Asalaam Aleiykum
Umepata kujiuliza kwanini mapenzi yakawa siri?. Jee unajua sababu yake?.Basi jiulize swali hili kwa njia ya kutaka kujua na hapo utakua umepanda mbegu ambayo haina kikomo katika kukua kwake, Haina mwisho katika kutoa Miti na Matunda yake. Napenda Uelewe nikizungumza neno Mapenzi sikusudii chembe yako ya mapenzi ya matamanio, sizungumzii upya wowote wa mapenzi unayo yafahamu wewe, au kama natoa (style)upate kupendwa na wanawake au wanaume, au wengine wakadhani natoa mbinu za upatikanaji wa mapenzi ya matamanio, hilo sio kusudio langu, kusudio langu ni kukufahamisha kuwa yapo mapenzi ya aina nyengine na kama utayapata daima utakua furahani, dhiki zitakuondoka, kila siku kwako itakua siku ya (Eid).
Mapenzi ninayokufahamisha leo ni jambo la siri, Kwanini ikawa siri kwa sababu ukiizungumza tu(Ushaipoteza) ladha yake inapotea, utamu wake unakatika, uchu wake unaondoka, kwa wale wenye kujua siri ya Mapenzi haya hawasemi chochote kwani wanajua siri ikisemwa inakua sio siri tena. Basi na mimi leo sitakwambia kwa uwazi hayo mapenzi ila ntaashiria ukakutane nayo Mwenyewe.
Basi kwanza ntakujulisha mapenzi uloyazoea ya Mwanamme na Mwanamke, au mapenzi ya kupenda nyumba yako, mapenzi ya kupenda farasi, gari na vitu vidogo vidogo ambavyo vimetajwa kwenye Quraan aya ya (14) Al-Imran.
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٲتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَـٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَـٰمِ وَٱلۡحَرۡثِۗ ذَٲلِكَ مَتَـٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَٱللَّهُ عِندَهُ ۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ
"Watu wametiwa huba(Mapenzi)ya kupenda wanawake na watoto na marundi ya dhahabu na fedha, Na Farasi wanaotunzwa vizuri, na wanyama na mashamba, Na hayo ni (kwa ajili ya)matumizi ya maisha katika dunia, Na kwa Mwenye enzi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri"
Mapenzi yako ya aina mbili, aina ya kwanza ndio hiyo ilotajwa hapo juu ulotiwa nayo, unayo tayari, huwezi kuikwepa ni muhimu kwa ajili ya maisha yako ya kidunia, bila ya hivyo maisha yako yatakua kama maiti, upo tu duniani unakera watu, kila kitu kwako kibaya, kutokana huna hata hayo mapenzi ambayo ni haki yako kuwa nayo, ambayo Mollah kampa kila mja wake, wewe hata hilo hukupata, ukifikia hali kama hiyo inafaa ujiulize kwanini?.
Na aina ya pili ya Mapenzi ndio hiyo siri yenyewe, sasa kabla ya kwenda mbele hebu tuirejee aya tutizame, ikisha tujiulize kwanini ikataja Wanaume na sio wanawake?. Ikiwa wewe unanifatilia vizuri utagundua ama kwa Wanawake wanayo tayari (Nature) ya (Love)Mapenzi, Mwanamke kwake rahisi ku(surrender)yuradhi kukiri na kumtii mpenzi wake, hiyo ndio hulka ya Mwanamke, anatuonesha vipi mapenzi yake yalivo katika kuwalea na kuwapenda watoto wake, Mwanamke kajaa Moyo wa mapenzi, Mwanamke hana shaka katika penzi lake, na hajui hata inakuaje ila yeye kajaa mapenzi, ndio maana kwa Mwanamke rahisi kwake kwenda kwenye hilo penzi la siri.
Kwanini ikawa hivyo?
Kwa sababu Mwanamke Mapenzi kazaliwa nayo, Mapenzi yako Moyoni, Na hiyo ni siri yake wala haisemi, anao uwezo na ujuzi wa kumpenda Mtu akanyamaza kimya, Na hiyo ndio tunapata ishara ya siri ya Mapenzi (alopewa mwanamke).
Ama kuhusu Mwanamme(Yeye alotiwa)Penzi, Penzi hilo lipo (Kichwani) na wala sio moyoni, Ndio maana "Mwanamme mara huku mara kule", Mara kapenda hichi mara kapenda kile, na hiyo ndio tafauti yao. Kwa hiyo kawaida hiyo inatujulisha Mwanamke yeye yuko tayari kuchupa kwenye Bahari ya Mapenzi ya siri, Ndio maana utaona wao hawendi vitani, (Wao sio Violence) kwa hiyo katika kwenda kwenye Penzi la siri Mwanamke yeye njia yake ni(One Way)(from the heart to the beyond). Lakini Mwanamme yeye ni (Two way)Lazima urudi chini, lazima utoke kwenye kichwa uende moyoni, lazima upate (Faminine Quality).
Ndio Maana utaona "Wacha Mungu"wapole, (Very Loving).
Kwa Mungu hakutakiwi Ujabali, Kwa Mungu hakutakiwi Kuua, Hakutakiwi(Violence)huko ni salama juu ya salama, hakutakiwi chuki, Hakutakiwi hamaki wala hasira.
Sasa leo wacha nikushike mkono labda utachupa na mimi kwenye hiyo bahari ya Mapenzi ya siri ili na wewe upate neema yake. Lakini ili usije ukaweka tamaa au kupanda kiburi kuwa utafanikiwa itabidi nikujulishe kuwa mapenzi haya wanayapata watu wa aina mbili kama ilivosema Quraan sura ya (Fussilat aya ya 34 na 35)
وَلَا تَسۡتَوِى ٱلۡحَسَنَةُ وَلَا ٱلسَّيِّئَةُۚ ٱدۡفَعۡ بِٱلَّتِى هِىَ أَحۡسَنُ فَإِذَا ٱلَّذِى بَيۡنَكَ وَبَيۡنَهُ ۥ عَدَٲوَةٌ۬ كَأَنَّهُ ۥ وَلِىٌّ حَمِيمٌ۬
Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa, ondosha (ubaya unaofanyiwa kwa mema)tahamaki yule ambaye baina yake kuna uadui atakua kama ni jamaa (Yako)mwenye kukufia uchungu.
وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٍ۬
Lakini (Jambo hili)hawatapewa ila wale wanaosubiri, wala hawatapewa ila wenye hadhi (Bahati)kubwa (Kwa Mwenye enzi Mungu)
Ipate maana ya maneno haya katika part 2
No comments:
Post a Comment