Tumeingia katika kumi la kusamehewa inafaa tumshukuru Mollah wetu alomtukufu katika kutuwekea Rehma hii ya kutusamehe katika mwezi huu wa Ramadhan, Imekujia habari kwamba kila jambo lina ishara katika ulimwengu huu, hujawahi kupata habari yakuwa wanyama wanakimbia masaa machache kabla ya kutokea kinmbunga au tetemeko la Ardhi katika mji, jee hujapata kuwatizama ndege wanavojificha robo saa kabla ya kuanza mvua, zote hizo ni ishara nyengine hata huzijui huna elimu nazo, kama mwili wako binaadamu miezi sita kabla hujaumwa unaleta ishara za ugonjwa lakini wengi hatujui, Hata mauti kwa wenye kujua miezi sita kabla wanajua safari ishawadia lakini tumo katika lepe lepe la usingizi hatuyajui hayo.
Aliuliza mtoto wa Bwana Mtume s.a.w bibi Fatma "Ewe Baba utakapokufa wewe mimi baada ya muda gani nitakufata""akajibiwa baada ya miezi sita wala si zaidi,na kweli baada ya miezi sita akafariki, "ndio maana utaona wale wacha Mungu wa kweli kweli anaweza kukwambia nimebakisha miezi mitatu au siku tatu katika ulimwengu huu, na hata watu wa kawaida hupata ndoto au ilham ikawa wanasema maneno ya kukuaga na wewe ukawa unashangaa, naam hivi ndivo ilivo kila kitu kina ishara na leo hii tunapita katika mti wa ishara sasa wacha tugusie hii ishara ya kusamehewa ambayo imehusu maudhui yetu ya leo.
Kwanini unasamehewa?, Kusamehewa ni Rehma itokayo kwa Mollah wako alompangia mja wake yoyote yule atakae muomba toba, "Akasema Mollah wako mlango huu wa Rehma ya Toba uko wazi kwa wale wafanyao madhanbi,wanoasi, na waloghafilika.
"Ewe nafsi Tubi"wewe umemaliza kumi la Rehma na sasa umo katika kumi la Maghfira basi ikiwa umefunga kwa Iman na ikhtisaba katika kumi hili wewe hapo ulipo umejaa Rehma za Mollah wako na yatosha hiyo pekee kuwa ishara ya kusamehewa, lau kama unataka uthibitisho ili uridhike kabla hatujaanza kuzichambua ishara nyengine basi yapitie maneno ya Mollah wako yaliyomo kwenye (surat-Zumar)
قُلۡ يَـٰعِبَادِىَ ٱلَّذِينَ أَسۡرَفُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡ لَا تَقۡنَطُواْ مِن رَّحۡمَةِ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ يَغۡفِرُ ٱلذُّنُوبَ جَمِيعًاۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
"Sema"Enyi waja wangu mlodhulumu nafsi zenu,msikate tamaa na Rehma za Mwenye-enzi-Mungu, Hakika Mwenye-enzi-Mungu husamehe dhanbi zote,hakika yeye ni Mwingi wa kusamehe na mwingi wa Kurehemu".
Ikiwa walotenda dhanbi hali hiyo, wanapewa ahadi ya kusamehewa dhanbi zao zote kutokana na Rehma ya Mwenye-enzi-Mungu, Nini habari yako wewe ulofunga katika mwezi huu na ukapita katika kumi la mwanzo lilojaa hizo Rehma, hujapata ishara zozote za huzuni katika moyo wako kuhusiana na dhanbi zako ulotenda ukaanza kuomba Toba,Na jee bado hayajakuingia majuto moyoni mwako kwa makosa uloyafanya, ikiwa hujapata bado ishara hizo mbili basi ikumbatie ishara hii ya (Taqwa)hebu miminika machozi kwa wingi katika kumi hili la msamaha upate kusamehewa dhanbi zako zilopita, isije ikakupita kumi hili ukawa huna hata ishara moja katika hizi tatu nilozitaja, usugue moyo wako labda kutu zimezidi uzidishie moyo wako imani ili Mollah wako akufunike kwenye bawa la Msamaha.
Sasa kwanini isiwe hivyo wakati umefanikiwa kupiga hatua moja kubwa ya kuirekebisha tabia yako kubwa kuliko zote ilokuganda ya kujizuia kula, ikiwa kwa muda wa siku kumi umeweza kupiga hatua hii umeonesha mfano sasa kwanini Mollah wako asikupe ishara za kukusamehe, Na ukitaka kuzijua ishara zilobakia zakwamba sasa una tamaa ya kusamehewa-enedelea sehemu ya pili.
No comments:
Post a Comment