Monday, June 18, 2012
DAWA YA DHANBI (SOMA UTAPOA)PART 1
By-Abdulla Baja
Asalaam-aleikum.
Limekuja swali, muulizaji anasema, Sheikh mimi nina matatizo kwanza nasumbuliwa moyoni mwangu halafu nina mashaka na aya ya quraan,mimi nasimamisha sala tano kipindi hakinipiti, mambo yote ya kheri mimi nipo mstari wa mbele, lakini matatizo yangu yanakuja katika swala la wanawake wananisumbua sana, siwezi kuacha vitendo hivi vya haramu, halafu tena mimi nafanya kazi serekalini watu wanapokuja nawasaidia sana, nikimaliza hunipa zawadi kwa msaada wangu, hayo ndio matatizo yangu, sasa mushkeli wangu unakuja katika hii aya inosema(hakika ya sala inakuepusha na mambo machafu na mabaya yanochukiza)sasa mimi najitahidi kusali lakini siachi vitendo viovu,nipe maarifa nini kimenisibu.
Kwanza kabisa jawabu lako ni rahisi lakini maelezo yake ni magumu, ama kuhusu jawabu lako kuwa unasali vipindi vitano havikupiti jijue huna sala hujawahi kupata sala.
Sasa tuje kwenye maelezo yake na uchambuzi, Kwanini huipati hiyo sala? sijibu mimi, inajibu aya katika Quraan sura ya (muumin-aya-1-2)anasemaje huyo mwenyewe mwenye kukubali hizo sala."قَدۡ أَفۡلَحَ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ (١) ٱلَّذِينَ هُمۡ فِى صَلَاتِہِمۡ خَـٰشِعُونَ (٢) "wamefuzu"(wamepata-wamefanikiwa)"wale ambao katika sala zao wanaleta unyenyekevu.
Haiwezekani kabisa maneno ya Mollah wako yakawa na khitilafu ndani yake, haitokei kabisa kukawa na batili ndani yake, pengine mja labda hujui nini huo unyenyekevu? hujawahi kufanya unenyekevu au moyo ushakufa haukai unyenyekevu, umo katika kupata dawa usijali dawa kakupa nani, wewe chukua ujaribu asaa yaweza kukuponesha, pengine watu wakuona wewe Sheikh mkubwa au Maalim mwenye elimu iso na mfano lakini maskini hujawahi kupata sala.
Sasa inakuwaje huo unyenyekevu, isikudanganye (hali ya nje)sijui watu wanakuona wewe mtu wa msimamo ibada hazikupiti, kumbe maskini moyoni wewe fakiri mkubwa ndani huna kitu hujawahi kukutana na Mollah wako."umeisoma ile hadith inosema muabudu Mollah wako kama unamuona", Huo ndio unyenyekevu unotakiwa, Iwe ukiingia katika Sala unaingia kwa mapenzi makubwa na kama huwezi mapenzi basi uingie kwa (ghushui)hofu ya aina gani? unakumbuka ulivokua mtoto umefanya kosa, ukiambiwa utasemewa kwa mzee wako hali yako inavokua(khofu na mtetemko)ulopata, Au sasa hivi umeshakua mtu mzima ukiambiwa chukua hii mihadarati(madawa ya kulevya) uipitishe(Uwanja wa ndege)unavokua ile khofu na mtetemeko unokupata umeambiwa maneno tu, basi yale ni maneno unakua katia hali hiyo,(na mifano iko mingi)z jee nini hali yako wewe yakwenda kukutana na Mollah wako, jee jiulize unapata hisia za (unyenyekevu na utiifu na mapenzi na hofu)ya kukutana na mollah wako, jee unaingia katika kila
Sala katika hali kama hiyo. Sio utegemee unakwenda kwenye Sala
umebeba makapo ya maudhi kichwani mwako halafu utaraji juu yake uipate hio Sala.
Elewa sala ina mafungu matatu(3)la kwanza mahusiano ya viungo, la pili mahudhurio yako kiroho, na la tatu faida zake baada ya hiyo sala.Na hapo ndio inaingia hiyo aya(Hakika sala inakuepusha na machafu na mambo ya munkari)lazima sala yako iwe kama alivosema:Mshairi;"Nilipogundua mimi ndani ya moyo wangu anakaa asokua wewe, nilifanya jitihada ya kuweka uongofu ulotoka kwako, mpaka ikawa hakai katika moyo wangu asokua wewe.Sasa ukiingia ndani ya hiyo sala kwa mifano niloitaja hapo juu, basi tambua hata ukimaliza kusali hisia hizo zinaendelea kuwepo, unyenyekevu huo unaendelea kuwepo sala hadi sala, hapo tena ndipo inaanza kukuepusha na kila maovu na machafu na mambo ya kipuuzi.Hivi ndivo muumin unavotakiwa kusimamisha sala, isije ikawa siku zote kazi yako kusindikiza watu wanosali na ikawa unasubiri wanosali wakipewa zawadi, wewe unasubiri ziwadondoke ili upate japo moja, fanya jitihada na wewe uwe kati ya hao wanosimamisha Sala.
Sasa ikiwa sala haifanyi kazi, ndio huipati, unaendelea kutenda dhanbi, sasa unahitaji dawa na dawa zipo za aina nyingi, bahari ya dawa ni kubwa, mwengine anaweza kuchota kigamboni, na mwengine akachota mangapwani, lakini bahari ni moja(sehemu ya kuchota hiyo dawa)ndio tafauti, kwa hiyo zisikushike ghaddhabu kwanini Sheikh wako kakupa dawa nyengine na mimi nakupa nyengine. Sasa kachukue dawa kwenye toleo la pili.
Mollah wangu anajua zaidi.
A.baja
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment