Asalaam Aleiykum
nimeona nikuleteeni japo kwa uchache dhumuni la hii funga ya Ramadhani najua Masheikh wakubwa wanaileza ipasavyo na kwa upeo mkubwa lakini na mimi nataka niizungumze kwa njia nyengine ili upate kujua siri ya (saum)pengine itakusaidia ikiwa unaona ina manufaa na wewe.
Enyi Mloamini melazimishwa kufunga(Saum)kama walivolazimishwa kufunga waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu.
Katika mada hii nitajaribu kugusia hasa dhumuni la kwanini ukalazimishwa, pametiwa ulazimu kutokana na miezi yote kumi na moja mwanaadamu umefungika katika shughuli iwe ya kumsahau Mollah wako au maasi yasokua na hesabu, Na kwanini isiwe hivo hali yakua wewe umeumbwa na uhuru kamili ufanye upendavo na katika uhuru huu wewe uko dhaifu, umekutana na mambo mengi huwezi kujizuia umemuasi Mollah wako na kutenda yalojiri mwenyewe unayajua,Sasa kwa mapenzi ya Mollah wako umefika mwezi huu kakutengea japo siku chache ikiwa wewe ni Muumin na una mapenzi ya Mollah wako basi sasa fanya (Taqwa)ucha Mungu.
kuna swali jengine hapa litakuzukia na kujiuliza mimi muumin najihesabu miezi hii yote kumi na moja nafanya taqwa nasimamisha sala,natoa sadaka, sasa leo vipi (Mollah)wangu ananitaka hususan katika mwezi huu nijifunge ili nifanye hiyo (Taqwa). Mambo yanakushangaza muumin, Sasa usipate taabu unaingia katika Ustaadh wa kulea (Roho)pata faida wewe na wenzako ili mwaka huu Ramadhan yako iwe ya aina nyengine kabisa na ujifunge kupata huo (Ucha-Mungu)unaotakiwa. Kabla ya kwenda mbele hebu tujiulize hili neno (Taqwa)lina maana gani, ukitaka kulitafsiri neno hili basi hata bahari haitoshi kuliandika tafsiri yake, lakini wacha tupate uchache wa maana yake ili tukiendelea mbele tujue nini tunachokizungumza, Nini (Taqwa) taqwa ni mapenzi ya kukurejesha kwa Mollah wako,Taqwa ni vitendo vyote vya kheri alivoridhia Mollah wako,Taqwa ni huruma,Taqwa ni kufa ukiwa hai kwa ajili ya Mollah wako(hii inataka ufafanuzi inshaalah siku za mbeleni),Taqwa ni subira na kama nilivosema zipo tafsiri nyingi ya maana ya neno hili na mwisho kabisa kufupisha tafsiri yetu niseme (Taqwa)ni kurejea nyumbani ulikotoka kwa Mollah wako.
Sasa kabla ya kupata hii Taqwa kuna kitu lazima ukipate ili kikuchukue kukupeleka katika hiyo Taqwa, kitu gani hicho kinacho kupeleka, tutegee sikio kuisikiliza hadith ilopokelewa na Sahaba Salman farsy r.a "Anasema Bwana Mtume s.a.w"Umekujieni mwezi Mtukufu wenye baraka, ndani ya mwezi huu kuna mafungu matatu,Fungu la kwanza Rehma,na la pili Maghfira, na la tatu kuipata Pepo na kuepushwa na Jahannam. Sasa kazi yangu ya leo nikukujulisha hiyo Rehma inapatikana vipi kama unajua basi hakuna ziada njema tembea na mimi ili tukachume mti huu wa Rehma ili tupate kujuwa hili tunda la (taqwa)lina ladha gani?.endelea part 2
No comments:
Post a Comment