Monday, June 18, 2012
DAWA YA DHANBI (SOMA UTAPOA)PART 2
By-Abdulla Baja
Asalaam-Aleikum
Napenda uelewe hakuna utajiri anopata mwanaadamu hapa duniani na akhera kama kusimamisha sala na kumuabudu Mollah wake kikamilifu, watu watakua na majumba ya kifahari na magari makubwa makubwa, lakini wewe ukipata sala basi umewashinda kwa kila kitu katika ulimwengu huu, utaona watu wamefurahi nje tuu lakini mashaka walokua nayo ndani ya nafsi mfano kama milima, lakini wewe ulopata sala ni tajiri wa (kiroho)hakuna kufilisika, ndani unacheka na nje unacheka hiyo ndio siri ya Sala, huku ndiko kupewa furaha hapa ulimwenguni na huko akhera.
Mwanaadamu ni kiumbe alobahatika kwani amepewa uwezo wa kuziona dhanbi zake, simba anaua lakini hajui kama anaua yeye anafahamu kile ni chakula, lakini mwanaadamu ana uwezo wa kutokuua na kutafuta chakula kingine hiyo ndio sifa ya mwanaadamu anafahamu kila kitendo chake, ndio maana akatambua dhanbi zimemganda. Sasa tunataka uthibitisho wa jambo hili ndani ya Quraan jee sisi tuna uwezo huu?. بَلِ ٱلۡإِنسَـٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٌ۬ ( وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُ
"Bali mwanaadamu ni mwenye kuiona nafsi yake(Anajua)" Japo analeta udhuru".
Vipi kuona huku na inakuaje?inakua hivi kwani ukifumba macho sasa hivi unaweza ukasafiri ukarudi iwe Pemba au Zanzibar au Daresalaam, na hivyo ndio inavokua unapotaka kutenda maovu(shari)au kheri unaona katika nafsi yako, unamsubiri mtu aondoke umsengenye, au anakuja kukuletea rushwa, au umepangana nae miadi ya kutenda zinaa, kila kitu unajua (in advance) sasa inakuaje ushajua hili ni kosa na unaendelea kutenda. Nini kinatokea hapa?, katika Gap hiyo ndogo ndipo anapoingia (SHETANI-IBILIS) kwa sababu ukibakia umacho mpaka mwisho hutendi kosa, utashtuka(utamuabudu Mollah wako hutotaka kumuasi) lazima ulale ukushike usingizi (hypnotism)hapo ndio Ibilis anafanya kazi yake, vipi anafanya hiyo kazi, wewe mwenyewe chunguza isiwe mimi nasema na wewe unakubali fanya uchunguzi, anafanya vipi, kwanza anakusahaulisha, ikisha anakutia nguvu hakuna chochote, halafu anakuhadaa unakua huna kizuizi. tizama wewe mwenyewe ikiwa mwanamme au mwanamke(akija mtu wako humuoni
yule mtu-hukumbuki kama ile Dhanbi)ila unaona mapambo yake,pengine unazama kwenye figa yake au
unakumbushwa vitu vyengine kabisa, au mtu ndio anakuletea rushwa tizama humkumbuki yule mtu bali unakumbuka kaja nazo, ngapi? atanipa vipi, au ikiwa kazi yako kusema watu unasubiri yule mtu ataondoka saa ngapi umzungumze, akizidi kukaa anakukera, hapo shetani ndio anakua kesha tawala chunguza mambo mengi kama hayo kuna kitu kinakulaza kitafute hasa kitu hichi kitu gani(mie nimekupa mifano michache), ndio maana utaona shetani hendi kwa mlevi kwa sababu yule keshajilaza mwenyewe, yeye anakutakeni nyinyi mnofikicha macho na kujitia mko macho. Sasa hapa ndio unahitaji dawa, hapa unahitaji msaada, pengine unakula mali ya Msikiti, au unadhulumu jamii, labda mali ya yatima wewe ndio huwezi kuikosa, au uzinifu ndio starehe yako kuubwa tena unaringa kwa idadi ya ulowapata, ukijiona mambo ya ufisadi kama hayo yamekuzunguka basi jijue wewe mgonjwa na kabla ya kupelekwa kwenye operesheni basi jaribu dawa hii.
Naam dawa yenyewe sharti lake usije ukasoma kama nyimbo mdomoni mwako, au fikira zako ziko kwengine ni lazima uwe hufikiri chochote wakati unasoma dawa hii, Utasoma mara tatu, kumbuka kabla ya kufanya hilo tendo lako labda kupokea rushwa, au kumsema mtu, au kumtukana mtu, kumbuka kabla hujaanza kwanza soma(aya hii sura ya Anbiyaa-aya ya 87)"وَذَا ٱلنُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَـٰضِبً۬ا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقۡدِرَ عَلَيۡهِ فَنَادَىٰ فِى ٱلظُّلُمَـٰتِ أَن لَّآ إِلَـٰهَ إِلَّآ أَنتَ سُبۡحَـٰنَكَ إِنِّى ڪُنتُ مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ"
(Na Dha-Nun, (Nabii yunus)alipondoka hali yakua ameghadhibika, akadhani labda hatutokuwa na uwezo juu yake, basi aliita akiwemo kwenye giza, hapana Mollah isipokuwa wewe Subhanna, Hakika mimi nilikuwa katika wenye kudhulumu)
Sasa wewe huna haja ya kuisema aya nzima, ila tumia neno alotumia Nabii Yunus a.s, alosema (LAA-ILLAH-ANTA-SUBHANNAKA-INNIY-KUNTU-MINNA-DHAALIMINA)kumbuka kabla ya kutenda hilo kosa,ndi usome dawa hii, sasa nini kinatokezea nitakupa kwa undani japo kidogo hicho kinotokezea, Kwa sababu umelala umo gizani, nini neno hili tukufu linafanya katika nafsi yako, kidogo kidogo linasafisha moyo wako ,kidogo kidogo unaanza kupata nuru na hiyo nuru iking'ara katika moyo wako basi, mapesa yatakua mbele yako huna haja nayo, wanawake au wanaume wako mbele yako huna haja nao, utakua humsemi mtu, hutaki mambo ya watu, hufanyi dhuluma ya aina yoyote utaridhika na ulokua nacho hapo unakua mweupe, na ukianza kuwa mweupe basi Sala inapatika bila ya taabu, bila ya vishindo, unaweza kujikuta umesimama mbele ya Mollah wako machozi yanakutoka (Mbele ya matuka-Sabur)hujijui kwanini, unajuta kwa uliyoyatenda zamani. Hapo unakua ushatoka gizani umeokoka kama aya ya (88)ya sura
hiyo hiyo, Inavomalizia (Hakika na
hvi ndivo tunavyo waokoa Waumini.
Hiyo ndio dawa nilokuletea jaribu ili upate kupona, kwa sababu hapo juu tumeambiwa nafsi zetu tunaziona japo tunaleta udhuru, basi kwa hiyo dawa hii ni ya kukumbuka huwezi kuendelea(kuleta udhuru) na kutenda dhanbi wakati unamtaja Mollah wako kutokea moyoni hiyo ni (Awareness), masisitizo yote ni katika(ZIKR)kukumbuka, huwezi kumkumbuka Mollah wako huku unamtii shetani, ukiona unasoma na chochote hakibadiliki, hee wewe tena unataka operesheni tena kubwa.Na tilia wasi wasi Imani yako.
Mollah wangu anajua zaidi.
A.Baja
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment