Asalaam Aleiykum
Tunakuomba Mollah wetu tudumishe katika kukumbuka wewe, tupe mazuri kama ulivyowapa walo wema walotangulia, Tukinge na Shari za Ulimwengu, tunusuru na Balaa za maangamizo, tuondoshee dhiki za Roho, tupe Riziki za Halali, tulinde na uadui na wafanyao uwadui, tunusuru na majanga yaangamizao, tukirimu kheri zisizokua na mwisho, tumiminie neema zisizokatika, Ewe Mollah wetu tukirim tahfif kwenye Maradhi yetu, tuponeshe magonjwa makubwa na madogo, tuondoshee dhiki za Nafsi, tuondoshee hamaki na chuki, Ewe Mollah wetu tuoneshe njia za kheri ili tuzifate, tunusuru na adhabu zako za Dunia na Akhera.
Ewe Mollah wetu tusamahehe makosa yetu, tunusuru na Moto wa Jahannam, utupe Pepo yako ulotuahidi Mollah wetu. Tupunguzie Mollah wetu adhabu za kutoka Roho, tujaalie kivuli kitokacho kwako ambacho wanakipata waja wako wema, Mollah wetu zikubali Saum zetu, zipokee Ibada zetu, na utufutie makosa yetu.
Mollah wetu wasamehe walo wetu walotangulia mbele ya haki yako, waondoshee adhabu, uwakirimu msamaha wako na uwape pepo yako ya Allah. Yarabi tuongozee vizazi vyetu viwe katika waja wema, wanasuru na upotevu unozidi kuvumbuliwa, wape Elimu ya manufaa itokayo kwako wewe Mollah wetu, tujaalie kwa uwezo wako tuifunge Ramadhani yako ya mwakani kwa Radhi zako Yaa Subhanna, na kama ukituhitaji mbele ya haki basi Mollah wetu tusamahehe kwa kila Mja wako atakaesoma na asiesoma Dua hii, hakika wewe ni mueza wa kila jambo, basi tunakuomba kwa wale walozama kwenye matatizo ya madawa ya kulevya Yaa Rabbi waondoshee mtihani huo waweze kuuwepuka kwa uwezo wako, wenye mataizo ya ulevi, kamari, na majanga mengine yenye madhara ya Akili Yaa Rabbi wewe ndio Mwenye Kuwamiliki hizo Akili zao, basi tunakuomba uwageuzie ili yawaondoke mashaka hayo, wenye dhiki na umasikini waondoshee dhiki zao, na kila mwenye shida yake Yaa Rabbi Mtatulie kwa uwezo wako Mollah wetu, Tunakuomba tuwe waja wako wakaribu kwa mapenzi na Ibada na kutaka kukujua wewe na njia zako Subhanna. Amin.
No comments:
Post a Comment