Saturday, February 27, 2016

KISOMO CHA AROBAINI(40) PART 2

Asalaam Aleiykum

Naam, Tumemuusia mwanadamu kuhusu wazee wake wawili, wasia huu umetokea wapi? Wasia huu unapewa kwa njia ya ufunuo, ni neema ya fahamu(Knowing) inokujia mara tu unapofikia Umri fulani, na hususan una shikana sana na Mama yako kutokana na ile (Bond) yako ya kukaa tumboni mwake kwa muda wa miezi (9) Mama yako kachukua Mimba hiyo kwa Tabu na misukosuko mizito, kwa vile (Body Chemical)yake inavobadilika kutokana na kukubeba wewe ndio Mara katamani (Mbirimbi) mara anaomba apewe(Udongo)siku katamani (Papa)alooza na kesho lazima apewe achari ya (Ndimu) na Tafrani zikizidi anaomba bora aletewe (Mavi ya Kuku)yatamsaidia kukata kichefuchefu, hivyo ndivyo Mama anavoteseka kwa ajili yako, na wewe uko (Bukheir)umetulia tumboni.
Tumboni huko kila kitu unafanyiwa, Mpaka pumzi unavutiwa. Huku nje Mama yako mzigo unamtesa takriban kwa muda wa miezi tisa, leo ukiombwa (Shilingi unakunja Uso)Tahadhari sana, ikisha zinafatia pirika za kuushusha mzigo, Machungu na dhiki anazozipata ndio kila kitu kinachafuka, mpaka Roho yake inatetemeka kwa juhudi za kukuzaa wewe.
Sasa Nini Arobaini? Arobaini kwa njia ya maneno ni Kisomo cha mzee yule kutoa Shukurani kwa kuvuka Salama kwenye (Daraja). Lakini zile siku zenyewe za Arobaini ndizo zilobeba maana ya hiyo (40).Wazee wenye Elimu ya Hisabati waligundua kwamba (Number 4)ni Namba ilobeba Furaha, Walipoichunguza sifuri(Zero O)wakagundua imejaa (Nothingness), Nikisema (Nothing) Nakusudia Nini?, Nakusudia Sifuri Peke yake inakua imetulia haina kitu, haina papara, haina thamani lakini imebeba kitu kikubwa chenye hazina ya utulivu, Kumbuka kwenye utulivu ndiko kwenye kutokea kila kitu.
Sifuri mpaka ikatulia ndio inaleta maana ya (Full circle)kukamilika, ndio maana utaona kwenye masahihisho ya Mitihani Mwanafunzi anatiliwa (Zero) unajua maana ya (Zero) Zero maana yake Mwanafunzi hajafahamu, baada ya jitihada zetu zote za kumsomesha tumeshindwa kumtoa kwenye Kiza (Sifuri)kumpeleka kwenye Nuru, kwa hiyo kwa ufupi sifuri inabeba utulivu na kwa Mwanafunzi ina maanisha hakushughulika au kuchangamsha Akili yake kuwa (Active)katika kusoma, lakini kwenye (Currency) ikiongezwa (Zero) mambo yanakua mengine, hesabu zinabadilika, au mfano mwengine mwanzo ulikua huna kitu(Sifuri)sasa umetajirika(From nothing to something) hayo ndio maelezo ya sifuri kwa ufupi ukitumia njia ya maneno.
Tumeizungumza Number 4 na number Zero O sifuri tumeziunganisha tumepata Arobaini(40)ndani yake tumepata Furaha na Utulivu, Ama Arobaini kwa vitendo siri yake ni Utulivu, inachukua siku Arobaini Roho na Mwili(Body)kuwa (Stable)kutulizana katika harakati za kimaumbile. Vipi?
Tuanze na Mama, Imetajwa kuwa anabeba Mimba kwa Tabu na anazaa kwa Tabu, (Chemical)Mwilini zinachafuka, Roho inatikisika, kila kitu kwenye mwili wa huyo Mama kinapepesuka, Akili inakua katika msukosuko mkubwa, hali hii inachukua siku (40) mambo hayo yote kutulia. Ndio maana wazee wetu wa (Africa) wakawa wanawapumzisha wazazi kwa siku (40) hapo zamani, na kama hajapumzika ndio siku hizi imegundulika anapata kitu kinaitwa(Post Natal depression).
Ndio Maana kama mzazi hajapumzika baadae matatizo yanajitokeza, Mara utasikia chumbani kabeba mtoto anambembeleza mwanae mwenyewe mara unasikia "Ntamtupa chini"kumbe maskini ana tafrani za Akili, Wenzetu wameligundua hilo wanawapa watu wao matibabu, lakini katika jamii yetu toka tulipoondosha Arobaini tumekula hasara, ndio utasikia Mke wangu toka kazaa kabadilika, kumbe Mtu ana Tafrani za (Mind) yake hapati msaada, hujamsaidia, maskini ana hangaika hajui afanye nini, Hiyo ndio Arobaini kwa Mama, Nini Habari ya Arobaini kwa Mtoto? Hapa kuna Siri itabidi uijue!!
Endelea Part 3

No comments:

Post a Comment