Saturday, February 27, 2016

KISOMO CHA AROBAINI(40) PART1

Asalaam Aleiykum

Nini Arobaini? Arobaini ni nne ilofungana na sifuri, kwa wale walo bahatika kupata elimu ya hisabati wanajua nini maana ya number 4, lakini inapofatiwa na sifuri maana yote ya number 4 inabadilika, kwanini ikabadilika itabidi uhudhurie siri ya sifuri ili ujue kwanini inabadilika, sifuri siri yake ni kama daraja(Bridge)yenye kuunganisha kisicho kuwepo kukifanya kiwepo, kukionesha kilichojificha kiweze kuonekana, sifuri ni kama kiza kipo lakini hakionekani, inapotiwa sifuri ndio hesabu zinabadilika.
Leo tuko katika kisomo cha Arobaini, tunachambua uwepo wa kisomo hichi na maana yake, kwanini kikaletwa? Jee kina maana gani katika mazingira ya (Dini) kwanza kabisa napenda uelewe kisomo cha Arobaini ni sehemu ya (Dua) ya wewe kutoa Shukurani zako kwa Mollah wako, kama ilivotajwa kwenye sura ya (Al-Ahqaf)aya ya 15.

وَوَصَّيۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ بِوَٲلِدَيۡهِ إِحۡسَـٰنًا‌ۖ حَمَلَتۡهُ أُمُّهُ ۥ كُرۡهً۬ا وَوَضَعَتۡهُ كُرۡهً۬ا‌ۖ وَحَمۡلُهُ ۥ وَفِصَـٰلُهُ ۥ ثَلَـٰثُونَ شَہۡرًا‌ۚ حَتَّىٰٓ إِذَا بَلَغَ أَشُدَّهُ ۥ وَبَلَغَ أَرۡبَعِينَ سَنَةً۬ قَالَ رَبِّ أَوۡزِعۡنِىٓ أَنۡ أَشۡكُرَ نِعۡمَتَكَ ٱلَّتِىٓ أَنۡعَمۡتَ عَلَىَّ وَعَلَىٰ وَٲلِدَىَّ وَأَنۡ أَعۡمَلَ صَـٰلِحً۬ا تَرۡضَٮٰهُ وَأَصۡلِحۡ لِى فِى ذُرِّيَّتِىٓ‌ۖ إِنِّى تُبۡتُ إِلَيۡكَ وَإِنِّى مِنَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ 
Na tumemuusia Mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake, Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu na akamzaa kwa taabu, Na kubeba (Huko)Mimba yake hata kumuwachisha ziwa(kipimo chake)ni miezi thalathini, hata anapofikia baleghe yake na akawa Mwenye Umri wa miaka Arobaini(Alo Mwema)husema "Ewe Mollah wangu niwezeshe nishukuru neema zako ulizo nineemesha mimi na wazazi wangu, Na niwezeshe nifanye vitendo vizuri unavyo vipenda, Na unitengenezee watoto wangu, kwa yakini nina tubu kwako, Na hakika mimi ni miongoni mwa waliosilimu(Wenye kunyenyekea kwako).
Hiyo ndio Arobaini maneno yaliyomo kwenye aya hii moja ni maneno mazito na mimi nitafanya kazi ya kuyanyanyua kidogo kidogo ili tupate kuyafikisha kwenye kilele cha vichwa vyetu, umo kwenye kisomo cha Arobaini usisimame ukapinga tu bila yakua na taaluma yoyote, kwanza zama ukiona hakuna faida basi una uhuru wa kupinga.
Aya inaanza kwa wasia, Tumemuusia Mwanadamu kuhusu Wazazi wake wawili(Baba na Mama) Hususan Mama, kwanini ikawa Mama? Na Wasia huu umepewa Lini?. Yapitie maandiko haya labda yaweza kuwa na faida na wewe, Unaweza kugundua maana ya kuachiwa Radhi, ukaelewa kumbe nikienda kinyume na Wasia wa Mwenye enzi Mungu basi huenda nikakosa Radhi za Wazee wangu.
endelea part 2

No comments:

Post a Comment