Asalaam Aleiykum
Sura ya Maryam aya (61,62,63).
"جَنَّـٰتِ عَدۡنٍ ٱلَّتِى وَعَدَ ٱلرَّحۡمَـٰنُ عِبَادَهُ ۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ إِنَّهُ ۥ كَانَ وَعۡدُهُ ۥ مَأۡتِيًّ۬ا"
Pepo za milele ambazo (Mollah)Mwingi wa Rehma amewaahidi waja wake katika siri, Bila shaka ahadi yake ni yenye kuja.
"لَّا يَسۡمَعُونَ فِيہَا لَغۡوًا إِلَّا سَلَـٰمً۬اۖ وَلَهُمۡ رِزۡقُهُمۡ فِيہَا بُكۡرَةً۬ وَعَشِيًّ۬ا"
Hawatasikia humo upuuzi ila Salama, Na watapata humo riziki yao asubuhi na jioni.
"تِلۡكَ ٱلۡجَنَّةُ ٱلَّتِى نُورِثُ مِنۡ عِبَادِنَا مَن كَانَ تَقِيًّ۬ا "
Hiyo ndio pepo tutakayowarithisha katika waja wetu wale ambao (Walikua)ni Wanamcha Mungu.
Aya tatu lakini zina tafsiri kubwa kabisa inataka siku nzima kuichambua tafsiri hiyo, lakini kwa ufupi tukio hilo linaashiria kwenye aya ya mwanzo kuwepo kwa uendelevu wa maisha,Maisha ambayo wewe utakua ni "Bwana" Utakua ni Mfalme, Jee wewe huitaki ahadi hii ya siri ya Mollah wako, kama ninavosema, (nasema kila mara)uhai ni kitu cha kudumu, ila maisha ndio kitu cha (Mpito)au(Temporary). Kwa hiyo hichi kitu kinachoitwa Pepo ni ahadi ya siri, Lakini daima ahadi ya Mwenye enzi Mungu ni yenye kutimia, kwa hiyo kaa ukijua utakapomaliza muda wa kuishi hapa Ulimwenguni kuna maisha mengine.
Na Maisha ya huko hayana porojo za wanasiasa, hakuna uongo wa wafanya biashara, mambo ya kipuuzi yote yana katika katika dunia hii, huko unakutana na hali ya usalama(Peace)tupu, hakuna chuki wala uhasama, na humo wewe ni Mwenye kuhudumiwa kila kitu chako unaishi maisha ya Kifalme, Sasa hivi unaona kwenye TV tu lakini huko na wewe utayapata, utakua Mwenye kupata riziki yako asubuhi na jioni, hakuna tena shida ya kutafuta wala kuhangaika.
Hiyo ndio hiyo pepo watakayorithi wale walokua na Mapenzi na Mollah wao, wakakubali yupo na kumtii kwa ajili ya Ibada na kufata amri na sheria zake. Lakini uingiaji wake una shuruti lazima uwe Maskini, Sasa Umasikini huu ukoje? (Quraan imeashiria jambo kwenye sura ya Ash-Shuura aya ya 20) inasemaje?.
مَن كَانَ يُرِيدُ حَرۡثَ ٱلۡأَخِرَةِ نَزِدۡ لَهُ ۥ فِى حَرۡثِهِۦۖ وَمَن كَانَ يُرِيدُ حَرۡثَ ٱلدُّنۡيَا نُؤۡتِهِۦ مِنۡہَا وَمَا لَهُ ۥ فِى ٱلۡأَخِرَةِ مِن نَّصِيبٍ
"Mwenye kutaka jaza ya Akhera tutamzidishia katika Jaza yake hiyo, Na anayetaka Jaza ya Dunia tutampa, Lakini Akhera hatakuwa na sehemu yoyote ya kheri".
Sasa kwanini ikawa moja utazidishiwa, na nyengine utapewa, kuna mambo yamejificha wewe huyajui, maana ya kusemwa hivyo kuna kitu wewe unacho tayari lakini hukijui, na kitofanyika ni kuzidishiwa, unaweza kukipata hapa hapa na ndio haki yako ikiwa utamcha Mwenye enzi Mungu, lakini kupewa ni kwa muda unaweza ukapoteza, unaweza kunyanganywa au kukupotea. Kwa hiyo tabia ya Mwanaadamu ni vigumu sana kuvitaka vyote vilotajwa kwenye aya hiyo.
Ni watu wachache sana wanoweza kufanikiwa, Na sababu kubwa viumbe hatuna (Balance), Ndio maana tukapewa uhuru wetu kwa yule Mwenye kutaka Dunia anapewa, na Mwenye kuitaka Akhera pia anapewa. Sasa Maskini yupi Mwenye kurithi huo Ufalme?, Usikilize ukweli unapo dhihiri, Yasome Maneno ya Mwenye enzi Mungu kupitia katika vinywa vya Mitume wake wanasemaje.
Anasema Isa a.s "Wamebarikiwa Maskini kwani wao ndio watorithi Ufalme wa Mwenye enzi Mungu" Kwanini likatajwa neno kubarikiwa(Blessing)Kwa sababu hao wamechagua kitu kizuri sana, Wao wamechagua (Both) wako kwenye (Balance) (Irejee aya juu imetaja kuzidishiwa na kupewa) maana ya kuzidishiwa tayari unacho, na kupewa ndio hicho cha ziada, ukichagua (Both) unakuaje? na ukichagua kimoja unakuaje?.
Ukichagua Dunia na ndio wengi tunaichagua unakua unajishughulisha sana na kutafuta mali, mashamba, ufakhari, Na ukichagua Akhera pekee unakua Mwenye kutaka kufa, ushachoka na maisha, kila kitu haramu, muradi wako unakua (Neurotic) kwa sababu huna (Balance). Sasa uchague vipi? chagua kama ilivosema katika Quraan, imesemwa vipi?
Endelea part 3
No comments:
Post a Comment