Friday, August 31, 2018

SHAHIDI WA SHUHUDA PART 3

Asalaam Aleiykum

Hapa sasa ndio tunaingia katika Muujiza wetu wa Shuhuda, Wewe Binaadamu ni (unique Being)Na katika hiyo (Being)yako ndio inapatikana (Taqwa)lakini lazima ujue au ufate (Process)zake ndio ufanikiwe, Sasa tuingie kwenye Darsa, Mnyama au Wewe nyote mkizaliwa mnapata sifa au sehemu ya kuona na kusikia, ndio maana utaona Mtoto anapita katika (Process)ya kuuliza hichi nini, yule nani, Kwa hiyo katika njia ya Shahidi anapatikana na Shuhuda.
Ntafafanua ili mpate kunifahamu, Wewe hapo ulipo ukitizama kitu unagawika mafungu mawili, mtazamaji na chenye kutizamwa, lakini huwezi kufahamu lazima kiingie cha tatu hapo, Nayo ndio hiyo Akili, kwa hiyo utaona Akili ni neema kubwa ya kuweza kutujulisha sisi hicho chenye kutizamwa ni kitu gani, ndio maana kama huna Akili utasikia lakini hujui umesikia nini, na utaona pia hujui umeona nini, Ndio maana Akili ikaitwa Neema Kubwa kutoka kwa Mollah wetu, Lakini sasa matatizo yetu tunabaki kwenye Akili, na hapo ndipo sote tuna haribikiwa, kwa sababu Akili ni yenye kukusanya Mambo na kutufundisha tu ndio kazi yake, ndio wengi tunasalia hapo, ikisha tunzunguka baina ya (Past and Future), Lakini ukizinduka utaelewa kiko kitu cha nne, tena nakwambia kwa uhakika hichi cha nne siwezi kukizungumzia sijui nini, lakini naweza kusema nimekutana nacho na miujiza yake haielezeki, ila ntakufahamisha ikiwa utanifahamu basi na wewe utafanya kazi ya kukitafuta hakiji kwa jitihada zako ila kwa Rehma za Mwenye enzi Mungu akitaka kukuonesha, na hicho ni kitu cha Nne ndio hiyo Shuhuda, ukipata hicho hutobaki kuwa Binaadamu wa kawaida maisha yako yatabadilika.
Sasa kumbuka ile aya ilotaja Mollah wako alipowaambia Malaika anataka kuumba Mwanaadamu, ikisha akamfundisha majina, rudi pale kabla ya kufundishwa, hiyo ndio (Being) yako, hapo ndipo inapoishi Taqwa, Kuna anaye tizama, kinachotizamwa ikisha inaingia Akili kutafisiri, sasa jiulize huyu wa Nne Mwenye kuyajua hayo yote nani?. ukiweza kufahamu utakua ushaingia kwenye Taqwa, na hapo ndio (Bliss)hutoki tena, na hayo ndio makaazi yako, hapo ndio nyumbani, lakini tumetoka haturudi mpaka siku ile ya kufa, ukirudi sasa hivi utakua furahani, utatoka msibani, madhila yatakupungua, dhanmbi hutendi tena, hamu zitakatika, katika hali hiyo haijui maradhi, kama vile isivojua kuzeeka, jichunguze kuna nyakati unajiona (Body) imezeeka lakini wewe bado hiyo ndio Shuhuda ipate hiyo upate Taqwa.

No comments:

Post a Comment