Asalaam Aleiykum
Jee umeshawahi kukutana na Shahidi wa Shuhuda?.
Basi ikiwa hujakutana nae Wacha nikuchukue katika safari ili tukamtafute huyu Shuhuda, Kwanini nikaitaja Safari kwa sababu safari ni muhimu sana katika kugundua mambo mepya, usikubali kukaa sehemu moja utakua hugundui au kujifunza mambo mepya, Ndio Maana Nabii Musa a.s akaambiwa nenda kwa Mja wetu tulompa elimu, Na wewe usikae pahala pamoja na ukasoma kitabu kimoja utakuja kuondoka Ulimwenguni hapa huna faida hata moja, nenda kasome pita ukitafuta huku na kule asaa kuna siku na wewe utafunguliwa Mlango wa Shuhuda, Na utakapo ingia katika Jumba la Shuhuda unakua Mtu Mwengine kabisa. Kila Mmoja wetu anao uwezekano huo ila tunashindana kati juhudi ya kuutafuta mji huu wa Shuhuda.
Leo nimeanza darsa yangu kwa kukuletea mfano wa safari, Ikiwa wewe Mweupe au Mweusi ntakupeleka Mji usika ili usipoteze lengo, Basi wacha tuanze na Mtu Mweusi kama nilivyo mimi, Kama wewe Mweusi Fikiria nimekutoa Tanzania nimekupeleka (Nigeria)katikati ya Jiji la lagos, huna Jina, hujui lugha, wala mtu yoyote yule, Na wala hao watu hawakujui umetokea wapi, (Label)zote zimepotea, Nini Habari yako itakua katika mji huo wa kigeni?. Hilo litakujulisha jambo moja kwamba kwenye Kwenye Ulimwengu huu Wewe umekuja huna Jina, huna Lugha, Hujui chochote, Ama kuhusu majina unapewa na Wazazi wako (Label)kama begi vile, ili ukitaka kutumwa au kusomeshwa wapate kukutambua, ikisha wanakurithisha na Lugha ili mpate kuwasiliana wanaita (Mother Tongue) vikikamilika hivyo sasa wanakupeleka (School)huko Shule ndipo unakwenda kuliwa nyama, umechunguza wewe kwamba huko (School) ndio unatumia masaa mengi kuliko nyumbani, hapo tena wanaijaza Akili yako mpaka ikijaa, wanakukabidhi kwenye Jamii ambako nako inafanyika kazi ya wewe Uishi vipi, kunaigia fujo ya kila aina mpaka unachagua kujijua na kujinata mie (Fulani) au nimetoka nchi fulani.
endelea part 2
No comments:
Post a Comment