Monday, August 1, 2016

MAPENZI NI SIRI YAKO PART 3

Asalaam Aleiykum

Mapenzi hayo ya siri yanapatikana kwa jitihada, kwa sababu yale ya aina ya kwanza umepewa na Mwenyewe, haya ya pili inatakiwa uyatafute Mwenyewe, Na hiyo ndio maana ya (Ibada)umepewa nusu na nusu uitafute, kwa sababu sasa hivi penzi lako ni (Fragment) vipande vipande, unatakiwa ufanye juhudi uliunganishe, kwanini ikawa vipande vipande, wacha nikujulishe ili upate kulijua penzi la siri likoje, na ukiliunganisha lina faida ipi. Ntakuonesha kwa mfano wa Quraan Al-Ahzab(35)
 إِنَّ ٱلۡمُسۡلِمِينَ وَٱلۡمُسۡلِمَـٰتِ وَٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَـٰتِ وَٱلۡقَـٰنِتِينَ وَٱلۡقَـٰنِتَـٰتِ وَٱلصَّـٰدِقِينَ وَٱلصَّـٰدِقَـٰتِ وَٱلصَّـٰبِرِينَ وَٱلصَّـٰبِرَٲتِ وَٱلۡخَـٰشِعِينَ وَٱلۡخَـٰشِعَـٰتِ وَٱلۡمُتَصَدِّقِينَ وَٱلۡمُتَصَدِّقَـٰتِ وَٱلصَّـٰٓٮِٕمِينَ وَٱلصَّـٰٓٮِٕمَـٰتِ وَٱلۡحَـٰفِظِينَ فُرُوجَهُمۡ وَٱلۡحَـٰفِظَـٰتِ وَٱلذَّٲڪِرِينَ ٱللَّهَ كَثِيرً۬ا وَٱلذَّٲڪِرَٲتِ أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُم مَّغۡفِرَةً۬ وَأَجۡرًا عَظِيمً۬ا 
Bila shaka Wanaume wenye kuufata (vizuri) Uislam, na wanawake wenye kuufata (vizuri) Uislam, Na Wanaume wanoamini (vizuri), Na Wanawake wanoamini(Vizuri), Na wanaume wanotii, Na wanawake wanotii, Na Wanaume wasemao kweli, Na wanawake wasemao kweli, Na wanaume wanosubiri, Na wanawake wanosubiri, Na wanaume wanonyenyekea, Na wanawake wanonyenyekea, Na wanaume wanotoa sadaka, Na wanawake wanotoa sadaka, Na wanaume wanofunga, Na Wanawake wanofunga, Na wanaume wanaojihifadhi tupu zao, Na wanawake wanaojihifadhi, Na wanaume wanomtaja Mungu kwa wingi, Na wanawake wanomtaja Mwenye enzi Mungu kwa wingi, Mwenye enzi Mungu amewaandalia Msamaha na ujira mkubwa.
Hapo utaona wametajwa wale wenye mapenzi lakini ya tafauti tafauti, huyu anatoa sadaka, huyu anatii, huyu anaamin, huyu anahifadhi tupu, wote hao wanafanya hayo kwa ajili ya mapenzi. Nini habari yako wewe kama utachanganya mambo hayo yote, siri yake ni kupata msamaha, na tunza yake ni kupata huo ujira mkubwa, ukisamehewa unaipata (Pepo), Na hapo ndio utakapo ipata (Mapenzi ni siri yako)jaribu kukusanya uone inakuaje, ipate hali kama hiyo ukutane na mambo ya ajabu.
Na hapo ndio unapata kujua kumbe Uislam ni Dini ya Mapenzi na amani, kwa vipi na imesemwa wapi.Siku zote si Mnasema (Love is Blind)kweli hamjakosea, lakini kwenye Uislam Mwenye enzi Mungu kayafanyia nini hayo mapenzi?. 
Quraan (Baqarah aya ya 2 mpaka ya 3) Ipate siri hii ya Mapenzi ili na wewe ufanikiwe.
 ذَٲلِكَ ٱلۡڪِتَـٰبُ لَا رَيۡبَ‌ۛ فِيهِ‌ۛ هُدً۬ى لِّلۡمُتَّقِينَ
"Hiki ni kitabu kisichokua na shaka ndani yake, ni uongozi kwa (wapenzi)wamchao Mwenye enzi Mungu".
Ukishampenda Mollah wako ni lazima upate uongozi ili usije ukapotea, usije ukajigonga na makuta, usije ukachaniwa majuba ndio unapewa hichi kitabu ili kikuongoze, Kwa sababu hayo wayafanyayo hao walotajwa hapo juu yote ni kwa ajili ya mapenzi.
Sasa wamefanyaje hata wakayapata mapenzi hayo.
ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَـٰهُمۡ يُنفِقُونَ
Ambao huyaamini  ya (Siri)yasionekana Na husimamisha Sala na hutoa katika yale tuliyowapa.
Kuamini ni jambo rahisi sana, kuamini ni kazi mtu mwengine kakufanyia wewe unakubali, lakini tafsiri sahihi ni lazima uende (deep)ukatafute siri za huo upande wa pili, lazima ujishughulishe sana kutaka kujua kuna nini kwa Mollah wako, ufanye jitihada zako ukipata uthibitisho wa mambo yalofichwa huko japo chembe hapo utakua huzini tene, hudhulumu tena, hupiti kuua, unachorudi nacho kutoka upande wa pili ni kusimamisha Sala, kumbuka kuna kusali na kusimamisha sala, Kwanini ikawa hivyo?, kilosimamishwa lazima kwanza kilikua kimekaa au kulala, sasa wewe kwanini unakisimamisha? kwa sababu Wingi wa Wanaadamu siwenye kusimamisha sala, Maana ya kusimamisha Sala kujaa na mapenzi kwa ajili ya Mollah wako, huwezi kuiba ikisha ukenda kusali, huwezi kupokea rushwa halafu ukasali, huwezi kuzini ikisha ukasimamisha sala, haiwezekani ukaweka mapesa (Bank)huku unasimamisha sala. Utakua unamdanganya Mollah wako,(Bado Umelala) Mwenye kusimamisha sala amejaa mapenzi na akimaliza sala anatoa kile alichopewa na Mwenye enzi Mungu, Unaona Mollah wetu alivojaa mapenzi anatupa uhuru, anatupa uhai, anatupa mali na mengi mengineyo, kwa hiyo yoyote yule Mwenye mapenzi lazima awe na athari ya kutoa, tena athari hiyo haihitaji maonesho ni siri yake na kila akitoa anasikia furaha ya mapenzi kwa wale awapao. Na hiyo ndio siri ya mapenzi unasisitizwa uipate. hapo utaona vipi (Mapenzi yanavo miminika kutoka Mbinguni).


No comments:

Post a Comment