Asalaam Aleiykum
Nakutakieni Rehma za Mollah wangu zimiminike kwa Waislam wote, Walofunga na pia wasofunga, Yeye Mollah wetu Mlezi ni Mwenye kutupenda sote viumbe vyake. Ametukuka yule ambaye kwenye Miliki yake kuna jambo la Furaha kwa ajili ya Viumbe vyake. Nini Furaha ya Eid?. Ni kujijua kwamba umeitwa na Mollah wako na wewe ukakubali mwito huo, Furaha yenyewe imo ndani ya nafsi ya kujua kwamba umeitekeleza Ibada hii kwa Uangalifu na unyenyekevu, umejizuia na yale yote aliyoamrisha Mollah wako uyawache, na wewe kwa ridhaa yako umeyaacha na mwezi mzima ukajifunga kumuabudu Mollah wako na kumkumbuka yeye, sasa kwisha kwa huu mwezi sio ndio mwisho wa kumtii Mollah wako nini unatakiwa kufanya?.
No comments:
Post a Comment