Friday, August 31, 2018

SHAHIDI WA SHUHUDA PART 2

Asalaam Aleiykum

Ukifika hapo "Mwenye enzi Mungu" anakuzindua ili ikuondoke Ari na kiburi na jeuri ilokuingia anakukumbusha (Quraan-Hujarat aya 13).
"يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّاسُ إِنَّا خَلَقۡنَـٰكُم مِّن ذَكَرٍ۬ وَأُنثَىٰ وَجَعَلۡنَـٰكُمۡ شُعُوبً۬ا وَقَبَآٮِٕلَ لِتَعَارَفُوٓاْ‌ۚ إِنَّ أَڪۡرَمَكُمۡ عِندَ ٱللَّهِ أَتۡقَٮٰكُمۡ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ۬ "
Enyi Watu Kwa hakika tumekuumbeni(nyote) Kwa Mwanaume(Mmoja Adam)Na Mwanamke (Mmoja Hawa) Na tumekufanyieni Mataifa na Makabila(Mbali mbali) ili mjuane, Hakika ahishimiwaye sana Miongoni mwenu Mbele ya Mwenye enzi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Mwenye enzi Mungu ni mjuzi, Mwenye habari (za Mambo yote).
Naam Maneno yana mazingatio makubwa, Unajulishwa wewe ni kiumbe ima uwe mwanamke au mwanaume hapa kwenye Ulimwengu huu huna chako, vyote vimezibitiwa na Mollah wako, umekuja Ulimwenguni hapa huna hata jina, na hayo mlopewa Utaifa au huo Ukabila wako ni njia ya kukufanya mjuane, msije mkapigana vikumbo, kwa sababu nyinyi ni viumbe, Umekuja Ulimwenguni hapa hata nguo hukuvaa, hushangai pale mtoto akizaliwa anaitwa nani? (Nameless)ni Mgeni au kiumbe kilovamia Dunia hii na kime(Surrender)kiumbe hiki kuna watu wata (Take care)Basi Nakukumbusha na siku yako ya kufa pia kuna Viumbe upande wa pili wana (Take care) tena kama ulivokuja mara ya mwanzo.
Hivyo vitu ulivyo navyo ni kwa Matumizi ya (Temprory) kwenye Ulimwengu huu, Sasa unatakiwa ufanye nini khasa ikiwa hivi vyote ni vitu vya mpito, Hapo ndio inaingia Maana ya Dini. Dini Mafundisho yake utafute Ukaribu na Mollah wako, ndio inaitwa (Taqwa)lakini vipi utapata ukaribu na Mollah wako wakati hupo karibu hata kwako Mwenyewe, Kuipata (Taqwa) lazima uwe umefika katika ( A state) au hali ya Ushuhuda, sasa swali vipi unakutana na hali hiyo ya Ushuhuda, ndipo unapoambiwa Shahidi kashuhudia.
Endelea part 3

No comments:

Post a Comment