Asalaam Aleiykum
Siku zote nasisistiza uielewe sifa ya Jaala ni yenye kuja na kuondoka, Na sifa hii inatosha kukuthibitishia kuwa Kiama kipo na kinakuja, ima utakua hai siku hiyo au utafufuliwa lakini siku hiyo ipo na inathibitishwa na sifa hii ya Jaala. Basi yachunguze wewe mambo makubwa makubwa kuhusishwa na sifa ya (Temporary).
sifa kama zipi?(1)sura ya Nabaa,
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَـٰدً۬ا
Je hatukuifanya ardhi kuwa (kama)Tandiko. Sasa kwanini likaitwa tandiko, kwa sababu wakati mwengine tandiko linaondoshwa au kuwekwa pembeni, na hayo yanafanyika katika ardhi ima kwa kudidimia au kwa mtetemeko wa ardhi.
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتً۬ا
Na tukaufanya usingizi wenu kama kufa. Na aya hii ndio inaigusa aya yetu moja kwa moja kwa kuondoshwa hayo majaaliwa ya kuona na kusikia.Ikisha unarejeshewa mambo hayo.
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسً۬ا
Na tukaufanya Usiku kama guo(Mnalofunikwa)kama utazingatia nyakati za kuzama jua utaona vipi kiza kinavo kuvaa na kukuondoshea nuru ya kuona.
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّہَارَ مَعَاشً۬ا
Na Tukaufanya mchana Kama kufufuka. Hayo yanataka mazingatio pale mwanzo unaporejeshewa kuona na kusikia ndio utajua vipi inakua huko kuona na kusikia.
وَجَعَلۡنَا سِرَاجً۬ا وَهَّاجً۬ا
Na Tukaifanya taa ingarayo na yenye joto kubwa.hilo ndio Jua lenye kutupa vitamin na nyenzo zengine za maisha, kama chakula na kadhalika. Hayo ni machache ambayo ni (Temporary)huja na kuondoka kutokana na anavopanga Mollah wako.
Ukichunguza maneno yangu utagundua siku zote nasisitiza kuwa sifa hii ya jaala ni yenye kuja na kuondoka, Na ikiwa umepewa Akili ya mazingatio basi pia litakuongezea nguvu za imani yako pale utakapoona kumbe sifa hii pia imo kwenye nafsi yangu, Ukajua kumbe yupo Mwenye kunipa sifa hii ya kuona na kusikia.
إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٍ۬ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَـٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا
Hakika tumemuumba Mwanaadamu kutokana na mbegu ya Uhai iliyochanganyika,( ya Mwanamme na Mwanamke)ili tumfanyie mtihani, kwa hiyo tukamfanya Mwenye kusikia na Mwenye kuona.
Sasa inakuaje majaaliwa haya, Nini kinatokezea?.
Wacha nikuchukue kwenye safari hii ambayo unaiogopa sana lakini huna budi ni lazima uende, si umeambiwa tukaujaalia huo usingizi wao kama kufa, Basi wacha na sisi tuanzie hapo kuhusu yale mambo niloyataja huko mwanzo ambayo yanaondoshwa taratibu(Slow motion)au labda uwe umechoka ndio unazimika ghafla. Lakini (Process)za kawaida ziko, wacha nikupe mfano ili uone jambo gani la mwanzo hilo lenye kuondoshwa taratibu?kwenye hiyo (Process).
Basi Jitizame katika kusinzia utaona nguvu zinakuishia, ndio maana utaona kama umekaa unataka kama kuanguka,(Balance)huna, nguvu zinachukuliwa taratibu, Na Jambo la pili kuondoshwa ni huo uwezo wa kuona kidogo kidogo huo unaondoshwa mpaka kupotea.
Na jambo la tatu uwezo wa kusikia nao unaondoshwa ndio maana utaona chakacha au disco inapigwa yeye kalala anakoroma, "Wewe unashangaa sauti hii huyu anakoroma" kumbe mwenzio pale kama maiti, (Tukaujaalia usingizi wao kama kufa)unaendelea kushangaa ngoma hizi na sauti hii na huyu kalala chini ya (speaker)bado hasikii kitu huyu.
Na Jambo la Mwisho kuondoshwa ni hiyo (Knowing) au ita (consciousness), hapo tena Mwanaadamu unakua kama maiti. Sasa kwa wale Wacha Mungu au wanasayansi wa ndani wao wanafanya maandalizi na kuomba ridhaa ya Mollah wao ili wapewe uwezo wa kushuhudia (Process) yote hii huku wamebakishiwa hiyo (Knowing) au (Consciousness)vile vitatu vinatoweka hichi kimoja kinabakia na hiyo ni Fadhila kubwa kutoka kwa Mollah wao.
Ukijaaliwa kuipata hali kama hiyo unakua umefuzu katika Ulimwengu na huko uendako kwa Mollah wako.
Sasa nini Habari yetu sisi viumbe wa kawaida ukipata bahati ya kushuhudia, kama utakua makini ni rahisi kwako kushuhudia kuamka kwako, (Process) ni ile ile, ila sasa inakuja kinyume chake, katika kuamka lile liloondoka mwisho ndio lenye kuja mwanzo, Yaani hiyo (Knowing) au (Consciousness)au (Fahamu) Napenda uelewe wewe upo ila viloondoshwa ni hivyo vitendea kazi vya kuona na kusikia, kwanini nikasema wewe upo, kwa sababu jiulize nani Mwenye kuona ndoto, ukipata jawabu endelea kusoma ili upate faida zaidi, niliposema hili la (Kufufuliwa) ni rahisi kulipata nimekusudia wakati mwengine inakutokezea lile jambo la mwanzo la kujua(Knowing)linapokuja unazinduka ukawa hujui uko wapi, wewe nani?, Halafu jambo la pili linafatia ni kusikia, unasikia watu wanazungumza kwa mbali, halafu hapo tena inakuja kuona ikifatiwa na nguvu, ukiyapata hayo kama mja Mwema unaamka na Alhamdullilah, Nakushukuru Mollah wangu kwa kunijaalia uhai baada ya Mauti yangu.Kuna mambo mengine yenye faida nitayazungumza nini ufanye wakati unapata Rehma hii ya kuamka, huko siku za mbele nikijaaliwa.
No comments:
Post a Comment