Mollah)wako, Na yeye ndo alotupa Elimu hii ya kuweza kutengeneza hawa (Ma Robot) tafauti yake yetu tunatumia chuma na hii ya mwili wetu imetumika (living organism), kuelewa hayo inabidi kwanza uamshwe kiroho kwa kutumia akili uelezwe kwamba wewe na huo Mwili wako ni vitu viwili tafauti. Mwili ni Jumba lilo na cheo kutukufu ambacho kakiumba Mwenye enzi Mungu kwa uwezo wake Mkubwa, vitu vyote katika Mwili huo vinafanya kazi yake (Automatic)bila ya wewe kuingilia kati kwa chochote kile na vyengine bila wewe hata kujua, kuvuta kwako Pumzi (Automatic) unakula chakula ukishatia Mdomoni yalobaki yote (Automatic) mpaka kwenda kwako chooni (Automatic)Unatoa sumu mwilini (Automatic) Mpaka hiyo (Sex)unayo ipenda ni (Automatic)Kazi nyingi katika hiyo (BODY) yako ni (Automatic)kwa sasa huwezi kuelewa mpaka ukae kwa utulivu na ukimya na mazingatio makubwa ndio utaweza labda kunielewa na huenda ukapata kwa uchache maarifa ya kujua maelezo yangu. Ukijua Maelezo yangu moja kwa moja utagundua hili Jumba ninalo Ishi ndani yake Mollah kalipangia muda wake, akatupa (Hint) kutudokeza tutakupeni nyinyi kuishi katika jumba hilo kiasi cha umri wa miaka 60 halafu tuta kuongezeni (Bonus)miaka 10 itakapo pita hiyo miaka 70 na ukaanza kuingia 80 basi hapo tena elewa baada ya hilo jumba kuitumikia Roho kwa muda wa miaka sabini sasa itakua zamu ya Roho kulitumikia Hilo Jumba, kwa njia gani? Mwanzo niliposema Roho ipo kwenye usingizi nikasema hailali sasa ule usingizi unaondoka na roho inaanza kutumika, na utumwa wa Roho ni kule nyakati zote kua (Alerts)nikupe mfano unapokua na afya Akili haijui nini Afya, jumba liko zima unaendelea kujitafutia mali , kufanya uharibifu, unafanya maasi ya kila aina, unakunywa pombe , unakula rushwa, unatesa wenzio, unjifaharisha na kila kitu, hukumbuki chochote umelala Kiroho, lakini subiri unaposhikwa na Maradhi umwa kidole au jino (Automatic Mode) inaondoka unaanza kuishi kwenye Roho, hapo ndio unajua tafauti yako na huo Mwili, hapo ndio unaweza kutafautisha baina ya wewe na huo mwili, wakati wote jino lilikuwepo , kidole kilikuwepo lakini ulikua huna habari, lakini Maradhi ndio yanakuzindua , yanakutoa usingizini, mpaka pale ukipewa dawa ukapona unarudi kwenye usingizi wako unaendelea kuyachapa maisha kama kawaida, sasa kwa watu wazima (BODY) haisikii tena dawa , maumivu yanakua yanaendelea Roho inatumikia mwili hakuna tena furaha ndio maana tabu sana kumkuta Mzee wa miaka 80 ana furaha ya kuendelea kwa sababu (constantly) yupo kwenye (alert)ya Maradhi wachunguze watu wazima utalijua hilo mambo ni (vice versa) Ni wakati wa Roho kutumikia Mwili , kwa hiyo utagundua sasa (full awareness)imepatikana kuwa sasa unaishi ndani ya (BODY)na una (Experience)kubomoka kwa jumba lako ambalo limemaliza muda wake wa kuishi. Ukiwa Mja Mwenye Akili utagundua sasa hivi wewe ni Mwenye Nyumba ila unatawaliwa na wapangaji. Katika Jumba hilo Mollah kakupa neema nyingi sana leo ntakutajia kwa uchache.

NYUMBA YA ROHO

 Umepewa Neema 5 mpaka kwa 6 labda nikikutajia utazinduka usingizini na kujijua wewe nani?. Sasa nakutaka ukumbuke hili, hilo jina sio wewe, wazee wamekupa ulipozaliwa ili wapate kukutambua, umepewa (Tag)ili watu wengine pia waweze kujua, kwa hiyo usije kudanganyika ukadhani wewe ni (Abdulla Au Khamis au Juma)wewe ni kitu chengine kabisa, nia yangu nakutaka ukitafute ujijue wewe nani, fanya hima ukijue kabla siku yako ya kufa ikifika siku hiyo utakua umeridhika kurejea kwa Mollah wako. Sasa wacha nikuoneshe njia labda huenda ukajiona au kujijua wewe nani?, Nakutaka uchunguze katika kadhia ya usingizini wako, baina ya kulala na kuwa macho (body machenism)inafanya tokeo la kuhamisha kutoka kwenye (Uko macho)kwenda katika hali ya( kulala)au kwa lugha ya kigeni(conscious to unconscious)ufanye uchunguzi mkubwa, inatakiwa jitihada ili wakati ule (Body)ina( Transfer from waking to sleep)jitahidi hapo mambo yanatisha lakini ukifanikiwa utabadilika kabisa, utakua mtu mwengine kabisa, utasema kumbe mimi ndio huyu hapo (Your being Reveal)hapo ndipo utakapojijua kumbe mimi ndio Roho, utajiona kama unavojiona kwenye kioo, tafauti yake kwenye kioo unaona body, baina ya usingizi na macho unajiona wewe Roho na mwili mko tafauti, hilo linawezekana usiogope fanya mazoezi hayo baada ya miezi 3 (New You) utakua mtu mwengine kabisa. Utajiuliza kwanini nikataja mambo haya?, Kwa sababu niliposema huu mwili ni (Robot)pengine wengine watakua ((upset)nimewakera kidogo, labda wanatembea mabega juu, labda mtu ana cheo au tajiri halafu ajione kumbe yeye ni jumba la (Robot)na atakapo kufa linarejea kwenye mchanga,dhumuni langu Acha kujigamba na udongo tafuta (Diamond within you)niliposema (Robot) nilikua naashiria kuwa Wewe ni (living organism) Umeumbwa na Mwenyewe aliye mtukufu mbora wa Uumbaji kakuumba na kitu (Self intelligence)kubwa ikisha akakuweka wewe kwenye Jumba hilo uishi kwa miaka 60 au zaidi kama alivokupangia. Kwenye Nyumba hiyo akakupa Neema ndani humo ukawa unazitumia bila ya kutoka kwa miaka yote unayoishi duniani, Umo kwenye Ufalme wako, kumbuka wewe ni Khalifa wewe ni (Master)Akakupa neema Tano kubwa kabisa ili ziwe mawasiliano yako wewe na (Body)yako pamoja na Ulimwengu ulo kuzunguka. Sasa neema gani umepewa katika jumba hilo?, (1)Umepewa Pua wewe ili upate harufu ya chakula kitamu, upate harufu ya manukato yalo mazuri, vyote hivyo vinatoka nje vinaingia ndani kwako. (2)Ukapewa raha ya Ulimi kuonja na kutest vyakula na vinywaji tafauti vya kila aina, (3)Ukapewa za kugusa(Feeling) na kupata raha na machungu, ikaonekana isitoshe (4)Ukapewa uzuri wa kusikia na huku kusikia elewa husikii kutumia sikio, sikio lako ni chujio tu ila kusikia ni njia nyengine kabisa ambayo hiyo na (5)Kuona ndio viko karibu zaidi na hiyo Roho yako, Kuona ni kitu Adhimu sana kilichopo karibu na Roho ili upate Ku (Experience) hii Dunia yako ambayo unaishi. Hizo ndio neema za Mwenye enzi Mungu kwako wewe Baba Mwenye Nyumba, Sasa ikiwa utafanikiwa kujijua wewe ni Roho sio kwa kuhadithiwa bali kujitambua mwenyewe kuwa mimi Naishi Kwenye Nyumba hii mvua ikinyesha hainipati, maumivu yakija yanaishia kwenye Nyumba, fikra zote hazinigusi zinaishia kwenye nyumba, hata mtu akinitukana anatukana nyumba ila sio mimi basi utajiandaa kwa mtazamo mwengine hususan ukijua au kuona Nyumba yenyewe ishaanza kuchakaa, nyumba yenyewe karibu itabomoka, msingi ushachoka magoti milingoti hii inauma au kuanza kutetemeka na sio imara tena, Maradhi ndio yanaanza kulishambulia Jumba lako ukilizingatia hilo ukajua kuwa nyumba hii ikibomoka natakiwa nirudi nilipotoka Kwa Mollah wangu aliyeniumba, swali unalotakiwa ujiulize narejea vipi kwa yule aliyeniumba ambaye amesema kila tendo ameshapitisha lilofanywa duniani lazima lilipwe, liwe la shari au kheri ni lazima ama kwa bahati mpaya yeye Mwenyewe ndio ataamua ama kwa lile la kusudi ujue lazima yafanyike malipo na hiyo ndio Hukumu iliyokatwa, kitacho kunusuru wewe ni kuzidi kwa yale yenye kheri ulowatendea wanaadamu wenzio sio kujenga majumba au kuchangia michango mikubwa mikubwa, kumbuka kinacho hesabiwa huko ni vitendo vya mbinguni vyenye kuhusu Roho. Unatakiwa wewe kama Roho ujiulize maswali haya?, wapi nimekosea , kwanini siwezi kujirekebisha, Tatizo liko wapi?, Utakumbuka niliposema Macho ndio yapo karibu na hiyo Roho, na ndio msingi wa maisha na ku (Experience)hii Dunia, ambayo ukichanganya na Akili utakuta viwili hivyo vyote ni sehemu ya hiyo Nyumba. Sasa tatizo limeanzia wapi ? , Tatizo kuna Kiumbe kiliingia kati akasema kutumia sauti ikisha akatuonesha Jambo ndio ikawa sababu yetu sote mpaka leo tumekuwa wateja(Addict) ukiangalia vizuri (Addiction) ziko za aina mbili moja hii ya nje ambayo tuinaona ya (Drugs)Na nyengine hii ya ndani ambayo hatuioni kila mmoja wetu anayo tokea tuliponjeshwa hakuna mwenye kuvuka isipokua atake Mollah wako au kwa jitihada zako utakapo kugundua wewe Roho una thamani zaidi na inakubidi uachane na uteja huu wa Maasi. Sasa ulianzia wapi uteja huu wa Ndani? Soma kwa utaratibu ili upate kujua dhanmbi hii ya kudumu imekugusa vipi wewe binafsi na jee ina epukika?

NYUMBA YA ROHO

 Dhanbi hiyo imetajwa ndani ya Quraan sura ya Al-Aaraf kwenye aya ya 20 mpaka aya ya 22 "Pale Shetani alipowafata (Nabii Adam a.s na Bibi Hawa)Alifanya nini Shetani ", Ukisoma kawaida utaona kawatia ushawishi wakala Tunda mara wakaona tupu zao, wakajiona wako (Uchi)Wakajifunika majani, Wao walikua wanaishi (Innocent)Mpaka Shetani alipokwenda akawavua (Guo Lao la Utiifu)Guo la Ucha Mungu, alifanya nini?, Jambo la kwanza alizungumza nao (Wakasikia)akawaambia na (Kuwaonesha)huo mti akazipata (Senses)Mbili za kusikia na kuona akawaambia kuleni ili mpate kuishi milele kwenye Raha hizi za Peponi au mpate kuwa Malaika, wakaenda kuushika na kuipata (sense) ya tatu na wakamalizia (Sense)ya Nne ya kula na kuonja ladha yake, wakakamilisha (sense)ya tano ya Harufu ndipo wakaamka kiroho (Au) niite (six sense). Kama umefahamu uzuri utajua tunda lilikua mtego wa kutizamwa Utiifu wetu au ita (Taqwa)Kwa Mollah wetu, tumeshindwa vibaya sana mpaka leo tunaendelea kushindwa, umekua mtihani mkubwa na kila Jambo ulifanyalo limefunikwa na kitu(Sex).Sasa guo lenyewe ni huo utiifu ulovikwa na Mollah wako lakini tumelivua sisi wenyewe kutoka kwenye Roho, likivuliwa guo hilo la Ucha Mungu utiifu unaondoka na wewe unahamia kwenye Akili, hapo tena unaendelea kuteseka mpaka utake Mwenyewe kulivaa tena hilo guo la utiifu hapo tena ndio linaitwa Taqwa, maana umelivaa kwa mapenzi yako ili kurudi kwa Mollah wako ukiwa Umetubu. Hiyo ndio Taqwa mwanzo ulivishwa na Mollah kwa mapenzi yake kwako na sasa unatakiwa ulivae Mwenyewe kwa ajili ya mapenzi kwa Mollah wako , huku ukijua Mollah wangu nimekuasi sana kwa umri ulonipa wa miaka 20 ama 30 au sasa nimefikia 60, ukilikumbuka tu kulivaa guo hilo basi hapo hapo ushaanza kupata (Transformation)sasa utaanza kuwapenda na kuwalisha maskini, utatunza mayatima, na vyote utakavyoruzukiwa utajua si vyako peke yako ila utatumia na wenzako, Usione naandika ukaona hiyo ni kazi Rahisi, Inatakiwa ifanyike kazi kubwa ili uweze kupigana na nafsi yako ambayo inaongozwa na Akili. Unatakiwa uwe na uwezo wa kui (control) Akili yako, ukiweza kulifanya hilo kitu cha mwanzo utajiona Mwenyewe na unatekeleza Amri zote za Mwenye enzi Mungu ukidumu katika hali hiyo kwa Mara ya mwanzo utajikuta umeanza kulivaa guo la ucha Mungu tena na unakwenda (Beyond Mind) na ukenda (Beyond) mfano wake kama umesahau Jambo, usishtuke hujapoteza Akili ila sasa (Source)Yako inakua (Direct )Kutoka kwenye Roho na wala haipitii kwenye hiyo nyumba, utakua unaona mambo (In Clarity)Utakua sasa unatumia hiyo wanoita (Six sense)Na ukianza kutumia hiyo (Sense)YA sita utajua kwa dalili hizi unaanza kuwa mkimya, hasira zinaondoka, utakua mpole, hapo tena mambo yanafunguliwa kwako na utaanza kufahamu wewe sio (Body)Nyumba yako ila ni kitu chengine tafauti, na hapo ndio utajua (You belong to know one and know one belong to you) utapata maarifa hata hii (Body)Nayo siku ya kufa naondoka naicha tunakua (separate)Kwa hiyo itakujia hekima huu Mwili nimepewa kama nyenzo ya kufanyia kheri na Ibada kwa ajili ya yule Aliyeniumba, basi ukielewa hivyo utakua umepata ufunuo huikumbatii tena dunia kwa Maasi na kula haram, kula Rushwa ,Kufanya Machafu, kujikusanyia mali , utapata uelewa umekuja na (Nothing) na utaondoka na (Nothing) ( In between) kila kitu Muachie Mungu utaona vipi unafunguliwa mambo usivotegemea ,Riziki zinakuja bila kutegemea au kutarajia na maisha yote yanakua furaha juu ya furaha Mpaka mwisho wako wa Uhai.