Wednesday, August 8, 2012

IJUWE LAYLATUL QADIR(KUMI LA DHAMANA YA MOTO)PART 2

Asalaam Aleiykum.

Kwanini usipate dhamana na wewe umeamrishwa na Mollah wako na umetii amri yake, lakini sasa linalofatia ni tatizo ulokua nalo mwanaadamu,  Tatizo ulokua nalo huitaki dhamana hii alokupa Mollah wako unaivunja hata husubiri siku ya pili, pengine siku ile ile umeandama tu unapiga simu kwa hawara, au umo katika (Yaum-shaka)ushaupiga mvinyo chopi umelewa,huna haja ya kujua umeandama au haujaandama hilo sio tatizo lako, Muumin unaanza kupanga mambo ya ufisadi hata mwezi haujaonekana.
"Enyi Waumin Dhamana hii mmepewa lakini hamdumu nayo kabisa hata wiki moja haifiki meshaivunja, Unajikuta mja ushachafua Book lako na hivi ndivo tulivo Mollah wetu katukirimu zawadi hii ndani ya kumi hili la mwisho akatupa zaidi nayo ni hii Laylatul Qadir kuwamo katika kumi hili lakini wapi.
Na ajitizame kila mtu vipi anaivunja Dhamana hiyo pengine huko kuitambua yaweza kuwa ndio dawa yako. Na kama huwezi kuitambua dawa yako basi wacha nikupe mimi dawa yangu ninayo ijua labda yaweza ikakutibu, Kwanza napenda uelewe kila mtu anaipata na kuwemo katika (Laylatu-Qadir)lakini inategemea inakukuta katika hali gani, kabla ya kuigusa hiyo Nyota ya jaha(Laylatul-Qadir)au kuipata hiyo Dhamana ni lazima kwanza ufe, yakukute mauti ungali (Hai),kwanini unaogopa kufa hali unajua kuna siku utafariki na wala hamna shaka katika hilo, Jee ushawahi kufikiri siku utayokufa? huku watu wameuchukua mwili wako, wengine wanalia, imeshakujia habari wakati mwili wako unapokoshwa na watu wengine ikisha wakauvika sanda halafu wakautia kwenye jeneza, wakawa wanaupeleka makaburini huku unapitishwa pengine kwenye baraza yako au mtaani kwako, na walokua marafiki zako wengine watakuja mazikoni kwako na wengine wanaendelea na biashara zao kama kawaida.
Watakapo kufikisha makaburini watakufukia haraka haraka ikisha hao wanashika njia na ndugu na marafiki zako wanaendelea na biashara zao kama kawaida wewe utabakia sehemu ilo kimya, hapiti mtu peke yako unasubiri siku ya kuhukumiwa na hapo huna dhamana tena.
Basi kabla ya kukuta Mauti hayo nakutaka ufe ungali hai ili upate ladha ya maisha yenye dhamana, Vipi sasa huko kufa ukiwa hai?.
Endelea part 3

No comments:

Post a Comment