Saturday, September 10, 2016

MAJAALIWA YA KUONA NA KUSIKIA PART 1

Asalaam Aleiykum

Zimekujia Fahamu za vitendo  viwili hivi vya kuona na kusikia,
Umepata angalau kujua kwanini unaona?, na uwezo huu unatokea wapi, unaijua fadhila ya kusikia na uzuri wa jambo hilo?, na nini habari yako wewe kama moja katika hilo litaondoshwa utakua katika hali gani, Uwe wewe (Tajiri wakupindukia) ichukuliwe tu (Jaala)hii ya kuona au kusikia ujitizame vipi unakua, ushawahi wewe kuumwa macho yakawa hayaoni au masikio yameziba ukawa husikii japo kwa siku moja unakuaje, vitu kama hivi tunavichukulia ni kama jambo jepesi sana, tunachukulia kama tuna vimiliki vitu hivi wala hatuna wasiwasi hata wakujua vinatokea wapi na kwanini tunapewa?.
Unakumbuka lini wewe umewahi kuamka bila ya kukumbushwa  ukamshukuru Mollah wako?, Ukashukuru tu Alhamdullilah(ahsante)Mollah wangu kwa kunipa tena siku hii ya leo kuona na kusikia, Imeshakufikia habari ile siku mambo mawili haya yatakapoondoshwa ukawa huoni wala husikii yaliyomo kwenye Ulimwengu huu. Basi ikiwa msahaulivu au una (Kiburi) fulani isome darsa hii upate kufungua macho yako, kwani wakati huu ulo nao  macho yako wazi lakini hayaoni.
Napenda kukumbusha uelewe jambo hili la kuona na kusikia imekua katika ihsan kubwa Mollah wako alizokufanyia  za kukufanya ukaribie Ufalme wake wakati ukiwa hai katika ulimwengu huu. Amekupa wewe (Sifat Basiran) Na akakuongezea (Wasifat Samian) Akakupa zaidi na (Sifa ya Aliim)Mwenye kujua, na pia kukupa wewe kiumbe hizo nguvu (Sifa ya Qawwiy) Amekupa mambo mengi nimeyataja hayo kwa uchache ili ujue vipi Mapenzi ya Mwenye enzi Mungu juu yako wewe Kiumbe. Kiumbe wewe huna malipo ila kumsahau, huna jengine isipokua ufisadi, Basi kabla ya kuzama kwenye Bahari hii ya kuona na kusikia wacha kwanza tuangalie nini kinatokea kabla ya kulala na kuondoshewa huko kuona na kusikia.
Endelea part 2

No comments:

Post a Comment