Asalaam Aleiykum
Tumemaliza Mwezi wa Ramadhani kwa salama, tunamshukuru Mollah, Pia tunamuomba atukubalie Saum zetu na atusamehe makosa yetu atupe Rehma zake sisi na walotangulia mbele ya haki kwa jumla.
Hatuna budi na sisi kuendelea kukumbushana kwa njia ya darsa zetu kama kawaida, ama kwa wale walopata Ucha Mungu ndani ya Mwezi huo Mollah awajaalie kuendelea katika hali hiyo, Na kwa wale ambao pengine hawakubahatika, pengine (Yaum Shaka)imewafanya warejee kwenye mambo ya kula mchana, kwa sababu kuna baadhi wanasubiri wakisikia umeandama tu, Na wao hao wanapanada (Appolo)kurejea kwenye mambo walo yaacha mwezi wa kula mchana, Na ukirejea katika hali hiyo unaanza kujitia kwenye mateso tena ya miezi 11.
Sasa ufanye nini kuepuka hali hiyo? Ndio nimekuletea Darsa hii ya (Pepo ya Dunia) nisiseme hivyo ukaanza kuleta tafsiri zako za Maajabu, ukadhani na gawa viwanja vya pepo duniani, dhumuni langu ni kukufanya uishi kwa (Amani)na hiyo ndio maana ya (Pepo nilokusudia) Nakufahamisha vitu kama utavifanya basi dhiki katika ulimwengu huu zitaondoka kabisa, utaishi katika ile aya ya mawalii isemayo(Hawana hofu wala hawahuzuniki).
Nini ntakuonesha?, Ntakuonesha Njia ilonyooka na kama utaifata basi na wewe utabadilika na moja kwa moja utajikuta Mcha Mungu bila hata ya kufanya juhudi kubwa, nikisema bila ya juhudi kubwa usidhani kazi rahisi, kwa sababu nafahamu (Mahadith na Mawaidha)vyote hivyo vishagonga Ukuta, Mja hubadiliki, kwa hiyo kazi niloifanya mimi sio mpya ni kukupa kwa urahisi mambo ya kufanya ili uziwache njia 10 za vichochoroni ili uipate hiyo njia moja ilonyooka ambayo ndio kila Mwanadamu na katika Dini zote zinasisitiza kufatwa.
Mimi ninachofanya ni kukumbusha kwa Mpango maalum wa urahisi pengine ukikumbuka unaweza kuzifata, na ukizifata zote kwa ukamilifu(Automatic)unakua Mcha Mungu, kwani utakua huna pengine kwa kwenda isipokua kwa Mollah wako.
Ili kuipata njia hii moja ilonyooka, iliyo sawa wacha tuzitaje na kuzichukua njia moja baada ya nyengine ili ukifanikiwa kuziacha hizi kumi, utawashinda matajiri, utawaonea huruma maskini, utawacheka Marais na wale wote wenye kugaragara kutafuta umaarufu, na wewe pekee ndio utakua ni mwenye kufuzu.
Sasa kuipata hali hiyo itabidi uyaache mambo yafatayo kumi, na ni lazima uyaache yote ndio uipate hiyo pepo ya Dunia(Bliss).
Mambo hayo yote yametajwa katika Quraan na yana kuhusu wewe ambaye unayo mambo hayo, na kama huna hata moja basi wewe Mcha Mungu, wewe umo furahani. Sasa nayataja mambo hayo ili tupate kuyaacha na muhimu uyaache yote, kwa sababu nitataja na madhara yake kwa hiyo fatilia kwa makini sana.
endelea part 2.
No comments:
Post a Comment