Thursday, July 26, 2012

BAHARI YA TAQWA(KUMI LA REHMA)PART 1

Asalaam Aleiykum,
Katika simulizi ya hadith ya hekima inasimuliwa kisa katika vitabu vya zamani kuhusiana na Mji katika miji karibu na Sham. Katika mji huo kulikuwa na wacha Mungu wakiishi na Waumini wa kawaida katika harakati za maisha ya kila siku, Ikawa kila mwaka wale wacha Mungu mmoja moja anachupa katika bahari kuogelea, lakini inatokea ajabu kila akipiga mbizi Mcha Mungu basi haji juu tena anapotea, basi kuona vile Waumini wa kawaida ikawashika shauku kutaka kujua nini kinaendelea, Kwanini Wacha Mungu wanagombea safari hii zamu yangu niachieni mimi nk. Waumini wa kawaida wakaamua safari hii achupe mmoja katika wao lakini lazima katika kukoga huko wamfunge kamba halafu apige mbizi ili wapate kujua huko chini kuna nini na kwanini watu wakenda hawataki kurudi.
Wakamfunga kamba mwenziwao ikisha akachupa alipokwisha kuchupa na kupiga mbizi baada ya muda wakaamua kuivuta kamba lakini alipokuja juu akaja na maradhi yaani akawa bubu, hakusema tena yale aloyaona huko chini(upande wa pili)watu wakashikwa na khofu ikawa sasa hata kuogelea hawendi tena.
Na hali kama hii ndio imetukumba mpaka sasa watu hawataki kabisa kujua upande wa pili kuna nini, Mambo ya dini yanawekera, habari za Mollah wao ndio mama hazitakiwi kabisa, inakua kusikiliza au kusoma mambo haya ni dhiki tupu, massage ya mwanzo kutupa ni ya mambo ya (Dini)anasema mtu usitutie dhiki na vitisho vyako, kumbe tumo katika kuwakumbusha zawadi na fadhila zilizopo upande wa pili (Akhera)ni nyingi na kubwa kuliko hizi chache zilizopo(duniani), Lakini wapi kila mtu anaogopa kuchupa bahari nyeusi (Deep sea)kiza kitupu watu wote wanaogopa. Naam Ucha Mungu unataka kujitolea muhanga upige mbizi hujui chini au (Upande wa pili kuna nini?).Ndio maana utaona watu wote wanalimbikiza vitega uchumi vyote hapa Duniani, Pengine ume (invest)kwenye mapenzi, au una vitega uchumi kwenye maduka, au pengine una majumba au una mashamba au una cheo serekalini na hicho ndio unacho kiabudu huna chengine hivyo unadhani utajishughulisha kutafuta (Taqwa),unaweza kufanya mazoezi ya (Taqwa)ukajihisi unayo taqwa na sijida kubwa ikakudanganya kumbe ni kovu tu, Lakini hiyo (Taqwa)lazima uweke vitega uchumi vya huko akhera, na vitega uchumi vya huko ni vigumu, kwanza unaambiwa nini katika Qura'an' 
ٱلۡمَالُ وَٱلۡبَنُونَ زِينَةُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا‌ۖ وَٱلۡبَـٰقِيَـٰتُ ٱلصَّـٰلِحَـٰتُ خَيۡرٌ عِندَ رَبِّكَ ثَوَابً۬ا وَخَيۡرٌ أَمَلاً۬ "Mali na watoto ni mapambo ya duniani,Vinavyobakia ni vitendo vizuri, na ni bora mbele ya Mollah wako kwa Thawab na matendo ya kheri"
Hizo mali mnazozichuma na kuziabudu na hao watoto mnaoringia Mwenye-enzi-Mungu anasema ni mapambo hamna uhusiano wowote wa kudumu baina yenu, ndio maana ukiumwa uko peke yako watoto wote wanakukimbia, ukifa peke yako, ukiwa mzee peke yako, kama ulivokuja peke yako na wao wamekuja peke yao kwa hiyo na hiyo mali imekuja isikushughulishe ukasahau yule alokuleta, mkumbuke yule anokupa usingizi, mkumbuke anokusaidia kuvuta pumzi, mkumbuke yule anaekufanya ukaona na kusikia, yule mwenye kukupa afya, basi huzioni Rehma zote hizo ukazinduka yakakutoka machozi kwa ajili ya Mollah wako ukaona hujafanya chochote katika mwezi huu wa Ramadhani kuitafuta hiyo Taqwa, sasa ufanye nini japo kuikaribia hiyo Taqwa. Endelea sehemu ya pili 2.

No comments:

Post a Comment