Asalaam Aleiykum,
Wengine unawakuta wakiwa katika hali ya maasi, wengine unawakuta wakiwa wamelala, na wengine umewakuta wako katika hali ya kufanya Ibada, Ndio maana kwa wale utakao wakuta wamo kwenye Ibada hii ya saum basi wao wanapata moja kwa moja dhamana ya kunusuriwa na Moto, na hususan katika kumi hili la mwisho.
لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ خَيۡرٌ۬ مِّنۡ أَلۡفِ شَہۡرٍ۬
"Hakika ya usiku huu ni bora kuliko miezi elfu"
Ukiupata usiku huu kweli kweli ikisha ukaamua sasa unakufa ukiwa hai, basi ubora wake ni kupita hiyo miaka 83 ya umri wako unao ishi, sababu dhanbi zote zinafutwa, maisha yako yote yanabadilika kuwa(Blissful)furaha tupu, unaridhika na kila kadara alokupangia Mollah wako na wala hutaki zaidi,huwi tena kama matajiri wetu wa kileo eti anaomba dua Mungu niongezee utajiri, hii wewe ushapewa basi unaomba uongezewe nini tena,mapesa yote, mali zote bado unaomba upewe zaidi, basi hujatosheka tu, ndio maana unaona ukiumwa jipu tu unaanza kuhuzunika unaona kifo hicho kinakuja kukutenganisha na mali yako.
Ukiiona au kuipata hiyo Qadir unakua huna khofu tena, inakuwa kwako ukifa sawa au ukiwa hai kwako sawa. Ukipewa umaskini sawa, ukishushiwa maradhi sawa, lakini ukiona mwezi wa Ramadhan umekwisha na wewe unaendelea kupigana na kadara za Muumba wako, unashindana kutafuta utajiri kwa nguvu zako basi jijue umo hasarani.
تَنَزَّلُ ٱلۡمَلَـٰٓٮِٕكَةُ وَٱلرُّوحُ فِيہَا بِإِذۡنِ رَبِّہِم مِّن كُلِّ أَمۡرٍ۬
"Huteremka Malaika(kwenye usiku huu)na Roho za (Wanaadamu)kwa idhini ya Mollah(wako)na kila amri (ya mambo yake)"
Huko ndiko kusafishwa, huku ndiko huko kuiona na ukawa umetakasika, msafi kwa kila hatua unayopiga mpaka mwisho wa umri wako,Mweupe unakua na (aura)fulani kila anaekuona au kukusikia anatamani awe karibu na wewe, dua zako hazirudi, mwenendo wa maisha yako unakua mfano wa Quraan unasikia tabu hata kutamka neno la uongo, unakuwa nuru tupu kuanzia tabia mpaka umbile lako lakini watu wakawaida hawawezi kuijua siri hiyo.
سَلَـٰمٌ هِىَ حَتَّىٰ مَطۡلَعِ ٱلۡفَجۡرِ
"Na ni salama(usiku)huu mpaka inapo pambazuka alfajiri"
Linapotamkwa neno salama basi jua ndani yake limebebwa neno la amani, na maana ya neno la amani ni (utulivu)ukimya ndio maana hata utaona vazi la kiislamu limekua rangi nyeupe, kumaanisha utulivu, utaratibu,utiifu,upole,uangalifu,ukimya na uvumilivu, Na hiyo ndio itakua hali ya wacha Mungu huko peponi ambayo sote tunatakiwa tuitarajie.
Naam hiyo ndio nyota ya (Jaha)unayoitaka timiza masharti yake ili upate kuiona, na ukiiyona mambo mawili yanaweza kutokezea nayo ima utahadithia au utanyamaza kimya kama wengine walochagua kufanya hivo.
Namalizia kwa kukupa habari kuwa hiyo Laylatul Qadir haionekani kwa haya macho ya kawaida, ikiwa wanaadamu hatujui nini umeme vipi leo unaweza kuijua nuru kwa macho ya kawaida. Jitupe kwa Mollah wako na Mollah wako ni mwenye kujua kama umejitupa kweli au unasubiri mwezi upite uanze visa vyako, na ukiwa umejitupa kweli basi Wallahi kuna siku utaondolewa pazia ili uone maajabu hayo ya Laylatul Qadir.
Sasa naomba dua, kwa kukutakieni kheri na mema kutoka kwa Mollah:Inshaallah darsa zitaendelea kama zilivo anza:
Mollah atujaalie Saum hii makbul na nyengine zinazofatia panapo majaaliwa.
"Ewe Mollah wangu kwa dhati ya uwezo wako niteremshie Nuru ninayoweza kuipokea, ambayo katika uwezo wako imeweza kuondoa kiza kilonizunguka,Ewe Mollah wangu nijaalie Nuru itakayongarisha mwili mzima ili yakinikuta marejeo katika ufalme wako niwe katika walofunikwa na nuru yako".
"Ewe Mollah wangu najikinga kwako na maneno yoyote ambayo yataleta usumbufu, maharibiko, au shaka kwa wale watokua hawajanifahamu, Kwako wewe Mollah wangu ndiko inapotokea hekima na mimi sina la zaidi ila kumuombea Bwana Mtume s.a.w na masahaba zake baraka zitokazo kwako. Amin
Abdulla Baja
No comments:
Post a Comment