Saturday, December 15, 2018

DALILI ZA KURUDI PEPONI PART 1

Asalaam Aleiykum

Zanzibar kuna msemo zamani ukitumika unasema "kavunja ukuta wa watu kwa harufu ya chakula kitamu". Maneno mazito yameficha maana kubwa yenye mazingatio kwa wenye uwezo wa kufikiri.
neno la mwanzo kabisa limetumika kuvunja ukuta,, inatuonesha lazima mvunjaji alikua na bidii, kafanya jitihada kubwa mpaka kuweza kuuvunja Ukuta, Ukuta wenyewe siwake, na sababu gani ilomfanya avunje?, Ni harufu tu ya chakula kitamu, swali kakijuaje kama chakula kitamu, hapo inaashiria kuwa lazima kawahi kukila chakula hicho ndio maana alivosikia tu harufu yake akaamua kuuvunja ukuta wa watu.
Ikiwa Ukuta Umevunjwa kwa ajili ya harufu ya chakula kitamu tu, hapo inaonesha mvunjaji lazima kashawahi kukionja chakula ndio maana akachukua juhudi za kuuvunja Ukuta huo, Basi katika hali kama hiyo na sisi Binaadamu tunatakiwa tufanye juhudi za kuuvunja Ukuta wa Shetani ili tupate kurudi peponi. Nikisema kuingia peponi ntakua nimekosea katika lugha ya kitaalamu iloambatana na ufahamu, lugha sahihi ya kutumika ni kurejea Peponi, kwa sababu Jinsi yetu kila Mmoja kashaonja Pepo, kilichotufanya tusahau ni kazi ya Shetani ambayo anaendelea kutusahaulisha kwamba hapo mwanzo alitutoa Peponi, Sasa nini kinachotufanya tuikumbuke Pepo?.
Endelea Part 2

No comments:

Post a Comment