Tuesday, July 5, 2016

WAFALME WA PEPONI PART 4

Asalaam Aleiykum

Ipate japo siku moja hata nusu saa, kuwa (Mad)kama (Shk Baja)kakae kwenye Bustani au kwenye(Garden) au nenda (Park)au hata shamba asubuhi na mapema, halafu kashuhudie vipi(Unconscious Being)wanavoishi, Wanaishi kama unavoishi, Wana Nyumba zao tena wamezijenga wenyewe, wana watoto wao na wake zao, wanatafuta chakula kama mfanyavo nyinyi, wanalala na kuamka, wanakwenda huku na kule kwenye bustani, mara kwenye mti huu mara kwenye mti ule, mara kwenye maji wanakunywa, mara kwenye mti wanapumzika, Na mara wanaimba kwa furaha na baraka alizowapa Mollah wao.
Wao katika Ufalme huo wanaishi kwa mapenzi kama utayafahamu, mara wanaruka mara wametulia wanatizama neema walizopewa na Mollah wao, Na wakishikwa na maradhi wao wako kwenye subra wanajua Mollah wao anawaponesha daima. Basi wao wapo kwenye (Mfano)wao wa pepo na ikifika wakati wanajifia na kurejea kwa Mollah wao(Blissful), Viungo vyao vinaanguka na kugeuka Mchanga kama wewe utakavogeuka wakati wa kifo chako.
Naam unapewa mifano hii ya pepo ili na wewe uchague vipi unataka. Na ukiwa utaridhia huo umasikini ukaipata hali hiyo niloitaja kwenye (Part 3)basi Ufalme gani utakaoupata wewe?
Quraan Waqiah aya ya 10.
"وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ"
Walioko mbele(Kwenye Ucha Mungu)nao ndio wlioko mbele
"أُوْلَـٰٓٮِٕكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ"
Hao ndio watakaokaribishwa(Kwenye Ufalme wa Mwenye enzi Mungu)
"فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ"
Katika Mabustani yenye Neema
" ثُلَّةٌ۬ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ"
Sehemu kubwa ni miongoni mwa (watu)wa mwanzo(Zamani)
Kwani ikawa zamani kwa sababu walikua wakiishi kwenye (Being)zao, wanaishi kwa (Feeling)kutumia moyo sio kwa njia za (Mind)Akili .
"وَقَلِيلٌ۬ مِّنَ ٱلۡأَخِرِينَ" 
"Na sehemu ndogo ni miongoni mwa watu wa mwisho
Huu wakati tulonao ni mashaka makubwa ya kurithi au kuyapata au kupata kuwa karibu na Mollah wetu kutokana na ujanja tulonao, kila mtu kabeba mzigo wa mawazo machafu, mawazo mabaya, dhuluma, magonvi, hasada, chuki, viburi. Na maelezo yanaendelea mpaka aya ya 26 kuwaeleza hao watakaorithi huo Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Ama wale waloshindwa kuupata huo umasikini lakini wakafanya kheri, na walotubia makosa yao nao imetajwa sehemu watakayokua wao nayo inaanzia aya ya 27 mpaka aya ya 40. Kwa hiyo bidii yako ndio itakayokufanya ima uwe Mfalme au Mtu wa kawaida, zisome hizo aya halafu utafanya uamuzi unataka vipi. Na kama umeshindwa kabisa basi jitaarishe na kundi la tatu ambalo litakua makaazi yako Motoni, Na kumbuka hiyo ni ahadi ya Mwenye enzi Mungu.

No comments:

Post a Comment