Monday, July 9, 2012
UMUHIMU WA DUA NA MAISHA YAKO(PART 2)
Asalaam-Aleiykum: Sasa nini chakufanya jambo la mwanzo unatakiwa uteremke katika katika moyo wako, kwani ndani ya huo moyo ndipo inapokaa imani yako, na ndani ya hiyo Imani ndipo inapotokea hiyo Dua (ndio maana mwanzoni katika ile aya ukaambiwa waniamini)ukiwa na hiyo Imani basi umeshapata(Miracle)hutaki Sheikh,wala Ustaadh au mwengine yoyote, na wala asipite mtu akakwambia ahh usiombe dua hivi na vile,haramu haifai, wote hao ni mabingwa wa kupanga maneno, wachunguze wenyewe hawana Imani ni maneno yanawatoka vinywani mwao hawana yakinifu yoyote, muulize vipi Dua itakua haramu au makosa wakati imeshuka kwa sababu ya hiyo haramu na makosa. Na kama itakupata shaka jitizame wewe mwenyewe ni dua tupu toka unaamka mpaka una lala,Maisha yako yote ni dua tupu, ukitaka kula dua, ukishikwa na kiu dua, kuvuta kwako pumzi dua kila kitu chako ni dua mpaka ukitaka kunyanyua mguu dua lakini masikini bado hujajua siku utakayo kuja kujua yatakutoka machozi Mollah wako akikufungulia (Elimu)hiyo. Nini Dua?. Dua ni mfano wa Ua likitaka kuchanua halisubiri eti mpaka wewe upite eti ndio lichanue, wakati ukifika halijali chochote linachanua tu umepita hukupita wala halichagui wakati na hivyo ndio dua ya imani itokayo moyoni, haijali pahala au aibu(haimuogopi sheikh eti atasikia na yeye kashanikataza)kwani humuoni Imam Mtu mzima anaomba dua machozi yanamiminika hajapigwa au kufanywa chochote na wewe kama uko nyuma yake au unatizama kwenye TV inakutoka (Amin)bila ya kukusudia wapi yule Imam dua ile imetokea na wewe kagusa vipi?hebu jiulize maswala haya usiwe unakubali mambo bila ya kuyafanyia uchunguzi. Naam hapo nyote wawili inakua mmepagusa pale panapotokea dua na hiyo ndio dua ya kweli inayotokea Moyoni hapakugusi hapo isipokua ujue kipimo cha Imani yako. Na usijizuie ukitaka kulia kwani hata Bwana Mtume s.a.w Alitokwa na machozi kama anavotuhadithia Ibn Umar r.a "Mtume s.a.w Alikwenda kumtizama Bwana Saad Bin Ubeidah r.a alipokuwa anaumwa kwa kuwa Bwana Mtume s.a.w ni mtu wa mapenzi na wakati wote akiishi katika moyo wa Imani machozi yakawa yanamiminika, Katika mahudhurio yale alikuwepo masahaba Abrahman bin Auf r.a Sad bin Waqas r.a na Abdullah bin Masoud r.a na wao machozi yakawa yanawatoka hizo ndizo imani hizo ndio hisia,Bwana Mtume s.a.w akwaambia sikilizeni Mollah hampi adhabu mtu kwa kulia au kuhuzunika ila ana adhibu au kusamehe kutokana na yale yalotamkwa na ulimi(Maasi-au Dua). Inasikitisha siku hizi unakwenda kwenye nyumba za misiba eti watu sijui wanaogopa au wamekatazwa(leo mpaka dua upewe ruhusa)lakini utakuta mwenye msiba yupo kimya walokwenda kutoa pole wanazungumza mambo ya kipuuzi au mpira (Lakini dua haramu)hususan wanaume na hivi ndio tulivofikia kujua kwetu sana kumetufikisha katika hali kama hii. Nakumbuka katika darsa zetu hapo zamani lazima itolewe (Riwaya)si hadith napenda uelewe ni riwaya za kuchangamsha (Darsa)lakini ndani yake kuna mafunzo makubwa,"Kilitolewa kisa cha (IBILIS)kitafakari sana kisa hiki halafu utafikia uamuzi kina mafunzo au hakina.(Mke wa Ibilis siku moja alimuuliza mumewe "Ewe Ibilis mbona siku hizi nakuona huna raha ukiingia umenuna ukitoka mnyonge"Akajibu Ibilis ninahuzuni kubwa kwani nimekuwa (Jobless)sina kazi siku hizi."Akasema yule mke hee mbona mambo makubwa haya kwani wewe si kazi yako ya milele""akajibu Ibilis Ahh bibie siku hizi wameingilia katia watu wanojiita masheikh watu hawa imekua dhiki juu yangu, wanawakataza watu wao kuelekea kwa Mungu,kumkumbuka Mollah wao sasa mpaka dua wanaziondosha, wanadhulumu waumini kazi zote nilokua nafanya mimi wamechukua wao. Na Hii ndio hali tulofikia watu wanaifanya kazi za Ibilis lakini huwezi kugundua mpaka uwe na upeo wa kuona. Sasa nakuusieni mkifikwa na misiba mtu aseme kabisa mnakuja mjue hapa tunasoma dua au tuna nyamaza kimya mpaka mnaondoka, pia tambueni Mollah wenu kakupeni siku hizi tatu kubwa akakutakeni mumkumbuke kwa dua katika siku hizi, lakini wapi sie ndio tumechagua siku hizi ndio kumsahau kabisa Mollah wetu, siku gani hizi, siku ya kuzaliwa mtoto, siku yako ya harusi au unapokufika msiba, asije akaja mtu akakwambieni vyengine hebu takeni ushahidi japo kidogo katika Qura'an asije mtu na hadith yake moja akakuondosheeni Rehema zote zilizomo ndani ya DUA. Sasa namuomba Mollah wangu kwa kusema"Ewe Mollah wangu Nakuomba kwa sifa za majina yako yote utuongeze nguvu za moyo wa imani na roho zetu asiweze yoyote yule kuja kuuingia nyoyo zetu akatwambia dua ni haramu na sisi tukamkubalia, Nakuomba Mollah wangu usafishe ulimi wangu uyathibitishe ukweli wa maneno yangu. Mollah wangu nipe mimi na waislamu wenzangu mioyo ya kimaskini wakutaka radhi zako katika kutukubalia maombi yetu(DUA)utie khofu moyo huu wa kukuogopa wewe na kuwa karibu na wewe,Mollah wangu yafanye maneno yangu yapokelewe kwa moyo mkunjufu kwa wale wenye Imani na wanokupenda wewe, Na mwisho Mollah wangu nipe ukaribu niwe karibu ya wale wenye kukujua wewe, namalizia kwa kumsalia kipenzi chetu Mtume s.a.w Amin. Abdullah Baja
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment