Thursday, July 26, 2012

BAHARI YA TAQWA(KUMI LA REHMA)PART 2

Asalaam Aleiykum.
Sasa unataka kuipata Taqwa umejiuliza katika mwezi huu wana hali gani wale wasokua na futari ili uwasaidie(Hiyo Taqwa)Nini hali ya wazee walokuwa wagonjwa(HiyoTaqwa)kwanini unaendelea kuzuia hizo pesa au mali yako kwa faida ya nani?,jikumbushe umekuja katika dunia hii huna kitu na utaondoka huna kitu, "Enyi matajiri nyinyi isifike siku ya kufukiwa na hali umeacha marundo ya mali duniani bado hujayatolea zaka au sadaka"atahadhari sana mtu kumfika siku hiyo mapesa yamelaliana bank hususan katika mwezi huu waRamadhan, Qura'an inatukumbusha:.يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلۡتَنظُرۡ نَفۡسٌ۬ مَّا قَدَّمَتۡ لِغَدٍ۬‌ۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ
"Enyi Mloamini mcheni Mwenye-enzi-Mungu na kila nafsi iangalie(kile)inachotanguliza kwa ajili ya huko (Akhera), Na mcheni Mwenye-enzi-Mungu, Hakika Mollah wenu ana habari(Anayajua)yale yote mnayoyatenda"
Naam vinatakiwa hapo vitendo vya Taqwa ndio vyenye uzito mkubwa kesho wakati umefunikwa vipande vya vitambaa, amali zote zishakatika, nafasi hii ulopewa uko hai hujaitumia umeshghulika na dunia, sasa ufanye nini upate hiyo Taqwa na malipo mema kwa Mollah wako Masharti yenyewe hata sio mengi hayafiki hata kumi huna haja hata yakutoa rushwa, sasa ufanye nini kinachotakiwa hapo kama wewe una mali sio tajiri limetumika neno una mali pesa pia zimo katika mali,nini tunatakiwa tufanye tuipate hiyo Taqwa na tuweke zawadi zetu za huko Akhera, la Mwanzo kabisa unatakiwa utoe hicho ulichokua nacho kwa mapenzi sio umenuna, toeni hiyo mali mnayoipenda ikiwa pesa au kitu chengine, kwanza kabisa wapeni walo jamaa zenu, halafu Mayatima, ikisha maskini, na wapeni wasafiri waloharibikiwa njiani, na wale wenye kukuombeni msiwakimbie, ikisha hayo yote sasa simamisheni sala na kutoa zaka, na mtekeleze ahadi mnazozitoa basi mkitenda hayo mtakua wacha Mungu wa kweli na wale wasokua na kitu kamataneni na kamba ya kumkumbuka Mollah wenu kwa wingiwa ibada, na mkitekeleza hilo moja tu basi na nyinyi mtakua katika wacha Mungu wa kweli, na hiyo ndio kheri anayokutakieni Mollah wenu na atakuruzukuni pasi na hisabu.Umo katika mwezi wa kulea Roho fanya japo machache ujikurubishe kwa Mollah wako.


Abdulla Baja










No comments:

Post a Comment