Saturday, September 10, 2016

MAJAALIWA YA KUONA NA KUSIKIA PART 2

Asalaam Aleiykum

Nini Kinatokea?

Katika maumbile yako ya kawaida mambo haya yanatokea ikiwa hujijui au huyajui, Kimaumbile Tabia uliyoizoea ni kama ile ya taa, kuwaka na kuzimika, ila unaona ukisema hivyo watu watakushangaa kwa hiyo umechagua jina la kudumu unaita kulala na kuamka.
Lakini kama utakua Mwanasayansi wa dini basi utakuja kugundua Kulala huko na kuamka kwako kuna (Process)kubwa lazima uipitie ndio uvipate viwili hivyo na vyengine, Maajabu yanotokea hapo ni makubwa, ni taabu kuyaeleza unaweza kuyaona lakini inataka ifanyike jitihada kubwa kuyashuhudia, Inatakikana upatikane ustahamilivu wa hali ya juu kuiona hali hiyo yenye kutisha, hali ambayo ikikutokea inaambatana na khofu ya umauti.
Kuishuhudia hali hiyo kunahitaji maandalizi makubwa yenye kuambatana na ushujaa, sisemi ni rahisi yaweza kukuchukua miaka au miezi, au pengine masiku kadhaa tu ukaliona tukio hilo kwa ukamilifu, Na zaidi yategemea Majaaliwa na Ridhaa kutoka kwa Mollah wako.
Usije ukaona mbona huyu anazungumza Mambo ya ajabu, au analeta mafunzo mepya, mambo yapo, yametajwa ndani ya (Quraan fussilat aya ya 53)
سَنُرِيهِمۡ ءَايَـٰتِنَا فِى ٱلۡأَفَاقِ وَفِىٓ أَنفُسِہِمۡ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَهُمۡ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّ‌ۗ أَوَلَمۡ يَكۡفِ بِرَبِّكَ أَنَّهُ ۥ عَلَىٰ كُلِّ شَىۡءٍ۬ شَہِيدٌ 
"Tutawaonesha (Ukweli)wa Alama zetu katika Nchi(Mbingu)za Mbali na katika Nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli. Je haikutoshi kwa Mollah wako kuwa yeye ni mjuzi wa kila kitu".
Wanasayansi wamekwenda kwanza (Nje)Mbinguni kama ilivosema (Quraan)Na Wacha Mungu wao wamekwenda kwanza ndani kwenye Nafsi kuipata Yakini, Na wewe nenda usiogope, hee mpaka unakufa hutaki kujua chochote cha upande wa pili.
Naam hivyo ndio hali ya mambo ilivyo, Sasa turudi nyuma ili tuendelee na darsa yetu ya kuona na kusikia.
Endelea part 3

No comments:

Post a Comment