Wednesday, January 7, 2026

WASIA WA NDOA

 Aslm alekum.  


Ukitaka ndoa ya uhakika yenye kheri sio ujitukuze Mwenyewe, Ufanye mambo peke yako, Uwe (Selfish)Hichi changu hichi chako hapo tayari ushaigawa ndoa, Usijitukuze peke yako hili nimefanya mimi, Watoto nimelea peke yangu, hizi ni mali zangu, ndoa ni kusaidiana , mkisimama mnasimama pamoja na mkianguka mnaanguka pamoja, kwenye ndoa lazima iwepo njia ya kusameheana, kuombana radhi na kuepuka mambo yanayo karibisha kuchafua ndoa, na kubwa la mwanzo katika hayo ni kukaribisha mtu wa tatu ambaye ni kimada, Kwanini ndoa ina haribika kwa sababu Roho inaona hususan ya Mwanamke, Ndio maana utaona Mwanamke Analia na Na Mwanamme anahuzunika unajua kwanini?, 



Kwa Sababu ikumbuke aya ya Mwenye enzi Mungu wewe ndio guo lake na yeye ni guo lake, Sasa vipi leo unakwenda kumchafulia guo lake, kwenye (Level) ya kiroho anapata habari kuwa sasa unacheza, ama hisi guo umerudi nalo chafu, kumbuka jambo moja mnapokutana Mke na mume kimwili Mollah kakujaalieni Maji tu mnasafika, Lakini ukiingiliana na Mwanamke wa Nje Uchafu unabakia (Wamefanya utafiti) na kugundua (DNA) yako inabakia kwa miezi kadhaa ndani ya guo lako na huyo mwengine, kama mtapimwa basi yatakutwa mahusiano yenu kwamba mlifanya tendo la maingiliano baina yenu, Ikiwa (Forensic science) Inakukamata ni habari yetu sisi kwa Mollah wetu, na maisha yetu ya ndoa hapo ndio kinaanza kifimbo cheza kutokea Mbinguni, hapa Ulimwenguni si hamfati sheria hampigani mijeledi 80, nini kinafatia unaanza kupigwa kwa Nakama, 


Yanaanza Maugonvi, Upungufu wa mali, matatizo ya Riziki, kwenye Nyumba hakuna utulivu, Pesa sasa haikai, kazi haipatikani, Machafuko mengi kwenye ndoa yenu na la mwisho mapenzi hayo yanakimbia. 


Naam lakini ukisikiliza Maneno ya Bwana Mtume s.a.w anakwambia nusu ya kwanza funga ndoa, halafu nusu ya pili mpende Mwenye enzi Mungu kwa Ibada na kumkumbuka nini kinatokea?, 


Mapenzi kama (Mirror) kioo ukijitizama unajiona ukipenda utapendwa na Mollah wako ndio hapo inatimia Ahadi yake ya kukushushia Mapenzi na Rehema zake zitokazo kwake Napenda uelewe kuna vitu viwili hata ukivitafuta huvipati ila vinakutafuta wewe kwa time yake, vitu hivyo ni Mapenzi na kifo, Hata ufanye nini huna uwezo nao isipokua atake Mwenye enzi Mungu, Ukimpenda Mungu ukafanya Mema basi Mollah anakuteremshia Mapenzi unampenda mkeo na mkeo anakupenda mapenzi makubwa mpaka nyote mnajiuliza hichi nini? 


Mbona kama layla na majnu, uko njiani unatamani chakula fulani ukirudi nyumbani unakuta hicho ndio kapika mambo yanakushangaza kila saa na dakika unajikuta umezama mapenzini, na hiyo ndio furaha ya dunia, furaha ndio afya ya mapenzi, hapo tena zina zidi kushuka Rehma na baraka nyingi nyingi kutoka kwa Mollah wenu Karim mnakua ndani ya (Bliss)Na maisha yanakwenda vizuri, mnaongezewa kizazi,, mnapewa riziki kwa wingi. Kuyapata yote hayo lazima mzijue siri ya maisha ndoa na kanuni zake kama vile kutobishana mbele za watu, kuwa wavumilivu, kuleta subra kwenye migogoro, umpende mkeo kiroho na awe rafiki yako, epukeni kubishana mbele za watu, himizaneni kwa njia ya upole kufanya ibada, msiambieni uongo, usimtukanie wazee wake na watu wake, tumia lugha nzuri, usiwe na wivu wakufikiri, na Inshaalah Mwenye enzi Mungu atakujaalieni Maisha ya Furaha.3

No comments:

Post a Comment