Sunday, September 30, 2018

MAZOEZI YA KUFA PART 3

Asalaam Aleiykum

Naam Nikamwambia Mwanangu nataka kukufundisha kitu, kwani unafahamu Mwanaadamu anasikia kwa kutumia nini? akanijibu masikio, Nikamwambia Tia Vidole vya kati masikioni uyazibe kabisa kwa nguvu, nikaanza kuongea, akanambia mwanzo ilikua (Silent)halafu (Very strange things happen)nikaanza kusikia kupitia kifuani, Nikamwambia hapo ndio inaptakiwa kutokea Nia, Dua na Sala yako, Na wewe Fanya (Experiment)utalijua hilo, Kama isivojulikana sauti inatokea wapi, Na huko kusikojulikana kunatakiwa kutoke Dua ya ikhlas, Kwa kuwa tumehama siku nyingi hatuna tena mapenzi kwenye nyoyo zetu, Na hususan wale wenye kuukimbilia Usheikh wajitahidi sana kuwa na mapenzi, yako mafundisho ntakupeni kama mtataka kurudi kwenye moyo, kama mtataka ku (Fall in love)Mfanye nini, Wacha nikufundishe njia hii labda unaweza kupata mapenzi, unaweza kuwa Mtu wa Taqwa, ufanye nini?.Mazoezi hayo mwanzo yatakushitua lakini hayana neno baada ya miezi utajiona vipi umebadilika, Raha kubwa itashuka juu ya nafsi yako, mazoezi haya yako ya aina mbili moja ni kurudi kwa hiyari nayo ni (Surrender) na ya pili (By force) ni Ku (Imagine)kila ukikumbuka jione huna(Imagine) (Kichwa).
Hapo utajiona vipi mawazo yanavotoweka, utaanza kuona ajabu baada ya kufikiri kwa Akili sasa unatumia moyo, kidogo kidogo utakua unashuka Moyoni, utaanza kupenda kila kitu, Wanyama, miti wanaadamu, Na hapo ndio utaanza kuupandisha mti wa Taqwa moyoni mwako, hapo ndio unaweza kuomba dua kwa ikhlas.
Naam tulikua tunachuma matunda ya fahamu sasa turejee kwenye darsa yetu ya Mazoezi ya kufa, kwanini makaburini, kwanini Maiti, ulipoambiwa uhudhurie viwili hivyo dhumuni ni kukufanya uzinduke na kukutana na kile chenye kuishi milele. Lakini mnakwenda Kuzika umebeba na duka lako, umebeba urafiki au hadith za mipira au za kisiasa. Kutokana na hali hiyo mambo muhimu yanakupita huyaoni kabisa. vipi unatakiwa ufanye ukenda kuzika, sio utupe maiti ikisha huyo ukimbie, Unatakiwa Fikra na mawazo yako yote yazingatie huyo maiti toka mwanzo mpaka mwisho anazikwa, upate nafasi uone vipi anatolewa, vipi anazikwa, vipi anafukiwa, nini kinatokea, ikiwa unakwenda mazikoni kikweli kweli basi itakua rahisi kwako wewe baada ya miezi kadhaa kugundua Almasi, kitu adhimu kabisa utakijua, kama mwanzo nilivokwambia kuna kitu baina ya kuvuta pumzi na kutoa na hapa makaburini, kiko kitu pia kama utakifatilia na kuzinduka, utaona (Energy) Maalum, utaona kinachozikwa ni kiwiliwili tu, Na wewe Kiburi kitakutoka kwa mara ya Mwanzo utakautana na kusutana na nafsi yako kwamba wewe ni (Nothingness)ukipata zawadi ya kuamka mazikoni(Your life)haitokua ile ile tena utagundua kitu muhimu sana, hutokubali tena kuondoka makaburini bila ya kuomba dua, utafunguliwa pazia na utapata kujua kwanini tunamsalia maiti, na huyu anosaliwa anafaidika vipi, hilo litakuandaa vizuri na mazoezi haya ya kufa, nakupa changa moto mengine kayatafute Mwenyewe Inshaallah Mwenye enzi Mungu atakufungulia kuyaona ili khofu ya kufa ikutoke kwa ajili ya matendo mema, kwa ajili ya kumpenda Mollah wako, nimekujulisha mawili matatu natumai yatakusaidia kwenye mazoezi yako. Nakuomba niombee kama ninavokuombea.
Mollah tupe takhfif wakati wa kutoka Roho zetu, tuletee Manukato mazuri ya Janat firdous yawe maliwazo yetu kwa ajili ya kukutana na Wewe,  utukutanishe na wenzetu walo wema, tudumishe kwenye Ibada utupe Mwisho Mwema, tuongoze katika njia ilonyooka kama ulivo waongoza walopita, wala usitutie Sheitani tukawa na viburi na kufanya mambo tusoyajua mpaka umetubainishia ukweli ulotoka kwako.
Amin

No comments:

Post a Comment