Asalaam Aleiykum
Unachotakiwa kufanya hivi sasa ni kuilinda hali hiyo ulonayo ili isikuponyoke, Sasa hivi wewe unangara Taa, basi usiruhusu kiza kikafunika kwa miezi mengine 11, jitahidi uendelee na hali hiyo ulonayo ya Ucha Mungu na hivyo ndio utakua siku zote umo ndani ya Furaha ya Eid, usiruhusu kughafilika kwa siku hizi za mwanzoni ndio maana ukapewa sunna ya (Kufunga)sita, siku saba za mwanzo zinakua ngumu kuiweka hali yako ya Ucha Mungu, vishawishi vyote vinakuvutia urejee katika hali ya zamani, kila aina ya matamanio inafunguka tena kukutizama kama kweli wewe Mcha Mungu, au unatania, basi Mwenye kuutaka Ucha Mungu na ailinde hali ya (Taqwa) ili apate kufanikiwa.
No comments:
Post a Comment