Asalaam Aleiykum
Aya ya 34 inaanza hivi "Mambo mazuri na Mabaya hayawi sawa" Mambo mazuri ni nini?, ndio hayo Mapenzi ya siri, ondosha Ubaya unaofanyiwa kwa mwema, Tahamaki yule ambaye baina yake kuna uadui atakua kama ni jamaa yako mwenye kukufia uchungu.
Hiyo ndio (Power of Love) sio kuwa umempa mtu pesa au gari au nyumba. Na wewe ukigeuka panga la Mapenzi, basi yule adui yako machozi yatamiminika akikuona tu, atapigana kwa uchungu, yuko tayari kufa kwa ajili yako.
Aya ya 35 inaendelea kuwataja, "Lakini (Jambo hilo)hawatapewa ila wale wanaosubiri" (Na)Wala hawatapewa ila wenye hadhi(bahati)kubwa kwa Mwenye enzi Mungu. Sasa hawa wenye kusubiri ni wepi na wenye hadhi ni wepi, hapo ndio tunaingia katika sehemu yetu ya pili ya hilo (Penzi Lenyewe).
Nini Mapenzi?
Mpaka leo hajatokea awezaye kulijibu swali hilo, halijibiki kwa njia ya maneno, hakuna lugha inayoweza kutafsiri, ile ya Mwanzo tumepewa jawabu na Mollah wetu, lakini hili la pili ndio hiyo siri yenyewe inayokupa ladha na furaha, inakupa na utulivu, inakupa maisha, sasa shuka chini ya huo mti uoneshwe hili shina, huu mzizi, na hii ndio mbegu yenyewe, itabidi uichukue mbegu hiyo uipande mwenyewe.
Nini Mapenzi?
Mapenzi ni (Mystic Force) inayotokea kwa mollah wako na kukuvaa, ni hali unayoipata ya kukumiminia (Bliss)Raha juu ya Raha, hali ambayo haina kikomo, sasa unayapataje Mapenzi haya.
Hapo juu wametajwa watu wa aina mbili wenye kusubiri na wenye hadhi.
Ama tafauti ya wawili hawa wenye kusubiri ni wale wenye kufanya mambo kidogo kidogo, Na wale wenye hadhi ni wale wenye kuendea kheri hizo kwa haraka. Vipi inakua hali hiyo ya Mapenzi ya siri?.
Endelea part 3
No comments:
Post a Comment