Aslm alekum Kwa hiyo guo la mwanzo ni Miti (Wood) ndio maana utakuta mti unaviashiria vya (Uhai) Kama vile kunywa maji na kadhalika, na guo la pili ni huo mwili wako ambao baada ya muda unakufa na kuuwacha ukazikwa, Ndio maana kwenye aya ya (187)Sura ya (Baqarah)Ilipitolewa Ruhusa ya kukutana kimwili na wake zenu usiku wa Ramadhani ikasemwa "Wake zenu ni nguo kwenu na nyie ni nguo kwao", Nataka Uelewe (Body)Yako ndio inokutana na mwenzako, ndio maana katika Uislam mnaamrishwa mkimaliza kukutana mkakoge kabla ya kufanya Ibada, Kwa sababu hiyo (Body)yako ni vazi la Ucha Mungu usilipeleke wakati hujakua (Tohara) sio msafi, Ndio Bwana Mtume s.a.w "Akasema Nusu ya mwanzo ni kuoa na nusu ya pili ni Kumcha Mungu.
Naam ukiyapata yote Mawili basi umekamilisha Dini, Sasa nini Ndoa ? Neno lilotumika kwa (Arabic ni Zawj)Ni sehemu moja ya (Pair) Ni wajibu wako kutafuta ile sehemu ya pili kukamilisha hiyo (Pair) Kwani ni kama (Viatu) Huwezi kukivaa kimoja lazima upate cha pili ndio utaweza kutembea vizuri, Wajibu wako kumtafuta (Soulmate) wako ambaye mtaishi pamoja kwenye Ulimwengu huu.
Huyo mwenza ni Roho nyinyi mloandikiwa mkutane na Mollah karim ili muishi kwa furaha na msaikilizano pale mtakapo kamilisha muungano wenu, Ndoa haina maana pekee ya mume na mke , ina maana ya upeo yakua huyo ni mwenzio mwenza Mollah alokukutanisha nae ili muwe pamoja, hakutaka Mollah wako uishi maisha ya upweke au peke yako, Na kumbuka kama ulivoambiwa ndoa ni kama mfano wa nguo hakikisha ina kaa vizuri kwenye (Body) yako ikikubana itakukera na ikipwaya itakuvuka kwa hiyo hakikisha inakaa sawa na kuku(Fit).
Ndoa ni kwa yule Atoridhi Roho yako na kuishi vizuri na wewe kwenye maisha haya, Pia iliposemwa Mke na mume ni kama nguo ilikua na maana nguo inakustiri , inaziba mapungufu yako, nguo ni kitu cha karibu kwenye (Body)yako, kwa hiyo ni lazima kihifadhi kasoro zako, Mke au Mume Mwenye mapenzi anahifadhi siri zako, Analinda heshima yako. Mume au Mke sio mtu ambaye Ana kununulia Maua tu, Mume ni Mtu ambaye ni mizani kwako wewe ni lazima mpate (Balance)Kwenye mizani yenu ya maisha, Kila kitu chenu kiwe kimoja, mawazo yenu yawe yanalingana, tafauti zenu ziwe zinayayuka kama barafu ilokutana na jua, mmoja akiwa juu basi mwengine akubali kujishusha na kuwa chini katika masikilizano, Quraan ilipomwita mume na Mke hakiua na maana ya cheo cha sheria ilikua inawaelekeza wawili nyie kusaidiana, kwa yale ambayo mwenzio atakua na mapungufu nayo, Ndoa sio kumtawala Mtu na kumfanya kama mali yako, Ndoa ni kipimo cha nusu kwa nusu kwenye kibaba cha mapenzi baina ya wawili nyie, Kwa hiyo kumbuka unapoitwa Mume wewe hujatimia peke yako mpaka apatikane mkeo ndio uwe kamili, Katika lugha ya kiarabu (Zawj)Haina maana (Spouse)Ina maana ni sehemu ya nusu ya mwenzio, bila ya mwenzio wewe hujatimia , kwenye ndoa umeambiwa ni sehemu ya kupumzika upate utulivu kwa mwenzio(Litaskun ilahiya) Haina maana utapata mbora katimia, hana doa laa ni sehemu ya kupata (Rest)Kupumzika kwa ukamilifu kutokana na mashaka yote ya Ulimwengu. 2
No comments:
Post a Comment