Tuesday, July 5, 2016

WAFALME WA PEPONI PART 3

Asalaam Aleiykum

(Quraan Baqarah aya ya 201)
وَمِنۡهُم مَّن يَقُولُ رَبَّنَآ ءَاتِنَا فِى ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةً۬ وَفِى ٱلۡأَخِرَةِ حَسَنَةً۬ وَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ
"Na Miongoni mwao wako wasemao Mollah wetu tupe mema duniani na (Tupe)Mema Akhera, Na utulinde na adhabu ya moto".
Kauli ni ile ile Mollah wangu nibariki kwa mambo mazuri hapa duniani(Blessing)na huko Akhera, Ikisha niepushe na adhabu ya moto, na unapoepushwa na adhabu ya moto kinachofatia ni kupewa au kuingizwa kwenye huo ufalme wa Mwenye enzi Mungu. Hao ndio watorithi Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Sasa tuwatizame warithi wenyewe ni Maskini wa aina gani?, (Usije ukadhani ni wale omba omba) Walotajwa ni wale Maskini wa Roho wenye kutafuta utajiri wa kumjua na kumpenda Mollah wao, Hao ni Maskini wa Ibada, Maskini wa kufanya mambo ya kheri, maskini wa Mapenzi, Maskini wa Huruma, Maskini wenye Uchu wa Kumkumbuka na kumtii Mollah wao, Maskini walokua hawana Kiburi, Maskini wenye hamu kubwa ya kumjua Mollah wao, Maskini ambao wakati wote wamo kwenye Dunia lakini mawazo na fikra zao zote wamejishughulisha kumkumbuka Mollah wao.
Hao ndio walochagua (Both) Dunia na Akhera, na ndivo inavotakiwa, ndivo ilivosema Quraan, ukiweza kufanya hivyo nini kinatokezea? (Quraan Ahqaf aya 13-14)
"إِنَّ ٱلَّذِينَ قَالُواْ رَبُّنَا ٱللَّهُ ثُمَّ ٱسۡتَقَـٰمُواْ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ "
Hakika wale waliosema Mollah wetu ni Mwenye enzi Mungu kisha wakatengenea(Kusimama kwenye kufanya yalo haki)hawatakua na hofu na wala hawatahuzunika.
"أُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَصۡحَـٰبُ ٱلۡجَنَّةِ خَـٰلِدِينَ فِيہَا جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ "
Hao ndio watu wa Peponi, watakaa humo (daima)ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda.
Sasa hapa duniani unapata nini?
Unapewa na Mwenye enzi Mungu mambo mawili hapa hapa duniani iwe mfano wa mambo yatakavokua huko Akhera kwenye Ufalme wenyewe. Jambo la Mwanzo Unateremshiwa (Body Guard) Malaika wawe na wewe popote uendapo, unapata ulinzi(Ukitaka kuwaona niandikie pembeni ntakufundisha vipi uwaone?, Najua utashangaa ndio maana ya kukwambia, kumbuka unakoga katika bahari usishangae maji kugusa)Naam na Jambo la pili ndio huo mfano wa pepo unapewa kitu adhimu sana, kitu hichi ukikipata ukaweza kudumu nacho basi kiumbe unakua ushafuzu katika maisha yako ya Ulimwenguni na huko akhera, Kitu gani hichi cha pili?, hakuna chengine isipokua kupewa (Control) ya (Mind) Akili yako, hapa itabidi nieleze vizuri ili upate kujua maana ya atakua hana khofu wala huzuni ikoje?.
Hali hii anaipata kila mtu lakini inakujia mara chache sana, kwa mimi naita hali hiyo (To make contact with your being) unapata baadhi ya Nyakati pale unapokua (Total engaged)Mfano, kama wewe mcheza mpira au unatizama kipindi chako kwenye TV, au unapozungumza hapo Akili au (Mind)inapotea, hakuna mawazo, unakua hufikiri chochote, kwa sababu Akili haiwezi kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja, basi hapo unakua (full Being)huna huzuni, huna khofu na ukiwa katika hali hiyo unakuwa huwezi kutenda kosa.
Hivyo ndio wanavokua "Hao Maskini walotajwa" wenye kurithi huo Ufalme, Wanakua ni wenye kudumu katika hali hiyo, sio kwamba hawana Akili ila ana uwezo wa kuitumia wakati anaotaka Mwenyewe kwa hiyo muda wote ulobakia yuko kwenye (Being)yake na hapo ndio kwenye hiyo (Bliss), Kwa hiyo tafauti yako na yeye wewe unatumia nyakati maalumu za kucheza mpira, kutizama TV, kuzungumza na yeye anaendelea kuwa nayo (Being)yake wakati wote, kwa hiyo hapo mambo yanakua (Vice Versa), Wewe unatumia (Mind)Akili wakati wote na yeye anatumia(Being) wakati wote. Na kama utakua na ubishi kwenye Nafsi yako basi jiangalie mara chache sana unaipata hiyo (Being)lakini muda wote umetawaliwa na mafikra, mawazo juu ya mawazo(Stress)zimekujaa, dhana za kila aina, wanawake au wanaume wanaishi humo, madeni yanaishi humo, chuki zinaishi humo binaadamu huna mapumziko, huzuni juu ya huzuni, mashaka na khofu chungu nzima, Na hiyo ndio Akili uliyoibeba na ndio ilokufanya uchague dunia dhidi ya Akhera. 
Sasa Wacha nikuchukue kwenye mfano wa Ufalme wa vinyama hususan ndege uone wanaishi vipi?.
Endelea Part 4


No comments:

Post a Comment