Saturday, February 27, 2016

KISOMO CHA AROBAINI(40) PART 3

Asalaam Aleiykum

Pata habari hii ili iweze kukusaidia katika safari yako ya kujitambua wewe nani?, Umetokea wapi?, Na unakwenda wapi?.
niliposema ijue siri nilikusudia kukufahamisha (Daraja)lenye kuunganisha (Body)Mwili wako na Roho yako.Daraja lenyewe ni hiyo (Hewa)yako unayovuta yaani (Oxygen)Nyuma ya hiyo (Oxygen)ndio kuna hiyo Roho(Nisiseme nyuma ukaanza kufasiri nyuma ya ukuta, nyuma ya kichwa)nimetumia neno hilo kuashiria jambo ambalo pengine utaligundua ukishajitambua (wewe nani).
Sasa inapoungana Roho hiyo na (Body)ndio inaitwa Uhai, Na ikiachana na huo Mwili inarejea katika hali yake ya mwanzo Mauti na baina yake ndio kuna kitu kinaitwa(Life)au kuishi milele, Tafauti ya viwili hivyo kimoja kinaoza(Body)na cha Pili (Roho) ni yenye kubaki daima(Eternal).
Sasa hivi huwezi kutafautisha lakini kuna wakati au siku ya kufa kwako ndio utakuja kujua alaa kumbe mimi sio (Body) ila mimi ni ile Roho ilokua ikizungumzwa, wakati huo unatenganishwa na (Body)wakati huo utaona (body)yako kumbe mimi nilikua miaka yote (70)nikiishi kwenye nyumba ile(Body), Naam ndio maana utakuta kitu cha mwanzo mtoto akizaliwa anatizamwa jee anavuta pumzi(Daraja analo)kalia japo kidogo, katoa sauti huyu, lakini kinachotizamwa zaidi ni (Breath)Pumzi au hiyo(Oxygen), Mtoto huyu anaweza kuhema Mwenyewe.
Na vilevile siku ya kufa kwako wanakuja kutizama jee kashabomoa (Daraja)huyu, tegemeo zima la Uhai ni hiyo (Hewa)ndio yenye kusema bado nipo au nishatoweka(Daraja lishavunjika)na sasa niko upande wa pili. 
Ama kuhusiana na huyo Mtoto mpaka daraja kuwa madhubuti yaani (Chemical) zake kutulia inachukua siku hizo (40). Wacha sasa tukuguse wewe Mtu mzima(Baba au Mama la Miraba saba)wewe umehusiana vipi na hii (40). Tumeona kwa Mama ni kitulizo, Kwa Mtoto ni ku(Solidify with the Body), Sasa kwako wewe vile vile ni kama ulivopewa taarifa kwenye hiyo (aya) nilotaja mwanzo, unapofika Umri wa miaka (40)unategemea utulie, (Unaondoshewa Dhamana)mpaka hapa sasa ukiendelea itakua ni jeuri, Sasa hivi huna sababu tena za kukufanya uendelee kucheza, (Nature)inakusuta(Chemical)zishatulia, ujana ushatoweka, nikisema ujana ushatoweka itabidi nifafanue kidogo, kwenye (Bible)kuna msemo huu (Three scores and ten)maana ya (score) ni kumi mbili, kwa hiyo (score) maana yake ni (20) kwa hiyo (Score)tatu ni sitini(60)na ile kumi ndio unapata (70), kwa hiyo kama umefika miaka (40)ina maana ushakula nusu na ushei hivi(Score)Mbili, umebakisha hiyo (30) tu, hata nusu huna tena.
Mwanzo vitu vyote vilikua vinakwenda (North) na sasa vinashuka (South)wakati unazidi kukuacha, ikiwa bado hujazinduka unaendelea kukera mbinguni na huku ardhini unaendelea kutia wanaadamu tafrani, watu wakikuona wanasema Baba yake fulani bado hajatulia, ukijikuta katika hali hiyo ndio unatakiwa ujisomee mwenyewe kisomo cha Arobaini ili upate kuzinduka.
Arobaini maana yake zinduka, kuwa na Furaha ya maisha na utulie, sasa turejee kwenye Tafsiri. 
Inaendelea aya ya (15)sura ya (Ahqaf)kwa kusema."Hata anapofikia Umri wa miaka (40)husema(Mja Mwema)Niwezeshe" Limetumika neno niwezeshe, ili uondoshewe jeuri ya kuji nasib kuwa kila kitu umefanya kwa uwezo wako, umepata kwa nguvu zako, "Niwezeshe nishukuru Neema zako ulizo ni neemesha" Neema hazihesabiki, (Pengine umenipa neema kuwa wazee wangu wa hai na afya zao)umenipa mali na watoto. Sasa wakati huu nilofikia niwezeshe nifanye matendo mazuri unayoyapenda, Na pia sasa nishapata watoto basi naomba kama ulivo niongoza mimi kwenye kheri, na Wanangu Mollah wangu niongozee, Na mimi  sasa natubu kwenye Enzi yako Mollah wangu, na kwako wewe na (Surrender)na kuwa Muislam kamili.
Hiyo ndio Arobaini kwa mtu mzima, unatakiwa utulie uwache ulo nayo ya ufisadi, balaa na mijidhanbi ili upate kuwa Muislam kamili. Na ukifa pia Imani zetu zina matumaini kuwa baada ya siku arobaini Roho yako ndio imepata utulivu na sisi huku tunasoma na kukuombea dua upate Shufaa kutoka kwa Mollah wako, akipokea Mollah wetu sawa na kama hakupokea pia hiyo ni uwezo wa khiyari yake. Hiyo ndio maana ya Kisomo cha Arobaini kwa hiyo watu wakisoma huna sababu ya kuwashangaa au kuwakataza tena, Kwani wanaomba dua na kumshukuru Mollah wao.

No comments:

Post a Comment