Sunday, July 26, 2015

PEPO YA DUNIA PART 2

Asalaam Aleiykum

Mwanaadamu una mambo kumi yamekuganda yanakutesa bila wewe kujijua, yamekukamata yanakuangamiza vibaya sana, tuliza akili uyafahamu ikisha yafanye kuwa Adui wako mkubwa.
Katika Mambo hayo kumi yamegawika mafungu matatu, Fungu la mwanzo lina mambo matatu ambayo yanategemea (Mwili) wako, Fungu la Pili lina mambo manne ambayo yanategemea (Mdomo) wako, na Fungu la tatu ambalo ni la mwisho linategemea (Akili)yako.
Sasa kabla ya kuyaingia mambo haya hebu tutizame sheria ya Mwenye enzi Mungu inasemaje kuhusu ukifanya katika hayo kumi, lolote lile lazima ujue utalipwa, tuhudhurie sura ya (Luqman aya ya 16)يَـٰبُنَىَّ إِنَّہَآ إِن تَكُ مِثۡقَالَ حَبَّةٍ۬ مِّنۡ خَرۡدَلٍ۬ فَتَكُن فِى صَخۡرَةٍ أَوۡ فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ أَوۡ فِى ٱلۡأَرۡضِ يَأۡتِ بِہَا ٱللَّهُ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ۬
Ewe Mwanangu kwa hakika jambo lolote liwe japo chembe ya (Atom)hardali, likawa ndani ya Jabali au Mbinguni au katika ardhi, Mwenye enzi Mungu atalileta(Amlipe aliyefanya) bila shaka Mwenye enzi Mungu ni mjuzi wa mambo yalofichikana na yalioyo dhahiri.
Kwa hiyo tumeona chochote kile kinalipwa ndio katika sheria ya Mwenye enzi Mungu na wala huna uwezo wa kuiepuka, na katika malipo hayo ndio yanakufanya maisha yako yote yawe dhiki tupu, kwa sababu unaendelea kutenda, na kifimbo cheza kinaendelea kukuchapa, ili malipo yasite basi na wewe unatakaiwa uwache matendo yako,ubadilike kabisa, kwa hiyo sasa tunaingia katika hayo mambo tupate kuyajua na kama tukiweza kuyaacha tutaishi tukiwa na furaha Duniani hapa. Kabla ya kwenda huko nataka kurahisisha mambo kwa kutaja aya zitobeba mambo hayo kwa jumla, badala ya kutaja moja baada ya jengine.
Ama yale ya Mwanzo ya Mwili(Body) yatabebwa na aya ya 68 sura ya (Furqan).
وَٱلَّذِينَ لَا يَدۡعُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَـٰهًا ءَاخَرَ وَلَا يَقۡتُلُونَ ٱلنَّفۡسَ ٱلَّتِى حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَا يَزۡنُونَ‌ۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٲلِكَ يَلۡقَ أَثَامً۬ا
"Na Wale wasiomuomba Mungu  mwengine pamoja na Mwenye enzi Mungu, Wala hawaui Nafsi aliyoiharamisha Mwenye enzi Mungu isipokua kwa haki, Wala hawazini, na atakae fanya hayo atapata Madhara.(hapa kwenye Ulimwengu)"
Ama yale ya Pili na ya Tatu ya (Mouth)Mdomo na (Thought)Dhana hayo yanatoshwa kubebwa na aya 12 ya sura ya hujurat isemayo,
يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱجۡتَنِبُواْ كَثِيرً۬ا مِّنَ ٱلظَّنِّ إِنَّ بَعۡضَ ٱلظَّنِّ إِثۡمٌ۬‌ۖ وَلَا تَجَسَّسُواْ وَلَا يَغۡتَب بَّعۡضُكُم بَعۡضًا‌ۚ أَيُحِبُّ أَحَدُڪُمۡ أَن يَأۡڪُلَ لَحۡمَ أَخِيهِ مَيۡتً۬ا فَكَرِهۡتُمُوهُ‌ۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ تَوَّابٌ۬ رَّحِيمٌ۬ .
"Enyi Mloamini Jiepusheni sana na Dhana, kwani dhana ni dhambi, Wala msipeleleze, Wala baadhi yenu wasiwasengenye (wasiwaseme)wengine, Je mmoja wenu anapenda kula nyama ya nduguye aliyekufa, la hampendi,Na Mcheni Mwenye enzi Mungu, Mwenye enzi Mungu ni Mwenye kupokea toba (na)Mwingi wa Kurehemu."
Naam kama unaitaka Pepo ya dunia uishi katika Ulimwengu huu kwa furaha bila ya matatizo yoyote itabidi ujiandae kuyaacha mambo 10 nitakayo yataja(ili uziepuke dhanbi), na ukifanya hivyo utakua hulipi tena madeni, hakudai mtu(Huna Dhanmbi), na kama hudaiwi basi ushakua(Free) na hiyo ndio ile aya ya wanobashiriwa wale Marafiki wa Mwenye enzi Mungu kuwa watakua hawana khofu hapa Ulimwenguni na huko Akhera wanapokwenda, sasa ili ujiunge nao ndio unatakiwa uwache mambo hayo na ukiyawacha tu unapata(Bliss)unakua rafiki wa Mwenye enzi Mungu hakuna kinachokupa shida tena. Sasa tunayaingia mambo yenyewe ili uyapate kuyajua na madhara yake.
Endelea part 3


No comments:

Post a Comment