Asalaam Aleiykum
Unapokwenda Hospital jambo la mwanzo unafanyiwa uchunguzi wa vipimo ili upate kujulikana unaumwa nini, Na Mimi leo katika darsa ya leo nimekuja na (Thermometer)langu ili nipate kukupima, nipate kujua na kukujulisha jee maradhi haya ya (Mara umeusahau mara umeukumbuka)unayo?. Na kama unayo basi wakati wa kupewa dawa ya kuyaondosha ushafika.
Sasa ni kitu gani hicho mara umekisahau mara umekikumbuka, maradhi haya unaweza kuyaita kwa majina mengi, lakini nakupa (mfano)wa matatu haya ambayo yatakuwezesha kujua kama kweli umekamatwa na maradhi haya. Sasa yaite upendavyo lakini la mwanzo kabisa ni Mollah wako, halafu linafatia Uislam wako na la tatu ni huo Ucha Mungu wako, hivyo ndio vitu ambavyo (Mara unavikumbuka mara unavisahau).
Sasa wacha tuangalie kabla ya kufanya uganguzi ni vipi Maradhi haya yamekuzunguka, Tuchukue (Mfano)wa kwanza(Uislam wako)umeutizama kwa makini katika mwenendo wako wa maisha, huoni kama unalivaa na kulivua koti hilo la (Uislam),Vipi inakua hali hiyo?, Ukenda kinyume na Amri yoyote ya Mollah wako wakati ule unakua (Umeusahau Uislam wako)Mfano:Umetoa au kupokea Rushwa, Unaiba kwa Mtu au kwa Watu au Serekalini, Uzinifu, Ukijaa Chuki, Ukisema Uongo, Kutegemea Waganga, Na Mengi mengineyo ya Ufisadi wakati huo wote unakua (Mara Umeusahau) Kwanini nikasema Mara, kwa sababu Mara nyengine Unakumbuka unarejea kwa kufanya Toba ndio nikaita (Mara Unaukumbuka)Uislam wako.
Hiyo ndio hali tulonayo sote, tumo kwenye kuyumba na lengine ama niite la pili ni hili kwenye(Ucha Mungu)wako, utafanya Ibada , utakua Mtiifu, Lakini wacha upate mtihani kidogo au Mtu akukwae, jiangalie vipi unavua ngozi ya kondoo, Watu wanakushangaa mbona kageuka chui, ana nini huyu? Huyu si Mcha Mungu, mbona hataki kusaidia wenzie, mbona matusi yanamiminika, umesahau kuwa wewe wiki ilopita ulikua (Mcha Mungu), vipi wiki hii hutaki kumsamehe Mtu, hutaki kuzungumza na Mtu, na ukifikwa na Mtihani wa kukosa cheo au Mali, au kula hasara au umekosa Mke au hujaipata kazi unayoitaka, hapo ndio mama wee unatizama Mbinguni kwa hasira, uso umeukunja, sala zote za sunna unaacha(Mara Umeusahau Mara Umeukumbuka).
Na Jambo la Tatu ni hilo la Mollah wako ambaye amekufanyia hisani ya kukuumba ukiwa Muislam, kutokana na yeye ukashuhudia hapana apasaye kuabudiwa kwa haki isipokua yeye Mollah wangu Mlezi, Na kwa kila kitu changu mimi na (Surrender)Nasilimu, Nakua Muislam kwa vitendo na mwenendo wa Tabia sasa Inakuaje (Mara Unamsahau mara Unamkumbuka)?
Endelea part 2
Sunday, August 23, 2015
MARA UMEUSAHAU MARA UMEUKUMBUKA PART 2
Asalaam Aleiykum
Unasahau Kutii Amri zake, Unasahau kumkumbuka hata kwenye hiyo Sala unashindwa kumkumbuka, na hiyo ndio hali yetu sote (Isipokua wachache)sasa ikiwa wewe umo katika kundi hili la (Mara Umeusahau Mara Umeukumbuka)unatakiwa sasa ujifanyie Matibabu, Vipi yanapatikana Matibabu hayo?, Ndio nakwambia kachukue dawa kwenye (Sura ya Fussilat aya ya 30 na 31)
إِنَّ ٱلَّذِينَ قَالُواْ رَبُّنَا ٱللَّهُ ثُمَّ ٱسۡتَقَـٰمُواْ تَتَنَزَّلُ عَلَيۡهِمُ ٱلۡمَلَـٰٓٮِٕڪَةُ أَلَّا تَخَافُواْ وَلَا تَحۡزَنُواْ وَأَبۡشِرُواْ بِٱلۡجَنَّةِ ٱلَّتِى كُنتُمۡ تُوعَدُونَ
"Wale waliosema, Mollah wetu ni Mwenye enzi Mungu, kisha wakenda mwendo mzuri, hao huwateremkia Malaika(Na kuwaambia)Msiogope wala Msihuzunike na Furahini kwa pepo mliyokua mkihaidiwa"
نَحۡنُ أَوۡلِيَآؤُكُمۡ فِى ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِى ٱلۡأَخِرَةِۖ وَلَكُمۡ فِيهَا مَا تَشۡتَهِىٓ أَنفُسُكُمۡ وَلَكُمۡ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ
"Sisi ni vipenzi vyenu katika maisha ya Dunia na (Huku)Akhera, Na Humo mtapata vitu vinavyopendwa na Nafsi zenu, Na Humo mtapata mtakavyovitaka".
Kwa wale walosema Mollah wetu ndie Mlezi halafu wakafata Amri zote ziloteremshwa, basi wakisema na kukamata huo msimamo wa mwendo mzuri, upi msimamo wenyewe? wakuto kusahau amri zake, na kumkumbuka Yeye Mollah wako kwa kadir ya uwezo wako, basi cha kwanza kinachofatia unaondoshewa usahaulivu na kubaki na hali ya kukumbuka daima, kwani wakati wa kusahau ndio wakati unaotenda Dhanmbi, lakini ukiwa katika hali ya kukumbuka hutendi dhanmbi abadan, na huo ndio "Uislam" mimi na wewe hatukua na haja ya kusema kauli hiyo kwa kuwa tumezaliwa ndani ya Uislam, lakini jee tumeishi Kiislam?.
Wacha basi nikujulishe maana na kusudio ya kauli hiyo, Kauli hii inatamkwa na yoyote yule ambaye Roho yake iko tayari Ku(Surrender) ni kauli ya badiliko la (conciousness)yako kuwa sasa mimi nishagonga ukuta, hapa nilipofika basi tena, na sasa nimekubali nafata amri zote wala sitoiacha hata moja Mollah wangu, mwanzo ni umo tu ndani ya Uislam ila sasa umeamua kuwa na Imani thabit ya Kiislam.
Umeamua kuanzia sasa kutambua Kiroho kuwa Mollah wako ndio alokuumba na kuanzia sasa unamuachia kila kitu yeye ndio awe mlezi wa matokeo yake, Sasa Roho hii yenye kuona haya inafikia vipi kugundua hilo?. Inatafakari Roho yako kwa nguvu za Fikra na kuzingatia(Mfano) Ufalme wa maisha ya Vinyama, kama Ndege au Kuku umtizame kwa undani kabisa utaona hata vinyama hivyo vina Family zao, vina makaazi yao, vina tafauta riziki kama mimi, vinalisha watoto wao, na wanyama wengine wananyonyesha, Mpaka Samaki hali kadhalika,vikiumwa ndie Yeye Mollah wangu anaviponesha,Vinyama hivi vinacheza kwa Furaha, vinalala kama ninavolala, ukiona hali hiyo kwa kutumia Roho yako na siyo Akili yako,Ndio unasema vyote hivi viko kwenye Rehma, Baraka na Neema ya Mwenye enzi Mungu, Nini hali yangu mimi nilopewa uwezo wa kumjua Mollah wangu? Mbona (Mara Nimemsahau Mara Nimemkumbuka)Basi ukigundua Ufalme huo lazima ujiulize kuwa hao hawakupewa uchaguzi huu, na mimi nimepewa uchaguzi wa Ima kusahau au kuchagua kukumbuka, basi kutokana na hali hiyo sasa Mollah wangu nakuachia kila jambo langu wewe ndio uwe Muamuzi wake, Na mimi nasimama kwenye njia ilonyooka yenye haki.
Huko ndio kukiri kwa Roho(Kauli ilotajwa mwanzo wa Aya), na kuamini kwa vitendo kuwa hakuna kinachotendeka isipokua kwa uwezo wa Allah, na unatakiwa useme kwa kutumia Roho yako na sio ulimi wako, basi ukiweza kutamka katika Roho yako ukawa umenuia kuisimamia Haki, Basi hapo hapo unateremshiwa (Body Guard) Kwanini inaitwa (Bodyguard) kwa sababu dhumuni kubwa ni kuulinda huo Mwili, lakini hao wanakua wa Kibinaadamu wanalinda nje lakini (Malaika) wao wanakulinda nje na ndani, vipi wanafanya hivyo?
endelea part3
Unasahau Kutii Amri zake, Unasahau kumkumbuka hata kwenye hiyo Sala unashindwa kumkumbuka, na hiyo ndio hali yetu sote (Isipokua wachache)sasa ikiwa wewe umo katika kundi hili la (Mara Umeusahau Mara Umeukumbuka)unatakiwa sasa ujifanyie Matibabu, Vipi yanapatikana Matibabu hayo?, Ndio nakwambia kachukue dawa kwenye (Sura ya Fussilat aya ya 30 na 31)
إِنَّ ٱلَّذِينَ قَالُواْ رَبُّنَا ٱللَّهُ ثُمَّ ٱسۡتَقَـٰمُواْ تَتَنَزَّلُ عَلَيۡهِمُ ٱلۡمَلَـٰٓٮِٕڪَةُ أَلَّا تَخَافُواْ وَلَا تَحۡزَنُواْ وَأَبۡشِرُواْ بِٱلۡجَنَّةِ ٱلَّتِى كُنتُمۡ تُوعَدُونَ
"Wale waliosema, Mollah wetu ni Mwenye enzi Mungu, kisha wakenda mwendo mzuri, hao huwateremkia Malaika(Na kuwaambia)Msiogope wala Msihuzunike na Furahini kwa pepo mliyokua mkihaidiwa"
نَحۡنُ أَوۡلِيَآؤُكُمۡ فِى ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِى ٱلۡأَخِرَةِۖ وَلَكُمۡ فِيهَا مَا تَشۡتَهِىٓ أَنفُسُكُمۡ وَلَكُمۡ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ
"Sisi ni vipenzi vyenu katika maisha ya Dunia na (Huku)Akhera, Na Humo mtapata vitu vinavyopendwa na Nafsi zenu, Na Humo mtapata mtakavyovitaka".
Kwa wale walosema Mollah wetu ndie Mlezi halafu wakafata Amri zote ziloteremshwa, basi wakisema na kukamata huo msimamo wa mwendo mzuri, upi msimamo wenyewe? wakuto kusahau amri zake, na kumkumbuka Yeye Mollah wako kwa kadir ya uwezo wako, basi cha kwanza kinachofatia unaondoshewa usahaulivu na kubaki na hali ya kukumbuka daima, kwani wakati wa kusahau ndio wakati unaotenda Dhanmbi, lakini ukiwa katika hali ya kukumbuka hutendi dhanmbi abadan, na huo ndio "Uislam" mimi na wewe hatukua na haja ya kusema kauli hiyo kwa kuwa tumezaliwa ndani ya Uislam, lakini jee tumeishi Kiislam?.
Wacha basi nikujulishe maana na kusudio ya kauli hiyo, Kauli hii inatamkwa na yoyote yule ambaye Roho yake iko tayari Ku(Surrender) ni kauli ya badiliko la (conciousness)yako kuwa sasa mimi nishagonga ukuta, hapa nilipofika basi tena, na sasa nimekubali nafata amri zote wala sitoiacha hata moja Mollah wangu, mwanzo ni umo tu ndani ya Uislam ila sasa umeamua kuwa na Imani thabit ya Kiislam.
Umeamua kuanzia sasa kutambua Kiroho kuwa Mollah wako ndio alokuumba na kuanzia sasa unamuachia kila kitu yeye ndio awe mlezi wa matokeo yake, Sasa Roho hii yenye kuona haya inafikia vipi kugundua hilo?. Inatafakari Roho yako kwa nguvu za Fikra na kuzingatia(Mfano) Ufalme wa maisha ya Vinyama, kama Ndege au Kuku umtizame kwa undani kabisa utaona hata vinyama hivyo vina Family zao, vina makaazi yao, vina tafauta riziki kama mimi, vinalisha watoto wao, na wanyama wengine wananyonyesha, Mpaka Samaki hali kadhalika,vikiumwa ndie Yeye Mollah wangu anaviponesha,Vinyama hivi vinacheza kwa Furaha, vinalala kama ninavolala, ukiona hali hiyo kwa kutumia Roho yako na siyo Akili yako,Ndio unasema vyote hivi viko kwenye Rehma, Baraka na Neema ya Mwenye enzi Mungu, Nini hali yangu mimi nilopewa uwezo wa kumjua Mollah wangu? Mbona (Mara Nimemsahau Mara Nimemkumbuka)Basi ukigundua Ufalme huo lazima ujiulize kuwa hao hawakupewa uchaguzi huu, na mimi nimepewa uchaguzi wa Ima kusahau au kuchagua kukumbuka, basi kutokana na hali hiyo sasa Mollah wangu nakuachia kila jambo langu wewe ndio uwe Muamuzi wake, Na mimi nasimama kwenye njia ilonyooka yenye haki.
Huko ndio kukiri kwa Roho(Kauli ilotajwa mwanzo wa Aya), na kuamini kwa vitendo kuwa hakuna kinachotendeka isipokua kwa uwezo wa Allah, na unatakiwa useme kwa kutumia Roho yako na sio ulimi wako, basi ukiweza kutamka katika Roho yako ukawa umenuia kuisimamia Haki, Basi hapo hapo unateremshiwa (Body Guard) Kwanini inaitwa (Bodyguard) kwa sababu dhumuni kubwa ni kuulinda huo Mwili, lakini hao wanakua wa Kibinaadamu wanalinda nje lakini (Malaika) wao wanakulinda nje na ndani, vipi wanafanya hivyo?
endelea part3
MARA UMEUSAHAU MARA UMEUKUMBUKA PART 3
Asalaam Aleiykum
Imesemwa katika aya ya 31 sisi ni vipenzi vyako hapa Duniani, na huko kulindwa kwa ndani unaondoshewa khofu kwenye Akili yako, Mtu akija na (Kinyamkela chake)Shetani au Uchawi,unakingwa bila hata ya Mwenyewe kujua, habari ya utakula nini kwako haikugusi kabisa, utalala wapi vyote hivyo unaondoshewa, unakua huna khofu, hata Mauti unayakubali,unatambua wakati wangu ushafika wakurudi nyumbani.
Halafu tena unaondoshewa na hiyo huzuni, nayo ni hayo Maradhi kwenye mwili wako, kwani viwili hivi vikikukamata Mwili unaumwa, unahuzunika na huku khofu inakuingia unajiuliza ndio nakufa, kwa hiyo utaona ikatajwa kwenye aya ya 30(Unabashiriwa na Malaika wakati wa kutoka Roho usikhofu wala kuhuzunika) wewe huwaoni lakini unakhisi, vipi hisia zenyewe unazipata(Wakati inapoondoka khofu na huzuni, kinachobaki ni) (Bliss), lakini lazima upate huo msimamo wa kukumbuka daima.
Basi wacha nifunge darsa hii kwa kukupa dawa ambayo huwenda ikakusaidia kuupata huo msimamo wa kukumbuka moja kwa moja bila ya kusahau, Nini kinachotakiwa?, dawa ya kwanza kabisa ni ile ya kukumbuka, utafanya vipi? utakunya kwa siku mara moja, chukua jina la Mwenye enzi Mungu na maana yake(Kama hujui niulize)na utalitamka moyoni mwako kuanzia Sala ya alfajiri mpaka kuingia sala ya alfajiri nyengine, utayasoma majina yote 99 ya Mollah wako bila ya kukosa hata siku moja, itakuchukua miezi mitatu na siku 9, na ukiona bado hujapata huo msimamo wa kukumbuka ina maana bado unaendelea(Mara Umeusahau Mara Umeukumbuka) basi anza tena hiyo dawa na inshaallah kuna siku hutosahau tena na utakua ushafuzu, utajua Mwenyewe nini nimekusudia, utaangua kicheko kujiona umo katika hali ya kukumbuka daima, na hapo huna haja ya kutangaza na kila ukikaa utaangua kicheko cha furaha kwa kujiona hutendi dhanmbi na hapo utaigundua maana ya (Bliss) na ile tafsiri ya "Wale Walosema Hakika Mollah wetu ndie mlezi wetu", utakua unaishi Ulimwengu mwengine kabisa ambao kila Mja mwema anatarijiwa kuishi katika hali hiyo yenye furaha na afya, neema na baraka. Mollah atujaalie sote katika hilo.
Imesemwa katika aya ya 31 sisi ni vipenzi vyako hapa Duniani, na huko kulindwa kwa ndani unaondoshewa khofu kwenye Akili yako, Mtu akija na (Kinyamkela chake)Shetani au Uchawi,unakingwa bila hata ya Mwenyewe kujua, habari ya utakula nini kwako haikugusi kabisa, utalala wapi vyote hivyo unaondoshewa, unakua huna khofu, hata Mauti unayakubali,unatambua wakati wangu ushafika wakurudi nyumbani.
Halafu tena unaondoshewa na hiyo huzuni, nayo ni hayo Maradhi kwenye mwili wako, kwani viwili hivi vikikukamata Mwili unaumwa, unahuzunika na huku khofu inakuingia unajiuliza ndio nakufa, kwa hiyo utaona ikatajwa kwenye aya ya 30(Unabashiriwa na Malaika wakati wa kutoka Roho usikhofu wala kuhuzunika) wewe huwaoni lakini unakhisi, vipi hisia zenyewe unazipata(Wakati inapoondoka khofu na huzuni, kinachobaki ni) (Bliss), lakini lazima upate huo msimamo wa kukumbuka daima.
Basi wacha nifunge darsa hii kwa kukupa dawa ambayo huwenda ikakusaidia kuupata huo msimamo wa kukumbuka moja kwa moja bila ya kusahau, Nini kinachotakiwa?, dawa ya kwanza kabisa ni ile ya kukumbuka, utafanya vipi? utakunya kwa siku mara moja, chukua jina la Mwenye enzi Mungu na maana yake(Kama hujui niulize)na utalitamka moyoni mwako kuanzia Sala ya alfajiri mpaka kuingia sala ya alfajiri nyengine, utayasoma majina yote 99 ya Mollah wako bila ya kukosa hata siku moja, itakuchukua miezi mitatu na siku 9, na ukiona bado hujapata huo msimamo wa kukumbuka ina maana bado unaendelea(Mara Umeusahau Mara Umeukumbuka) basi anza tena hiyo dawa na inshaallah kuna siku hutosahau tena na utakua ushafuzu, utajua Mwenyewe nini nimekusudia, utaangua kicheko kujiona umo katika hali ya kukumbuka daima, na hapo huna haja ya kutangaza na kila ukikaa utaangua kicheko cha furaha kwa kujiona hutendi dhanmbi na hapo utaigundua maana ya (Bliss) na ile tafsiri ya "Wale Walosema Hakika Mollah wetu ndie mlezi wetu", utakua unaishi Ulimwengu mwengine kabisa ambao kila Mja mwema anatarijiwa kuishi katika hali hiyo yenye furaha na afya, neema na baraka. Mollah atujaalie sote katika hilo.
Sunday, August 9, 2015
ZAWADI KUTOKA MBINGUNI PART 1
Asalaam Aleiykum
Mwenye enzi Mungu ni mwenye kumimina Zawadi za kila aina kwa waje wake, ziko nyingi kubwa na ndogo za kila aina, lakini leo nataka kuzizungumza hizi tatu zenye kumfanya Mwanaadamu awe furahani, awe kila saa na dakika yumo kwenye hicho kitu kiitwacho (Bliss) ikiwa ataweza kuyapata mambo matatu haya kwa pamoja. basi atakua Mwenye kufuzu kuliko kukubwa,
Mambo yenyewe ni "Mapenzi", "Imani", na "Huruma".
Nikiangalia Jamii wakati huu tulo nao yananijaa masikitiko moyoni kuona sio watu wengi wenye kuzipata neema hizo tatu zilizo muhimu, Nini kimetokezea?.
Naweza kuhadithia lakini siwezi kufanya tathmin ya mambo yalivo haribika katika kipindi kifupi cha miaka 40 ilopita, Sisi tuloshuhudia mwisho mwisho tulikuta bado japo kwa uchache "Mapenzi, Imani na Huruma"zimo kwenye nyoyo za watu, Na ulikua ukiwauliza walikua hawana jawabu la kukupa, isipokua wanakujibu tulishikana, tulikua kama ndugu, tukisaidiana, tukipendana, hilo ndio lilikua jawabu lao.
Ukumbuke uzuri enzi hizo elimu ya Dini ilikua haipatikani kirahisi, si watu wengi walokua wakisoma madrsa au kusikiliza mawaidha, sasa nini kilikuwepo wakati huo?. Kilokuwepo wakati huo ni hicho kitu kiitwacho "Imani", Na huwezi kujua kama kilikuwepo mpaka uisome aya hii iliyomo kwenye sura ya (Hujurat aya ya 14)
قَالَتِ ٱلۡأَعۡرَابُ ءَامَنَّاۖ قُل لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ وَلَـٰكِن قُولُوٓاْ أَسۡلَمۡنَا وَلَمَّا يَدۡخُلِ ٱلۡإِيمَـٰنُ فِى قُلُوبِكُمۡۖ وَإِن تُطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُ ۥ لَا يَلِتۡكُم مِّنۡ أَعۡمَـٰلِكُمۡ شَيۡـًٔاۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ۬ رَّحِيمٌ
"Walisema Waarab (Wanokaa jangwani)tumeamini, sema (Uwaambie)hamjaamini, lakini semeni tumesilimu, maana Imani haijaingia vyema nyoyoni mwenu bado. Na mkimtii Mwenye enzi Mungu na Mtume wake, hatakupunguzieni chochote katika vitendo vyenu(Thawabu), kwa yakini Mwenye enzi Mungu ni mwingi wa kusamehe na Mwingi wa kurehemu."
Katika mtizamo wa aya hiyo inaonekana Kusilimu kuna kuja mwanzo(Surrender) na ukisilimu tu unapewa zawadi itokayo Mbinguni nazo ni moja katika hizo tatu(Na ukiona huna katika hizo tatu basi jijue huja Surrender)Nawauliza baadhi ya Masheikh, hivyo wewe Sheikh mzima hebu nipe ukweli mbona naona tabia zako zina Mushkeli, hivyo katika matatu hayo kuna chochote kilichotokezea katika nafsi yako, Jawabu hakuna, utawaona Masheikh mawaidha makali, maneno mengi lakini hajawahi katika nafsi yake kupata Mapenzi, Imani wala Huruma, hao ndio Masheikh wana hali gani Maamuma?.
Naam wakati huo ulopita ndio ulokua wakati wa hizo (Bidda hassan)zimekithiri, ulikua wakati wa (Madhikiri, wakati wa Maulid, wakati wa Mahitima, wakati wa Manyiradi) wakati huo ndio ule watu walofungamana na Hadith sahihi ya Bwana Mtume s.a.w ilosema "Yoyote yule atakae leta jambo zuri katika Uislam atapata ujira wake kwa jambo hilo". Nimefurahi hivi karibuni kuwasikia wanazuoni Wakubwa wa Kiislam kwenye Baraza la Eid lilofanyika Abu Dhabi wametoa wito au (Fatwa) wakitaka turejee kwenye zile zama za (Bidda hassan), kuliko kubakia kwenye nakama na Moto tulo nao hivi sasa wa uharibifu wa Dini hii ya Kiislam, Makala hiyo iloandikwa kwenye (AP-na Yahoo tarehe 19 July ninayo au mtu anaweza kufatilia akasoma mwenyewe).
Naam Tunaendelea na Darsa yetu ya kutaka kuelewa wapi vitu vitatu hivi vinatokea, tunajikumbusha zama zilopita watu wakiwa wame(Surrender) walipata zawadi gani kutoka mbinguni?.
Endelea part 2
Mwenye enzi Mungu ni mwenye kumimina Zawadi za kila aina kwa waje wake, ziko nyingi kubwa na ndogo za kila aina, lakini leo nataka kuzizungumza hizi tatu zenye kumfanya Mwanaadamu awe furahani, awe kila saa na dakika yumo kwenye hicho kitu kiitwacho (Bliss) ikiwa ataweza kuyapata mambo matatu haya kwa pamoja. basi atakua Mwenye kufuzu kuliko kukubwa,
Mambo yenyewe ni "Mapenzi", "Imani", na "Huruma".
Nikiangalia Jamii wakati huu tulo nao yananijaa masikitiko moyoni kuona sio watu wengi wenye kuzipata neema hizo tatu zilizo muhimu, Nini kimetokezea?.
Naweza kuhadithia lakini siwezi kufanya tathmin ya mambo yalivo haribika katika kipindi kifupi cha miaka 40 ilopita, Sisi tuloshuhudia mwisho mwisho tulikuta bado japo kwa uchache "Mapenzi, Imani na Huruma"zimo kwenye nyoyo za watu, Na ulikua ukiwauliza walikua hawana jawabu la kukupa, isipokua wanakujibu tulishikana, tulikua kama ndugu, tukisaidiana, tukipendana, hilo ndio lilikua jawabu lao.
Ukumbuke uzuri enzi hizo elimu ya Dini ilikua haipatikani kirahisi, si watu wengi walokua wakisoma madrsa au kusikiliza mawaidha, sasa nini kilikuwepo wakati huo?. Kilokuwepo wakati huo ni hicho kitu kiitwacho "Imani", Na huwezi kujua kama kilikuwepo mpaka uisome aya hii iliyomo kwenye sura ya (Hujurat aya ya 14)
قَالَتِ ٱلۡأَعۡرَابُ ءَامَنَّاۖ قُل لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ وَلَـٰكِن قُولُوٓاْ أَسۡلَمۡنَا وَلَمَّا يَدۡخُلِ ٱلۡإِيمَـٰنُ فِى قُلُوبِكُمۡۖ وَإِن تُطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُ ۥ لَا يَلِتۡكُم مِّنۡ أَعۡمَـٰلِكُمۡ شَيۡـًٔاۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ۬ رَّحِيمٌ
"Walisema Waarab (Wanokaa jangwani)tumeamini, sema (Uwaambie)hamjaamini, lakini semeni tumesilimu, maana Imani haijaingia vyema nyoyoni mwenu bado. Na mkimtii Mwenye enzi Mungu na Mtume wake, hatakupunguzieni chochote katika vitendo vyenu(Thawabu), kwa yakini Mwenye enzi Mungu ni mwingi wa kusamehe na Mwingi wa kurehemu."
Katika mtizamo wa aya hiyo inaonekana Kusilimu kuna kuja mwanzo(Surrender) na ukisilimu tu unapewa zawadi itokayo Mbinguni nazo ni moja katika hizo tatu(Na ukiona huna katika hizo tatu basi jijue huja Surrender)Nawauliza baadhi ya Masheikh, hivyo wewe Sheikh mzima hebu nipe ukweli mbona naona tabia zako zina Mushkeli, hivyo katika matatu hayo kuna chochote kilichotokezea katika nafsi yako, Jawabu hakuna, utawaona Masheikh mawaidha makali, maneno mengi lakini hajawahi katika nafsi yake kupata Mapenzi, Imani wala Huruma, hao ndio Masheikh wana hali gani Maamuma?.
Naam wakati huo ulopita ndio ulokua wakati wa hizo (Bidda hassan)zimekithiri, ulikua wakati wa (Madhikiri, wakati wa Maulid, wakati wa Mahitima, wakati wa Manyiradi) wakati huo ndio ule watu walofungamana na Hadith sahihi ya Bwana Mtume s.a.w ilosema "Yoyote yule atakae leta jambo zuri katika Uislam atapata ujira wake kwa jambo hilo". Nimefurahi hivi karibuni kuwasikia wanazuoni Wakubwa wa Kiislam kwenye Baraza la Eid lilofanyika Abu Dhabi wametoa wito au (Fatwa) wakitaka turejee kwenye zile zama za (Bidda hassan), kuliko kubakia kwenye nakama na Moto tulo nao hivi sasa wa uharibifu wa Dini hii ya Kiislam, Makala hiyo iloandikwa kwenye (AP-na Yahoo tarehe 19 July ninayo au mtu anaweza kufatilia akasoma mwenyewe).
Naam Tunaendelea na Darsa yetu ya kutaka kuelewa wapi vitu vitatu hivi vinatokea, tunajikumbusha zama zilopita watu wakiwa wame(Surrender) walipata zawadi gani kutoka mbinguni?.
Endelea part 2
ZAWADI KUTOKA MBINGUNI PART 2
Asalaam Aleiykum
Katika zama hizo kulikua hakuna magonvi ya dini wala madhehebu, Hakuna ubaguzi huyu Mkiristo au huyu Baniani au yule nani, nakumbuka mpaka vijana wa Kikiristo walikua wakila halua misikitini mwetu, sisi tukisoma vitabu vyao na wao wakisoma vitabu vyetu, tulikua hatujui hata maana ya madhehebu ndio nini?.
Tukiona wazee wetu wakichanganyika na watu wa kila aina, wakishirikiana katika kila jambo, Watu walikua wame (Surrender) mambo na hukumu zote wamemuachia Mollah Muumbaji, Heshima na adabu zikitawala wakati huo, Watu walikua wakijizuia na Machafu na Uzinifu, Na ukijizuia na Uzinifu unakua unaondosha jambo la (Sex) kutoka chini na linakwenda juu kwenye Akili(Mind)na kugeuka (Romantic), ndio maana utaona Watu wa zamani Nyimbo zao, Mashairi vyote vizuri mpaka lugha yao ilikua na (Romancy) ndani yake.
Sasa wacha tuanze Darsa yetu kukijua nini kilotokea baada ya hapo hata mambo yakenda (Wrong) au kuharibika. Kilotokea baada ya hapo hakielezeki kwa maneno matupu, amekuja (Ibilis) na kutuonesha Mti wa elimu, akatwambia mkila tunda lake mtakua wasomi, Naam tukaonja tunda lile na ndio lilipotufikisha hapa tulipo leo, jambo la kwanza tulolifanya ni kuondosha yale yote yalo wafanya Umma wa wakati huo (Usilimu) au (Surrender).
Haijambo wazee wetu waliridhia matakwa ya Mwenye enzi Mungu, wakapata kitu tunaweza kuita (Romantic way of life), Sasa nini tulopata sisi tulosoma, elimu zetu zimetupeleka kuondosha yale yote yalokua yamewafunga na kuwalea Umma hizo zilopita, nini kimetokezea?, Hakuna tulichokipata ila ni (Split Mind) mgawanyiko wa Akili, ukiacha kufungumana na Mollah wako unapata mambo haya mawili ima werevu wako na Elimu usoijua itakupanda juu ikupe kiburi, au itashuka chini ikusahaulishe Mollah wako na igeuke (Sexually), ndio maana unaona sasa tumegawika makundi mawili .
Kundi la kwanza limejifunga kwenye (Sex) na kundi la pili limejifunga kwenye (Disturb Mind) na kujiona wao ndio wako (Perfect) katika mahusiano na Mwenye enzi Mungu wao, yote hayo ni matatizo na mashaka makubwa, maradhi yameingia kwa wenye kufata dini na wenye kuendekeza dunia, sijui nani ato mtibu mwenzie. Kwa sababu Mwanaadamu akijifunga kwenye (Ngono)basi Maisha yake yanakua sawa na mnyama, mnyama hana mapenzi inakua tafauti yako wewe unajificha na mnyama anafanya hadharani, lakini huko kujificha kwako kunakua kimwili(Body) lakini kwenye Akili(Mind)unakua kama Mnyama, ukilishiriki jambo hilo kila kitu kinaondoshwa unakua huna Mapenzi, Imani wala Huruma.
Na hili kundi letu sisi wenye kujifanya tuna funguo za Pepo na kutoa Hukumu ndio tunamilikiwa na chuki na (Confused Mind) tunaanza kupata (Haluccination) huyu ndie huyu sie, tunapata ugonjwa wa Kiburi hatujui nini Mapenzi, nini Imani na nini Huruma. Vipi leo uwe Mtu wa Dini halafu uwe katili, huoni kama sote tunateseka, ndio mwisho tunaishia kujidhuru wenyewe au kuwadhuru watu wengine wasio na hatia.
Swali la kujiuliza mbona huko nyuma hayakuwepo mambo haya katika Ulingo wa Dini?.Kwanini tuteseke?, hivo hakuna njia nyengine za kujivua kwenye mateso haya?, jawabu njia nyengine ipo nayo ni kujitahidi uyapate mambo haya matatu"Mapenzi""Imani"na "Huruma" utakua umepata zawadi itokayo Mbinguni na hutoteseka tena.
Endelea part 3
Katika zama hizo kulikua hakuna magonvi ya dini wala madhehebu, Hakuna ubaguzi huyu Mkiristo au huyu Baniani au yule nani, nakumbuka mpaka vijana wa Kikiristo walikua wakila halua misikitini mwetu, sisi tukisoma vitabu vyao na wao wakisoma vitabu vyetu, tulikua hatujui hata maana ya madhehebu ndio nini?.
Tukiona wazee wetu wakichanganyika na watu wa kila aina, wakishirikiana katika kila jambo, Watu walikua wame (Surrender) mambo na hukumu zote wamemuachia Mollah Muumbaji, Heshima na adabu zikitawala wakati huo, Watu walikua wakijizuia na Machafu na Uzinifu, Na ukijizuia na Uzinifu unakua unaondosha jambo la (Sex) kutoka chini na linakwenda juu kwenye Akili(Mind)na kugeuka (Romantic), ndio maana utaona Watu wa zamani Nyimbo zao, Mashairi vyote vizuri mpaka lugha yao ilikua na (Romancy) ndani yake.
Sasa wacha tuanze Darsa yetu kukijua nini kilotokea baada ya hapo hata mambo yakenda (Wrong) au kuharibika. Kilotokea baada ya hapo hakielezeki kwa maneno matupu, amekuja (Ibilis) na kutuonesha Mti wa elimu, akatwambia mkila tunda lake mtakua wasomi, Naam tukaonja tunda lile na ndio lilipotufikisha hapa tulipo leo, jambo la kwanza tulolifanya ni kuondosha yale yote yalo wafanya Umma wa wakati huo (Usilimu) au (Surrender).
Haijambo wazee wetu waliridhia matakwa ya Mwenye enzi Mungu, wakapata kitu tunaweza kuita (Romantic way of life), Sasa nini tulopata sisi tulosoma, elimu zetu zimetupeleka kuondosha yale yote yalokua yamewafunga na kuwalea Umma hizo zilopita, nini kimetokezea?, Hakuna tulichokipata ila ni (Split Mind) mgawanyiko wa Akili, ukiacha kufungumana na Mollah wako unapata mambo haya mawili ima werevu wako na Elimu usoijua itakupanda juu ikupe kiburi, au itashuka chini ikusahaulishe Mollah wako na igeuke (Sexually), ndio maana unaona sasa tumegawika makundi mawili .
Kundi la kwanza limejifunga kwenye (Sex) na kundi la pili limejifunga kwenye (Disturb Mind) na kujiona wao ndio wako (Perfect) katika mahusiano na Mwenye enzi Mungu wao, yote hayo ni matatizo na mashaka makubwa, maradhi yameingia kwa wenye kufata dini na wenye kuendekeza dunia, sijui nani ato mtibu mwenzie. Kwa sababu Mwanaadamu akijifunga kwenye (Ngono)basi Maisha yake yanakua sawa na mnyama, mnyama hana mapenzi inakua tafauti yako wewe unajificha na mnyama anafanya hadharani, lakini huko kujificha kwako kunakua kimwili(Body) lakini kwenye Akili(Mind)unakua kama Mnyama, ukilishiriki jambo hilo kila kitu kinaondoshwa unakua huna Mapenzi, Imani wala Huruma.
Na hili kundi letu sisi wenye kujifanya tuna funguo za Pepo na kutoa Hukumu ndio tunamilikiwa na chuki na (Confused Mind) tunaanza kupata (Haluccination) huyu ndie huyu sie, tunapata ugonjwa wa Kiburi hatujui nini Mapenzi, nini Imani na nini Huruma. Vipi leo uwe Mtu wa Dini halafu uwe katili, huoni kama sote tunateseka, ndio mwisho tunaishia kujidhuru wenyewe au kuwadhuru watu wengine wasio na hatia.
Swali la kujiuliza mbona huko nyuma hayakuwepo mambo haya katika Ulingo wa Dini?.Kwanini tuteseke?, hivo hakuna njia nyengine za kujivua kwenye mateso haya?, jawabu njia nyengine ipo nayo ni kujitahidi uyapate mambo haya matatu"Mapenzi""Imani"na "Huruma" utakua umepata zawadi itokayo Mbinguni na hutoteseka tena.
Endelea part 3
ZAWADI KUTOKA MBINGUNI PART 3
Asalaam Aleiykum
Cha Msingi kama walivosema hao Wanazuoni turejee kwenye zama zilopita kwenye Mapenzi, Imani, na Huruma. Mwenye Enzi Mungu anasema katika sura ya (Anfal aya ya 53).
ذَٲلِكَ بِأَنَّ ٱللَّهَ لَمۡ يَكُ مُغَيِّرً۬ا نِّعۡمَةً أَنۡعَمَهَا عَلَىٰ قَوۡمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُواْ مَا بِأَنفُسِہِمۡۙ وَأَنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ۬
"Hayo ni kwa sababu Mwenye enzi Mungu habadilishi kabisa neema alizowaneemesha watu, hata wabadilishe wao yaliyomo nyoyoni mwao, Na hakika Mwenye enzi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kulijua kila (Jambo)".
Na kweli tumebadilisha kila kitu kwenye Ulimwengu wa leo,
Tizama kwenye nyoyo yako kiko nini?, kama umeshika Dini basi umejaa chuki, ghadhabu na ukatili, na kama umeshika Dunia basi ni (sex) wizi, dhuluma hakuna jengine ama uko pembeni ya kushoto au katikati ya kushoto lakini mwiko kwako kuwepo upande wa kulia.
neema ndio zimeondoshwa, hakuna tena neema ya mapenzi wala imani au huruma. Sasa ukitaka kubadilika lazima ujue nini Mapenzi, na yanatokea wapi?.
Quraan (Al-Room aya ya 21)
وَمِنۡ ءَايَـٰتِهِۦۤ أَنۡ خَلَقَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٲجً۬ا لِّتَسۡكُنُوٓاْ إِلَيۡهَا وَجَعَلَ بَيۡنَڪُم مَّوَدَّةً۬ وَرَحۡمَةًۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَـٰتٍ۬ لِّقَوۡمٍ۬ يَتَفَكَّرُونَ
"Na katika ishara zake nikuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsi yenu ili mupate utulivu kwao, na amejaalia mapenzi na huruma baina yenu, bila shaka katika haya zimo ishara kwa watu wanaofikiri".
Lazima uwe Mtu Mwenye kufikiri vipi utayapata mapenzi, na kwanini kitu hicho kitajwe kuwa utulivu, sababu kama huna mapenzi unateseka ndio nikaita(Split Mind)Mchafu koge. Na Bila shaka zimo ishara, ishara zenyewe lazima utulie, ndio utaona nini raha ya mapenzi, nini faida ya huruma, na nini busara za Imani, ukiweza kuyajua hayo unaweza kurudi kama zamani, au ukaishi na mazuri yaliyokuweko wakati huo.
Kama tulivo ona katika hiyo (Aya) kuwa mapenzi yanatokea kwa Mwenyewe Muumba wa Mbingu na Ardhi, kuna kitu kinatokea ndani ya (Ufalme wa Uhai wako)unaoitwa(Being),Kitu hichi mapenzi,huruma na imani hakipatikani kwa ukamilifu mpaka utimize masharti yake, utajiuliza masharti gani hayo?. Kwa kifupi ni (Taqwa) Kwa lugha ya mzunguko ni uwe (Pure)huna chuki au hamaki, sio (corrupted)na mambo yoyote machafu au dhuluma, kusema uongo, uzinifu na kiburi, (au soma darsa ya pepo ya dunia katika yale mambo 10 niloyataja uyawache)ukiwa huna vitu hivyo ndio Mollah wako anakuteremshia zawadi yake kutoka Mbinguni nayo ni hiyo (Tatu kwa moja).
Matatizo yanatokea unapoamua kujichafua na kugawanya hiyo zawadi na kuifanya ya mafungu tafauti, Mapenzi yakishuka huwa yanakuja (Full pack) ndio ikasemwa kama utakua Mja mwema ukatulia ukawa hufanyi machafu yoyote basi ukioa au kuolewa moja kwa moja unateremshiwa zawadi hii ya mapenzi.
Sasa Mapenzi yanatokea wakati gani?
Wakati ule Akili(Mind)inapokutana na (Heart)Moyo, kwanini nikaitaja Akili mwanzo kwa sababu Akili ni ngumu sana kukiri, mpaka ikakubali kushuka chini na kukutana na moyo hapo ndio inapatikana hiyo (Surrender)unakua (Muslim + Muumin) kwa wakati mmoja, unatokezea mripuko wa wewe kupotea, na penzi pekee kutawala maisha yako. Basi neema ilioje ikiwa wawili nyie mepata kupokea hiyo zawadi kwa pamoja, Hakika huyu anamuona mwenzie (Lulu Maknoon) na wewe unamuona mwenzio (Mukhaladun) mnapotea kabisa katika Ulimwengu huu na kuishi Ulimwengu mwengine kabisa, basi nini habari yetu sisi ikiwa viwili hivyo yaani Moyo na Akili vikiungana na hicho kitu cha tatu ambacho ni Roho, hapo kinazaliwa kitu kipya kabisa, inapatikana sasa (Unity). Mapenzi yanabebwa na Moyo, Imani inabebwa na Akili, na huruma inabebwa na Roho vikiungana vitatu hivyo au ukipata nafasi kuviunganisha basi hapo hapo matatizo yote yanakwisha.
Unakua mtu wa aina nyengine kabisa, tamaa inapotea kabisa katika maisha yako, unakua maridhia,unampenda kila mtu, na watu wanakupenda isipokua wale wenye matatizo, wao watakushangaa lakini wewe Mwenyewe unajua nini kimetokea ila unakua huna amri katika hiyo (Unity) ilotokezea, hapo tena Sala zako zinabadilika, Maisha yako yanabadilika, Unapata Nuru, na hiyo Nuru huwa inamurika kila mtu kwa mapenzi yako, kwa ukarimu wako, kwa huruma zako, kwa usaidizi wako, kwa usafi wako wa nafsi, pamoja na Ucha Mungu wako, na wala husubiri tena mpaka ufe ndio uombewe kaburi lako litiwe nuru, ukipata zawadi hiyo ndiyo ushapata chanzo cha Afya na Furaha ya maisha ya Duniani na Akhera.
Hapo tena Mapenzi yako yanakua ya aina nyengine kabisa unabadilika kukipenda kile kisicho onekana na hiyo ndio Imani, Na pia unageuka kuvipenda vyote vyenye kuonekana na hiyo ndio Huruma na yote hayo mzizi wake ni mapenzi na huo ndio Ucha Mungu na ndio Mwenendo wa kila mwenye kuifata Dini ya haki.
Cha Msingi kama walivosema hao Wanazuoni turejee kwenye zama zilopita kwenye Mapenzi, Imani, na Huruma. Mwenye Enzi Mungu anasema katika sura ya (Anfal aya ya 53).
ذَٲلِكَ بِأَنَّ ٱللَّهَ لَمۡ يَكُ مُغَيِّرً۬ا نِّعۡمَةً أَنۡعَمَهَا عَلَىٰ قَوۡمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُواْ مَا بِأَنفُسِہِمۡۙ وَأَنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ۬
"Hayo ni kwa sababu Mwenye enzi Mungu habadilishi kabisa neema alizowaneemesha watu, hata wabadilishe wao yaliyomo nyoyoni mwao, Na hakika Mwenye enzi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kulijua kila (Jambo)".
Na kweli tumebadilisha kila kitu kwenye Ulimwengu wa leo,
Tizama kwenye nyoyo yako kiko nini?, kama umeshika Dini basi umejaa chuki, ghadhabu na ukatili, na kama umeshika Dunia basi ni (sex) wizi, dhuluma hakuna jengine ama uko pembeni ya kushoto au katikati ya kushoto lakini mwiko kwako kuwepo upande wa kulia.
neema ndio zimeondoshwa, hakuna tena neema ya mapenzi wala imani au huruma. Sasa ukitaka kubadilika lazima ujue nini Mapenzi, na yanatokea wapi?.
Quraan (Al-Room aya ya 21)
وَمِنۡ ءَايَـٰتِهِۦۤ أَنۡ خَلَقَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٲجً۬ا لِّتَسۡكُنُوٓاْ إِلَيۡهَا وَجَعَلَ بَيۡنَڪُم مَّوَدَّةً۬ وَرَحۡمَةًۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَـٰتٍ۬ لِّقَوۡمٍ۬ يَتَفَكَّرُونَ
"Na katika ishara zake nikuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsi yenu ili mupate utulivu kwao, na amejaalia mapenzi na huruma baina yenu, bila shaka katika haya zimo ishara kwa watu wanaofikiri".
Lazima uwe Mtu Mwenye kufikiri vipi utayapata mapenzi, na kwanini kitu hicho kitajwe kuwa utulivu, sababu kama huna mapenzi unateseka ndio nikaita(Split Mind)Mchafu koge. Na Bila shaka zimo ishara, ishara zenyewe lazima utulie, ndio utaona nini raha ya mapenzi, nini faida ya huruma, na nini busara za Imani, ukiweza kuyajua hayo unaweza kurudi kama zamani, au ukaishi na mazuri yaliyokuweko wakati huo.
Kama tulivo ona katika hiyo (Aya) kuwa mapenzi yanatokea kwa Mwenyewe Muumba wa Mbingu na Ardhi, kuna kitu kinatokea ndani ya (Ufalme wa Uhai wako)unaoitwa(Being),Kitu hichi mapenzi,huruma na imani hakipatikani kwa ukamilifu mpaka utimize masharti yake, utajiuliza masharti gani hayo?. Kwa kifupi ni (Taqwa) Kwa lugha ya mzunguko ni uwe (Pure)huna chuki au hamaki, sio (corrupted)na mambo yoyote machafu au dhuluma, kusema uongo, uzinifu na kiburi, (au soma darsa ya pepo ya dunia katika yale mambo 10 niloyataja uyawache)ukiwa huna vitu hivyo ndio Mollah wako anakuteremshia zawadi yake kutoka Mbinguni nayo ni hiyo (Tatu kwa moja).
Matatizo yanatokea unapoamua kujichafua na kugawanya hiyo zawadi na kuifanya ya mafungu tafauti, Mapenzi yakishuka huwa yanakuja (Full pack) ndio ikasemwa kama utakua Mja mwema ukatulia ukawa hufanyi machafu yoyote basi ukioa au kuolewa moja kwa moja unateremshiwa zawadi hii ya mapenzi.
Sasa Mapenzi yanatokea wakati gani?
Wakati ule Akili(Mind)inapokutana na (Heart)Moyo, kwanini nikaitaja Akili mwanzo kwa sababu Akili ni ngumu sana kukiri, mpaka ikakubali kushuka chini na kukutana na moyo hapo ndio inapatikana hiyo (Surrender)unakua (Muslim + Muumin) kwa wakati mmoja, unatokezea mripuko wa wewe kupotea, na penzi pekee kutawala maisha yako. Basi neema ilioje ikiwa wawili nyie mepata kupokea hiyo zawadi kwa pamoja, Hakika huyu anamuona mwenzie (Lulu Maknoon) na wewe unamuona mwenzio (Mukhaladun) mnapotea kabisa katika Ulimwengu huu na kuishi Ulimwengu mwengine kabisa, basi nini habari yetu sisi ikiwa viwili hivyo yaani Moyo na Akili vikiungana na hicho kitu cha tatu ambacho ni Roho, hapo kinazaliwa kitu kipya kabisa, inapatikana sasa (Unity). Mapenzi yanabebwa na Moyo, Imani inabebwa na Akili, na huruma inabebwa na Roho vikiungana vitatu hivyo au ukipata nafasi kuviunganisha basi hapo hapo matatizo yote yanakwisha.
Unakua mtu wa aina nyengine kabisa, tamaa inapotea kabisa katika maisha yako, unakua maridhia,unampenda kila mtu, na watu wanakupenda isipokua wale wenye matatizo, wao watakushangaa lakini wewe Mwenyewe unajua nini kimetokea ila unakua huna amri katika hiyo (Unity) ilotokezea, hapo tena Sala zako zinabadilika, Maisha yako yanabadilika, Unapata Nuru, na hiyo Nuru huwa inamurika kila mtu kwa mapenzi yako, kwa ukarimu wako, kwa huruma zako, kwa usaidizi wako, kwa usafi wako wa nafsi, pamoja na Ucha Mungu wako, na wala husubiri tena mpaka ufe ndio uombewe kaburi lako litiwe nuru, ukipata zawadi hiyo ndiyo ushapata chanzo cha Afya na Furaha ya maisha ya Duniani na Akhera.
Hapo tena Mapenzi yako yanakua ya aina nyengine kabisa unabadilika kukipenda kile kisicho onekana na hiyo ndio Imani, Na pia unageuka kuvipenda vyote vyenye kuonekana na hiyo ndio Huruma na yote hayo mzizi wake ni mapenzi na huo ndio Ucha Mungu na ndio Mwenendo wa kila mwenye kuifata Dini ya haki.
Subscribe to:
Posts (Atom)