Sunday, July 15, 2012

SIRI YA RAMADHAN(VIPI UPATE TAQWA)PART 3

Asalaam Aleiykum:
Siku zote mnaambiwa Shetani katika mwezi huu anafungwa na mimi leo nakwambieni vifaa vya shetani havifungwi viko wazi na mnaendelea kuvitumia kama kawaida.
Sasa funga ina maana gani? maana yake vile vitu vyote vyenye kukuondoa au kukufanya mwaka mzima ukamsahau Mollah wako basi sasa uvifunge, kama TV, kama Karata,kama Senema,kama Baraza za mambo ya kipuuzi, kama kucheza Game au Video za harusi, kama kusikiliza nyimbo, kama kutizama mambo ya maasi na kuyatenda na mengine mengi nyinyi mnayajua sina haja mimi kutaja kimoja kimoja.
Funga maana yake katika mwezi huu usiruhusu kupita kitu chochote katika akili yako kika kusahaulisha kumdhukuru Mollah wako hata dakika moja na ukaacha kumkumbuka, sababu hayo yote yanakunyima fursa ya kuipata hiyo Rehma na kuishi ndani ya (Taqwa).
Sasa wacha tuiguse maana ya kufunga ili tujue Rehma inapatikana vipi, kufunga ni kufanya gap au kujenga daraja baina ya Roho na kiwiliwili,au maana nyengine kuwa(aware-alert)au kuwasha nuru au taa katika umbile lako kwa yale masaa yote unayofunga au siku zote yategemea funga yako ya aina gani, na la muhimu linachowasha hiyo taa au kukufanya (aware)au kukupa hiyo nuru ni hicho chakula, mimi hapa leo nitagusia hili moja la chakula kwa kuwa funga zetu ndio zinanzia hapo na kuishia hapo hapo.
Jee umeshawahi kujiuliza kwanini hasa ukifunga kutwa unakua unafikiri chakula, mara madizi mabivu, mara kalmati n.k imekupitikia katika akili kwanini inakua hivyo, kumbuka tena Shetani kafungwa lakini nyenzo zake zinaendelea ikiwemo akili haitaki kabisa kumkumbuka Mollah wake lakini imeshghulika na chakula mchana kutwa, na hilo ni moja linalo kukuondoshea ghushui na taqwa na kuikosa Rehma ya Mollah wako, nimechagua kulizungumza hili la chakula kwa kuwa ni rahisi kwangu kukuonesha njia za rahisi kuipata hiyo Rehma, njia ziko nyingi lakini zengine ni ngumu kwako, natumai hili la chakula linaweza kukusaidia.
Sasa ikiwa hiyo akili inakupeleka katika kukumbuka vyakula basi tambua ina uwezo wa kukupeleka katika upande mwengine, nini kinyume cha shibe ni njaa hata siku moja hujawahi kuifikiria njaa, wengi wetu tunakula hata bila ya kushikwa na njaa, tunakula kwa ajili ya tabia usibishe fanya uchunguzi wewe mwenyewe hivyo ushawahi kushikwa na njaa ukenda kula, au wakati wa kula ndio umefika unakwenda kula?na hilo unalitenda lakini huna njaa yoyote na unachofanya ni tabia, Sasa leo nataka kukufundisha hiyo njaa inaweza kuwa hilo daraja la kukuvusha ukenda sehemu nyengine, siku zote njaa inakupeleka wewe pasi na kujua unaanza kufikiri chakula, basi kuanzia leo kaa makini isubiri pale njaa inapokuja kuna wakati njaa inakuja lakini wewe fikira zako zote zinapelekwa katika chakula, sasa kuanzia leo subiri ikija njaa anza kuifikiri hiyo njaa,teremka chini kwenye tumbo, kuna kitu utahisi baina ya kitovu na mbavu kinakaa kwa muda mchache ukiweza kua (aware)na kitu hicho basi mara moja utaona njaa inapotea na nguvu zake zinakua (transform)katika hali nyengine kabisa, ukimaliza hapo kukigundua kitu hicho kamata (Mashafu)au kakae msikitini, nenda katizame wagonjwa, au kasaidie wazee na hali itakayokutokezea hapo ndio hiyo Rehma na hapo kama huna cha kufanya aya ya mbele inakwambia kakae itikafu, utaona unakua mpole, hamaki zitakuondoka,utaanza kuwa (alert)kama taa ilowaka hapo utaipata (siri ya ramadhan),lakini usije ukababaishwa na uangukaji wa damu(low blood sugar)lazima ujue tafauti yake.
Napenda uelewe njaa ni kitu kilichomo katika mwili wako na hizo ni Rehma katika uweza wa Mollah wako itumie ikubadilishe kutoka katika kuwaza mambo ya vyakula ikupeleke kwengine.Njaa inakufanya (alert)ndio maana huwezi kukuta mtu ana njaa akatafuta mambo ya uasherati n.k kwa kuwa wakati ule yuko (alert)kasha washa taa lakini ya kumurika chakula sasa imurike neema ya Mollah wako kwa kufanya (Taqwa)uwe katika walofuzu, napenda kukujulisha pia ndio maana mkaambiwa mkifutari msishibe sana kwani shibe inakupelekeni katika kiza mnakua hamuezi kutenda ibada wala kumkumbuka Mollah wenu, ukiacha hayo nilokwambia mwanzoni, ukaacha kauli za kipuuzi na kuchunga ulimi wako, ukajikinga na mambo ya maasi basi Bwana Mtume s.a.w anakwambia katika hili kumi la mwanzo utapata Rehma na mambo mawili yatafatia nayo ni.endelea part 4.

No comments:

Post a Comment